Duru: Hatima ya Muungano na dalili za kuvunjika mapema

Mchambuzi ahsante sana kwa ufafanunuzi. Hoja ya JFC inatumiwa kufidia mapungufu na kukwepa ukweli.
Tumeuliza sana, kama znz haichangii kwasababu hakuna JFC,ni mfuko gani unaoiwezesha kupata 4.5% ambayo sasa imepanda na kuwa 7%. Hakuna anayekuja na jibu, wanarudia hoja ile ile dhaifu

Tumeuliza, kwasasa znz inapata Bilioni 1.75 kwa mwezi. Je, zinatoka mfuko gani wa pamoja? Hakuna jibu, wanarudi na hoja ile ile isiyo na maana kwasababu hawana majibu.

Tumeuliza, watimishi wa muungano wanalipwa na frdha kutoka mfuko gani wa pamoja? Hakuna jibu, wanarejea hoja wanayojua haina mashiko.

Tunauliza, zile pesa za kusaidia bajeti ya znz kutoka JMT zinatoka mfuko gani? Hakuna jibu, wameshikilia pale wasipo na jibu

Inapofika wakati wa kudai masilahi wznz ni wazuri sana wa kuumba na kudai. Wakati wa kuwajibika, hukimbilia hoja za kipuuzi kama hii ya JFC.

Kwa mtu mwenye akili angejiuliza

Na mwisho, tumewauliza formuala gani zinatumika kwa znz kupata mafao ya muungano, ambazo haziwezi kutumika katika kuchangia muungano? Hakuna jibu, wanasema misaada na mikopo. Tumewaonyesha ni kiasi gani znz inapata kutoka muungano bila kujua kwanini na kwa njia gani. Hawana jibu, wanaturudisha kule kule kule wasiko na mjibu

Ni kwa msingi huo, utawasikia wznz wakizungumzia kugawana vyeo, kupata nafasi zaidi kwasababu mentally wanaaamini kuwa huu muungano unajiendesha kwa solar energy, na wajibu wa kuhudumia hiyo solar system ni wa Tanganyika.
Wao wanawajibu wa kukusanya tu.

Kwa sasa tunawaambia Watanganyika lazima mambo yatenge, na shughuli zishsughuikiwe na nchi husika. Tanganyika irudi, znz ikae kama mshirika mwenza katika kuzungumzia nafasi yake ndani ya muungano na si nani anakuwa spika, waziri au vyeo. Lazima znz wawajibike katika muungano katika kuuendeleza, si kufanya Tanganyika shamba la mavuno.

Hakuna haki isiyo na wajibu, na waznz sasa ni wakati watambue kuwa Watanganyika wamechoka si kuudumia muungano peke yao bali pia uzito walioubeba ambao return yajke ni questionable

Kwa kila dimension, Tanganyika inaumizwa sana na mfumo wa sasa. Kwa mfano, tukiangalia hesabu rahisi tu tena in practice (mapato na matumizi) ni hivi:

Mapato ya Zanzibar kwa mwaka(ndani, nje, na kutoka tanganyika) ni kama tsh 700b. Hizi ndio fedha za bajeti ya znz kwa mfano kwa mwaka huu wa fedha. Ukigawanya hii kwa kila mzanzibari (1.3mil) unapata mgao wa bajeti kwa kila mzanzibari ni tsh kama 540,000. Ukiondoa waznz kama 500,000 ambao wapo Tanganyika, ni kama tsh 870,000 per mzanzibari. Kwa watanganyika, mapato yao ni kama sh.19 trillion. Hii ndio bajeti ya muungano pia. Ukigawanya hii kwa kila mtanganyika, unapata ni kama tsh 440,000. Katika hizi, bado nyingine nyingi tu zinaenda znz wakati zile 540,000 za znz n kwa ajili ya matumizi yao wenyewe tu. Mtanganganyika hagusi kitu hapo.
 
Last edited by a moderator:
Kwa kila dimension, Tanganyika inaumizwa sana na mfumo wa sasa. Kwa mfano, tukiangalia hesabu rahisi tu tena in practice (mapato na matumizi) ni hivi:

Mapato ya Zanzibar kwa mwaka(ndani, nje, na kutoka tanganyika) ni kama tsh 700b. Hizi ndio fedha za bajeti ya znz kwa mfano kwa mwaka huu wa fedha. Ukigawanya hii kwa kila mzanzibari (1.3mil) unapata mgao wa bajeti kwa kila mzanzibari ni tsh kama 540,000. Ukiondoa waznz kama 500,000 ambao wapo Tanganyika, ni kama tsh 870,000 per mzanzibari. Kwa watanganyika, mapato yao ni kama sh.19 trillion. Hii ndio bajeti ya muungano pia. Ukigawanya hii kwa kila mtanganyika, unapata ni kama tsh 440,000. Katika hizi, bado nyingine nyingi tu zinaenda znz wakati zile 540,000 za znz n kwa ajili ya matumizi yao wenyewe tu. Mtanganganyika hagusi kitu hapo.
Kwasasa znz inapata Bilioni 1.75 kama kodi ya wafanyakazi wa muungano.

Kodi hiyo ni kutoka kwa mwananchi wa Iramba, Tunduru anayefanyakazi halmashauri ambayo si jambo la muungano.
Sasa ukichanganya na mfano wako hapo juu, ina maana yule masikini wa Geita anamchangia mzanzibar ambaye kipato chake tu ni kikubwa.

Tumeuliza, kama wznz walaitaka 21% ya ajira, formula gani imetumika. Hakuna mwenye jibu.

Hapa maana yake ni kuwa fursa za ajira kwa wznz zoinatolewa kwa gharama za Watanganyika.

Kwamba, mznz anaajiriwa serikali za mitaa au wizara ya afya au miundo mbinu kwa kigezo cha 21% na kumpora Mtanganyika fursa zake. Halafu yule Mtanganyika alioyeporwa fursa anapolipa kodi kwa njia nyingine anaadhibiwa kwa kupeleka kodi ile ile aliyoikosa kwa 21% kule znz. This is insane!

Atokee mtu hapa atueleze, mkoa gani unaopata 1.75Bilioni kwa mwezi. Halamashauri zote chini ya waziri mkuu zinapata Bilioni 500 kwa pamoja. Ukigawanya kwa kila mmoja utashangaa ni kiasi gani kinapatikana. Yet eneo linalozalisha ajira ka Dar halipati kiasi kinachopelekwa znz. Na ikumbukwe, ajira ni kwa faida yao, kwanini Watanganyika waadhibiwe kwa hilo?

Wznz wanajinasibu kuwa wanaweza kufianya nchi yao Dubai ya Afrika.
Ni kweli kabisa, si kutokana na uwezo wa uchumi wao, ni kutokana na ukweli kuwa pesa zao ni za kujenga miundo mbinu, huduma za elimu na afya. Hawana habari na ulinzi na usalama, mambo ya ndani n.k. Hata bajeti yao haionyeshi hilo.

Wanaweza kwasababu 7% wanayopata inatokana na pato la Mtanganyika.
Kwamba Mtanganyika akikusanya kodi zaidi mzanzibar hatakiwi kufanya kazi yoyote, yeye anapata 7%

Ndio maana tunasema huu ni mzigo mzito sana, na bila uwepo wa Tanganyika znz itaendelea kujificha nyuma ya koti la Tanzania ikivuna, wakati wa kulima na kupalalilia wao si Watanzania, wakibanwa wanasema hakuna mfuko wa JFC.

Kile unachokiita Riwaya ya Chenge ndio jeneza la kuhakikisha Mtanganyika anaumia zaidi. Kwa mfano, Riwaya pendekezwa ya Chenge inasema, kikatiba znz ikikopa mdhamini ni Mtanganyika. Kwasasa znz hailipi madeni ya ndani wala ya nje, riwaya inawapa nafasi zaidi za kukopa makaimati na mzigo huo ataubebea mwananchi wa Ileje, Ilembula na Makindani.

Riwaya pendekezwa ya Chenge haikulenga kumsaidia au kutafuta suluhu. Kilichokuwa kimekusudiwa nai shamra shamra ili suala la escrow lipotee. Na hapo ndipo Watanganyika wanatakiwa kusimama na si kukataa bali kususa hata kuongelea riwaya.
 
ASILIMIA 21 YA AJIRA HAIELEZEKI

ILIPANGWA NA WAZANZIBAR BILA FORMULA

NDILO CHIMBUKO LA BILIONI 1.75 KWA MWEZI KUTOKA TANGANYIKA

Tumeulizani kanunigani ilitumikakupata asilimia21 ya ajira kwa wazanzibar?

Hakunamwenye jibu, tunachojua zipo 21% kutoka kila kona, hata maeneoyasiyoya muungano.

Ni 21%ndiyoinayotoapato la kodi za wafanyakazi wamuungano wakiwemowa idarana taasisi zisizozamuungano. 21%ndiyo inayozaa adhabukwaWatanganyika kwa nafasi za ajira hatazisizo za muungano.


Adhabuni kulipa bilioni 1.75 kwa mwezi. Ukichukulia mikoa kama 30 kwa mfanotu, hiyo ni sawa na makusanyoyakodiza kilamkoa katika milioni takribani 50. Hukomikoani hakunawafanyakaziwa muungano, wengiwao ni wa serikaliza mitaa.


Chimbuko la21% limeanzabaada ya kuwepokwa utaratibuusiowa kikatiba wavikao vya muungano.
Vikao hivyo
vilihusuZanzibar na JMT ambayo znz ipo pia.



Awali,vikaovilihusisha waziri mkuu kwaupandewa JMT na waziri kiongozikwaupande wa SMZ.

