Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

mkuu mkandala bila kuwa biased jaribu kucheki kwa jicho la 3 chama cha ACT na viongozi wake na waraka wa akina Mkumbo, si vibaya kama utarudia kusoma kwa makini hoja za Nguruvi3 kuanzia mwanzo wa thread hii.
Nimemsoma vizuri lakini kwa mwenye kutaka kuelewa akiwa nje ya Box la Uchama atagundua kuwa hizi ni njama nyinginezo kwa jicho la kujenga chuki dhidi ya watu hawa. Kwa vyovyote itakavyokuwa Kitila na Zitto wamefukuzwa na chama tena kwa sababu za Kichama. Kwa nini mnafikiri Zitto na Kitila wapo hapo kusambaratisha Upinzani waklati wao wamejiunga na Upande huo badala ya kuingia CCM moja kwa moja. Milango ilikuwa waiz tena toka vyama vyote wakikaribishwa na hadi kubwa kubwa lakini wamekataa katu na kuunda chama chao wenyewe.

Kwa siasa za Bongo, Zitto angeweza kujiunga CCM na akaendelea kupeta kisiasa. Angeweza kujiunga NCCR na huko hata Uenyekiti angepewa kwa jinsi navyowafahamu jamaa hao kutaka umaarufu. Kitila angeweza kujiunga CCM na kawa na nafasi bora zaidi ndani ya chuo na nje ya chuo kwani hatuwafahamu CCM.. Lakini hawa watu wamepitia mangapi? Zitto keshajitoa mhanga kwa jina la Upinzani, Kitila kisha punguzwa hadi makali yake chuo Kikuu kwa sababu ya msimamo wake kisiasa na kwa kuitetea Chadema lakini leo hii hawa ndio wabaya wa Chadema. Hao wengine wamepitia machungu gani, hao wanaopiga vuvuzela hata siku mojka hawajawahi kupanda jukwaani akapigwa mawe na kuzomewa.

Pamoja na makosa waloyafanya hadi wakafukuzwa. Swala la wao kujiunga na ACT au CCM liwe swala walolitegemea Chadema Na hivyo wagange yaliyopo. Hivi kweli mlitegemea Zitto baada ya kufukuzwa angerudi Kigoma kuvua migebuka! au mlitegemea nini. Na kwa nini haiwezekani mtu yeyote anayejiunga na chama kingine nje ya Cjhadema ni pandikizi la CCM lakini sio hao waliomo Chadema wanaojaribu kwa kila Hila kuhakikisha Chadema inapoteza mwelekeo!

zumbemkuu, Mkuu niliipenda sana Chadema lakini kwa mwendo huu na kutokana na yale nayofahamu juu ya baadhi ya watu walojiunga Chadema kwa kutafuta ajira na wengne kutumiwa kisiasa, nadiriki kusema waswahili walosema KIKULACHO KII NGUONI MWAKO hawakuwa mbali na ukweli. Hawa watu tunaowapokea kwa sababu ya darasa au kauli zao za ULIMI pasipo kujua dhamira zao kujiunga na Chadema ndio hawa watakao kivuruga chama zaidi kwa sababu utawasikia matamshi yao pindi wanapobanwa na hoja zile akili nyingi huondosha maarifa kabisa wakaonekana sura zao halisi.

Kuendeleza haya na kuwafuatilia kina Kitila na Zitto ni dalili za wazi kabisa kwamba inatuuma kila tunapoona wanafanikiwa. Maana binafsi yangu siamini kwamba CCM wameishiwa mbinu hadi wawatumie Zitto na Kitila ambao tayari wameisha athirika kisiasa. Nia mna malengo ya wengi ni kuwaona watu hawa wamekwama kisiasa hata bkama wana malengo mazuri kwa Taifa letu. Na wanapotukosoa tunakataa kuyaona makosa kwa ubishi ule ule ulopelekea kuwafukuza chama japo tuliwahitaji Kitaifa!
 
zumbemkuu Nadhani Mkandara anaendeshwa sana na 'emotion' kiasi anashindwa kusoma mabandiko ya watu vema.

Ukisoma bandiko la mwanzo hadi la tano, tumeeleza mtiririko mzima wa matukio.
Na mara zote nimesema wazi kuwa hakuna tatizo la Kitila kuunda chama. Duru tumetetea hata mikakati yake ya siasa.

Ukimsoma Mchambuzi , pengine tofauti na sisi, yeye hakuchukua hata neno moja nje. Alichokifanya ni kuchukua maeneno ya Kitila ya jana na kulinganisha na ya leo.

Tulichofanya sisi wengine ni kuonyesha jinsi akina Kitila walivyokosa sera. Nashangaa Mkandara anapozungumzia suala la sera, mbona ndiyo hoja kuu.

Tumesema Kitila hahitaji siasa za kugawana wanachama na CDM anachotakiwa ni kuwa na sera zitakazovuta watu wote. Yameandikwa wazi tena tkuisema ''across the board'

Hata hivyo tumeonyesha unafiki wa kina Kitila kwa kuchukua Waraka na yale yanayoendelea sasa hivi.
Mfano Kitila anawezaje kuchagua mwenyekiti wakati chama hakina hata katiba?

Tukasema, hana haja ya kutangaza ujio wa ZZK, anachopaswa kufanya ni kumshauri aondoe kesi. Njia za kutangaza ili aondoke na kundi lake ni za chini sana kwa kiwango chao.

Tumeonyesha jinsi mbinu za kmuondoa ZZK zinavyosukwa, tukasema hatudhani hilo ni jambo la siri, anachotakiwa ni kuondoa kesi mahakamani kwasababu bunge la katiba alilokuwa anategemea lina matatizo.

Mkuu Mkandara kabla hajasoma tayari ameshajenga antigen na reaction hapo hapo.
Kila alichosema tumekisema tofauti ni kuwa sisi tunaonyesha umma mambo yalivyo, yeye ana reactions tu.

Mkuu Mkandara, naomba usome I-V kwanza, kinyume chake itakuwa taabu sana kujadiliana.
Unatakiwa ufahamu kinachojadiliwa kwanza kabla yua mambo mengine.
Hujasoma bandiko unapata wapi ushujaa wa kuchagia?

Kila ulilouliza mbona jibu lake lipo? Rudia kusoma tena kama alivyokushauri zumbemkuu
 
Last edited by a moderator:
zumbemkuu Nadhani Mkandara anaendeshwa sana na 'emotion' kiasi anashindwa kusoma mabandiko ya watu vema.

Ukisoma bandiko la mwanzo hadi la tano, tumeeleza mtiririko mzima wa matukio.
Na mara zote nimesema wazi kuwa hakuna tatizo la Kitila kuunda chama. Duru tumetetea hata mikakati yake ya siasa.

Ukimsoma Mchambuzi , pengine tofauti na sisi, yeye hakuchukua hata neno moja nje. Alichokifanya ni kuchukua maeneno ya Kitila ya jana na kulinganisha na ya leo.

Tulichofanya sisi wengine ni kuonyesha jinsi akina Kitila walivyokosa sera. Nashangaa Mkandara anapozungumzia suala la sera, mbona ndiyo hoja kuu.

Tumesema Kitila hahitaji siasa za kugawana wanachama na CDM anachotakiwa ni kuwa na sera zitakazovuta watu wote. Yameandikwa wazi tena tkuisema ''across the board'

Hata hivyo tumeonyesha unafiki wa kina Kitila kwa kuchukua Waraka na yale yanayoendelea sasa hivi.
Mfano Kitila anawezaje kuchagua mwenyekiti wakati chama hakina hata katiba?

Tukasema, hana haja ya kutangaza ujio wa ZZK, anachopaswa kufanya ni kumshauri aondoe kesi. Njia za kutangaza ili aondoke na kundi lake ni za chini sana kwa kiwango chao.

Tumeonyesha jinsi mbinu za kmuondoa ZZK zinavyosukwa, tukasema hatudhani hilo ni jambo la siri, anachotakiwa ni kuondoa kesi mahakamani kwasababu bunge la katiba alilokuwa anategemea lina matatizo.

Mkuu Mkandara kabla hajasoma tayari ameshajenga antigen na reaction hapo hapo.
Kila alichosema tumekisema tofauti ni kuwa sisi tunaonyesha umma mambo yalivyo, yeye ana reactions tu.

Mkuu Mkandara, naomba usome I-V kwanza, kinyume chake itakuwa taabu sana kujadiliana.
Unatakiwa ufahamu kinachojadiliwa kwanza kabla yua mambo mengine.
Hujasoma bandiko unapata wapi ushujaa wa kuchagia?

Kila ulilouliza mbona jibu lake lipo? Rudia kusoma tena kama alivyokushauri zumbemkuu
Kosa kubwa la hoja zenu ni kwamba mnazungumzia WATU. Hapa topic nzima ni Zitto na Kitila hiyo ACT imetumika tu kuashirioa dhamira yenu maana historia yake inafahamika na kila mwana JF. Kwa kuwasoma hata jkama Zitto na Kitila wangejiunga na chama kingineo bado msimamo wenu juu ya hawa watu ungebakia vile vile. Umewahi kusikia wanaCCM wakizungumzia viongozi wenzao ama kuwalaumu baada ya kuenguliwa!

Laukama mada hii ingelenga kuzungumzia chama hiki ch ACT, itikadi yaosera zao ingetufunza zaidi ya kuweka hadith ndefu juu ya swala ambalo kila mwana JF kaligfuatilia kwa makini na wanajua karibu yote mloandika maana tumekuwa tukifuatilia humuhumu JF.
Na unapiosema Unafiki wa Kitila ina maana tayari umeshamhukumu hivyo hakuna jipya utakalo kuwa muwazi kuhusiana na mtu huyu halafu unanambia nisome toka 1 hadi V wakati nimekusoma na kuelewa jinsi hgani unavyomchukia Kitila Na Zitto. Huu sii ushauri bali ni majigambo sawa na kumshauri mwanamke alokuwa aondoe kesi ya abuse mahakamani ili aokoe ndoa yake kama vile mke ni tegemezi kwa bwana.

