East Africa Federation na Hatma ya Tanzania

Venus Star

JF-Expert Member
Dec 6, 2018
19,680
59,798
1693891522340.png

Kabla ya wakoloni kuja Africa tuliishi kwa namna yetu. Bahati mbaya historia ya Afrika imepotezwa kwa makusudi au kupotoshwa.
EAST AFRICA COMMUNITY KWA SASA

  1. The Republic of Burundi
  2. The Democratic Republic of the Congo
  3. The Republic of Kenya
  4. The Republic of Rwanda
  5. The Republic of South Sudan
  6. The Republic of Uganda
  7. The United Republic of Tanzania
Nchi zinazotarajiwa kujiunga
  1. Somalia
  2. Comoros
  3. Mozambique
  4. Sudan
  5. Ethiopia
  6. Angola
  7. Republic of Congo
  8. Zambia
Kuna mpango ambao ulianzishwa wa kuelekea kwenye Political Federation of the East African states. Tayari kuna hatua ambazo zinatakiwa kupitiwa ili kufikia katika hatua hiyo:-
  1. Customs Union
  2. Common Market
  3. Monetary Union
Na mwisho wa siku tunafikia katika kujenga nchi moja itakayokuwa na kiongozi mmoja.

Tayari Custom Union ilishapitishwa tangu mwaka 2005. Unaweza ukaipitia hapa na kusoma mambo kadha wa kadha Customs

Tayari Common Market ilishasainiwa mwaka 2010 na ilikuwa inatarajiwa kuanza kutumika mwaka December 2015. Kuna mambo kadha wa kadha yalitokea lakini ipo katika hatua za kuanza kutumika. NB: Kama sisi watanzania tutaendelea kulala mabadiliko yatafika na sisi bado tunabishana ndani ya nchi huku wenzetu wakijiandaa kutumia fursa.

Monetary Unioni ilishasainiwa mwaka 30th November 2013. Na ilikuwa inatakiwa ndani ya miaka 10 iweze kuanza kufanyiwa mikakati. Tayari kwa sasa tumo ndani ya miaka hiyo. Huenda baada ya muda hii itawekwa kwenye action.

NINI HATMA YA TANZANIA NA SIASA ZETU?
Tusipowekeza katika human capital na kuendeleza siasa hizi za kizamani, watu wa Tanzania watakuja kuachwa kutokana na fursa zitakazoendelea katika nchi mpya itakayozaliwa. Hili jambo kuna wengine wanaliona kama ndoto. Lakini kutokana na mabadiliko ya siasa za kidunia naliona linaenda kutokea siyo muda mrefu.

Sasa basi viongozi wetu wanawaandaa vipi watanzania kuweza kuingia katika hatua hizo zinazokuja? Itafikia wakati Tanzania itashindwa kuwa na sauti kutokana na kuzidiwa kura na wengine. Maana nchi zinazidi kuwa nyingi na influence ya Tanzania inazidi kupotea.

Tanzania tulikuwa tunaringa kwa kuwa na rasilimali nyingi. Ona sasa kiburi hatuna tena kutokana na jambo hilo maana DRC tayari naye ni member. Tanzania imekuwa nchi ya kawaida tu ndani ya EAC. Kama tutaendelea kuchelewesha mambo haya wenzetu watafanya wao na kutukuta sisi tunaachwa, au wachache wananufaika na mtangamano huu.

Nitaendelea kweka Statistical Data na References ili kufumbuana macho...
 
POPULATION ZIKIJIUNGA NA NCHI ZINGINE 7 NA KUWA NCHI 14
Kutokana na population ya sasa kwa nchi zote 15 zilizomo kwenye EAC na zile zinazotegemewa kuingia kwa sasa ni 616,023,170 ambapo itakuwa ni nchi ya tatu kwa population duniani. Hakika itakuwa moja ya nchi zenye nguvu duniani kwa upande wa population
  1. Burundi
  2. Democratic Republic of the Congo
  3. Kenya
  4. Rwanda
  5. South Sudan
  6. Uganda
  7. Tanzania
  8. Somalia
  9. Comoros
  10. Mozambique
  11. Sudan
  12. Ethiopia
  13. Angola
  14. Republic of Congo
  15. Zambia
SIsi kama Tanzania kwa sasa tunajiandaa vipi kuweza kushiriki katika nchi hii?
 
Kwa upande wa GDP kwa sasa kama leo tutaamua kuungana na kuwa nchi tutakuwa na $309,152,653,121. Kwahiyo itakuwa ni nchi ya 44 kwa uchumi mkubwa duniani.
 
Tukiweza kuungana nchi zote 15 tutakuwa na GDP ya $665,932,001,997 itakuwa ni nchi ya 21 kwa GDP kubwa duniani.

Nadhani kuna watu wanakuwa na uoga wa jambo ambalo halipo. Dunia imeanza kuwepo miaka mingi zana kumekuwa na muunganiko wa nchi nyingi tu na wanatofautina katika tamaduni.

Kwa mfano USA walikuwa na utofauti mkubwa mno maana kuna sehemu walikuwa wanaongea kihispania na kunasehemu walikuwa wanaongea Kingereza lakini ona sasa. USA ni kati ya mataifa yenyenguvu duniani.

Hata tukienda kwa upande wa Urusi vivyo hivyo wapo na Tamaduni zinazotofautiana lakini waliweza kuungana na kuunda nchi yenye nguvu.

Tukiamua tunaweza na ndio itakuwa moja ya ukombozi wa kweli wa mwafrika.
 
Tatizo ni commitment. Mpaka Sasa Kuna shida ya uchangiaji EAC mpaka mahakama ya EACJ imeshindwa kutatua kesi nyingi kisa pesa hakuna.
 
Kwa upande wa ukubwa wa eneo EAc federation ya sasa itakuwa na ukubwa wa square KM 4,785,779. Ambapo eneo kubwa litakuwa lifaa kwa kilimo. Na kuna mito mingi ambayo imo kwenye nchi hiyo. Vile vile maziwa makuu ya Africa yatakuwa ndani mwa EA Federation.

Kwa maana hiyo itakuwa nchi ya 7 kwa ukubwa duniani.
 
Tukiungana nchi zote hizo 15 maana yake ukubwa wake utakuwa ni square km 11,558,568. Itakuwa ni nchi ya 2 kwa ukubwa duniani.
 
Nadhani kuna watu wanakuwa na uoga wa jambo ambalo halipo. Dunia imeanza kuwepo miaka mingi zana kumekuwa na muunganiko wa nchi nyingi tu na wanatofautina katika tamaduni.
Wanaungana halafu baada ya kuungana ? Wanagawanyika tena si ndicho unataka ?
 
Kwa mfano USA walikuwa na utofauti mkubwa mno maana kuna sehemu walikuwa wanaongea kihispania na kunasehemu walikuwa wanaongea Kingereza lakini ona sasa. USA ni kati ya mataifa yenyenguvu duniani
U.S.A mpaka leo sio stable kuna majimbo yanataka kujitenga hizi huwa ni failed ideas huwezi unganisha watu wasio ona faida ya kuungana. Ndio hiki hiki cha Tanganyika na Zanzibar muungano wa kipumbavu hata huo wa EAC utakuwa version 2.0 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar
 
AU ndio mkombozi wa afrika.
Lakini kuna michezo michafu inachezwa nyuma ya pazi afrika isifikie lengo.
Inasikitisha sana.
 
Back
Top Bottom