Hadi hapo tu, kunauharamu. Huwezi kuwa na kikao kati ya JMT ambayo znz ni mshiriki halafu upandewa pili ukawa na znz,huko ni kuwanyima
Watanganyika fursa ya kutetea masilahi nanchi yao.


Katika haliisiyokuwa ya kawaida, upande wa JMT ukawa unawakilishwa na makamu wa Rais waJMT na znz makamu wa pili wa Rais. Wajumbe wa vikao hivyo nipamojana waziri anayeshughulikia muungano, waziriwa fedha kwa uchache wa kuwataja.

Hawa wote niwazanzibar wanaokaa upande mmoja na mwingine wakiwa JMT na znz.


Ndipoilipozaliwa asilimia 21 baada ya kujipangia ni kiasi gani wanadhaniwznz wanahitajina watapata kodi kiasi gani kutokana na hilo.

Hali hiyo,hakuna anyeweza kueleza asimia 21 imetokana na utaratibu gani.
Nirahisi
sana watukubuni kuwa ni zao lavikaovya wazanzibar ambavyo Watanganyika waliachwa nje.



Vikaohivyovyawznzhavikuwahikuzungumziakuhusuwajibuwa znz katika muungano.

Ni vikao
vilivyokuwavimelenga masilahi yaznz kwa gharama za Watanganyika.

Na hapo ndipo katiba ya 1977 ilipowaachaWatanganyika njia panda, na sasa wanatupiwa riwaya pendekezwa ya Chengewajifunge kitanzi.



Ukisomarasimu ya Warioba, yote hayo yalikuwa na ufumbuzi.
Ilikuwa ni washirika wawiliwakae pamoja kukiwa na msuluhishi katika kupata muafaka.



Tusemezane
 
J
Barubaru,

Katiba ya JMT (1977) inatambua uwepo wa AKAUNTI YA PAMOJA, kama sehemu ya mfuko mkuu wa hazina ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kusema kwamba - kutawekwa fedha yote itakayochangiwa na serikali mbili kwa kiasi kitakachoamuliwa na tume ya pamoja (Joint Commission). Serikali mbili zinazotajwa hapa ni ile ya Mapinduzi Zanzibar na nyingine ya Tanzania Bara. Utata unakuja kwa sababu serikali ya Tanganyika haipo, badala yake iliyopo ni serikali ya Tanzania ambayo nayo haipo kivyake kama ilivyo kwa serikali ya Zanzibar kwani chini ya serikali mbili, serikali ya Tanzania Bara remains to be synonymous to serikali serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akaunti ya pamoja haitekelezeki kwa sababu mfumo wa serikali mbili hauruhusu mazingira hayo. Tuangalie kwa undani zaidi. Tume ya pamoja (JFC) ipo kwa mujibu wa katiba ya JMT (1977) katika ibara ya 133, lakini ipo pia ndani ya riwaya ya andrew chenge. Majukumu yake yanaainishwa kama ifuatavyo:

1. Kuchambua mapato na matumizi yanayohusu utekelezaji wa mambo ya muungano na kutoa mapendekezo kwa serikali mbili juu ya mchango na mgao wa kila serikali.
Swali: Ni mambo yepi hayo ya muungano ambayo yametenganishwa na yale ya Tanganyika (ukipenda Tanzania Bara)?Bila ya kuyatenganisha masuala husika, jukumu #1 la JFC hapo juu haliwezi kutekelezeka.

2. Jukumu la pili la JFC - Kuchunguza wakati wote mfumo wa shughuli za fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na uhusiano wa kifedha baina ya serikali mbili.
Swali: Mfumo wa shughuli za fedha chini ya mfumo wa serikali mbili unachunguzwa vipi bila ya kutenganisha masuala ya muungano na yale yasiyo ya muungano kwa pande zote mbili za washirika wa muungano?

Huku ni kupoteza tu muda na fedha za walipa kodi kwani JFC inajikuta ikifanya kazi ndani na chini ya mfumo wa muungano wenye wizara/taasisi zenye sura kuu tatu:

1. Mambo ya muungano pekee yake.
2. Mambo ya Tanzania bara.
3. Mambo mchanganyiko.

Tuangalie mifano hai:

a) Ofisi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haina mamlaka Zanzibar kasoro kwenye "Suala la Usajili wa vyama vya siasa", kitengo ambacho kipo chini ya waziri mkuu, na ni moja ya masuala ya muungano. Kwa maana hii, ofisi kubwa kama ya waziri mkuu ina mchanganyiko wa masuala ya muungano (Vyama vya siasa) na mengineyo ambayo ni ya bara tu. Katika hali hii, JFC itafanya vipi kazi zake?

b) Wizara ya katiba ya sheria, wizara hii ni ya Tanzania bara peke yake lakini ina idara ambazo ni za ki-muungano, kwa mfano idara ya mahakama (inayokusanya mapato mengi tu), Katika hali hii, JFC itafanya vipi kazi zake?

c) Wizara ya uchukuzi chini ya Samuel Sitta, wizara hii ni ya Tanzania bara tu lakini ina idara ambazo zina sura za ki-muungano kama vile TCAA, TMA, TPA, ATC (zinazokusanya mapato mengi tu). Katika hali hii, JFC itafanya vipi kazi zake?

d) Wizara ya Sayansi na Tekinolojia kwa Mbarawa na mwenzake Makamba, hii ni wizara ya Tanzania bara tu, lakini ina idara ya TCRA ambayo ni ya muungano, idara ambayo inakusanya mapato mengi tu, katika hali hii, JFC itafanya vipi kazi zake?

e) Wizara ya Viwanda na biashara, hii nayo ni ya Bara tu lakini ina idara za kimuungano kama vile Brela na TBS, na idara hizi zinakusanya mapato mengi tu, katika hali hii, JFC itafanya vipi kazi zake?

f) Wizara ya fedha, kuna NMB, CHC, NIC, na humu yapo ya muungano na yasiyo ya muungano.

g) Wizara ya mambo ya ndani ya nchi, humu pia kuna mchanganyiko. Faini anayopigwa mtanganyika kwa kuvuka taa nyekundu kwenye taa mpya pale Mianzini arusha, faini hiyo inavuka kwenda Zanzibar kwa sababu ni wizara ya muungano, lakini faini za zanzibar, hizi hazivuki kuja Tanganyika.

h) Wizara ya Nishati na Madini, hii ni ya Tanzania Bara pekee lakini TPDC inafanya kazi kimuungano.
Kumbuka, vyanzo vya mapato ya kuendesha muungano yamegawanyika katika makundi mawili:

1. Mapato yatokanayo na kodi. Humu kumejaa utata mwingi sana juu ya makusanyo ya wapi yanapelekwa wapi.
2. Mapato yasiyotokana na kodi. Haya tumejadili hapo juu, faini za polisi, mahakama, brela, etc.

Awali tuliona majukumu ya JFC kwa mujibu wa katiba ya JMT (1977). Kama tupo pamoja hadi hapa, je JFC itaweza vipi kuchambua mapato na matumizi yanayohusu utekelezaji wa masuala ya muungano wakati yapo mapato chini ya wizara zisizo za muungano bali za Tanzania Bara lakini wizara hizi zina sura ya ki muungano? Mapato ya aina hii yanazidi shilingi Trilioni moja kila mwaka.

Natumaini Barubaru umepata majibu kwa swali lako ambalo huwa unalirudia sana. Ningeomba kuanzia sasa tusaidiane kuyaweka haya wazi, lakini muhimu zaidi, kuhimiza juu ya haja ya Tanganyika kuzinduka.

Mchambuzi,

Ahsantum sana kwa maelezo yako. ILA NILIPO RED Hizo sio Idara za muungano. Mfano katika idara ya mahakama. Muungano upo katika mahakama ya Rufaa tu lakin sio mahakama kuu na chini yake.

Vile vile TCRA inafanya ujanja tu lakin si chombo cha muungano kwani haina sura ya kimuungano kama lilivyo baraza la mitihani NECTA na wengineo japo zinafanya kazi mpaka Znz. Kuna vyombo kama ERB (Engineers Reg Board), Contractor Reg Board na zingine zimeshitukiwa na sasa Znz wanazo za kwao.

Vitu vyenye sura ya muungano vinakuwa na muundo wa kimuungano kama mfano mfumo wa BoT, Tume ya haki za Bin'Adam au mfumo wa wizara kama mambo ya nje , mambo ya ndani etc.

Sababu ulizobainisha za kushindwa kuanzishwa kwa JFC ni sababu za kitoto sana na hazina mashiko hata moja. Kumbuka kuwa katika kila bajeti ya wizara kila idara au Taasisi inakuwa na Bajeti yake ndani ya Wizara hiyo husika. nayo inawekwa bayana ukiwa unasoma bajeti au kama utasikia wabunge wanapitisha bajeti ya wizara kifungu kwa kifungu ambavyo ndio utenganisho uliopo

Nakupa mfano mdogo tu wa ripoti ya TRA ya kila robo mwaka ambayo ina mamlaka ya kukusanya kodi zote huko Tanzania inaonyesha kila mkoa imekusanya kiasi gani, na wanaweza kwenda mbali zaidi wakakuonyesha motor vehicle wamekusanya kiasi gani, kodi za ushuru wa mazao mbalimbali kiasi gani na kodi nyinginezo kwa kila mkoa. JE ITASHINDWAJE kuonyesha Tgk wamekusanya kiasi gani na Znz kiasi gani na mwisho wa siku kila mtu kuweza kulipa kile mlichokubaliana.

Nashangaa unaposema kodi anayolipa kosa la barabarani pale mianzini au sanawari inakwendaje Znz wakti nako kuna taa za malindi na darajani?