Chadema kama chama ndio kiliwahitaji Zitto na Kitila sio wao walokitegemea chama maana chama ni watu sii viongozi na kwa makosa hayo chama kiliamua kuwafukuza kuuonyesha Umma kwamba wanaweza bila Zitto na Kitila sasa hizi habari za kuwafuata wao hadi chooni inahusu? wameunda chama chao waacheni waunde chama, pilipili msokula inawawasha nini? Hivi kweli wewe unaamini Zitto na Kitila wanaweza kuuangamiza Upinzani kwa hadith uloitoa?

Jamani kuweni wakweli maana binafsi yangu sikosi usingizinkabisa hata kama kesho Mbowe au Slaa wakifungua chama chao wenyewe maana nachopigania mimi ni maisha biora kwa WATANZANIA na mtu yeyote atakaye simama kutetea wanyonge nitamsikiliza na kumuunga mkono. Walisema hivyo hivyo kuwa Chadema imeunda ili kuiangamizia CUF lakini ukweli ni kwamba CUF walivurunda wenyewe na sii kosa la Chadema, Lwakatale wala Rashid, chama siku zote kinahitaji watu na ushindani ndani ya chama ni sehemu ya demokrasia tuloichagua. Huu uchu wa madaraka ndio silaha kubwa ya CCM wakijua kwamba sisi wote njaa tu ndio inatusumbua. hakna mwanasiasa wa ukweli!

Hizi habari za ACT kusika mpini wa CCM ni kujenga chuki kwa wananchi wasijiunge ama kuwafuata hawa jamaa. Na haiwezekani kufikiriaa hivyo pasipo kuwa na WOGA (FEAR) wa maamuzi yalofanywa na viongozi maana hawa watu wamefukuzwa na sii kwa hiari yao. Kwa nini hii isiwe njama dhidi yao ila wao ndio wawe na njama dhidi ya Upinzani walikoanzisha wao na sii kujiunga! Mimi nitamuogopa sana mtu alotoka nje na kujiunga na Chadema kwa sababu siojui kilichomzukuma hadi kuingia chama kuliko yule aloanzisha chama chake mwenyewe.

Toka kufukuzwa kwao Chadema tumeshindwa chaguzi vibaya vibaya, kifupi tunagalagazwa. Kila tunapogusa magoli, Lakini kama ile Chadema ya Mbowe, Zitto na Slaa ingekuwepo leo hii, ile Chadema ya mwaka 2004 - 2010 ambayo ilikuwa ikionyesha umakini ktk kujenga hoja dhidi ya chama tawala, ikifuata zaidi sauti za wananchi na sii sauti za wanachama wachumia tumbo na wasanii wa CCM wanaobeba mabango huku roho zao bado zipo CCM, basi nina hakika Ridhwan asingeshinda uchaguzi wa Chalinze! Na nina mashaka sana kama uchaguzi wa mwaka 2015 tutaweza kurudisha majimbo tuloshinda mwaka 2010 kwa sababu leo hii Chadema inazungumzia WATU sii sera wala Kukemea Ufisadi, ila kutafunana wenyewe baada ya kushindwa mbinu za ushindani na CCM.

Umeniomba nirudie kusoma, sasa nami nakuomba wewe, ondoa majina ya Zitto na Kitila kisha tuone kama utabakia na hoja zaidi ya kichwa cha mada!
 
Mkandara
Hapa hakuna cha Uchadema, UCCM

Tunaongelea kile kilichosemwa jana, na kinachosemwa leo.
Ndio, ni unafiki kulaani ukanda wa CDM, kulindana kwa CCM, huku mtu akichagua Uswahiba.

Usiondoke kwenye mada, suala ni moja, je ni sahihi Kitila kuteua mwenyekiti wa chama ambacho hakina katiba
Je, ni sahihi mwanachama wa CDM kuwa mwenyekiti wa ACT at the same time
Je, ile demokrasia ya watu kuchagua na kushindana ndani ya chama iliyomo katika waraka, ndiyo inayotekelezwa sasa.

Je, uanachama ni sera za chama au ni kitu gani? Iweje mwenyekiti ateuliwe ikiwa hajui hata sera za chama.

Halafu soma makala za Kitila na linganisha na anachokifanya.

Usiondoke katika mada, uzi hauzungumzii ugomvi wa CDM na wanachama wao au CCM
Uzi unazungumzia ya Kitila kama alivyonukuliwa na kumhusisha ZZK hivyo ni halali kuwajadili kwani si mara ya kwanza kuandikwa. Na Kitila hakujificha alisema katika vyombo vya habari.

Tafadhali usitoke katika mada.
 
Sasa Mkuu Nguruvi3, kama unatambua kama kuna uongozi wa ACT nje ya kauli za Kitila, kwanini utoe hukumu ya jumla kwa chama kuwa kinatumika na CCM kwa kauli ya mwanachama mmoja tu (Kitila)? Ulishasikia uongozi wa ACT ukitamka hayo au kuunga mkono? Unaujua msimamo wa uongozi wa chama hicho juu ya kauli za Kitila?
Kutumia kauli za Kitila ku-generalize yote kuhusu ACT ni kutokitendea haki chama hicho!
Kitila alitangaza kuwa yeye ni mwanachama wa ACT, akaropoka hulka na hisia zake juu ya Zitto, lakini ACT si Kitila wala Zitto, kilitambulishwa kwa wananchi nje ya hao watu! Aje wao leo wabebe rangi ya hicho chama kufikia hatua ya kuwatumia wao kutoa hukumu kwa chama? Aje kama kesho ACT watakuja na kauli kinzani na ya Kitila?
Nadhani huu si wakati muafaka wa kuzungumzia kila kitu kuhusu ACT, tuvute subira kidogo. Upuuzi wao au Werevu wao utadhihirika wazi.
Mungu wetu anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3 naona umeamua kuanza kujenga ukuta kuzuia wapita njia wakati hufahamu hata kama kweli kuna wapita njia.

Kwanza, Naomba tu unieleze, hivi kama hawa binadamu unaowajadili wangehamia let say, TLP au CUF ungejenga hoja kama wanaua upinzani (CHADEMA). Kama sivyo, kwa nini wanapohamia ACT unaanza kujenga hoja kama wanataka kuua nguvu za CHADEMA badala ya CCM.

Kwa nini CHADEMA wakimbizane na kurumbana na ACT?. Na kama CHADEMA watarumbana na kukimbizana na ACT, kwa nini walaumiwe ACT badala ya CHADEMA.

Pili, Andiko lako limejichanganya sana kihoja. Umeanza kwa kusema hivi,
Kitila katika waraka alidai kutokuwepo kwa demokrasia ndani ya Chadema ikiwa ni pamoja na ukanda.Alinanga viongozi wa Chadema kama wenye akili ndogo.
Katika mahojiano ya wiki iliyopita Kitila kasema atamshawishi Zitto ajiunge na ACT na agombee uenyekiti.

Kitendo hicho ni cha kula ‘matapishi yake’.
Kitila alikuwa na haki ya kumwambia Zitto ajiunge na ACT kama mwanachama.


Kitendo cha kumtaka awe mwenyekiti ni kwenda kinyume cha demokrasia.

Mwenyekiti anaomba na kuchaguliwa, alichokifanya Kitila ni kutumia influence yake kuwashawishi wanachama kuwa Zitto anafaa kuwa mwenyekiti hata kabla hajasoma wala kujua sera za chama
Hiki kipande cha hoja yako umesema Kitila ana haki ya kumshawishi Zitto kujiunga na ACT, kitu ambacho hakina tatizo lolote kwa mtazamo wako kutokana na angalizo lako. Kitu ambacho umejichanga ni pale unaanza kujenga hoja kama vile yule atakayeshawishiwa hataomba kuchaguliwa halafu cha kushangaza unajenga hoja za kusema kuna watu ACT kwa sasa wanafanya kazi mchana na usiku kwa maana kuwa wale wa kuja hawafai kupewa uongozi kwa sababu hawajatoa jasho katika uwepo wa chama. Hoja yako ni kama ile inayotumia sana na baadhi ya vyama vya upinzani kutaka kuzuia wananchama wengine kugombea uongozi. Kwenye hivyo vyama kuna "Wenye chama na wakuja".

Hoja yako inaonyesha kama vile Mh. Zitto akishawishiwa na kukubali kuwa Mwanachama basi atampindua mwenyekiti wa sasa kama vile hakutakuwa na uchaguzi.

Dr. Kitila kumshawishi Zitto kugombea Uenyekiti siyo jambo jipya kwenye fikra za Dr. Kitila. Hili ni jambo ambalo lilikuwa mzizi wa waraka uliomfanya wa Dr. Kitila kufukuzwa CHADEMA. Sasa sielewi hayo matapishi yake unayatoa wapi.

Kwenye hoja yako hii hapa chini, unajichanganya pia katika maelezo yako. Kama hawa binadamu ndiyo waanzilishi wa ACT, kitu gani kinakufanya udhanie kuwa ACT haina Katiba au Kanuni ambazo hawazifahamu na hazieleweki.

ACT kinaundwa na kundi la wanachama wa Chadema ‘waliofukuzwa’ kutokana na kile kilichojulikana kama Waraka wa siri. Fuatilia uzi huu. Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

Mkuu, hadi sasa ACT haina katiba wala kanuni za kueleweka.
Hoja zako zinanikumbuka kipindi kile ambacho Augustino Lyatonga Mrema aliondoka CCM na kujiunga na NCCR-Mageuzi ambapo wanaCCM kwa kutumia vyombo vya dola wakaanza kumfuata fuata mpaka Mwl. Nyerere akawapiga stop na kuwaambia kumfuata fuata ni kumuongezea washabiki. Wamwache tu afanye anavyopenda na CCM wajikite kwenye misingi ya chama ambayo ni kuuza sera.
 
Mkuu Nguruvi3 naona umeamua kuanza kujenga ukuta kuzuia wapita njia wakati hufahamu hata kama kweli kuna wapita njia.

