Last week nilikuwa mkoani Iringa, Sumbawanga na Mbeya.
Mbeya ndiko nilikaa zaidi, nilitembelea karibu wilaya zote. Nilipokuwa Sumbawanga nilishuhudia Mhe. Lowassa akitua kwa Chopa na kuchukua maandamano hadi ofisi za CCM. Mmoja wa rafiki zangu pale alinieleza kuwa vijana wa bodaboda wanapewa buku10 kila moja kwa kupamba maandamano. Chopa aliyotua nayo naambiwa ni ya Askofu mkuu Gwajima wa Ufufuo na Uzima. Nilipata picha fulani.
Mbeya - tangia Tunduma nilishuhudia gari Suzuki carry ikitangaza na kutafadhalisha wananchi wenye mapenzi mema kwenda kumpokea na kumdhamini Lowassa siku mbili baadaye, barabara nzima hadi Mbeya kulikuwa na gari 3 tofauti zikihimiza watu, wengine wakisema nauli siyo tatizo.
Jijini Mbeya nilishuhudia pia gari 2 zikitangaza ujio wa EL. Kesho yake tulikwenda Kyela hadi Kasumulo, kote kulikuwa na matangazo magari yakizunguka, tulirudi kupitia Mbarali na kutokea Chunya kwenda Singida, kote watu wanaitwa kwenda Mbeya!!!
Ahaaaa! nilitambua Lowassa ni nani, amejitambulisha kwa fedha, fedha za kumwaga, kama ni zake au marafiki sijui, ila nachosema ni kuwa hakuna chengachenga kuwa utafutaji wake wa nfasi ya kwenda magogoni umetawaliwa na matumizi makubwa ya fedha. Narejea hotuba ya mwalimu kuhusu wanaotafuta urais kwa fedha!
Kwa maoni yangu, nasema aheri Lowassa kajidhihiri, wengine je? The floor is open....