Labda nikupe mwangaza zaidi KATIKA FANI YA KIUHASIBU MAMBO YOTE ULIYOSEMA YANAWEZEKANA tena hata ukitaka wakwambie kila mtu amechangia kiasi gani katika mwaka husika na kodi zake zote alizochangie kwa mnyumbulisho. NI JAMBO LA KUWEKA NIA NA KUTENGENEZA MFUMO MZURI WA KUKUSANYA NA KUTENGANISHA MAPATO na MATUMIZI KWA VILE MLIVYOTAKA.

Moja katika kaanun za Fedhwa hususan wa nchi hizi mbili ni namna ya kuthibiti matumizi na mapato. Kumbuka kuwa Fedhwa zote za SUK Znz zinakaguliwa na kudhibitiwa na CAG Znz na sharia za matumizi na mapato yake inatungwa na BLW la Mh Pandu Ameir Kificho.

Pesa zote za JMTz zinakaguliwa na kudhibitiwa na CAG Tz na sharia za matumizi na mapato yake inatungwa na Bunge la JMTz la Mh Makinda.

Sasa katika kaanun za fedhwa tunajiuliza.
1. Je Znz achangie katika mfuko gani pesa zake za muungano? Je Tgk anachangia katika mfuko gani pesa za muungano?
2. Je Znz au Tgk kila nchi inatakiwa ichangie kiasi gani katika muungano?
3. Je nani atakuwa mdhibiti mkuu wa mapato na matumizi ya fedhwa hizo zikijumuishwa na mikopo na misaada?.

Jibu la masuala hayo hapo juu ambayo ndio yanayoleta mtafaruku mkubwa sana wa kutoaminiana, kutuhumiana na kulalamikiana solution yake ni kuundwa kwa Joint Finance Commission (JFC) ili chombo hichi kiweze kusimamia mapato, matumizi na kudhibiti mfumo wa fedhwa wa nchi hizi na kuupeleka kwa mujibu wa Katiba na Bunge la Muungano.

Sasa unaposema huwezi kutenganisha mapato katika vyombo vya muungano au idara za muungano hilo sio sahihi kabisa kwani kila idara kwa mujibu wa bajeti ya kila mwaka ya kila wizara INATENGEWA BAJETI YAKE. kama utapitia bajeti ya wizara ya Katiba na Sharia ya JMtz 2014/2015 wametenga 106 Bilion kwa ajili ya Mahakama ya Rufaa tu. na mahakama kuu na nyingine za chini yake zimetengewa fungu lake.

Kumbuka kuwa kila kitu ni NIA na laazima ukubali wawakilishi wenu Bungeni wana akili Timamu na walijadili kwa kina sana kupitisha Sharia hii ya JFC.

Suala lipo pale pale JMTz inapata wapi kiburi cha kutotekeleza sharia hii iliyopitishwa na Bunge? wanakhofia nini kutekeleza sharia hii ya kuanzishwa JFC?

Akhasantum

 
Kwa kila dimension, Tanganyika inaumizwa sana na mfumo wa sasa. Kwa mfano, tukiangalia hesabu rahisi tu tena in practice (mapato na matumizi) ni hivi:

Mapato ya Zanzibar kwa mwaka(ndani, nje, na kutoka tanganyika) ni kama tsh 700b. Hizi ndio fedha za bajeti ya znz kwa mfano kwa mwaka huu wa fedha. Ukigawanya hii kwa kila mzanzibari (1.3mil) unapata mgao wa bajeti kwa kila mzanzibari ni tsh kama 540,000. Ukiondoa waznz kama 500,000 ambao wapo Tanganyika, ni kama tsh 870,000 per mzanzibari. Kwa watanganyika, mapato yao ni kama sh.19 trillion. Hii ndio bajeti ya muungano pia. Ukigawanya hii kwa kila mtanganyika, unapata ni kama tsh 440,000. Katika hizi, bado nyingine nyingi tu zinaenda znz wakati zile 540,000 za znz n kwa ajili ya matumizi yao wenyewe tu. Mtanganganyika hagusi kitu hapo.

Mchambuzi.
Nilipo RED.

Mapato ya Znz kwa mujibu wa bajeti yake ya 2014/2015 ni 400 Bil na sio 700 Bil.

Na kwa upande wa JMTz kwa mujibu wa bajeti yake ya mwaka 2014/2015 ni 12 Trillion na sio 19 Tril.

Mchanganuo wa Utekelezaji wa bajeti 2014/15. Hususan kwa kuangalia vyanzo vya mapato vya JMTz . nakuwekea hapa for your reference

Tsh (Trillion)
1 MAPATO YA NDANI
i.Mapato ya kodi TRA11,318,222/=
iiMapato yasiyo ya kodi859,812/=
Jumla ya mapato ya ndani12,178,034
iiiMapato ya halmashauri
458,471/=
ivMapato ya misaada ya nje
2,941,599/=
vMikopo ya ndani
2,955,227/=
viMikopo ya masharti ya kibiashara1,320,000/=





 
Mchambuzi.
Nilipo RED.

Mapato ya Znz kwa mujibu wa bajeti yake ya 2014/2015 ni 400 Bil na sio 700 Bil.

Na kwa upande wa JMTz kwa mujibu wa bajeti yake ya mwaka 2014/2015 ni 12 Trillion na sio 19 Tril.

Mchanganuo wa Utekelezaji wa bajeti 2014/15. Hususan kwa kuangalia vyanzo vya mapato vya JMTz . nakuwekea hapa for your reference

Tsh (Trillion)
1 MAPATO YA NDANI
i.Mapato ya kodi TRA11,318,222/=
iiMapato yasiyo ya kodi859,812/=
Jumla ya mapato ya ndani12,178,034
iiiMapato ya halmashauri
458,471/=
ivMapato ya misaada ya nje
2,941,599/=
vMikopo ya ndani
2,955,227/=
viMikopo ya masharti ya kibiashara1,320,000/=





Barubaru, Kama ulinisoma vyema, nimejumuisha na fedha za nje ambazo zinachanganywa na kutengeneza bajeti, suala ambalo ndio hasa nililenga.
 
Last edited by a moderator:
....

Mchanganuo wa Utekelezaji wa bajeti 2014/15. Hususan kwa kuangalia vyanzo vya mapato vya JMTz . nakuwekea hapa for your reference

Tsh (Trillion)
1 MAPATO YA NDANI
i.Mapato ya kodi TRA11,318,222/=
iiMapato yasiyo ya kodi859,812/=
Jumla ya mapato ya ndani12,178,034
iiiMapato ya halmashauri
458,471/=
ivMapato ya misaada ya nje
2,941,599/=
vMikopo ya ndani
2,955,227/=
viMikopo ya masharti ya kibiashara1,320,000/=



hii nimeichomoachomoa kutoka Bajeti ya serikali ya Zanzibar

[B said:
Hotuba ya Bajeti ya Serikali Mapinduzi Zanzibar, 2014/2015[/B]]

MWELEKEO WA BAJETI YA MWAKA 2014/15-ZANZIBAR


A. MAPATO
…… Kwa mwaka 2014/15 Serikali inatarajia kukusanya jumla ya TZS 707.8 bilioni …….. Mapato ya Ndani …. jumla ya TZS 365.8 bilioni zinatarajiwa kukusanywa kama mapato ya ndani katika mwaka 2014/15. …. Kati ya makadirio ya 2014/15:
  1. ZRB inakadiriwa kukusanya jumla ya TZS 199.7 bilioni yakiwemo na makusanyo ya Mawizara ya TZS 18.4 bilioni.
  2. kwa upande wake, TRA inakadiriwa kukusanya TZS 166.1 bilioni sawa na ziada ya asilimia 25.7 ya mapato halisi yanayotarajiwa kwa mwaka 2013/14 ya TZS 132.1 bilioni.
  3. Aidha, Mapato yanayotokana na wafanyakazi wa SMT wanaofanya kazi Zanzibar yanakadiriwa kufikia TZS 21.0 bilioni kwa mwaka 2014/15
  4. Serikali kwa mwaka wa fedha 2014/15 inatarajia kukopa ndani jumla ya TZS 15.0 bilioni ili kufidia nakisi ya bajeti.
Mapato ya Nje Serikali kwa mwaka 2014/15 inakadiria kukusanya Jumla ya TZS 305.4 bilioni :Kati ya mapato hayo,:
  1. TZS 265.4 bilioni ni Mikopo na Ruzuku kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo. Kiasi hicho ni ongezeko la TZS 82.5 bilioni sawa na asilimia 45.1 ikilinganishwa na matarajio ya kipindi cha Julai hadi Juni 2014 ya TZS 182.9 bilioni (ikiwemo matarajio ya msamaha wa Madeni wa TZS 1.9).
  2. Kiasi kilichobakia cha TZS 40.0 bilioni ni Msaada wa Kibajeti


B. MATUMIZI
Serikali inakadiria kutumia jumla ya TZS 707.8 bilioni mwaka 2014/15 …. Matumizi ya Kazi za Kawaida:

  1. matumizi ya kazi za kawaida yanatarajiwa kufikia jumla ya TZS 376.5 bilioni .Mchanganuo wa matumizi hayo ni kama ifuatavyo:
i. Mishahara ya Serikalini TZS 184.5 bilioni
ii. Ruzuku kwa Taasisi za Serikali TZS 50.3 bilioni
iii. Matumizi ya Mfuko Mkuu wa Serikali TZS 69.8 bilioni
iv. Matumizi mengineyo ya kuendeshea Serikali ni TZS 71.8 bilioni
Matumizi ya Kazi za Maendeleo Kwa ajiri ya Mpango wa Maendeleo, Serikali inatarajia kutumia jumla ya TZS 331.3 bilioni mwaka 2014/15. Kati ya matumizi hayo:
  1. TZS 265.4 bilioni ni Misaada kutoka nje, ikiwemo TZS 66.3 bilioni za Ruzuku kutoka kwa Washirika wa Maendeleo na
  2. TZS 199.1 bilioni ni Mikopo. SOURCE:http://www.zanzibarassembly.go.tz/budget/2014/Hotuba-ya-bajeti-ya-serikali-2014-2015.pdf.