Kwanza, Naomba tu unieleze, hivi kama hawa binadamu unaowajadili wangehamia let say, TLP au CUF ungejenga hoja kama wanaua upinzani (CHADEMA). Kama sivyo, kwa nini wanapohamia ACT unaanza kujenga hoja kama wanataka kuua nguvu za CHADEMA badala ya CCM.

Kwa nini CHADEMA wakimbizane na kurumbana na ACT?. Na kama CHADEMA watarumbana na kukimbizana na ACT, kwa nini walaumiwe ACT badala ya CHADEMA.

Pili, Andiko lako limejichanganya sana kihoja. Umeanza kwa kusema hivi,

Hiki kipande cha hoja yako umesema Kitila ana haki ya kumshawishi Zitto kujiunga na ACT, kitu ambacho hakina tatizo lolote kwa mtazamo wako kutokana na angalizo lako. Kitu ambacho umejichanga ni pale unaanza kujenga hoja kama vile yule atakayeshawishiwa hataomba kuchaguliwa halafu cha kushangaza unajenga hoja za kusema kuna watu ACT kwa sasa wanafanya kazi mchana na usiku kwa maana kuwa wale wa kuja hawafai kupewa uongozi kwa sababu hawajatoa jasho katika uwepo wa chama. Hoja yako ni kama ile inayotumia sana na baadhi ya vyama vya upinzani kutaka kuzuia wananchama wengine kugombea uongozi. Kwenye hivyo vyama kuna "Wenye chama na wakuja".

Hoja yako inaonyesha kama vile Mh. Zitto akishawishiwa na kukubali kuwa Mwanachama basi atampindua mwenyekiti wa sasa kama vile hakutakuwa na uchaguzi.

Dr. Kitila kumshawishi Zitto kugombea Uenyekiti siyo jambo jipya kwenye fikra za Dr. Kitila. Hili ni jambo ambalo lilikuwa mzizi wa waraka uliomfanya wa Dr. Kitila kufukuzwa CHADEMA. Sasa sielewi hayo matapishi yake unayatoa wapi.

Kwenye hoja yako hii hapa chini, unajichanganya pia katika maelezo yako. Kama hawa binadamu ndiyo waanzilishi wa ACT, kitu gani kinakufanya udhanie kuwa ACT haina Katiba au Kanuni ambazo hawazifahamu na hazieleweki.


Hoja zako zinanikumbuka kipindi kile ambacho Augustino Lyatonga Mrema aliondoka CCM na kujiunga na NCCR-Mageuzi ambapo wanaCCM kwa kutumia vyombo vya dola wakaanza kumfuata fuata mpaka Mwl. Nyerere akawapiga stop na kuwaambia kumfuata fuata ni kumuongezea washabiki. Wamwache tu afanye anavyopenda na CCM wajikite kwenye misingi ya chama ambayo ni kuuza sera.
Si tuu anajichanganya ila nashangaa ya Firaun wa hawa watu kusambaza sumu ktk mto kwa sababu ya mtu mmoja! maana kama hawa kina Kitila na ZZK ndio waanzilishi wa chama hiki ACT (waliofukuzwa Chadema) inakuwaje ZZK kugombea Uenyekiti ama Kitila kumuomba Zitto agombee uenyekiti liwe tatizo, ati kuna wenyewe walokitokea jasho chama? hao wengine ni kina nani ikiwa una hakika waasisi wa chama hiki ni wale waliofukuzwa kutoka Chadema!. Wangapi wale walofukuzwa Chadema!

Waasisi wa TANU walimuomba mwalimu Nyerere agombee uenyekiti na hakika walimpa nafasi hiyo ktk silver plate maana hata mgombea mwenza Marehemu AbdulWahid aliowamba wajumbe wamchague Nyerere kabla ya kura za pili.. Huyo Mbowe naye aliombwa kama hajui historia ya Chama chake, sasa leo imekuaje Kitila awe mtu wa kwanza kufana kosa la kupendekeza mtu kukiongoza chama kama sii kwa kutumia sheria zao. Tunaambiwa ZZK kafukuzwa CDM na hatakiwi mara bado inaonyesha kuwa ni mwanachama, Kitila atamuomba ZZK ajiunge na ACT mara inaonekana tayari ni mwachama maana ndiye mwanzilishi!.

Sisi Watanganyika wajuzi sana wa kujenga Fitna na hii itatumaliza kwa sababu hatutaki kuona mafanikio ya mtu mwingine hata siku moja na akianguka wataweka mabango mitaani kuitangaza. Hata media zetu wanajua hilo hivyo huandika majanga zaidi ukurasa wa kwanza maana yanauzika kuliko mafanikio..
 
Sasa Mkuu
Nguruvi3, kama unatambua kama kuna uongozi wa ACT nje ya kauli za Kitila, kwanini utoe hukumu ya jumla kwa chama kuwa kinatumika na CCM kwa kauli ya mwanachama mmoja tu (Kitila)? Ulishasikia uongozi wa ACT ukitamka hayo au kuunga mkono? Unaujua msimamo wa uongozi wa chama hicho juu ya kauli za Kitila?

Kutumia kauli za Kitila ku-generalize yote kuhusu ACT ni kutokitendea haki chama hicho!

Kitila alitangaza kuwa yeye ni mwanachama wa ACT, akaropoka hulka na hisia zake juu ya Zitto, lakini ACT si Kitila wala Zitto, kilitambulishwa kwa wananchi nje ya hao watu! Aje wao leo wabebe rangi ya hicho chama kufikia hatua ya kuwatumia wao kutoa hukumu kwa chama? Aje kama kesho ACT watakuja na kauli kinzani na ya Kitila?
Nadhani huu si wakati muafaka wa kuzungumzia kila kitu kuhusu ACT, tuvute subira kidogo. Upuuzi wao au Werevu wao utadhihirika wazi.
Mungu wetu anaita sasa!
Mkuu JFS, kwanza, niseme tutakuwa tunafumba macho mchana na kudhani tumelalala usiku kama hatukubali kuwa kile chama mbadala alichotabiri Kitila ni ACT na kwamba jitihada zake na kauli za kuyumba ni political stunt

Bandiko la mwanzo nimetoa benefit of doubt kwa kusema Kitila kama Raia ana haki ya kujiunga na shughuli zozote za kisiasa. Na ACT kama chama kina haki ya kutumia mikakati ya kisiasa.

Nilisema pia hadi sasa hakuna katiba ya ACT kwa mujibu wa uongozi wa sasa.
Sikuwahi kusema Kitila ni kiongozi au Zitto, ila kama nilivyosema awali hawa ni ACT
Hakuna tatizo la wao kufanya shughuli za kisiasa na wala hilo si kosa.

Hoja kubwa iliyoko mbele ambayo wengi wanaikimbia ni ukweli kuwa Kitila amesema atamshawishi Zitto ajiunge na ACT na awe mwenyekiti wa chama.
Hapa pia kuna political stunt, Kitila anasema wanashea maono na mitazamo sawa ya kisiasa.

Huko nyuma walishea siri nzito ya Waraka. Kitila kasimama mbele ya microphone na kusema ZZK hahusiki, leo tunajua wanashea mitazamo sawa, hivyo hakuna shaka mtazamo wa ACT wanashea pia.

Moja, ni uongo kusema ZZK hakushiriki waraka kwasababu down the road Kitila amethibitisha pasi na shaka.

Mbili, ZZK ni mwanachama wa CDM hadi sasa na kesi ipo mahakamani, iweje Kitila amteue kuwa kiongozi wa ACT

Tatu, hakuna taabu kama anamshawishi, kitendo cha kutangaza ni political stun na hakina tabu, shida ni pale Kitila anayefanya kazi nyuma ya pazia la ACT anapojitokeza na kuwachagulia wanachama Mwenyekiti.

Huko alikotoka, Kitila alilalamika kuhusu Udikteta. Hivi kitendo cha yeye kuwachagulia mwenyekiti akifahamu kuwa yeye ni brain behind ACT si cha udikteta?

Huyo ZZK hajajiunga na ACT na wala hajasoma na kuzijua sera za ACT, wapi Kitila anapata nguvu za kumsimika uenyekiti? Hapo hajafakamia matapishi yake kuhusu udikteta.

Kitila anataka kumsimika ZZK uenyekiti kwa influence yake. Huko alikotoka alipiga kelele kuhusu ukanda, vipi hili la kumchagua swahiba, je huo si uswahiba kama ambavyo CCM ina ufisadi n.k. Hapa hajala yale matapishi kweli!!

Nne, Kitila na ZZK katika waraka walilamika sana kuhusu kukosekana kwa demokrasia. Hivi kitendo cha Kitila kutafuta mwenyekiti nje ya wanachama, na bila kupitia sanduku la kura ndiyo demokrasia aliyokuwa anahubiri?

Tano, Kichwa cha bandiko kinasema 'Chama cha ACT mpini wa kumaliza upinzani'
Bandiko I-V ynaeleza mahusiano ya ACT /Kitila na ZZK
Kuna hoja A-F zinazoeleza scenario zote na political stunt za kina Kitila

Kwanini ACT itakuwa mpini na shoka ni CCM?
Jitihada zote za Kitila ni kuhakikisha anapata wafuasi kutoka CDM hasa waumini wa ZZK
Hilo halina tatizo kama mkakati.

Mbinu hiyo iwe nzuri au mbaya kwa mtazamo wa kila mmoja, ina hoja kubwa kadhaa
1. NCCR ilisambaratika na kuzaa TLP. Hadi leo NCCR ni maheruhi
2. CUF ikagawanya wanachama wa Hamad Rashid na Seif, hadi leo ni majeruhi

Huko kote waliacha makovu ya udhaifu wa upinzani, wakimwacha nyangumi CCM akiogelea kwa raha zake. Kitila haonekani kujifunza kutokana na mkosa hayo.
Anachokifanya ni kuchgiza ujio wa mwenyekiti ZZK na wanachama wake.

