alpha1
JF-Expert Member
- Sep 16, 2010
- 245
- 123
Wana jf naombeni kuuliza, niliagiza mzigo flani kutoka ebay na kesho natarajia nikafanye payment, kuna mtaaram anaye jua makato ya TRA, afu mzigo ukishafika na dhl unapigiwa cm kwa ajili ya malipo ya tra au, naomba msaada cpo shwali kwenye hayo mambo, pls
Kama ulichagua na kulipia kusafirisha mzigo kwa DHL, aliyekuuzia anakutumia tracking number ambayo itakuwezesha kufuatilia na kujua mahali mzigo wako ulipofika na nini kinafanyika juu ya huo mzigo. Ukishapata tracking number unaenda website ya DHL unaingiza tracking number sehemu ya ku-track mzigo halafu unabonyeza track. Taarifa zote zinazohusiana na mzigo zitaonekana , muda, mahali ulipo na nini unafanyiwa. Kwa DHL, mzigo wowote ambao ni Non-document, lazima upitie taratibu za ushuru wa forodha mara tu unapoingia Bongo(DHL Head Office-Dar), ambako wataangalia kama unastahili kulipiwa kodi au la. Kama unastahili,DHL Agents watakupigia simu kuomba TIN (Tax-payer Identification Number) yako ili watu wa customs waitumie kufanya clearance.Gharama zote za kodi zinalipwa na agent wa DHL kwa niaba yako, na wakati wa kupokea mzigo ukishafika mjini kwako, unajulishwa na kwenda kulipa hizo gharama na zingine za DHL ndipo unachukua mzigo na kusaini.
Kiwango cha kodi kinatgeana na mzigo wenyewe na declared value, japokuwa watu wa customs kwa sasa wana-search kwenye internet kuangalia wastani wa thamani ya mzigo iwapo watahisi declared value ni ndogo. Kuna baadhi ya bidhaa hazilipiwi ushuru km PC na accessory inazoambatana nazo etc.
NB: Kabla hajatuma mzigo, muuzaji ataomba namba zako za simu kama haziko kwenye anuani yako.
Haya maelezo ni kwa mujibu wa ufahamu wangu.