Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Ndugu zangu,
Nikitafakari mwenendo wa nchi yetu kisiasa, kiuchumi na kijamii katika kipindi cha uongozi wa JK, nashawishika kuhitimisha kuwa pengine kuna laana fulani inayoitafuna nchi hii. Hivi sasa, wakati wenzetu waganda, wakenya na warwanda wakiendelea kujenga uchumi wao kwa kasi nzuri, sisi ndiyo tunazidi kudidimia. Hali ya maisha imeendelea kuwa ngumu kwa wananchi wa kawaida. bidhaa mitaani hazishikiki kwa bei kubwa. Jambo linalosikitisha ni kwamba kati ya nchi nilizotaja hapo juu, hakuna hata moja yenye rasilimali nyingi kama Tanzania.
Mwishoni nimeishia kulia tu moyoni mwangu"Ee mama yangu Tanzania ni lini watoto wako watapata furaha ya maisha kama wengine!!".
Nikitafakari mwenendo wa nchi yetu kisiasa, kiuchumi na kijamii katika kipindi cha uongozi wa JK, nashawishika kuhitimisha kuwa pengine kuna laana fulani inayoitafuna nchi hii. Hivi sasa, wakati wenzetu waganda, wakenya na warwanda wakiendelea kujenga uchumi wao kwa kasi nzuri, sisi ndiyo tunazidi kudidimia. Hali ya maisha imeendelea kuwa ngumu kwa wananchi wa kawaida. bidhaa mitaani hazishikiki kwa bei kubwa. Jambo linalosikitisha ni kwamba kati ya nchi nilizotaja hapo juu, hakuna hata moja yenye rasilimali nyingi kama Tanzania.
Mwishoni nimeishia kulia tu moyoni mwangu"Ee mama yangu Tanzania ni lini watoto wako watapata furaha ya maisha kama wengine!!".