Duru tulidhani kuwa njia muafaka ilikuwa kutangaza sera za ACT ili ku-win uungwaji mkono pengine kutoka CCM zaidi kuliko CDM. Sivyo, jitihada ni zile zile za Mrema kuondoka na wanachama.

Duru za siasa tunasema, hapana! hilo si sahihi kwasababu chama kinaundwa na kuungwa mkono kwa sera na si mtu au watu. Chama kinaendeshwa kwa misingi ya demokrasia, si uteuzi wa viongozi kama anavyofanya Kitila.

Endapo Kitila aliandika waraka ili kuendesha CDM kisayansi na kwa demokrasia, waraka huo ameutupa na sasa anakula matapishi yale yale aliyoyatoa CDM kupitia waraka.

Na mwisho tuseme kuwa Kitila alioanza political stunt za chama mbadala hilo halikuwa hoja. Alipfikia mahali anadanganya umma na kutufanya sote mazuzu tunasimama na kusema, hapana!

Kitila alitabiri ujio wa chama mbadala, akajiunga na mbadala. Kinachotakiwa amwambie ZZK aondoe kesi mahakamani na atakuwa si mwanachama wa CDM.
Achukue uanachama wa ACT, asome sera, akitangaze chama na kisha agombee uongozi.
Hayo hayahitaji kuufanya umma wote mazuzu, yanawezekana tu bila hila na ni haki yao.

Tusichokubali ni leo kusema hivi na kesho kutenda vile.
Tusichokubaliana na endelezo la siasa za ulaghai, miaka 50 ya CCM na 20 ya upinzani tumeiona na tumechoka. Tusipowaambia watatutfanya mazuzu kila uchao.
 
Si tuu anajichanganya ila nashangaa ya Firaun wa hawa watu kusambaza sumu ktk mto kwa sababu ya mtu mmoja! maana kama hawa kina Kitila na ZZK ndio waanzilishi wa chama hiki ACT (waliofukuzwa Chadema) inakuwaje ZZK kugombea Uenyekiti ama Kitila kumuomba Zitto agombee uenyekiti liwe tatizo, ati kuna wenyewe walokitokea jasho chama? hao wengine ni kina nani ikiwa una hakika waasisi wa chama hiki ni wale waliofukuzwa kutoka Chadema!. Wangapi wale walofukuzwa Chadema!

Waasisi wa TANU walimuomba mwalimu Nyerere agombee uenyekiti na hakika walimpa nafasi hiyo ktk silver plate maana hata mgombea mwenza Marehemu AbdulWahid aliowamba wajumbe wamchague Nyerere kabla ya kura za pili.. Huyo Mbowe naye aliombwa kama hajui historia ya Chama chake, sasa leo imekuaje Kitila awe mtu wa kwanza kufana kosa la kupendekeza mtu kukiongoza chama kama sii kwa kutumia sheria zao. Tunaambiwa ZZK kafukuzwa CDM na hatakiwi mara bado inaonyesha kuwa ni mwanachama, Kitila atamuomba ZZK ajiunge na ACT mara inaonekana tayari ni mwachama maana ndiye mwanzilishi!.

Sisi Watanganyika wajuzi sana wa kujenga Fitna na hii itatumaliza kwa sababu hatutaki kuona mafanikio ya mtu mwingine hata siku moja na akianguka wataweka mabango mitaani kuitangaza. Hata media zetu wanajua hilo hivyo huandika majanga zaidi ukurasa wa kwanza maana yanauzika kuliko mafanikio..
Hapana, si kweli. Tunakataa siasa za kilaghai. Huwezi kulaani jambo moja ukarudi kulifanya kwa upoande mwingine tukakaupa pass.

Katika bandiko la I nimeeleza scenario A-F, hakuna anayekataa kuwa si kweli.
Siasa za kubeba watu kwa mkumbo sasa tumechoka. Siasa za watu na si sera tumechoka.

Kitila anamteua vipi mtu asiyejua sera za chama? Hili ni swali hamjibu hata kidogo
Kitila anamteua vipi mtu asiye mwanachama kuwa mwenyekiti?

Kitila aliyekataa udikteta si huyu anauendeleza kwa namna nyingine.
Alichopaswa kufanya ni kutangaza sera za chama chake ili watu wasizosome na wavutike.
Kutangaza mtu na si sera, sasa basi tunataka siasa za kisayansi.

Hakuna fitna ya aina yoyote kwasababu sina sababu za fitna. Nimeleeza na ninasomeka kwa misimamo isiyoangalia makunyanzi.

Tatizo la nchi hii halipo kwa wapinzani, lipo kwa sera za nchi chini ya nyangumi.
Siasa za kubeba watu na kuamini wao ndio wenyewe na wala si sera za chama hizo zifike mwisho.

Kitendo cha Kitila kumteua Zitto kama mwenyekiti akiwa hajui katiba, katiba haipo na wala hajasoma sera za chama hicho ni udanganyifu na usimikaji wa viongozi kwa hila. Ilitosha sana Kitila kusema anahama na Zitto na si kuanza kutulaghai tena akimeza matapishi yake.

Tulitegemea wasahihishe makosa waliyoyaona katika waraka, hainoekani hivyo.

Wananchi wa Tanganyika wanahitaji sera si mtu au watu. Kitila asimamie sera na demokrasia na si kutangaza wasifu an wajihi wa CEO katika chama cha siasa. Kitendo cha kutotangaza sera na kukimbilia kumteua mwenyekiti Zitto ni upungufu mkubwa sana wa siasa za kisayansi. Kitila atambue vyama haviendeshwi na taswira ,wajihi bali sera, uadilifu na uongozi.

Uongozi ni kusimamia kile unachokiamini ni sahihi,ni kuoneysha njia na mifano. Ni kusikiliza na kusema, kuchambua na kutambua. Mwendo wa Kitila ni ule wa siasa za 'huyo huyo' au amepita bila kupingwa au mtu na chunga.
Hapana zama hizo zimekwisha.
 
Mkuu JFS, kwanza, niseme tutakuwa tunafumba macho mchana na kudhani tumelalala usiku kama hatukubali kuwa kile chama mbadala alichotabiri Kitila ni ACT na kwamba jitihada zake na kauli za kuyumba ni political stunt

Bandiko la mwanzo nimetoa benefit of doubt kwa kusema Kitila kama Raia ana haki ya kujiunga na shughuli zozote za kisiasa. Na ACT kama chama kina haki ya kutumia mikakati ya kisiasa.

Nilisema pia hadi sasa hakuna katiba ya ACT kwa mujibu wa uongozi wa sasa.
Sikuwahi kusema Kitila ni kiongozi au Zitto, ila kama nilivyosema awali hawa ni ACT
Hakuna tatizo la wao kufanya shughuli za kisiasa na wala hilo si kosa.

Hoja kubwa iliyoko mbele ambayo wengi wanaikimbia ni ukweli kuwa Kitila amesema atamshawishi Zitto ajiunge na ACT na awe mwenyekiti wa chama.
Hapa pia kuna political stunt, Kitila anasema wanashea maono na mitazamo sawa ya kisiasa.

Huko nyuma walishea siri nzito ya Waraka. Kitila kasimama mbele ya microphone na kusema ZZK hahusiki, leo tunajua wanashea mitazamo sawa, hivyo hakuna shaka mtazamo wa ACT wanashea pia.

Moja, ni uongo kusema ZZK hakushiriki waraka kwasababu down the road Kitila amethibitisha pasi na shaka.

Mbili, ZZK ni mwanachama wa CDM hadi sasa na kesi ipo mahakamani, iweje Kitila amteue kuwa kiongozi wa ACT

Tatu, hakuna taabu kama anamshawishi, kitendo cha kutangaza ni political stun na hakina tabu, shida ni pale Kitila anayefanya kazi nyuma ya pazia la ACT anapojitokeza na kuwachagulia wanachama Mwenyekiti.

Huko alikotoka, Kitila alilalamika kuhusu Udikteta. Hivi kitendo cha yeye kuwachagulia mwenyekiti akifahamu kuwa yeye ni brain behind ACT si cha udikteta?

Huyo ZZK hajajiunga na ACT na wala hajasoma na kuzijua sera za ACT, wapi Kitila anapata nguvu za kumsimika uenyekiti? Hapo hajafakamia matapishi yake kuhusu udikteta.

Kitila anataka kumsimika ZZK uenyekiti kwa influence yake. Huko alikotoka alipiga kelele kuhusu ukanda, vipi hili la kumchagua swahiba, je huo si uswahiba kama ambavyo CCM ina ufisadi n.k. Hapa hajala yale matapishi kweli!!

Nne, Kitila na ZZK katika waraka walilamika sana kuhusu kukosekana kwa demokrasia. Hivi kitendo cha Kitila kutafuta mwenyekiti nje ya wanachama, na bila kupitia sanduku la kura ndiyo demokrasia aliyokuwa anahubiri?

Tano, Kichwa cha bandiko kinasema 'Chama cha ACT mpini wa kumaliza upinzani'
Bandiko I-V ynaeleza mahusiano ya ACT /Kitila na ZZK
Kuna hoja A-F zinazoeleza scenario zote na political stunt za kina Kitila

Kwanini ACT itakuwa mpini na shoka ni CCM?
Jitihada zote za Kitila ni kuhakikisha anapata wafuasi kutoka CDM hasa waumini wa ZZK
Hilo halina tatizo kama mkakati.

Mbinu hiyo iwe nzuri au mbaya kwa mtazamo wa kila mmoja, ina hoja kubwa kadhaa
1. NCCR ilisambaratika na kuzaa TLP. Hadi leo NCCR ni maheruhi
2. CUF ikagawanya wanachama wa Hamad Rashid na Seif, hadi leo ni majeruhi

Huko kote waliacha makovu ya udhaifu wa upinzani, wakimwacha nyangumi CCM akiogelea kwa raha zake. Kitila haonekani kujifunza kutokana na mkosa hayo.
Anachokifanya ni kuchgiza ujio wa mwenyekiti ZZK na wanachama wake.