Mkuu ni kushukuru kwanza kwa kunipa ari ya kuitafuta na kuisoma bajeti ya Zanzibar, baada ya kuona extracts zako za bajeti ya JMT. Ni kwa mara ya kwanza nimeweza kuifuatilia bejeti hii ya Zanzibar.

Nikirudi kwenye lengo la kunukuu baadhi ya vipengele vya Bajeti ya Zanzibar, ni kuwa ninaomba unipe ilimu/elimu juu ya haya nitakayouliza(rejea nukuu ya Bajeti ya Zanzibar hapo juu), maana ni kwa mara ya kwanza leo nimefuatilia bajeti hii, Pia naomba uniilimishe kwa lugha nyepesi :

Mapato- Mapato ya ndani:

1. -TRA inakadiriwa kukusanya TZS 166.1 bilioni
Tunaambiwa TRA inafanyakazi Tanzania Bara/Tanganyika tu kwa sasa (huko mna ZRA), TRA hii ya kwenu ni ipi? Je. mapato haya yanakusanywa huko Zanzibar ama yanakusanywa Tanganyika na TRA ya Tanganyika?

2.Mapato yanayotokana na wafanyakazi wa SMT wanaofanya kazi Zanzibar yanakadiriwa kufikia TZS 21.0 bilioni kwa mwaka 2014/15:
Yale ya wafanyakazi wa Zanzibar wanofanya kazi Tanzania bara ni kiasi gani ? jibu hili uwenda likategua kitendewili cha asilimia ya 4.5% ambayo sasa ni 7% ya pato la JMT linalokwenda Zanzibar. Ila ukrasa wa 48 kuna jedwali lina maelezo ya 4.5 % bilioni ni Msaada wa Kibajeti . Sijajua kama hii ndiyo Nguruvi3 huwa anaizungumzia ambayo inatoka Tanganyika.

3. kukopa ndani jumla ya TZS 15.0 bilioni - Hii mna maanisha kukopa kwenye mabenki/ama taasisi nyingine za kifedha yanayofanya kazi zake Zanzibar ama hata yale ya Tanganyika?

4. Ukrasa wa 11 na ule wa 16 wa hotuba hiyo pameandikwa kuwa Zanzibar ilitarajia kupata PAYE kutoka URT (nadhani ni United Republic of Tanzania) TZS 16.2 bilioni (2013/2014) lakini ilipata jumla ya TZS 15.8 bilioni kutokana na Kodi ya wafanyakazi wa Muungano waliopo Zanzibar (PAYE). Je. Mwaka 2014/2015, mapato haya yamesimamishwa kuletwa, maana hayapo kwenye kipengele cha mapato ya serikali...!?

5.Ukrasa wa 24 imeandikwa kuwa Asilimia 88 ya deni la nje imedhaminiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na asilimia 12 ilidhaminiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). napenda kujua mikopo/madeni haya mgawanyo wa udhamini unapatikanaje/ ni wapi Zanzibar inaweza kujidhamini na wapi haiwezi.

Mapato-Mapato ya Nje:

1.TZS 265.4 bilioni ni Mikopo na Ruzuku kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo- Ningependa kujua mikopo ni kiasi gani na inatoka wapi, pia ningependa kujua Ruzuku ni kiasi gani na inatoka wapi

2.msamaha wa Madeni wa TZS 1.9 - nani alisamehe deni hili.

Matumizi-Matumizi ya Kazi za Kawaida:
1 . Matumizi ya Mfuko Mkuu wa Serikali TZS 69.8 bilioni - Nini kazi ya mfuko huu.

2.Matumizi mengineyo ya kuendeshea Serikali ni TZS 71.8 bilioni- ni matumizi gani haya na kwa ajili ya nini ?


3. Washirika wa Maendeleo- Hawa ni akina nani ?

4.TZS 199.1 bilioni ni Mikopo- ningependa kujua mlikopa nini, lini na kwa nani ?
 
Last edited by a moderator:
hii nimeichomoachomoa kutoka Bajeti ya serikali ya Zanzibar
[/LIST]

Mkuu ni kushukuru kwanza kwa kunipa ari ya kuitafuta na kuisoma bajeti ya Zanzibar, baada ya kuona extracts zako za bajeti ya JMT. Ni kwa mara ya kwanza nimeweza kuifuatilia bejeti hii ya Zanzibar.

Nikirudi kwenye lengo la kunukuu baadhi ya vipengele vya Bajeti ya Zanzibar, ni kuwa ninaomba unipe ilimu/elimu juu ya haya nitakayouliza(rejea nukuu ya Bajeti ya Zanzibar hapo juu), maana ni kwa mara ya kwanza leo nimefuatilia bajeti hii, Pia naomba uniilimishe kwa lugha nyepesi :

Mapato- Mapato ya ndani:

1. -TRA inakadiriwa kukusanya TZS 166.1 bilioni
Tunaambiwa TRA inafanyakazi Tanzania Bara/Tanganyika tu kwa sasa (huko mna ZRA), TRA hii ya kwenu ni ipi? Je. mapato haya yanakusanywa huko Zanzibar ama yanakusanywa Tanganyika na TRA ya Tanganyika?

2.Mapato yanayotokana na wafanyakazi wa SMT wanaofanya kazi Zanzibar yanakadiriwa kufikia TZS 21.0 bilioni kwa mwaka 2014/15:
Yale ya wafanyakazi wa Zanzibar wanofanya kazi Tanzania bara ni kiasi gani ? jibu hili uwenda likategua kitendewili cha asilimia ya 4.5% ambayo sasa ni 7% ya pato la JMT linalokwenda Zanzibar. Ila ukrasa wa 48 kuna jedwali lina maelezo ya 4.5 % bilioni ni Msaada wa Kibajeti . Sijajua kama hii ndiyo Nguruvi3 huwa anaizungumzia ambayo inatoka Tanganyika.

3. kukopa ndani jumla ya TZS 15.0 bilioni - Hii mna maanisha kukopa kwenye mabenki/ama taasisi nyingine za kifedha yanayofanya kazi zake Zanzibar ama hata yale ya Tanganyika?

4. Ukrasa wa 11 na ule wa 16 wa hotuba hiyo pameandikwa kuwa Zanzibar ilitarajia kupata PAYE kutoka URT (nadhani ni United Republic of Tanzania) TZS 16.2 bilioni (2013/2014) lakini ilipata jumla ya TZS 15.8 bilioni kutokana na Kodi ya wafanyakazi wa Muungano waliopo Zanzibar (PAYE). Je. Mwaka 2014/2015, mapato haya yamesimamishwa kuletwa, maana hayapo kwenye kipengele cha mapato ya serikali...!?

5.Ukrasa wa 24 imeandikwa kuwa Asilimia 88 ya deni la nje imedhaminiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na asilimia 12 ilidhaminiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). napenda kujua mikopo/madeni haya mgawanyo wa udhamini unapatikanaje/ ni wapi Zanzibar inaweza kujidhamini na wapi haiwezi.

Mapato-Mapato ya Nje:

1.TZS 265.4 bilioni ni Mikopo na Ruzuku kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo- Ningependa kujua mikopo ni kiasi gani na inatoka wapi, pia ningependa kujua Ruzuku ni kiasi gani na inatoka wapi

2.msamaha wa Madeni wa TZS 1.9 - nani alisamehe deni hili.

Matumizi-Matumizi ya Kazi za Kawaida:
1 . Matumizi ya Mfuko Mkuu wa Serikali TZS 69.8 bilioni - Nini kazi ya mfuko huu.

2.Matumizi mengineyo ya kuendeshea Serikali ni TZS 71.8 bilioni- ni matumizi gani haya na kwa ajili ya nini ?


3. Washirika wa Maendeleo- Hawa ni akina nani ?

4.TZS 199.1 bilioni ni Mikopo- ningependa kujua mlikopa nini, lini na kwa nani ?
Brilliant!!! Nitashangaa kama utajibiwa. Watu watakimbia halafu wanaibukia eneo jingine na hoja ya JFC haipo. Ngoja tusubiri.
 
Muungano uliopo ni muungano wa KISIASA, sio muungano wa KIUCHUMI. Mfumo wa Muungano wa sasa unaichukulia Zanzibar kama sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sio moja ya nchizi zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Suala la uchumi halipo katika masuala ya muungano, hivyo basi kila kila upande unatakiwa uwe na mawaziri wake wanaosimamia na kutekeleza sera za uchumi na mipango na kila upande ulitakiwa uwe na bajeti yake. Suala la Bandari ni suala la kiuchumi, linahitaji sera ya mipango, uchumi, lakini muhimu Zaidi, mikakati ya kibajeti kupitia sekta husika (Fedha, Miundo Mbinu, Biashara n.k). Ni kwa mantiki hii, naunga hoja ya Nguruvi3 hapo juu.
mkuu niliyasema haya nitarudia tena kuyasema ya kwamba mnatafuta sababu za kisiasa na kiuchumi zaidi kuzungumzia Muungano wetu ilihali tayari imeshaelezwa kwamba muungano wetu ni wa WATU na kwa vile ardhi ni eneo la watu hao wanamoishi ndio maana tumekuwa na nchi mbili. sababu hizi zimeelezwa katika vitabu kibao lakini nyie hamtaki isipokuwa mnachotaka wenyewe.

