EFD: Igunga wafanyabiashara wagoma kufungua maduka!

EFD: Igunga wafanyabiashara wagoma kufungua maduka!

Sijui kama unaelewa unachokisema, kwani hizo machine hua zinaangalia kinachonunuliwa dukani? Si ni muuza duka ndio anaeingiza DATA? Kwamfano nimenunua shati la Tsh 25,000/= hivi muuzaji akiamua kuandika Tsh 18,000/= machine itakataa? Yaelekea unaishi ulimwengu mwingine na sio hu, hizo machine sio suruhisho hata kidogo, twende hata kwenye mishahara kwafano, mishahara ya Wabunge, mawaziri ni ya kawaida sana tu (ambayo inastahiri kukatwa PAYE) lakini angalia miposho (hua haiandikwi kwenye salary slip) mafuta lita 50@2500 kila siku, posho za kukaa, 200k, matengenezo ya gari, dereva na mfuko wa jimbo, ukijumlisha vyote vinaleta kama Tsh 12,000,000/= lakini mshahra wa Mbunge kwa maana ya basic salary 1,800,000/= tu na hizo ndizo zinazokatwa kodi. Kwa kusema hivyo hata mfanya biashara nae akitaka anafanya tu hivyo hivyo!
Wewe ndio unajikoroga kbs ni bora hata serekali ijue kwenye 18000 kodi kapata 18% kuliko sasa ambapo unapewa risiti ambayo TRA vitabu vinafichwa kwa hiyo hata hiyo kdg nayo haifiki.Au hujui wafanyabiashara huwa wanavitabu zaidi ya kimoja kwenye risiti za mauzo?We lazima mgeni hiyo mashine usione wanazipiga vita hata ukiuza book lazima kodi upeleke TRA sasa hicho hawataki.Suala la kukata posho hilo ni mambo ya kisheria hayahitaji siasa kwakusaidia pitia INCOME TAX ACT utakuta nini kinakatwa kodi na nini hakikatwi kodi nikiongea nitakudanganya sababu hiyo act sina karibu hapa.
 
I smell rat, a big rat.
reminds me Tunisia and that machinga, no one expected what happened, only time will tell. Lets pray for the best.
 
Back
Top Bottom