Duru tulidhani kuwa njia muafaka ilikuwa kutangaza sera za ACT ili ku-win uungwaji mkono pengine kutoka CCM zaidi kuliko CDM. Sivyo, jitihada ni zile zile za Mrema kuondoka na wanachama.

Duru za siasa tunasema, hapana! hilo si sahihi kwasababu chama kinaundwa na kuungwa mkono kwa sera na si mtu au watu. Chama kinaendeshwa kwa misingi ya demokrasia, si uteuzi wa viongozi kama anavyofanya Kitila.

Endapo Kitila aliandika waraka ili kuendesha CDM kisayansi na kwa demokrasia, waraka huo ameutupa na sasa anakula matapishi yale yale aliyoyatoa CDM kupitia waraka.

Na mwisho tuseme kuwa Kitila alioanza political stunt za chama mbadala hilo halikuwa hoja. Alipfikia mahali anadanganya umma na kutufanya sote mazuzu tunasimama na kusema, hapana!

Kitila alitabiri ujio wa chama mbadala, akajiunga na mbadala. Kinachotakiwa amwambie ZZK aondoe kesi mahakamani na atakuwa si mwanachama wa CDM.
Achukue uanachama wa ACT, asome sera, akitangaze chama na kisha agombee uongozi.
Hayo hayahitaji kuufanya umma wote mazuzu, yanawezekana tu bila hila na ni haki yao.

Tusichokubali ni leo kusema hivi na kesho kutenda vile.
Tusichokubaliana na endelezo la siasa za ulaghai, miaka 50 ya CCM na 20 ya upinzani tumeiona na tumechoka. Tusipowaambia watatutfanya mazuzu kila uchao.
Mkuu kwa kila jitihada za kuonyesha kwamba hawa watu wawili Kitila na ZZK ni wasaliti, ndivyo unavyozidi kujenga maswali mengi zaidi kwenu kiasi kwamba hawa jamaa watapata wafuasi zaidi.

Binafsi yangu nachioweza kusema hawakutendewa haki ila kwa sheria za Uchadema. Hivyo kwa kila hoja mnayoandika dhidi yao mnawaongezea Umaarufu zaidi na hakika watapata wafuasi wengi zaidi kwa sababu wanachoweza kufanya wao ni kuonyesha mapungufu ya uongozi ktk nchi hii, Ukiukaji wa miiko na maadili (Responsibility /Accountability) na zaidi kabisa kuwajali wananchi WAKULIMA na WAFANYAKAZI.

Wakiweza hili haitajalisha kuna CCM, Chadema wala CUF maana wananchi wamechoka na siasa za kutumikia WATU. Ni Chadema inayotakiwa kubadilika na kurudi ktk asili yake, sababu zake, malengo yake na sii kubadilika na kuwa chama cha wachumia tumbo wanaojiita wanaharakati ambao wanatafuta Umaarufu kupitia majukwaani kwa habari za mipasho.
 
Mkuu kwa kila jitihada za kuonyesha kwamba hawa watu wawili Kitila na ZZK ni wasaliti, ndivyo unavyozidi kujenga maswali mengi zaidi kwenu kiasi kwamba hawa jamaa watapata wafuasi zaidi.

Binafsi yangu nachioweza kusema hawakutendewa haki ila kwa sheria za Uchadema. Hivyo kwa kila hoja mnayoandika dhidi yao mnawaongezea Umaarufu zaidi na hakika watapata wafuasi wengi zaidi kwa sababu wanachoweza kufanya wao ni kuonyesha mapungufu ya uongozi ktk nchi hii, Ukiukaji wa miiko na maadili (Responsibility /Accountability) na zaidi kabisa kuwajali wananchi WAKULIMA na WAFANYAKAZI.

Wakiweza hili haitajalisha kuna CCM, Chadema wala CUF maana wananchi wamechoka na siasa za kutumikia WATU. Ni Chadema inayotakiwa kubadilika na kurudi ktk asili yake, sababu zake, malengo yake na sii kubadilika na kuwa chama cha wachumia tumbo wanaojiita wanaharakati ambao wanatafuta Umaarufu kupitia majukwaani kwa habari za mipasho.
Mimi sioni tatizo na umaarufu wao. Hadi sasa ni maarufu na nawatakia heri ya umaarufu siku za usoni.
Baada ya hayo nataka nikuambie kuwa umarufu wao haufungi macho yetu.

Tutaonyesha umaarufu wao bila kusita na mapungufu yao bila kuona haya.

Sisi wengine tunaongozwa na mitazamo huru, kwa hili la siasa tunaangalia sera, maadili, na uadilifu.
Hatuangalii nani anabebwa katika machela nanai anatembea. Mrema alikuwa maarufu tu wala hakuna tatizio.

Nisichokubali katika akili yangu ni kudanganywa.
Leo ZZK anasema anasimamia demokrasia na haki kwenda mahalamani. Tunajua bunge la katiba ndilo lilimweka.
Njia ya kuchomoka ni Kitila kudai anamshawishi tena akimtangaza kuwa mwenyekiti hata pale zzk hajui sera za chama.

Hii habari ya siasa za 1947 tumechoka , tunataka siasa za kisayansi. Halafu uangalie watu wanaofanya hivyo wana nafasi gani katika jamii.Wapi uliona mwenyekiti wa chama cha siasa anateuliwa kama CEO.

Kitila amekosea, hilo la kwanza
Amekula matapishi yake hilo la pili
Anafanya siasa zisizolingana naye
 
Mkuu Nguruvi3 na wengineo katika mjadala huu nadhani wakati mwingine tujifunze kuwa kilichopo kwa mwanachama mpya Dr.Kitila Mkumbo ni kuwa mapenzi yake kwa ZZK,

a)Yanamfanya awe kiziwi,kiasi cha kuamini from his heart-desire hawezi kukosea maana ampendaye ni malaika.Hivyo kwake popote atakapo mtaja Zitto ni kama kamtaja Mungu hivyo,hawezi kukosea maana sote twajua linapokuja suala la imani watu huamini hakuna kukosea.

b)Inawezekana kala yamini kuhusu Zitto,na hivyo hakuna mtu anayeweza kumuamini zaidi ya Zitto na hapo anaweza kuimba demokrasia kwa hisia na si kwa utashi. Ni kweli ndugu huyu ni msomi mzuri lakini kwenye siasa za Kisasa na kizalendo amepwaya sana tena kabla hajafikia malengo.

Jambo jingine ni kuwa angependa ahubiri siasa safi na demokrasia,lakini ni siasa na demokrasia asiyoijua,wachambuzi wanamwona kama mwenye kutapatapa na kupoteza mwelekeo.Nadhani anaipenda siasa lakini siasa haimpendi.

Mwisho,ni kama wenzangu msemavyo anakula matapishi yake mwenyewe na hivyo kuongeza mashaka ya chama hiki cha ACT kuundwa kwake,madhumuni yake na namna kitakavyoendesha siasa zake. Nikionacho mimi ni kuwa wanasiasa hawa vijana wanakwenda kufa kisiasa katika wakati ambao hawajajiandaa,you will see it soon!
 
Last edited by a moderator:
Ningeomba kupata ufafanuzi zaidi juu ya chama hiki..

Tumeambiwa kuwa chama hiki ni chama cha uwazi (Allince for change and Transparency.. lakini cha ajabu kuanzia kuanzishwa kwake, waasisi wake, jinsi kilivyopata usajili ni usiri usiri tu hakuna uwazi.. Mfanoi Kitila anasema atamshawishi Zitto awe Mwenyekiti lakini hapo hapo Zitto anasema yeye ni Chadema (mpaka kesi iliyoko mahakani iamuliwe) sasa hapo mie ndio sielewi unawezaje kumpa unyekiti mwanachama tena kiongozi wa chama kingine?? ingekuwa jambo bora kama angesema kutoka na sera zetu tutajaribu kuwashawishi watanzania na watu mbali mbali kama Zitto wajiunge na ACT walau hapo ningemuelewa...

Pia tunasikia kuwa Zitto na Kitila ni Waasisi chama hiki, kwangu mimi ni jambo jema na la kujivunia kwani sio kila mtu anaweza kuanzisha chama maana kuanzisha chama kunahitaji muda, pesa, wataalamu nk. lakini cha ajabu wao wanajificha ficha, hivi kuna ugumu gani wa kusema ndio mimi ni muwasisi wa chama hiki? sasa kwa hili ambalo ni jambo dogo tu watu wanaficha ficha je uwazi tunaoubiriwa huko wapi?

Mwanzoni waliposema uwazi nilitegemea haya mambo ya siri siri sasa mwisho, tutarajie kujua wanzilishi wa chama hiki ni akina nani, sera zao ni zipi, wafadhali wao, na nk.. lakini cha kusikitisha zaidi hawa watu wanaotuhubiria uwazi walishindwa hata kutuonesha mikutano ya kutafuata wadhamini katika mikoa mbali mbali, walicho fanya ni kuleta picha ya mkoa wa Mwanza na yenyewe kuna walio sema huo ulikuwa ni mkutano wa mikopo na nk. ok inawezekani kuwa labda haikuwa ni muhimu kwao lakini unapohubiri uwazi ni lazima huwe muwazi kweli kama utashidwa kuwa muwazi kwa vitu vidogo vidogo je yakapokuwa mambo makubwa itakuwaje?

Wakati ufikie wanasiasa waache uongo, watekeleze wanachohubiri tumechoka kuwa wafuasi wa watu wanatumia umasiki wetu kujitajirisha.. kila mara ulaghai laghai tu ......
 
Mimi sioni tatizo na umaarufu wao. Hadi sasa ni maarufu na nawatakia heri ya umaarufu siku za usoni.
Baada ya hayo nataka nikuambie kuwa umarufu wao haufungi macho yetu.

Tutaonyesha umaarufu wao bila kusita na mapungufu yao bila kuona haya.

