Effects za UKUTA

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,105
Reaction score
829,003
Leo tarehe mosi mwezi wa tisa ni siku iliyoingia kwenye vitabu muhimu vya historia

Kimataifa ni siku jua lilipopatwa. Wizara ya utalii? Imetuangusha sana hii ndio ilikuwa siku ya kuitangaza nchi na kupiga pesa ya kufa mtu..! Kupatwa kwa jua kama leo kutakuja kutokea tena miaka takribani 300 ijayo! HATUTAKUWEPO lakini maandishi haya inshallah yatakuwepo

Kitaifa ni Kichekesho kidogo! Leo ndio majeshi yetu yametimiza miaka 52 tangu kuanzishwa kwake (kubadilishwa)kwa mara ya kwanza kwenye historia ya maadhimisho ya majeshi yetu leo yalipanga kufanya yafuatayo

-kurusha ndege zetu/zake za kivita kwenye anga la Dar

-kufanya usafi kwenye maeneo na mitaa ya jiji la Dsm

-Kushiriki uchangiaji wa Damu Muhimbili na kwingineko

Shughuli hizi za majeshi zilipooza vibaya sana kwa sababu anuwai
Leo ndio ilikuwa iwe ndio uzinduzi wa maandamano bila kikomo ya UKUTA! Tunajua fika maandalizi yaliyokuwa yamefanywa na mamlaka za nchi!

Majeshi yalikuwa kwenye alert kubwa sana! Niliamua kufanya ziara Dar na kujionea hali halisi. Maeneo mengi kulikuwa na magari ya polisi yenye vioo vya giza (Ashok za mhindi)full equipped...

Yani jeshi lilikuwa haliamini bado kama hakuna maandamano ya UKUTA.. maeneo hayo ni

-Mabibo kuelekea uwanja wa Sahara

-Ubungo mitaa ya riverside

-Kawe Tanganyika packers

-Kidongo chekundu

-Jangwani

-Temeke Mwisho

-Uwanja wa sifa mtoni kwa kabuma/nyuma ya saba saba

-Mbagala Zakhem

-kona ya Tandika sweet corner

Kwa ujumla hakukuwa na foleni na mji ulikuwa umepoa mno
Nimerejea nyumbani salama
Lakini effects za ukuta zimewakumba hata members wenzetu hapa jamvini..wengi wako kifungoni japo asubuhi na mapema tulikuwa nao


UKUTA ni phenomenon ambayo haitaki hasira jabza wala kukurupuka kwakuwa walioibuni hawakuwa na hizi elements..

Kuahirishwa kwa UKUTA limekuwa ni tukio kubwa na la aina yake litakalodumu kwenye vitabu vya historia
 
"Kuahirishwa kwa UKUTA limekuwa ni tukio kubwa la aina yake litakalodumu kwenye vitabu vya kumbukumbu"....!!!!

..kazi tunayo, vitabu vya kumbukumbu teh!! Hata vizazi vijavyo vitasoma kuwa UKUTA uliahirishwa, lilikuwa tukio kubwa Tanzania haijawahi kushuhudia...
 
Leo pia Mkwepa kodi Mkubwa Mbowe amefukuzwa billicanas.

Je makamanda watamchangia?? Au ndio kazi yao kulialia kwenye keyboard tu bila msaada wowote kwa DJ.
 
 
Leo pia Mkwepa kodi Mkubwa Mbowe amefukuzwa billicanas.

Je makamanda watamchangia?? Au ndio kazi yao kulialia kwenye keyboard tu bila msaada wowote kwa DJ.
Aisee
 
Unakazana kaka.... Hahahahahah
Fungua na thread nyingine
 

Mtu mzima usihangaike kufungua thread nyingi kutaka jamii iamini kuwa ukuta una effect kwa serikali wakati in reality huo ukuta umewaletea negative effect nyingi sana nyinyi kama chadema.

Atleast tungemuona salimu mwalimu akiwa nje na sio mahabusu, au jeshi lingeacha kuranda mitaani hapo tungejua ukuta una effect na serikali imeufyata.

Hakuna lalamiko lenu hata moja katika vile viashiria vya udikteta mlivyovitaja iweje useme ukuta umeleta effects?
 
Aisee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…