Mimi nawaelewa vizuri sana madai yenu, lakini nyie mnataka kulazimisha kujenga sababu zenu kuwa ndio muungano maana siasa na Uchumi ni vitu vinavyounda utawala baada ya na sii muungano. Na sababu hizi za Kisiasa na Kiuchumi ndizo zimekawiza hata muungano wa Afrika nzima au hata EAC kwa sababu kila mtu anafikiri muungano ni kama biashara ama ubia unamtazama mwenzako kaingia na kitu gani kumbe Muungano ni kama Yamini ya kuuunda UNDUGU wa watu wake ktk maeneo wanayoishi kama ndoa na sii ubia.

Pili swala la muundo wa serikali, nilisema pia ya kwamba muundo wa serikali 3 sio hoja ya kiuchumi bali ni akili finyu ya kutotazama kwanza mazingira tuliyopo sisi tofauti na nchi nyinginezo na kisha ukachagua kinachoweza kupeleka maendeleo kwa wananchi na sii returns au uta gain nini dhidi ya mwingine kutokana na muundo. Na ukweli ni kwamba matatizo yetu hayatokani na muundo wa serikali isipokuwa tofauti zetu. SCOTLAND hadi leo wanakereka na serikali 2 huko Uingereza, na QUEBEC wanakereka na serikali 3 huko Canada miaka yote. Lakini ukitazama kwa makini wote hawa wameshindwa kutatua tatizo la tofauti zao kama jamii moja (WATU) kutokana na mapungufu ya kiutawala kuunda jamii moja. Serikali ngapi haiundi jamii moja, isipokuwa ni usimamizi wa utekelezaji wa shughuli za serikali.

Nirudi kwetu, Sisi tukiwa na serikali 3, ni muhimu tufuate kanuni za uundwaji wa serikali 3 ambao serikali kuu ndiye mshika mpini. Sawa serikali ndogo zitakuwa na mamlaka ya kupeleka maendeleo kwa wananchi lakini mwenye nguvu ya kukopa na kupitisha mikataba mikubwa ya nje ni serikali kuu maana ndiye anayetambulika nje na hata credit rate yetu inapimwa kwa JMT na sio Tanganyika au Zanzibar. Hapa ndipo penye utata mkubwa na tutakapo liwa mchana kweupe kwa sababu viongozi wetuhawana uzalendo wala uchungu kwa mustakabali wa nchi hii.

Hivyo basi kama nilivyosema serikali ya 3 ambayo ni serikali kuu itakuwa kama mume mwenye wake wawili independent. Tatizo linakuja kwamba fedha zinazopatikana zitamgharamia mke wa kwanza na wa pili lakini pia huyu mume, serikali kuu ya 3 atakuwa na gharama zake ambazo zitatokana na mapato ya hawa wake wawili. Hivyo unapokuwa na serikali kuu gharama za mahitaji yake yatatoka serikali hizi 2 na Tanganyika ndiyo itaumia zaidi kwa sababu Zanzibar hawana watu na pato kubwa wala pato lao haliwezi kuchangia zaidi ya asilimia 5. Hivyo gharama zote za serikali kuu zitakuwa za Tanganyika. Kumbukeni tu sisi kiutamaduni kila mtu ana kwao, mke akiolewa bado ana baba na mama yake na mume ana wazazi vile vile msukumano huo hautaisha kwa kuunda serikali ngapi.

Pili, maadam tuna mfumo wa kibepari hizi serikali kazi yao ni utunzi wa policies na kusimamia utekelezaji, hii serikali kuu itakuwa na mkono mkubwa juu ya ukopeshaji wa fedha za nje na kwa hali ya Ufisadi uliopo nchini, viongozi kukosa kabisa Uzalendo, Uadilifu wala kutowajibika, hizi serikali za Tanganyika na Zanzibar zitakuwa sawa na wake waloolewa ktk ndoa ya abusive na mume mlevi, muhuni na malaya asiyejali maana sote tutakuwa watoto wa nje. Kwa njia moja ama nyingine hawa kina Chengelisious wataweza jificha vizuri ndani ya serikali hiyo ya 3 na wasiulizwe maswali magumu. majibu yao - U HAVE PROBLEM CHECK WITH YOUR GOVERNMENT!

Hii ndio hofu ambayo wengi mnashindwa kuitazama kutokana na kwamba madai yenu ni ya kisiasa zaidi, na hamjui muundo wa serikali 3 huendeshwa vipi na ndio maana madai yenu mnayaweka kuwa ya kisiasa na kiuchumi ktk kuutazama muungano wetu, badala ya kutazama utekelezaji wa serikali hizi una hitilafu gani na wapi kuna matatizo. I will say and say it again kuwa matatizo yetu kisiasa na kiuchumi ni kutokuwa na kutokuwa na UTAWALA BORA. Zile sifa za mwalimu akisema - Ili tuendelee tunahitaji 3.Siasa safi na 4. Uongozi bora - Hakuna for the long time toka mwalimu atutoke!

Zanzibar wataendelea kupiga makelele kutokana na kwamba wao wanajiona tofauti na sisi na sababu kubwa mimi binafsi nadhani ni imani ya DINI kutokana na jinsi wanavyojitetea. Kama wa Quebec na kujiona wao Wafaransa wana tamaduni zao, au Scotland na Udini (Romans) japo wanaficha kama sisi na nchi yetu haina dini.

Hizi ndizo tofauti zitakazo tumeza ama kuvunja muungano sio swala la serikali 2 au 3 ama Wazanzibar hivi ama vile. Serikali 3 sio solution mimi naishi nchi yenye serikali 3 na nawaona Quebec wakiendelea kujiona wao tofauti as a distinct society na tamaduni za Muingereza hivyo ule muungano wa WATU Canada ndipo unapopata matatizo kama tulokuwa nayo sisi. Tukiweza kuondoa Udini sidhani kama swala hili litahitaji muundo wa serikali ngapi..
 
hii nimeichomoachomoa kutoka Bajeti ya serikali ya Zanzibar


[/LIST]

Mkuu ni kushukuru kwanza kwa kunipa ari ya kuitafuta na kuisoma bajeti ya Zanzibar, baada ya kuona extracts zako za bajeti ya JMT. Ni kwa mara ya kwanza nimeweza kuifuatilia bejeti hii ya Zanzibar.

Nikirudi kwenye lengo la kunukuu baadhi ya vipengele vya Bajeti ya Zanzibar, ni kuwa ninaomba unipe ilimu/elimu juu ya haya nitakayouliza(rejea nukuu ya Bajeti ya Zanzibar hapo juu), maana ni kwa mara ya kwanza leo nimefuatilia bajeti hii, Pia naomba uniilimishe kwa lugha nyepesi :

Mapato- Mapato ya ndani:

1. -TRA inakadiriwa kukusanya TZS 166.1 bilioni
Tunaambiwa TRA inafanyakazi Tanzania Bara/Tanganyika tu kwa sasa (huko mna ZRA), TRA hii ya kwenu ni ipi? Je. mapato haya yanakusanywa huko Zanzibar ama yanakusanywa Tanganyika na TRA ya Tanganyika?

2.Mapato yanayotokana na wafanyakazi wa SMT wanaofanya kazi Zanzibar yanakadiriwa kufikia TZS 21.0 bilioni kwa mwaka 2014/15:
Yale ya wafanyakazi wa Zanzibar wanofanya kazi Tanzania bara ni kiasi gani ? jibu hili uwenda likategua kitendewili cha asilimia ya 4.5% ambayo sasa ni 7% ya pato la JMT linalokwenda Zanzibar. Ila ukrasa wa 48 kuna jedwali lina maelezo ya 4.5 % bilioni ni Msaada wa Kibajeti . Sijajua kama hii ndiyo Nguruvi3 huwa anaizungumzia ambayo inatoka Tanganyika.

3. kukopa ndani jumla ya TZS 15.0 bilioni - Hii mna maanisha kukopa kwenye mabenki/ama taasisi nyingine za kifedha yanayofanya kazi zake Zanzibar ama hata yale ya Tanganyika?

4. Ukrasa wa 11 na ule wa 16 wa hotuba hiyo pameandikwa kuwa Zanzibar ilitarajia kupata PAYE kutoka URT (nadhani ni United Republic of Tanzania) TZS 16.2 bilioni (2013/2014) lakini ilipata jumla ya TZS 15.8 bilioni kutokana na Kodi ya wafanyakazi wa Muungano waliopo Zanzibar (PAYE). Je. Mwaka 2014/2015, mapato haya yamesimamishwa kuletwa, maana hayapo kwenye kipengele cha mapato ya serikali...!?

5.Ukrasa wa 24 imeandikwa kuwa Asilimia 88 ya deni la nje imedhaminiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na asilimia 12 ilidhaminiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). napenda kujua mikopo/madeni haya mgawanyo wa udhamini unapatikanaje/ ni wapi Zanzibar inaweza kujidhamini na wapi haiwezi.

Mapato-Mapato ya Nje:

1.TZS 265.4 bilioni ni Mikopo na Ruzuku kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo- Ningependa kujua mikopo ni kiasi gani na inatoka wapi, pia ningependa kujua Ruzuku ni kiasi gani na inatoka wapi

2.msamaha wa Madeni wa TZS 1.9 - nani alisamehe deni hili.

Matumizi-Matumizi ya Kazi za Kawaida:
1 . Matumizi ya Mfuko Mkuu wa Serikali TZS 69.8 bilioni - Nini kazi ya mfuko huu.

2.Matumizi mengineyo ya kuendeshea Serikali ni TZS 71.8 bilioni- ni matumizi gani haya na kwa ajili ya nini ?


3. Washirika wa Maendeleo- Hawa ni akina nani ?

4.TZS 199.1 bilioni ni Mikopo- ningependa kujua mlikopa nini, lini na kwa nani ?

Masuala ni mazuri sana na IshaAllah nitakujibu nikifika nyumbani kwani nitakuwa na reference .

Kuwa na subra
 
Brilliant!!! Nitashangaa kama utajibiwa. Watu watakimbia halafu wanaibukia eneo jingine na hoja ya JFC haipo. Ngoja tusubiri.