Sisi wengine tunaongozwa na mitazamo huru, kwa hili la siasa tunaangalia sera, maadili, na uadilifu.
Hatuangalii nani anabebwa katika machela nanai anatembea. Mrema alikuwa maarufu tu wala hakuna tatizio.

Nisichokubali katika akili yangu ni kudanganywa.
Leo ZZK anasema anasimamia demokrasia na haki kwenda mahalamani. Tunajua bunge la katiba ndilo lilimweka.
Njia ya kuchomoka ni Kitila kudai anamshawishi tena akimtangaza kuwa mwenyekiti hata pale zzk hajui sera za chama.

Hii habari ya siasa za 1947 tumechoka , tunataka siasa za kisayansi. Halafu uangalie watu wanaofanya hivyo wana nafasi gani katika jamii.Wapi uliona mwenyekiti wa chama cha siasa anateuliwa kama CEO.

Kitila amekosea, hilo la kwanza
Amekula matapishi yake hilo la pili
Anafanya siasa zisizolingana naye
Mkuu kwa nini unazunguka mbuyu. Kwetu sisi tulokusoma tunajua fioka unaficha ya kwamba ZZK na Kitila ndio waasisi wa chama ACT, hivyo unachojaribu kusema hapa ni kwamba haiwezekani Kitila amualike ZZK ACT ili aje kuwa mwenyekiti wakati ni yeye alokianzisha. Sema hivyo tutakuelewa kuliko kuzunguka Kuzungumzia historia ambayo sote tunaijua hapa JF.

Hiyo siasa ya Kisayansi ndio ipi ikiwa uongozi wa CDM walishindwa kusimamia demokrasia ndani ya chama nanyi mkawaunga mkono?... Itakuwa nje! Mimi nimewapinga na nitaendelea kuwapinga kwa maamuzi ambayo yamekiathiri chama na kwa sababu za ubinafsi wao. Cheo ni dhamana na hakuna nidhamu ya kumuogopa kiongozi yeyote! sintosimamamia nidhamu ya woga na unafiki.
 
Ningeomba kupata ufafanuzi zaidi juu ya chama hiki..

Tumeambiwa kuwa chama hiki ni chama cha uwazi (Allince for change and Transparency.. lakini cha ajabu kuanzia kuanzishwa kwake, waasisi wake, jinsi kilivyopata usajili ni usiri usiri tu hakuna uwazi.. Mfanoi Kitila anasema atamshawishi Zitto awe Mwenyekiti lakini hapo hapo Zitto anasema yeye ni Chadema (mpaka kesi iliyoko mahakani iamuliwe) sasa hapo mie ndio sielewi unawezaje kumpa unyekiti mwanachama tena kiongozi wa chama kingine?? ingekuwa jambo bora kama angesema kutoka na sera zetu tutajaribu kuwashawishi watanzania na watu mbali mbali kama Zitto wajiunge na ACT walau hapo ningemuelewa...

Pia tunasikia kuwa Zitto na Kitila ni Waasisi chama hiki, kwangu mimi ni jambo jema na la kujivunia kwani sio kila mtu anaweza kuanzisha chama maana kuanzisha chama kunahitaji muda, pesa, wataalamu nk. lakini cha ajabu wao wanajificha ficha, hivi kuna ugumu gani wa kusema ndio mimi ni muwasisi wa chama hiki? sasa kwa hili ambalo ni jambo dogo tu watu wanaficha ficha je uwazi tunaoubiriwa huko wapi?

Mwanzoni waliposema uwazi nilitegemea haya mambo ya siri siri sasa mwisho, tutarajie kujua wanzilishi wa chama hiki ni akina nani, sera zao ni zipi, wafadhali wao, na nk.. lakini cha kusikitisha zaidi hawa watu wanaotuhubiria uwazi walishindwa hata kutuonesha mikutano ya kutafuata wadhamini katika mikoa mbali mbali, walicho fanya ni kuleta picha ya mkoa wa Mwanza na yenyewe kuna walio sema huo ulikuwa ni mkutano wa mikopo na nk. ok inawezekani kuwa labda haikuwa ni muhimu kwao lakini unapohubiri uwazi ni lazima huwe muwazi kweli kama utashidwa kuwa muwazi kwa vitu vidogo vidogo je yakapokuwa mambo makubwa itakuwaje?

Wakati ufikie wanasiasa waache uongo, watekeleze wanachohubiri tumechoka kuwa wafuasi wa watu wanatumia umasiki wetu kujitajirisha.. kila mara ulaghai laghai tu ......
Sikia dada dhana ilokuwepo kwa wengi wetu ni kwamba Zitto na Kitila baada ya kufutwa uanachama Chadema walikwenda na kuanzisha chama cha ACT. Na ndivyo bado akioli ya wengi inawashauri hivyo lakini ukiwasoma hawa watu kwa makini utagundua kwamba Kitila ana kundi lake ambalo ndio wameanzisha chama hiki kama mwalivyoweza kuandika Waraka ule pasipo kumshirikisha ZZK.

Inavyoonyesha katika mikakati yao, na mahesabu yao Zitto angekwisha fukuzwa Chadema na hivyo wanaiacha nafasi hiyo wazi. Swala la mwenyekiti mara nyingi sana hasa wakati chama kinaanzishwa huteuliwa na waasisi wenyewe kwa muda hadi pale uchaguzi wa kwanza wa chama utakapo fanyika. Binafsi sioni tatizo lolote ikiwa hutaamini kwamba ZZK yupo ktk mpango wa kuanzishwa kwa ACT sawa kabisa na ule mpango wa kufanya mageuzi ya viongozi ndani ya Chadema uloandaliwa na kina Kitila. ZZK alihusishwa na waraka ule na sasa anahusishwa na kuundwa kwa ACT.

Hivyo watu hawataki kuamini kwamba ZZK sii mwanzilishi wala hahusiki kwa sababu walikwisha lishwa ujinga huo na kina Yudahadi baadhi ya watu kumchukia ZZK ttoka wakati wa waraka. Na kuna wale walomkana ZZK baada ya jogoo la tatu, hivyo ukichanganya yote haya lazima ZZK asulubiwe!

ZZK ana mapungufu yake na kubwa zaidi ni kwamba sii mwanasiasa aliyekomaa bado, mbinu nyingi za kisiasa zinamshinda badala yake anataka sana kutumia elimu yake ya darasa na Uzalendo wake kwa wananchi walalahoi. Siasa haziendi hivyo, hata kidogo ni lazima usimamie itkkadi kwanza, sera na kwa imani hiyo ndio unaamini kuwa njia pekee ya kuwapatia wananchi wako maendeleo. Waswahili wana sema akili nyingi huondoa maarifa ndio tatizo la vijana wetu!
 
Again kama ilivyokuwa kwenye mjadala wa Waraka wa Mwigamba, nguruvi3 amejitokeza tena na kuanza kushambulia watu badala ya hoja. ili hoja iwe na nguvu ni lazima ijengwe katika misingi ya kweli za kisayansi au kweli ambazo tayari zimeshathibiti, kwa bahati mbaya hoja ya Nguruvi3 haina component hata moja ya hivyo vitu, nitaeleza.

Siyo kweli kwamba Kitila na Zitto ni Wasaliti, bali hawa ni watu mashujaa, wanademokrasia wa kweli, watu wenye kusimamia maslahi mapana ya jamii, historia ziko wazi katika utendaji wa Zitto ndani na nje ya bunge na katika chama chake, na pia utendaji wa Kitila katika chama cha Chadema uko wazi. kilichotokea katika waraka wa Mwigamba ni mkakati wa kushinda uchaguzi halali katika chama, mkakti ulioandaliwa na Kitila na Mwigamba huku wakipanga kumuomba Zitto ashike usukani katika kinyag'anyiro cha uchaguzi ambao ungekuja kufanyika baadae, huu siyo usaliti huu ni uanademokrasia makini, hakuna mtu aingiaye katika uchaguzi bila mkakati. ni katika watu wa aina yamleta hoja wanaodhani kuwa unaweza kuingia katika uchaguzi wowote ule bila kujiandaa na bila mkakati wowote!!!.

Wasaliti ni wakina nani?
Ni wale wanaotumia ruzuku za chama vibaya, ni wale wanaoshawishi Bunge liwapangie vimada wao safari zisizo na tija ili wakaponde raha, ni wale wenye nafasi kuu ndani ya chama, na kutumia nafasi zao kuvunjua katiba ya chama ili waendelee kuongoza bila ya kushindanishwa na upinzani ulio credible!!!.

je kauli ya kitila ndiyo kauli ya ACT?
Nguruvi3 anafahamu kabisa kauli ya mwanachama mmoja mmoja siyo kauli ya chama, iwapo Nguruvi3 angekuwa ni mwenye kuamini katika demokrasia iliyo makini, isiyo na uzandiki bila shaka angefahamu kabisa kuwa Kuilink ACT kwa kauli ya mwanachama mmoja, tena ambaye hana uongozi ndani ya chama ni katika jitihada za kukizushia chama uongo!, Hata hivyo Kitila kutoa kauli yake kama mwanachama wa ACT juu ya mtu amabye angependa akiongoze chama hicho, bila ya kuitwa katika vikao na kuchukuliwa hatua za kufukuzwa uanachama, ni dalili njema kabisa kwamba ACT ni chama cha demokrasi, na cha watu wenye busara, naamini mwanachama wa chadema leo angetamka wazi kuwa mtu fulani tofauti na mwenyekiti wa sasa aje chadema agombee uenyekiti angepewa adhabu kali pengine hata kuvuliwa uanachama!!!

