Rais ajaye ni Lowassa. Hilo halina mjadala.
tena sioni sababu ya kufanya uchaguzi wa rais , hizo pesa tungepeleka kuweka umeme na barabara vijijini, EDWARD atangazwe aanze kazi mara moja
Rais ajaye ni Lowassa. Hilo halina mjadala.
Alikuibia wapi? Na kama alikuibia uliwahi kumshitaki? Wewe ndiwe unavutiwa na hela zake sio mimi nachovutiwa na utendaji wake wa kazi na uwajibikaji na sio vinginevyo usiwe unaongea vitu usivyo na uhakika navyo pia umegusia kuhusu uchawi wa TB Joshua mimi siamini ktk uchawi na siujui we endelea kuvutiwa nao
CCM wanachezea shillingi shimoni,shauri yao,baba piga kazi sisi makamanda wako tuko nyuma yako na tunaamini mungu atakufikisha amina
Utendaji gani wa firauni lowasa?Au wa kuleta Richmond?
hujui kusoma hata picha huoni?Kasema nani?
* Ya Mbeya sio gharika wala mafuriko bali ni MARAMZAMISI...
* Kwa mara nyingine Lowassa avuna wadhamini zaidi ya elfu hamsini na tatu (53,000+)...
* Aweka historia Mbeya...
Baada ya ile gharika ya jana mkoani Kilimanjaro leo hii yaliyotokea mkoa wa Mbeya yamenifanya nikose jina sahihi. Ndipo nilipompigia babu yangu kisha kumueleza na kumuuliza haya yaliyotokea Mbeya tuyaiteje?, manake naona ni zaidi ya gharika ama mafuriko..
Babu akaniambia mjukuu wangu hayo yaliyotokea Mbeya ni maramzamisi, akimaanisha (Maporomoko ya mvua za radi yaliyokuwa yanatokea katika mlima SINAI)...
Ni wazi jiji la Mbeya limefanya kile ambacho hakijawahi kutokea katika historia ya nchi hii... Lowassa kwa mara nyingine kavunja rekodi kwa kuvuna maelfu na maelfu ya wadhamini kutoka katika mkoa huo (zaidi ya wadhamini 53,000+)....
Pamoja na hilo umati mkubwa sana umejitokeza kutoka pande na viunga vyote vya jiji hilo ili kumlaki na kumsalimia Lowassa, ambaye ameonekana akiwa na nyuso ya furaha alipoona wananchi walivyo na matarajio makubwa ya kuanza safari ya matumaini...
"Hii haijawahi kutokea na sijawahi kuona tokea nizaliwe, huyu ndio mkombozi wetu wa maendeleo tunayemtarajia. Nafikiri hapa ni suala la muda tu ndio linasubiriwa mafuriko haya yanatoa picha halisi ya nguvu ya Lowassa" amesikika Mzee Mole akiongea...
My take: Hii ndio safari ya matumaini, mchakamchaka wa maendeleo...
Asante Mbeya
View attachment 261709
View attachment 261710
View attachment 261711
Leo ilikua ni zamu ya watu wa mbeya kuvuna mapesa ya Fisadi mkuu.
Hivi mikoa 15 bado......tushachoka habari za huyu mharibifu (Fisadi)