Pole saaaana ahali yangu.

Suala la JFC mbona nimeshalimaliza tayari kulisasambua au unahitaji ziada yake?

Ngoja nikupe kiduchu. JMTz haitaweza kutekeleza sharia ya bunge yakuanzshwa JFC kwa kukhofia madaraka ya waziri wa fedhwa wa muungano yatachukuliwa na JFC hivyo yeye atakosa kazi za kufanya.kwani kazi zake zoote zitafanywa na kamishna mkuu wa JFC.

Tupo pamoja hapo au wataka ziada nyingine?

Pole sana
 
Mkandara;11828266]mkuu niliyasema haya nitarudia tena kuyasema ya kwamba mnatafuta sababu za kisiasa na kiuchumi zaidi kuzungumzia Muungano wetu ilihali tayari imeshaelezwa kwamba muungano wetu ni wa WATU na kwa vile ardhi ni eneo la watu hao wanamoishi ndio maana tumekuwa na nchi mbili. sababu hizi zimeelezwa katika vitabu kibao lakini nyie hamtaki isipokuwa mnachotaka wenyewe.
Kwa kuanzia, unaposema tuna nchi mbili ambazo huzitaji hapo tu umeshakosa point ya msingi wa hoja. Pili, muungano wa watu unaweza kuwepo bila kuwa serikali. Zanzibar na Tanganyika zilikuwa na mahusiano miaka dahari. Kilichosababisha muungano ni sababu za kiuchumi na kisiasa. Otherwise tunaweza kuishi bila muungano na watu wakawemo katika ardhi husika bila matatizo.
Mimi nawaelewa vizuri sana madai yenu, lakini nyie mnataka kulazimisha kujenga sababu zenu kuwa ndio muungano maana siasa na Uchumi ni vitu vinavyounda utawala baada ya na sii muungano. Na sababu hizi za Kisiasa na Kiuchumi ndizo zimekawiza hata muungano wa Afrika nzima au hata EAC kwa sababu kila mtu anafikiri muungano ni kama biashara ama ubia unamtazama mwenzako kaingia na kitu gani kumbe Muungano ni kama Yamini ya kuuunda UNDUGU wa watu wake ktk maeneo wanayoishi kama ndoa na sii ubia.
Kama si sababu za kiuchumi na kisiasa tusingekuwa na India, pakistan na Bangladeshi kama nchi tofauti.

Tusingekuwa na Eritrea na Ethiopia. Wala tusingekuwa na Egypt na Syria au Ogaden na Somalia. Senegambia walijaribu kwa mahaba, leo wapo wapi?

Tusingekuwa na EU au mataifa ya ulaya yenye vinchi vidogo sana. Hakuna muungano unaotokea tu kwasababu ya mahaba.

Muungano lazima uwe na sababu na hapa ni za kiuchumi na kisiasa. Huko nyuma muungano ulilenga zaidi kisiasa, siku hizi hakuna muungano bila uchumi. Uchumi si biashara tu ni ulinzi, na sababu za ulinzi nyingi ni za kisiasa.

Hivyo uchumi umechukua nguvu ya siasa kutokana na umuhimu wake katika karne ya sasa. Kumbuka uchumi ndio nguvu katika dunia ya sasa.Kama muungano ni Yamini, kwanini tusile Yamini na wakongo au Wazambia, simple as that!
Pili swala la muundo wa serikali, nilisema pia ya kwamba muundo wa serikali 3 sio hoja ya kiuchumi bali ni akili finyu ya kutotazama kwanza mazingira tuliyopo sisi tofauti na nchi nyinginezo na kisha ukachagua kinachoweza kupeleka maendeleo kwa wananchi na sii returns au uta gain nini dhidi ya mwingine kutokana na muundo.Nirudi kwetu, Sisi tukiwa na serikali 3, ni muhimu tufuate kanuni za uundwaji wa serikali 3 ambao serikali kuu ndiye mshika mpini. Sawa serikali ndogo zitakuwa na mamlaka ya kupeleka maendeleo kwa wananchi lakini mwenye nguvu ya kukopa na kupitisha mikataba mikubwa ya nje ni serikali kuu maana ndiye anayetambulika nje na hata credit rate yetu inapimwa kwa JMT na sio Tanganyika au Zanzibar. Hapa ndipo penye utata mkubwa na tutakapo liwa mchana kweupe kwa sababu viongozi wetuhawana uzalendo wala uchungu kwa mustakabali wa nchi hii.
Hapa unaongea na wazanzibar nadhani. Kwa miaka mingi kama tunavyoonyesha znz imepewa kipaumbele ili kupata maendeleo.

Kwamba, ni kisehemu kidogo sana cha nchi kinachochukua sehemu kubwa sana ya pato la nchi kuliko eneo jingine.

Pamoja na hayo, malalamiko yao yamekuwa kunyonywa na kuonewa. Kwa maneno mengine wanalalamika kuwa wanachokiweka si sawa na wanchopata.

Hapo ndipo Tanganyika inakuja na kusema, wait a minute, kwani unaweka nini wewe? Jibu hakuna wanachoweka.

Sasa kama hakuna wanchoweka kwanini wanakuwa source ya distabilization ya taifa?

Kama hoja yako inasimama katika ukweli, basi wewe usingesimama jamvini mara 10 ukisema znz inanyimwa misaada na mikopo.

Ndio msingi wa Watanganyika kuweka wazi kuwa hakuna kunyimwa wala kuonewa. Na njia rahisi ni kutenganisha mambo ili kuwe na weupr katika kile kinachopataikana na kile kinachotoka. Bila hivyo znz itakuwa ni tatizo kwa taifa, na Tanganyika itatumia rasilimali zake nyingi kuwatuliza. Limeshindikana miaka 48 sijui kama litawezekana.
Hivyo unapokuwa na serikali kuu gharama za mahitaji yake yatatoka serikali hizi 2 na Tanganyika ndiyo itaumia zaidi kwa sababu Zanzibar hawana hata nayo wala pato lao haliwezi kuchangia zaidi ya asilimia 5. Hivyo gharama zote za serikali kuu zitakuwa za Tanganyika. Kumbukeni tu sisi kiutamaduni kila mtu ana kwao, mke akiolewa bado ana baba na mama yake na mume ana wazazi vile vile msukumano huo hautaisha kwa kuunda serikali ngapi.
Si kweli! Kwasasa gharama ni kubwa sana kuliko S3.

Hoja hapa si kuchangia, ni kuwa na fairness.
Rasimu ya Warioba imeonyesha mapato na matumizi ya serikali kuu ambayo ni machache kuliko ya S2 za sasa.

Kwa watu wasioona, wanadhani kuwa gharama za muungano ni pungufu kwa S2.

Si kweli, tutakapokuwa na S3 tutakuwa tumepunguza gharama sana.
Unachoogopa kusema ni kuwa mzigo utapungua kwa Tanganyika.

Nitakupa mfano. Kwasasa znz inaapta 7% ya pato tusilojua ni la Tanganyika au bajeti ya Tanganyika.

Tunajua si mikopo na misaada bali pato la Tanganyika. Tunajua znz inapata 1.75Bilioni kila mwezi kutoka Tanganyika.
Tunajua znz haina bajreti ya mambo mazito kama ulinzi na usalama, mambo ya ndani, nje na taasisi za muungano.

Hivyo unaposema S3 ni kuongeza gharama, labda kama unasema kwa upande wa znz.

Kwa upande wa Tanganyika itapunguza mzigo mzito wa kuhudumia muungano.

Ukisoma rasimu ya Warioba mambo ya muungano ni 7. Ukisoma riwaya ya Chenge mambo ni 16 ambayo ukiyanyumbulisha ni kama 21.
Ni juha pekee anayeweza kudhani kuwa huduma kwa mambo 21 ni rahisi kuliko mambo 7.

Hadi wakati huu Tanganyika ndiyo emebeba muungano.

Sijui, labda ueleze uwepo wa S3 utaongeza nini ambachoTanganyika haikibebi sasa hivi.

Sana sana utasaidia kupunguza gharama zisizo na maana anazobeba Mtanganyika.

Ndani ya S2 inaonekana kuna unafuu wa gharama kwasababu znz ina jina na hivyo kuona kuna msaada(tupo wawili)

Ukweli ni kuwa S2 znz imejificha tu hakuna msaada. Sasa wangekaa kimya ingeweza kujenga hoja, wanapokuwa mstari wa mbele wa kudai kisicho chao kama haki ndipo Watanganyika wanapochemka na hapo muungano upo ukiongoni.

Nakupa challenge, tuonyeshe S2 inapunguza vipi gharama Vs serikali 3.

Sisi tutakuonyesha S3 zinapunguza vipi gharama.
 
hii nimeichomoachomoa kutoka Bajeti ya serikali ya Zanzibar
[/LIST]

Mkuu ni kushukuru kwanza kwa kunipa ari ya kuitafuta na kuisoma bajeti ya Zanzibar, baada ya kuona extracts zako za bajeti ya JMT. Ni kwa mara ya kwanza nimeweza kuifuatilia bejeti hii ya Zanzibar.

Nikirudi kwenye lengo la kunukuu baadhi ya vipengele vya Bajeti ya Zanzibar, ni kuwa ninaomba unipe ilimu/elimu juu ya haya nitakayouliza(rejea nukuu ya Bajeti ya Zanzibar hapo juu), maana ni kwa mara ya kwanza leo nimefuatilia bajeti hii, Pia naomba uniilimishe kwa lugha nyepesi :

Mapato- Mapato ya ndani:

1. -TRA inakadiriwa kukusanya TZS 166.1 bilioni
Tunaambiwa TRA inafanyakazi Tanzania Bara/Tanganyika tu kwa sasa (huko mna ZRA), TRA hii ya kwenu ni ipi? Je. mapato haya yanakusanywa huko Zanzibar ama yanakusanywa Tanganyika na TRA ya Tanganyika?