Nguruvi3 anadai lengo la Kitila ni kuchukua kundi la wanachama kutoka Chadema kuwaleta ACT, kusema kweli hii ni kauli ya Ajabu, ni tusi kwa wanachadema, ni kujaribu kuimply kwamba wanachadema wanaweza kukikacha chama hicho kwa ajili ya mtu tu!!. kiukweli kabisa, mtu yeyote awe mwanachadema, au mwanaCCM yupo katika chama hicho kwa utashi binafsi, yupo huru kwa fikra zake kabisa na uhuru wake kuamua kujiunga na chama chochote ilimradi chama hicho kinakidhi matarajio yake, HIVYO BASI IWAPO KUNA WANACHADEMA WATAKAOONA KUWA CHAMA CHAO KIMEKOSA MWELEKEO, NA WAKAAMINI KABISA HAWANA NAFASI YA KIDEMOKRASI NDANI YA CHAMA HICHO KULETA INFLUENCE YOYOTE YA KUOKOA JAHAZI, BASI WANA HAKI YA KUJIONDOA KATIKA CHAMA HICHO NA KUANZISHA KINGINE AU KUJIUNGA NA KINGINE, NA HILI SIYO KOSA HATA KIDOGO, NA WALA HUWEZI KUMLAUMU ZITTO, MWIGAMBA AU KITILLA KATIKA HILI.!

Again ni lazima tuwapongeze Mwigamba Kitila na Zitto kwa kutuonyesha njia, hawa ni kizazi kipya chenye uzoefu na siasa za upinzani katika zama mpya (new age) ambao wataongoza juhudi za kushika dola kutoka CCM, hawa ni wapinzani wa kisayansi, na si wapinzani matukio, rekodi yao iko wazi, na JUHUDI ZA WAHAFIDHINA WA CHADEMA KUVUNJA KATIBA YAO WENYEWE ILI KUWAKOMOA HAWA IMEKUWA NI BLESSING IN DISGUISE YA WATANZANIA KUWAJUA WAPINZANI WA UKWELI NI WEPI NA WAPINZANI MADARAKA NI WEPI!!

ACT tuihukumu kwa sera, itikadi, maamuzi itakayofanya na juhudi itakazotumia na si vinginevyo!.

Hauisadii Chadema iwapo Hauiambii ukweli kwamba sasa imekosa mwelekeo, imejikaanga yenyewe kwa maamuzi ya Kijuha yanayosigina katiba yao wenyewe.
Pamoja na mbeleko hii ya Ukawa iliyosheheni wapinga muungano kama Lissu na Mtikila, ni kihoja kikubwa kuunganisha nguvu na vyama vilivyokataliwa na wananchi, huku ukitegemea kuja kupewa sapoti na wananchi!. Ukiachilia mbali kupungua kwa nguvu kwa Chadema kutokana na migogoro ya ndani ya chama chao,
HII RHETORIC YA KUMPUT DOWN MWALIMU NA LEGACY YAKE, NA IMPLICATION YOYOTE YA KUUBEZA MUUNGANO NI KARATA TOSHA KABISA YA CCM KUWABWAGA VIBAYA MNO MNO CHADEMA KATIKA UCHAGUZI UNAOKUJA, KWA SABABU WATANZANIA WENGI WANAMHESHIMU MWALIMU, WATANZANIA WENGI WANATAKA MUUNGANO!, BADALA YA WAPINZANI KUSIMAMIA SERIKALI TATU KAMA HOJA YA KUIMARISHA MUUNGANO, WAO WAMESIMAMIA SERIKALI TATU KWA IMPLICATION YA KUVUNJA MUUNGANO, NA WATANZANIA HAWATAKI HILI!
 
UOTE=Mkandara;9525787]Sikia dada dhana ilokuwepo kwa wengi wetu ni kwamba Zitto na Kitila baada ya kufutwa uanachama Chadema walikwenda na kuanzisha chama cha ACT. Na ndivyo bado akioli ya wengi inawashauri hivyo lakini ukiwasoma hawa watu kwa makini utagundua kwamba Kitila ana kundi lake ambalo ndio wameanzisha chama hiki kama mwalivyoweza kuandika Waraka ule pasipo kumshirikisha ZZK.

Asante sana mkuu Mkandara kwa majibu yako hapo juu.
Kwa hiyo Kitila na kundi lake wameanzisha chama na wanataka kipate promo kwa kupita mgongo wa ZZK? Sasa kama ni hivyo kwa nini ZZK asijitokeze na kueleza umma juu ya jambo hili? huoni ZZK kukaa kimya kwa sisi ambao hatuna info za ndani tutaamini ZZK ni ndumila kuwili yaani yuko Chadema kimasilahi na yuko ACT kimatendo..




Inavyoonyesha katika mikakati yao, na mahesabu yao Zitto angekwisha fukuzwa Chadema na hivyo wanaiacha nafasi hiyo wazi. Swala la mwenyekiti mara nyingi sana hasa wakati chama kinaanzishwa huteuliwa na waasisi wenyewe kwa muda hadi pale uchaguzi wa kwanza wa chama utakapo fanyika. Binafsi sioni tatizo lolote ikiwa hutaamini kwamba ZZK yupo ktk mpango wa kuanzishwa kwa ACT sawa kabisa na ule mpango wa kufanya mageuzi ya viongozi ndani ya Chadema uloandaliwa na kina Kitila. ZZK alihusishwa na waraka ule na sasa anahusishwa na kuundwa kwa ACT.

Hapa sijakupata vizuri ina maana huu ni mkakati wa akina Kitila ila ZZK hana habari na mkakakti huu?
Kwangu mimi sina tatizo na ZZK kuunda chama au ZZK kuwa Mwenyekiti ila tatizo langu ni kuwa wanatangaza uwazi lakini wanatenda matendo yao kisiri siri.. Kama ZZK anajua huu mkakati na yeye hausiki na ACT kwanini hasisimame hadharani na kusema ukweli? na kama ni mmoja wa waanzilisha wa ACT kwanini hasisimame hadharani ni kusema? hapo ndipo tatizo langu lilipo. Uwazi unaoambiwa mbona kinakuwa kiini macho tena kwa vitu vidogo vidogo?


Hivyo watu hawataki kuamini kwamba ZZK sii mwanzilishi wala hahusiki kwa sababu walikwisha lishwa ujinga huo na kina Yudahadi baadhi ya watu kumchukia ZZK ttoka wakati wa waraka. Na kuna wale walomkana ZZK baada ya jogoo la tatu, hivyo ukichanganya yote haya lazima ZZK asulubiwe!

Nafikiri kama kuna watu wanamchukia ZZK basi hao ni wachache sana ila wanachochukia ni matendo yake ya undumila kuwili.. huu usiri siri husio na kicha wa miguu.. ZZK amesimamia mambo mengi katika taifa ili tena mambo ya hatari lakini hakuficha ficha lisimama akaongea anachofikiri ni sahihi..Sasa kwa sasa anashindwa nini kusimama na kuweka mambo sawa? kama ni ACT aseme na kama ni Chadema aseme.. Zaidi ya hapo mie naona yuko Chadema kimaslahi zaidi kitu ambacho ninaanza kujiuliuza juu ya uzalendo wake.


ZZK ana mapungufu yake na kubwa zaidi ni kwamba sii mwanasiasa aliyekomaa bado, mbinu nyingi za kisiasa zinamshinda badala yake anataka sana kutumia elimu yake ya darasa na Uzalendo wake kwa wananchi walalahoi. Siasa haziendi hivyo, hata kidogo ni lazima usimamie itkkadi kwanza, sera na kwa imani hiyo ndio unaamini kuwa njia pekee ya kuwapatia wananchi wako maendeleo. Waswahili wana sema akili nyingi huondoa maarifa ndio tatizo la vijana wetu![/QUOTE]

Hapa tuko pamoja ila kwenye uzalendo ninaanza kuwa na wasiwasi.. Tatizo la ZZK ni pupa, dharau, na kupenda kusifiwa na katika hili la sifa ana marafiki wazuri tu na ana marafiki ambao sio wazuri kwake na wanaomuimbia nyimbo za sifa anazopenda kusikia hali huku wakimchonganisha kwa viongozi wake na jamii kwa ujumla, na hawa marafiki waimba sifa wanapata misaada ya aina mbali mbali kutoka kwake kwani ZZK ana roho ya ubindamu sana tena sana tu.
 
Moja ya hoja za msingi za Nguruvi3 ni kwamba kwa chama cha ACT, mpinzani wake mkuu ni Chadema kuliko CCM. Wachangiaji kadhaa humu wamepinga hilo wakati huu ni ukweli ambao hata Dr. Kitila Mkumbo ameuthibitisha katika makala yake miezi kadhaa iliyopita titled: "Tunahitaji Chama Mbadala wa CCM na Chadema". Kitila anasema hivi:

"Kuna sababu zingine nyingi kwa nini tunahitaji mbadala wa CCM na CHADEMA. Kwanza, kuna uwezekano halisi kabisa ya CCM kushindwa katika Uchaguzi Mkuu ujao kama vyama vya upinzani, na hasa CHADEMA, vitapenda kushinda. Ikitokea CCM ikashindwa mwakani chama hiki kitakufa. CCM itakufa kwa sababu haina wanachama wala washabiki kwa maana halisi ya maneno haya. CCM ni chama dola, na hakuna popote duniani ambapo chama dola kilibaki baada ya kunyang’anywa dola. Vyama dola hushikiliwa na dola, na wanachama na washabiki waliopo katika vyama hivi kimsingi hushabikia dola na mara dola inapowatoroka na wanachama nao husepa. Ilikuwa hivyo Zambia kwa UNIP. Ilikuwa hivyo Kenya kwa KANU na ipo hivyo katika nchi nyingi za Afrika pale ambapo vyama vilivyokuwa vinatawala vilipoteza dola. Katika mazingira haya kuna hatari kubwa sana tukazalisha chama kingine dola mara CHADEMA kitakapokuwa madarakani kwa sababu ya upinzani dhaifu."

Kwanza hoja nzima ya Kitila inajengwa katika mazingira ya "uwezekano", sio uhalisia. Hapo juu anasema kwamba "kuna uwezekano halisi kabisa ya CCM kushindwa katika Uchaguzi Mkuu ujao kama vyama vya upinzani, na hasa CHADEMA, vitapenda kushinda ".

