Edward Lowassa special thread

Edward Lowassa special thread

Labda wewe sio raia wa nchi hii lakini kama ni raia wa hii nchi ni mambo mengi sana ambayo lowasa kafanya
 
* Ya Mbeya sio gharika wala mafuriko bali ni MARAMZAMISI...

* Kwa mara nyingine Lowassa avuna wadhamini zaidi ya elfu hamsini na tatu (53,000+)...

* Aweka historia Mbeya...

Baada ya ile gharika ya jana mkoani Kilimanjaro leo hii yaliyotokea mkoa wa Mbeya yamenifanya nikose jina sahihi. Ndipo nilipompigia babu yangu kisha kumueleza na kumuuliza haya yaliyotokea Mbeya tuyaiteje?, manake naona ni zaidi ya gharika ama mafuriko..

Babu akaniambia mjukuu wangu hayo yaliyotokea Mbeya ni maramzamisi, akimaanisha (Maporomoko ya mvua za radi yaliyokuwa yanatokea katika mlima SINAI)...

Ni wazi jiji la Mbeya limefanya kile ambacho hakijawahi kutokea katika historia ya nchi hii... Lowassa kwa mara nyingine kavunja rekodi kwa kuvuna maelfu na maelfu ya wadhamini kutoka katika mkoa huo (zaidi ya wadhamini 53,000+)....

Pamoja na hilo umati mkubwa sana umejitokeza kutoka pande na viunga vyote vya jiji hilo ili kumlaki na kumsalimia Lowassa, ambaye ameonekana akiwa na nyuso ya furaha alipoona wananchi walivyo na matarajio makubwa ya kuanza safari ya matumaini...

"Hii haijawahi kutokea na sijawahi kuona tokea nizaliwe, huyu ndio mkombozi wetu wa maendeleo tunayemtarajia. Nafikiri hapa ni suala la muda tu ndio linasubiriwa mafuriko haya yanatoa picha halisi ya nguvu ya Lowassa" amesikika Mzee Mole akiongea...

My take: Hii ndio safari ya matumaini, mchakamchaka wa maendeleo...

Asante Mbeya


View attachment 261709

View attachment 261710

View attachment 261711
 
  • Thanks
Reactions: PPM
Lowasa hashikiki
 

Attachments

  • 1434715032521.jpg
    1434715032521.jpg
    95.7 KB · Views: 104
  • 1434715092582.jpg
    1434715092582.jpg
    138.3 KB · Views: 98
  • 1434715251392.jpg
    1434715251392.jpg
    118.2 KB · Views: 97
  • 1434715321384.jpg
    1434715321384.jpg
    94.3 KB · Views: 92
Hivi hao watu hawana shughuli muhimu za kufanya?
 
Sasa hapo anajilinganisha na nani ambae keshaanza kampeni kama yeye? Anachekesha huyu bingwa wa kufisadi
 
Kesho Lowassa atakuwa Ruvuma kumaliza kazi.
 
Nilikuwa nampinga sana ila imebidi nianze kumkubali tu kwani kinywa kimeonekana kuzidiwa na nafsi... Jamani enhee tusipoteze muda, huyu ndiye rais wa Tanzania. Upinzani tujipange na upya kwa mechi ijayo 2020, ila hii ya 2015 ina wenyewe , na wenyewe ni wa kina Lowasa na CCM yao.

N.B:Mimi ni #CHADEMA damu damu, hata ukinichanja damu inatoka CHADEMA.
 
Back
Top Bottom