2.Mapato yanayotokana na wafanyakazi wa SMT wanaofanya kazi Zanzibar yanakadiriwa kufikia TZS 21.0 bilioni kwa mwaka 2014/15:
Yale ya wafanyakazi wa Zanzibar wanofanya kazi Tanzania bara ni kiasi gani ? jibu hili uwenda likategua kitendewili cha asilimia ya 4.5% ambayo sasa ni 7% ya pato la JMT linalokwenda Zanzibar. Ila ukrasa wa 48 kuna jedwali lina maelezo ya 4.5 % bilioni ni Msaada wa Kibajeti . Sijajua kama hii ndiyo Nguruvi3 huwa anaizungumzia ambayo inatoka Tanganyika.

3. kukopa ndani jumla ya TZS 15.0 bilioni - Hii mna maanisha kukopa kwenye mabenki/ama taasisi nyingine za kifedha yanayofanya kazi zake Zanzibar ama hata yale ya Tanganyika? ?

Jitegemee,

Nikianza na suala lako la mwanzo ni KUWA TRA CHOMBO CHA MUUNGANO NA KINAFANYA KAZI ZNZ NA TGK kukusanya kodi zote za Serikali ya JMTz.
ZRB sio ZRA kwa maana ya Znz Revenue Board ni chombo kinachokusanya kodi zote za SMZ.

2. Mapato ya wafanyakazi wa Znz wanaofanyakazi katika taasisi , Idara na wizara za muungano JMTz PAYE hizo zimebainishwa katika bajeti hiyo hiyo imebainishwa katika fungu la mapato.

Hili la mgawo kwa Znz 7% nafikiri nimelisasambua kwa kina sana huko nyuma lakin kifupi bajeti za nchi hizo mbili yaani TGK na Znz zote TEGEMEZI zinategemea misaada na mikopo ili ziweze kujitosheleza.

Nilisema kuwa hiyo 4.5% ni pesa za msaada wa kibajeti ZINAZOTOKANA NA MIKOPO NA MISAADA KUTOKA NJE. Pitia bandiko no 309 nimeweka bayana yake hapo.

3. Mikopo ya ndani maana yake ni kukopa katika taasisi za fedhwa na mabenk ya ndani. Kwa Znz inajumuisha ZSSF etc au PBZ na mengineyo yanayofanya kazi Znz.



4. Ukrasa wa 11 na ule wa 16 wa hotuba hiyo pameandikwa kuwa Zanzibar ilitarajia kupata PAYE kutoka URT (nadhani ni United Republic of Tanzania) TZS 16.2 bilioni (2013/2014) lakini ilipata jumla ya TZS 15.8 bilioni kutokana na Kodi ya wafanyakazi wa Muungano waliopo Zanzibar (PAYE). Je. Mwaka 2014/2015, mapato haya yamesimamishwa kuletwa, maana hayapo kwenye kipengele cha mapato ya serikali...!?

5.Ukrasa wa 24 imeandikwa kuwa Asilimia 88 ya deni la nje imedhaminiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na asilimia 12 ilidhaminiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). napenda kujua mikopo/madeni haya mgawanyo wa udhamini unapatikanaje/ ni wapi Zanzibar inaweza kujidhamini na wapi haiwezi.

4. Suala hilo la PAYE kutoka JMTz kutokana na wafanyakazi wake katika taasisi, idara na wizara za muungano kwa 2014/15 kuwa halipo kama mapato. Hakika hilo sina ujuzi nalo na siwezi kutoa jibu kuwa hayaletwi au kwanini yamesimamishwa.

5. Kwa mujibu wa mkataba wa muungano wa JMTz baina ya Tgk na Znz, mambo yoooote ya Nje ni suala la muungano. Hivyo Znz haiwezi kukopa au hata kupata msaaada kutoka nje bila JMTz kuidhinisha. Na Znz haiwezi kujidhamini kwa deni la nje.

12% ya Mkopo wa nje Znz imejidhamini hiyo inatokana na makubaliano baina yake na JMTz. Ikumbukwe kuwa kuna kima ambacho akiruhusiwi kuzidi 7% ya deni lote la JMTz. Lakin Mikopo hii mara nyingi inakuwa na muda mrefu na kwa ajili ya special project. Hivyo Znz ili overdraft huo mkopo ili itekeleze miradi yake kwa mwaka 2013/14 na hivyo itasaidia mikopo hiyo kupungua katika mwaka 2014/15.

Hivyo katika lugha ya KIHASIBU tunapeleka kusema kuwa Znz imejidhamini yenyewe japo imedhaminiwa na JMTz lakin katika mwaka 2014/15 itakopa kidogo ili kufidia mkopo huo katika mwaka huu wa fedhwa.

Mapato-Mapato ya Nje:
1.TZS 265.4 bilioni ni Mikopo na Ruzuku kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo- Ningependa kujua mikopo ni kiasi gani na inatoka wapi, pia ningependa kujua Ruzuku ni kiasi gani na inatoka wapi

2.msamaha wa Madeni wa TZS 1.9 - nani alisamehe deni hili.
  1. Hilo limebainishwa katika bajeti ya Znz katika hotba hiyo hiyo katika kipengele cha misaada na mikopo ya masharti ya kibiashara. Soma vizuri imewekwa bayana.
  2. Msamaha wa DENI la nje hii inatolwa katika 7% ya deni ambalo JMTz inakuwa imesamehewa.
Kumbuka kuwa hiyo 7% Znz anayochukua ni DENI na laazima alilipe. Sasa JMTz ikisamehewa basi the 7 % ya msamaha huo wanasamehewa Znz. Kwani kila mtu anapokopa ni laazima alipe kutokana na deni lake.
Haiwezekani TGK ikakopa alafu deni hilo apewe Znz. Kwani hizo zote ni nchi huru japo zimeungana. Kinachoangaliwa na wachumi ikiwa muungano utavunjika laazima kila mtu ajue deni lake na laazima alilipe.

Matumizi-Matumizi ya Kazi za Kawaida:
1 . Matumizi ya Mfuko Mkuu wa Serikali TZS 69.8 bilioni - Nini kazi ya mfuko huu.

2.Matumizi mengineyo ya kuendeshea Serikali ni TZS 71.8 bilioni- ni matumizi gani haya na kwa ajili ya nini ?


3. Washirika wa Maendeleo- Hawa ni akina nani ?

4.TZS 199.1 bilioni ni Mikopo- ningependa kujua mlikopa nini, lini na kwa nani ?
1& 2 hayo ni matumizi ya kila siku ya kuendeshea Serikali na taasisi zake. Kumbuka katika bajeti kunakuwa na mafungu mawili tu.

  1. Matumizi ya kawaida ya Serikali
  2. Matumizi ya maendeleo.

WASHIRIKA WA MAENDELEO hawa ninchi, taasisi zote za nje mnazoshirikiana nazo katika kukuza maendeleo ya nchi . Hawa ndio wadau wakuu wa maendeleo ya nchi yenu wanaosaidia au kufadhwili sekta mbalimbali za maendeleo kama kilimo, afya, miundombinu etc.
MIKOPO hili ni suala la lazima kwa JMTz na Znz kwani bajeti zao haziwezi kujitosheleza. Hivyo Sehemu kubwa ya mikopo hiyo inatumika katika sekta ya maendeleo ya kiuchumi katika sekta za afya, kilimo, miundombinu etc.

Kujua zilikopwa lini hilo ni vizuri pitia bajeti mija moja za mika ya nyumba na utekelezaji wa bajeti hiyo utakuja kujua na hata kufikia kujua kuwa Znz inadaiwa kiasi gani cha mukopo ya nje.

JMTz mpaka kufikia 31st April 2014 ilikuwa inadaiwa pesa za nje zaidi ya TSh 38 Tril.
 
jitegemee njoo usome majibu! TRA uliyouliza inakusanya mapato ya znz na kuyapeleka wapi, imekimbiwa.
Mengine hana ujuzi nayo bado anayaongelea. Wamemkimbia wanasubiri mada isonge mbele waje na wimbo wao.
 
Kwa kuanzia, unaposema tuna nchi mbili ambazo huzitaji hapo tu umeshakosa point ya msingi wa hoja. Pili, muungano wa watu unaweza kuwepo bila kuwa serikali. Zanzibar na Tanganyika zilikuwa na mahusiano miaka dahari. Kilichosababisha muungano ni sababu za kiuchumi na kisiasa. Otherwise tunaweza kuishi bila muungano na watu wakawemo katika ardhi husika bila matatizo. Kama si sababu za kiuchumi na kisiasa tusingekuwa na India, pakistan na Bangladeshi kama nchi tofauti.

Tusingekuwa na Eritrea na Ethiopia. Wala tusingekuwa na Egypt na Syria au Ogaden na Somalia. Senegambia walijaribu kwa mahaba, leo wapo wapi?

Tusingekuwa na EU au mataifa ya ulaya yenye vinchi vidogo sana. Hakuna muungano unaotokea tu kwasababu ya mahaba.

Muungano lazima uwe na sababu na hapa ni za kiuchumi na kisiasa. Huko nyuma muungano ulilenga zaidi kisiasa, siku hizi hakuna muungano bila uchumi. Uchumi si biashara tu ni ulinzi, na sababu za ulinzi nyingi ni za kisiasa.

Hivyo uchumi umechukua nguvu ya siasa kutokana na umuhimu wake katika karne ya sasa. Kumbuka uchumi ndio nguvu katika dunia ya sasa.Kama muungano ni Yamini, kwanini tusile Yamini na wakongo au Wazambia, simple as that! Hapa unaongea na wazanzibar nadhani. Kwa miaka mingi kama tunavyoonyesha znz imepewa kipaumbele ili kupata maendeleo.