Pili, anathibitisha hoja ya nguruvi3 kwamba mpinzani mkuu wa ACT ni chadema kuliko ccm kwani tayari anakiona chadema kama chama dola kijacho pale anaposema:
Katika mazingira haya kuna hatari kubwa sana tukazalisha chama kingine dola mara CHADEMA kitakapokuwa madarakani kwa sababu ya upinzani dhaifu."

Kitila hazungumzii uhalisia uliopo bali uwezekano, hajadili uhalisia unaotokana na ushahidi kwamba mwenyekiti mtarajiwa wa ACT, Zitto Kabwe, alitumiwa na CCM kuivuruga chadema. Ushahidi mwingi umetolewa ikiwa ni pamoja na mawasiliano yaliyonaswa, bank transfers etc. Sio Zitto Wala Kitila wamekanusha haya.

Katika mazingira haya, Kitila anaacha maswali kuliko majibu pale anaposema kwamba "ushindi wa upinzani 2015 unawezekana hasa iwapo chadema itapenda kushinda". Je alipokuwa chadema hakupenda chadema ishinde? Kilichopunguza uwezekano huo ilikuwa ni nini? Jibu ni waraka na madhara yake. Waraka ulikiuka kanuni, na kama tutakavyo ona, yeye anasema solution ilitakiwa iwe busara na hekima, sio sheria na kanuni.

Kufuatia sakata la waraka, Kitila yupo sahihi kwamba wana chadema wengi wangependa kushinda mwakani. Lakini anasahau kwamba moja ya njia za kufanikisha lengo hilo ni pamoja na kushughulikia tatizo la zitto haraka na kumalizana nalo. Na hivyo ndivyo kamati kuu iliamua kufanya.

Lakini Kitila anashauri jinsi gani sakata lao lingeshughulikiwa, anasema kwamba:

"Sheria na kanuni hazijawahi kuwa nyenzo ya kutatua migogoro katika siasa. Migogoro ya kisiasa hutatuliwa kwa busara, hekima na uvumilivu, mambo ambayo hayapo katika uongozi wa sasa wa CHADEMA na ndio chama kinapoteza mweleko kwa kasi".

Hapa anaacha maswali kuliko majibu kwani yeye akiwa mmoja wa washauri wakuu wa zitto wamemshauri kwenda kuweka pingamizi mahakamani jambo ambalo ni la kisheria na kikanuni zaidi kuliko busara na hekima. Uamuzi wa zitto kwenda mahakamani umembomoa kuliko kumjenga. Busara na hekima ilikuwa ni kukiri kushiriki kwenye waraka, kukiri ilikuwa kinyume cha kanuni na kuomba msamaha. Basi. Chadema ingesonga mbele. Kwa maana nyingine, waraka ule ulikuwa kinyume cha kanuni, na solution yake ingekuwa matumizi ya busara na hekima kwa upande wa zitto, hasa baada ya uongozi wa chadema kumtetea wa muda mrefu. Hapa Kitila anajichanganya.
Nguruvi3 ana hoja nyingine kwamba kitila analaumu chadema kwa kuminya demokrasia halafu anaenda kurudia yale yale ACT. Kitila anathibitisha hoja hii anaposema:

"Ndani ya vyama vyetu hivi kuna wateule na wateuliwa. Kama haupo katika makundi haya huna nafasi na hii sio sifa njema ya chama cha kidemokrasia".

Je haoni kwamba nguruvi3 yupo sahihi kwamba zitto tayari ni mwenyekiti mteule wa ACT? Je wale ambao watapingana na Kitila juu ya uteuzi huu huo ACT watakuwa na nafasi? Je haya ya kitila ACT ni sifa njema ya chama cha kidemokrasia?

Tumalizie kwa kuangalia kwa undani hoja za Kitila juu ya kwanini mbadala wa ccm na chadema unahitajika. Anasema:

"Tunahitaji mbadala wa CCM kwa sababu chama hiki kimelewa madaraka na sasa hakioni wala kusikia, na haielekei kwamba ulevi huu utaisha, zaidi kuwa na dalili zote za usugu.

Tunahitaji sana mbadala wa CHADEMA kwa kuwa chama hiki nacho kimeanza kulewa sifa zinazotokana na umaarufu. Viongozi wa chama hiki wameshaanza kulewa na ndio maana wanaweza wakafanya maamuzi wanayoyaita ni magumu lakini ni ya hovyo bila woga wala hofu. Wanafanya hivi kwa sababu wanajua wanachama na wapenzi wao watawaunga tu mkono kwa sababu hawana namna madamu hawaitaki tena CCM.

Wanasahau kwamba kwa ulevi huu wa umaarufu wanatengeneza mazingira yaleyale ya CCM. Watakapoingia madarakani umaruufu utaisha na wataanza kulewa madaraka, na kwa ubabe wanaounyesha kabla ya dola kuna kila dalili kwamba ulevi wao wa madaraka utakuwa balaa.

Tunahitaji mbadala chama cha siasa cha upinzani kitakachojikita katika kupinga mawazo na falsafa za chama tawala, na sio kupinga sura za watu. Tunahitaji chama kitachokajengwa katika misingi ya demokrasia ya wanachama na sio demokrasia ya viongozi na waasisi wa chama. Tunahitaji chama kitachozingatia misingi ya uadilifu katika maisha binafsi ya viongozi na utumishi wa umma kwa sababu msingi wa uadilifu katika utumishi wa umma unajengwa katika uadilifu binafsi.

Tunahitaji chama ambacho kitalea viongozi ambao watakuwa na ujasiri wa kukiri makosa inapotokea wamekosea na sio kuyahalalisha. Kwa kifupi tunahitaji sana mbadala wa CCM na CHADEMA, na kujenga chama cha namna hii hatuhitaji miongo miwili. "

---------end quote-------------

nguruvi3 ameuliza - upo wapi utaalamu wa kisayansi? Na kwanini utaalamu huo unaungwa sana mkono na chama ambacho sayansi hiyo inalenga kukifanya kuwa mbadala yani chama cha mapinduzi?


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu JFS, kwanza, niseme tutakuwa tunafumba macho mchana na kudhani tumelalala usiku kama hatukubali kuwa kile chama mbadala alichotabiri Kitila ni ACT na kwamba jitihada zake na kauli za kuyumba ni political stunt.

ACT ni chama, kina wanachama wake na uongozi wake. Kitila ni mwanachama, awe kama mwanachama Muasisi au Mtabiri wa ujio wa chama hicho, bado haihalalishi kutuaminisha sisi kuwa Wanachama wake watafuata mkumbo wa ZIDUMU FIKRA ZA MUASISI. Wapi mwenzetu unakopata uhalali wa kuwasemea wanachama wa ACT kilichomo fikrani mwao? Unachotaka kufanya ni Ku-discourage watu ambao wanafikra za kujiunga na chama hicho, hali kuwa ni chama kipya na wao ndio wenye nafasi ya kui-shape ACT waitakayo.

Ni chama kipya, hakina hata Katiba, aje unataka kutuaminisha kuwa wanachama wake ni vipofu kuweza kuja na katiba na sera bora kabisa kwa kutumia tu kile unachoona amekosea mwanachama mmoja? Mtei wa CHADEMA alishawahi sema 2015 ni Dr. Slaa tu, kwa kauli hiyo ulishawahi tamka kuwa CHADEMA ni Mpini wa CCM kuumaliza upinzani Tz? Ulikosoa tu kistaarabu, ACT ina nini kwako kuwafanyia attacks aina hii?

Umefikia hatua hata ya kudai Kitila amemteua Zitto kuwa M/kiti ACT, hivi kweli ni halali kusema hivyo tu kwa kauli kuwa nitamshawishi achukue kadi ya chama na agombee uenyekiti? Mi kwangu ni kama dharau kwa wanachama wa ACT, hali kuwa ulichopaswa ni kutoa tahadhari kwa wanachama dhidi ya wanachama au waasisi aina ya Kitila.


Inavyoonekana Mkuu ulikuwa unatafuta nafasi yoyote ya kuteleza kwa ACT ili ushushe attacks hizi. Bado nachalea kukuelewa kwa kauli ya Kitila tu basi inahalalisha Shutuma zote ulizotoa dhidi ya ACT. SI SAHIHI. Kwa kauli kama hizo leo ungekuwa umeandika zaidi ya mara 10 kuwa CDM ni mpini wa CCM. Nadhani hoja zako zinazinaweza kuwa sahihi hapo baadea lakini kwa wakati huu HAPANA. ACT bado ina nafasi ya kufanya vizuri kuliko hiki unachowabashiria.

Anaita sasa!
 
Moja ya hoja za msingi za Nguruvi3 ni kwamba kwa chama cha ACT, mpinzani wake mkuu ni Chadema kuliko CCM. Wachangiaji kadhaa humu wamepinga hilo wakati huu ni ukweli ambao hata Dr. Kitila Mkumbo ameuthibitisha katika makala yake miezi kadhaa iliyopita titled: "Tunahitaji Chama Mbadala wa CCM na Chadema". Kitila anasema hivi:

Na hili ndio kosa Mkuu. Aje tuanze kukitazama chama kichanga kwa kuuanza kumtafuta Mpinzani wake Mkuu? Hivi hakuna mengine muhimu zaidi kuyajadili kuhusu hiki chama ila tu kumtafuta mpinzani wake? Aje kama huyo mpinzani ni yule tunayemuhusudu sisi? Ni wasiwasi wangu kuwa hoja zilizopo hapa ni zile zinotokana na hilo.

Kosa kubwa ni kuanza kuichambua ACT kwa kuangalia mpinzani wake ni nani. Tunachopaswa kujadili ni nafasi ya Sera za chama husika katika kuleta ustawi kwa Watanzania, kisha nafasi ya watekelezaji katika kufanikisha sera hizo. Tukishaiona katiba ya chama ambayo tunataraji ibebe falsafa na sera za chama, tutaanza kusema yule na yule wanaweza kutekeleza hili ama laa.

Ni mapema mno kuanza kuwaita ACT majina mabaya, japo kama sehemu ya propaganda kufagilia chama fulani ni sahihi!

Anaita sasa!
 
Back
Top Bottom