Edward Lowassa special thread

Edward Lowassa special thread

Alikuibia wapi? Na kama alikuibia uliwahi kumshitaki? Wewe ndiwe unavutiwa na hela zake sio mimi nachovutiwa na utendaji wake wa kazi na uwajibikaji na sio vinginevyo usiwe unaongea vitu usivyo na uhakika navyo pia umegusia kuhusu uchawi wa TB Joshua mimi siamini ktk uchawi na siujui we endelea kuvutiwa nao

Toa mifano mitano tu ya utendaji wake unaousifia, halafu umalizie na mtazamo wako juu ya:-

1. Mkataba na kampuni fake ya richmond iliyoliingiza taifa hasara hadi leo tunateseka.

2. Udanganyifu wake kuwahadaa watu kwamba eti shule za kata alianzisha yeye wakati ulikuwa ni mpango ulioachwa na awamu ya tatu ambao ulikuwa utekelezwe katika awamu ya nne.

3. Yeye akiwa kama waziri mkuu wakati shule za kata zinatekelezwa, suala la viwango vya elimu katika majengo hayo linabeba uzito gani katika majigambo yake hewa ya uanzilishi?

5. Mtazamo wake kuhusu ufisadi na rushwa ni upi na ana maoni gani kuhusu team yake ya yeye na akina Rostam, Chenge, Ngeleja na mafisdi wote?

6. Hizo fedha wanazotumia yeye na Rostam Aziz katika kulazimisha uraisi, wanazirudishaje baada ya kupewa nchi?

Haya ni machache. Mengine nitakuongezea ukijibu haya.
 
Sasa Shuzana, nchi hii nani atakataa kulipwa posho ya kuhudhuria mkutano wa hadhara?
 
hakuna mwanasiasa mjanja ndani ya ccm kama lowasa. alianza kampeni ya kusaka urais miaka 3 iliyopita. ameunda chama ndani ya chama kwa kila pande ndani ya taifa hili. amehonga wajumbe karibu wote wa NEC na mkutano mkuu toka bara mpaka zanzibar.kwa anayemjua lowasa hawezi shangaa juu ya umati unaojitokeza kumpokea huko mikoani... ccm wana hali mbaya saana...
 
Kwa elfu kumi kumi ni million 530,000,000/= tu. Ameishatoa kiasi hicho kwa makanisa na misikiti zaidi ya mia tangu 2010.
 
Pamoja na mbwebwe zote hizo wadhamini 450 mikoa yote bado hajapata Lowasa anatumia pesa kuwatishia mafisadi mwenzake wa ccm.
VOTE FOR UKAWA
 
Umechoka nini mpumbavu kama umechoka nyamaza kama walivyonyamaza makuwadi wenzio muache simba angurume nini mikoa 15 atatembea nchi nzima wewe kama umechoka kunywa sumu lowassa jembe wenzio washaanza kuona mafuriko yanakuja kwa kasi wanaanza kutafuta pa kukimbilia nyoka wa mdimu na mtoto wa mkulima wanakimbilia kwa mwandosya huko khofu imewatawala wakati walikuwa wanajitapa wanaungwa mkono na boss, boss naye kawamwaga live. Lazima itakuwa tu safari ya matumaini lazima.
 
Lowassa amevunja rekodi ya kukusanya watu kwa kuwahonga!!!!!????? Hiyo siyo sifa, ni fedheha! Kule Lindi bodaboda wanalia, Lowassa amewatapeli pesa waliyokubaliana, alipowakusanya kuja kumtengenezea mafuriko (RAIA TANZANIA, Ijumaa 19.6.15). Akawalipe kwanza huko, ndiyo aendelee na mafuriko yake ya kutengeneza! OVYOOOOOOOOOO!!!!!!!

Unafikiri kwa kutumia rai Tanzania. Kwanza Lindi kwa nani? Mambo ya kitoto na kijinga ungetegemea kusikia kutoka huko.
 
huyu jambazi alikuja mwanza akatulaghai tukajitokeza nyomi.Mpaka sasa hela yetu hatujalipwa na Laurence Masha.El ni laghai tulipeni hela zetu au tutatoa siri zake zote

Nasisi tutao siri zako honoget ya kuisaliti nyumba yako na kuwadhumu wadogo zako alizoaacha baba!
 
Lowassa,
Ni mtoto tu,ccm hawezi kuisaidia kuua rushwa,kwani imegeuza polisi,mahakama,usalama ni miongoni mwa wanufaika wa ufisadi,sishangai kesi za wezi zinalindwa si wenzake!
 
Lowassa raisi, pm chenge, rostam mshauri wa raisi, karamagi madini, R1 mambo ya ndani, ......

Yaani amchague Rizmoko kwenye baraza lake. Hata kama mnasema ni mgonjwa hajasahau samko la huyo kijana alipokuwa uvccm. Labda kwani wanasema kwenye siasa hayupo adui wa kudumu kama asivyokuwepo rafiki wa kudumu.
 
Ndugu wana JF
Lowasa ana nguvu sana katika safari yake ya matumaini. Katengeneza mtandao ambao yeye anauita marafiki!! Na hao marafiki wengi wao ni wafanyabiashara na watu wenye pesa ambazo bilashaka zimepatikana kwa njia zisizo sahihi. JK alipoingia madarakani aliwekwa na watu wa namna hiyo kwenye awamu yake ya kwanza. Na wote tunajua ni nini kilitokea alipounda serikali yake. Sasa watanzania tunatakiwa kuwa makini sana kwenye sanduku la kura October endapo CCM watatupitishia Lowasa. Sidhani kama tutakuwa salama kwani tuliyotendewa na JK yanatosha.
Watanzania wenzangu zindukeni semeni yatosha sasa.
 