Kwamba, ni kisehemu kidogo sana cha nchi kinachochukua sehemu kubwa sana ya pato la nchi kuliko eneo jingine.

Pamoja na hayo, malalamiko yao yamekuwa kunyonywa na kuonewa. Kwa maneno mengine wanalalamika kuwa wanachokiweka si sawa na wanchopata.

Hapo ndipo Tanganyika inakuja na kusema, wait a minute, kwani unaweka nini wewe? Jibu hakuna wanachoweka.

Sasa kama hakuna wanchoweka kwanini wanakuwa source ya distabilization ya taifa?

Kama hoja yako inasimama katika ukweli, basi wewe usingesimama jamvini mara 10 ukisema znz inanyimwa misaada na mikopo.

Ndio msingi wa Watanganyika kuweka wazi kuwa hakuna kunyimwa wala kuonewa. Na njia rahisi ni kutenganisha mambo ili kuwe na weupr katika kile kinachopataikana na kile kinachotoka. Bila hivyo znz itakuwa ni tatizo kwa taifa, na Tanganyika itatumia rasilimali zake nyingi kuwatuliza. Limeshindikana miaka 48 sijui kama litawezekana. Si kweli! Kwasasa gharama ni kubwa sana kuliko S3.

Hoja hapa si kuchangia, ni kuwa na fairness.
Rasimu ya Warioba imeonyesha mapato na matumizi ya serikali kuu ambayo ni machache kuliko ya S2 za sasa.

Kwa watu wasioona, wanadhani kuwa gharama za muungano ni pungufu kwa S2.

Si kweli, tutakapokuwa na S3 tutakuwa tumepunguza gharama sana.
Unachoogopa kusema ni kuwa mzigo utapungua kwa Tanganyika.

Nitakupa mfano. Kwasasa znz inaapta 7% ya pato tusilojua ni la Tanganyika au bajeti ya Tanganyika.

Tunajua si mikopo na misaada bali pato la Tanganyika. Tunajua znz inapata 1.75Bilioni kila mwezi kutoka Tanganyika.
Tunajua znz haina bajreti ya mambo mazito kama ulinzi na usalama, mambo ya ndani, nje na taasisi za muungano.

Hivyo unaposema S3 ni kuongeza gharama, labda kama unasema kwa upande wa znz.

Kwa upande wa Tanganyika itapunguza mzigo mzito wa kuhudumia muungano.

Ukisoma rasimu ya Warioba mambo ya muungano ni 7. Ukisoma riwaya ya Chenge mambo ni 16 ambayo ukiyanyumbulisha ni kama 21.
Ni juha pekee anayeweza kudhani kuwa huduma kwa mambo 21 ni rahisi kuliko mambo 7.

Hadi wakati huu Tanganyika ndiyo emebeba muungano.

Sijui, labda ueleze uwepo wa S3 utaongeza nini ambachoTanganyika haikibebi sasa hivi.

Sana sana utasaidia kupunguza gharama zisizo na maana anazobeba Mtanganyika.

Ndani ya S2 inaonekana kuna unafuu wa gharama kwasababu znz ina jina na hivyo kuona kuna msaada(tupo wawili)

Ukweli ni kuwa S2 znz imejificha tu hakuna msaada. Sasa wangekaa kimya ingeweza kujenga hoja, wanapokuwa mstari wa mbele wa kudai kisicho chao kama haki ndipo Watanganyika wanapochemka na hapo muungano upo ukiongoni.

Nakupa challenge, tuonyeshe S2 inapunguza vipi gharama Vs serikali 3.

Sisi tutakuonyesha S3 zinapunguza vipi gharama.
Unajua kuzungumza na wewe ni sawa na kumfukuza kichaa nikiwa uchi bora nikuache na hadith zenu endeleeni na fikra za kusadikika! I thought jukwaa hili lina watu great thinker kumbe nimejaa Great Sinker!
And who are they. Sinker will fall for anything out there and they did, hook and sinker!
 
Unajua kuzungumza na wewe ni sawa na kumfukuza kichaa nikiwa uchi bora nikuache na hadith zenu endeleeni na fikra za kusadikika! I thought jukwaa hili lina watu great thinker kumbe nimejaa Great Sinker!
And who are they. Sinker will fall for anything out there and they did, hook and sinker!
Mkuu kinachoongelewa hapa ni hoja. Tumekujibu hoja zako na pengine ungettuelewesha kama hatuelewi.

Hatuwezi kukaa kimya hata pale tunapoona unapotosha. Unaposema mfano wa Canada na Tanzania ni sawa, tutasema hapana! Unaposema issue siyo uchumi, wakati madai ya wznz ni kuhusu kuonewa kiuchumi nawe ukiwasadidia katika mikopo na misaada, tuakwambia no, uchumi ndilo tatizo.

Ukitaka tuamini kuwa znz inaonewa, tutakuonyesha haionewei.
Ukisema S2 ni nafuu kuliko 3, tutakuuliza, tuonyeshe unafuu ulipo.

Nashangaa kukuuliza utuonyeshe unafuu wa S2 unakuwa mbogo. Ni hoja mkuu, matusi na kashfa hazina nafasi.

Unataka kubabaisha umma kuwa unaishi Canada, wakati mfumo wenyewe huelewi. Hakuna wabunge wa majimbo wanaoingia federal gov na hakuna wa fed wanoingia majimboni. Tanzania si Canada, mfumo upo tofauti na hakuna mwingine kama huu duniani.

Ulipokuja na hoja ya bima ya afya, tuliweka sawa hata pale usipopajua ingawa unatumia bima hiyo.Tunausaidia umma dhidi ya wapotoshaji na wababaishaji.

Tunakwenda kwa hoja. 'If you can't take the heat get out of the kitchen'
 
jitegemee njoo usome majibu! TRA uliyouliza inakusanya mapato ya znz na kuyapeleka wapi, imekimbiwa.
Mengine hana ujuzi nayo bado anayaongelea. Wamemkimbia wanasubiri mada isonge mbele waje na wimbo wao.

Nguruvi3,

Punguza munkar, chuki na jazba na pupa ya kuyaendea mambo. Ni vizuri kama utatuliza mwili na akili zako na kuruhusu hewa ipite kwa wingi katika ubongo kisha kusoma tartiiiibu kwa NIA YA KUELEWA na SIO KUPINGA na insh'Allah darsa utalipata.

Kwa kukusaidia, Suala la TRA nimelijibu vilivyo kabisa. Nimesema hivi TRA inakusanya kodi zote za JMTZ na makusanyo hayo yanawakilishwa katika wizara ya fedhwa Muungano. ZRB inakusanya mapato yote ya Znz na makusanyo hayo yanapelekwa hazina Znz.

Kwa nyongeza zaidi pesa wanazokusanya TRA zitaonekana katika bajeti ya muungano wa JMTz na pesa wanazokusanya ZRB zitaonekana katika bajeti ya nchi ya Znz.


Kwa kukusaidia zaidi mfumo wanaotumia TRA na ZRB katika kukusanya mapato katika Znz ni sawa kabisa na mfumo unaotumiwa na Halmashauri za JMTz na Serikali kuu katika kukusanya ushuru katika halmashauri.

Kama utatembea utaona vizuizi vya ukaguzi wa mazao na maliasili za misitu sehemu mbali mbali katika barabara za JMTz. hapo utaona kuna Kodi utalipia halmashauri na Kodi unalipia serikali kuu. Mfano mzuri pita pale Vikindu njia ya kwenda mkuranga au Kibiti wilaya ya Rufiji njia kwenda Lindi. utaona hivyo.

Kwa jibu fupi pesa inayokusanywa na TRA znz inapelekwa hazina JMTz na kwa mwaka 2014/2015 TRA wanakusudia kukusanya Mapato ya kodi Tsh 11,318,222/= kwa mujibu wa makadirio ya bajeti ya 2014/15.

Na hapo niliposema sina ujuzi napo hilo ni suala la kisera na kaanun ambazo zinabadilika kila kukicha. Kwa muungwana kama kitu hafahamu basi anasema bayana SINA Ujuzi nalo hilo.

kama unazaidi na wewe katika kiu yako ya JFC au 4.5% mgawo wa Znz basi karibu saana.

Pole saana

 
Unajua kuzungumza na wewe ni sawa na kumfukuza kichaa nikiwa uchi bora nikuache na hadith zenu endeleeni na fikra za kusadikika! I thought jukwaa hili lina watu great thinker kumbe nimejaa Great Sinker!
And who are they. Sinker will fall for anything out there and they did, hook and sinker!

Mkandara,

Mimi nakunasihi ahali yangu TUZIDI KUMSAIDIA Nguruvi3 katika upambanuzi wa mambo. Japo ana ilmu kiduchu lakin ana kiu kubwa ya kutaka kujua mambo haya hususan ya kijamii kama siasa na uchumi ingawa na mvivu wa kutafuta material au kwenda skuli.

Ni laazima tufahamu kuwa NI VIZURI KUWA NA WATU HAWA NDANI WAKIKOJOLEA NJE KULIKO KUWA NAO NJE WAKIKOJOLEA NDANI.

Tuzidi kumpa darsa na insh'Allah siku moja atafahamu tu japo mwenyewe ana masikio lakin anajifanya asikii, ana macho anajifanya aoni na ana pua anajifanya hawezi kunusa.

Pamoja na kumpa polee lakin tuzidi kumsaidia.

Nakunasihi zidi kumpa darsa kwani tupo wengi sana tunafyonza ilmu na upambanuzi wako.

Ahlan wa sahalan Mkandara.

 
Back
Top Bottom