TRUMP NA UHALALI WA URAIS WAKE
Leo kumetokea jingine likirudia, kwamba, kulikuwa na fraud ya wapiga kura 3-5milioni
Hoja: Uthbitisho wa madai yake ya wapiga haramu ni study zilizofanyika 2012 ambazo pia hazikuwa na conclusion ya kutosha ya ku back up madai hayo
Trump ni Rais ana uwezo wa kuagiza uchunguzi. Kwanini asifanye ili ukweli ujulikane
Katika tuliozungumzia uzi uliotangulia baadhi yanapata uelekeo.
Suala la fraud ya watu milioni 3-5 waliopiga kura limechukua sura mpya.
Rais Trump anategemewa kupitisha exec order ili uchunguzi ufanyike.
Hili ni swali tulilouliza mapema, kwani hafanyi hivyo
Katika hali nyingine , aliyeandika study inayotumiwa na Trump na wasaidizi 'amejitokeza'
Katika aliyoeleza ilikuwa study na yaliyotokana ikipingana na madai ya fraud
Wasaidizi wametafuta study inayoonyesha mamia ya fraud na baadhi kushtakiwa
Hapa kuna mambo mawili au matatu yatakayotokea
1. Kufanya uchunguzi kutapunguza uzito wa tuhuma zisizo na ushahidi wa kisayansi
Tuhuma zisizo za kisayansi: GOP wanaona madai hayana msingi. Hawamuungi mkono
GOP wanajua matokeo hayabadili ukweli. Wanatambua kuweka 3-5M ni kujifunga'kitanzi'
Republicans wana magavana wengi na hiyo itazua maswali, fraud ilifanyikaje wakitazama
Na je uchunguzi unaweza kutoa matokeo yanayofikirisha katika wapiga mamilion ?
2. Limeanza kutibua Democrats, wanasema hiyo ni mbinu ya kuweka voter 'suppression'
Waliofuatilia uzi wa 'uchaguzi wa US' tumeongelea voter suppression na Gerrymandering.
3. Uchunguzi utachagiza uchunguzi wa Russia na Tax returns
Kama kuna fraud inachunguzwa 'hacking ya Russia'' itakuwa na nguvu na kufuatiliwa
Trump atajfunga kamba, hawezi kukataa uchunguzi wa hacking akifanya wa fraud.
Kama mtakumbuka Obama alitoa msamaha kwa askari aliyetoa habari kwa Wikileaks.
Ilichukua masaa GOP wakaja juu. Ulikuwa mtego na walipobaini, habari imekufa kabisa
Trump haongelei kwasababu kuna suala la ku encourage hacking alilowahi kusema.
Ni ngumu sana ku square mambo matatu kwa wakati mmoja