Watanzania hakuna rais ataetupeleka kwenye nchi ya ahadi zaidi ya Lowasa,Lowasa kachaguliwa na Mungu kutukomboa watanzania
 
Siku ya udhamini 19/6/2015 mkoani kwa E. Lowassa.

Majira ya saa nane, EL ametinga ofisi za CCM mkoa akiambatana na marafiki zake na amekutana na umati mkubwa uliojitokeza kumpokea.

YALIYOJIRI:

1. Wakati anaingia ofisini, alishindwa hata kutoa mkono kwa wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa. Alikuwa akivuta mguu wake wa kulia na mara alipoketi kwenye kiti chake alionekana kabisa kuwa ana tatizo la kiafya. Aliomba kupumzika kwanza kabla hajatoka nje huku akisema, "naombeni tupumzike kidogo nimechoka sana."

2. Wakati anatoka ofisini kwenda nje kuhutubia watu, alicheleweshwa kidogo akasimama na hapo ndo tulipata kushuhudia namna mzee EL alivyo. Mikono ilikuwa inatetemeka na ikabidi aifiche mfukoni. Ni ukweli usiopingika kuwa mzee Lowassa afya yake si nzuri kwa nafasi ya urais.

3. Sasa baada ya kuwasalimia wana Mbeya, la kushangaza ni kuwa hawakuondoka, wakijua kuwa kuna pesa waliyokuwa wameahidiwa na wafuasi wa EL. Umati wa watu ulibaki eneo la tukio wakisubiri pesa.

Mara mzee akaondoka. Ikabidi wafanye vurugu wakitaka kuvunja mlango wa ofisi ya CCM mkoa ili wapewe pesa, hadi kiongozi mmoja ikabidi awatishie kutoa bunduki kama watavunja mlango wa ofisi. Ilikuwa tafrani kweli.

4. Pamoja na udhamini wote wa watu 53,000, lakini fomu muhimu ya udhamini ilikuwa inapungukiwa na wadhamini 3 hadi jana saa moja, jambo lililopelekea Guninita kuchukizwa na 4U movement waliokuwa Mbeya kuwa hawajafanya lolote. Lakini fomu za udhamini wa Lowassa zimekua mkoani hapa kwa siku 15 sasa wakitafuta wadhamini, sasa wanashindwa kujua kwanini haikukamilika.

5. Mwisho, hadi sasa wana Mbeya wanajuta kwa kudanganywa kuwa watapewa pesa ambazo mwisho wa siku hawakupewa na wanasema kama isingekuwa hizo pesa wasingekuja kabisa.

Hapa wa kulaumiwa ni familia ambayo imekubali kumwacha mzee kutafuta majukumu makubwa ya kuongoza nchi huku wakijua kuwa afya yake si nzuri. Ingefaa familia kukataa ili kumtunza mzazi wao, kadhalika kumlindia heshima yake.

Pia naomba tuanze kuchunguza vizuri majina yaliyoandikwa kwenye fomu hizi na uhalisia. Maana mkoa wa mbeya hauna wanachama wengi kiasi hicho. Yaani kwa lugha nyepesi, huyu bwana anagushi watu na hata saini zao.

Huenda vitabu vya zamani ambavyo vina majina hata ya watu waliokufa vinatumika, na hili linaonekana sana katika wilaya zote ambazo amepata wanachama wengi waliomdhamini.

Chukulia mfano Mbeya ambapo alipata umati wa watu wengi. Ndipo hapo CCM ilishindwa kupata kura japo elfu 10. Nenda Moshi Mjini na Arusha Mjini pia.

Ni muda mzuri sasa kwa chama kuangalia vyema hili zoezi, maana haya matumizi makubwa ya hela na Nguvu ili kuonyesha ulimwengu kuwa anakubalika ni mazingaombwe ambayo lazima yatafutiwe majawabu.

Maana CCM inaweza kuangalia kuwa zoezi hili linakipa nguvu chama, kumbe kuna mtu anatembea na kadi zake na kuwasajili wanachama hewa.

Nimecopy na kupaste hapa kwa mtazamo sahihi.
 
Mkakati wa hawa watu kuitishia kamati ya maadili kupitia mitandao ya kijamii ni ya kitoto na kijinga.

Hoja Kwamba Lowassa akikatwa mara chama kitakufa, maana ana wafuasi wengi sana. Mara akikatwa ataenda ACT. Basi mnaambiwa mtakatwa. Anzeni safari yenu ya matumaini na ACT

Lowassa hana wafuasi wengi. Ana wasaka fedha na wasaka tonge. Na hata Huko ACT tutajua mbivu na mbichi. Ila mtambue kwamba, CCM itukufa vibaya ikiachwa mikononi mwa mafisadi na wahuni kama Lowassa na Genge la Mafisadi papa

Hacheni huu utoto wa intimidation kwenye mitandao, mnamuharibia Lowassa wenu. Fisadi hasafishiki hata kwa dodoki na jiki. Pengine atumie Mkorogo atatakata
 
haa haa mkuu vipi mtawakata na wale wafuasi wake waliojazana NEC na kamati kuu? maana huko wale wjumbe wa NEC na mkutano mkuu hawapumui mbele ya lowasa..
 
Back
Top Bottom