Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 10,502
- 16,712
Kushindwa kwa Urusi kuiteka Ukraine kwa haraka na kukimbizwa Marekani kule Afghanistan na wanamgambo wa Taliban kumedhihirisha kwa mara nyengine kuwa kwa sasa dunia hakuna tena taifa kubwa.
Baada ya Urusi kupeleka msururu mrefu wa vikosi vya jeshi vinavyofikia kilomita 4 kuuzunguka mji mkuu wa Ukraine,Kiyv tulitaraji shughuli ingekuwa imekamilika si zaidi ya wiki.Kumbe sehemu kubwa ya ule msururu wa jeshi umeangamia mikononi mwa askari wa Ukraine.
Pamoja na hilo hata wale askari wa Urussi waliosalimika wamerudi mikono mitupu bila vifaru vyao na silaha nyengine muhimu katika jeshi hilo.
Inasemekana mtambo muhimu wa kuongoza jeshi nao umechukuliwa na Ukraine na wameahidi kuupeleka Marekani ili kufichua siri zake.
Hii si mara ya mwanzo kwa Urusi kurudishwa nyuma katika vita namna hii.Mara ya mwanzo ni 1979 kule Afghanistan ambako vifaru vyao vingi na askari walipotea na hata wingu la ndege za kijeshi angani havikusaidia.
Safari nyengine ni kule Chechnya mwaka 2006 ambako hatimae walilazimika kutumia mbinu ya kuwagawa wachechnya badala ya kupigana nao.
Marekani kwa upande mwengine imeshindwa kabisa kupigana wala kuwaondoa madarakani viongozi kadhaa mahasimu dhidi yao mfano Venezuela,Syria,Irani,Korea kaskazini n.k.
Wamelazimika kufanya unyama mkubwa katika nchi za Iraq na Libya ambazo nazo zote wananchi wake hawajaridhika kukaliwa na taifa hilo na ndio maana kila siku wakipata fursa wanalipiza kisasi kinachopelekea Marekani kurudi nyuma.
Baada ya Urusi kupeleka msururu mrefu wa vikosi vya jeshi vinavyofikia kilomita 4 kuuzunguka mji mkuu wa Ukraine,Kiyv tulitaraji shughuli ingekuwa imekamilika si zaidi ya wiki.Kumbe sehemu kubwa ya ule msururu wa jeshi umeangamia mikononi mwa askari wa Ukraine.
Pamoja na hilo hata wale askari wa Urussi waliosalimika wamerudi mikono mitupu bila vifaru vyao na silaha nyengine muhimu katika jeshi hilo.
Inasemekana mtambo muhimu wa kuongoza jeshi nao umechukuliwa na Ukraine na wameahidi kuupeleka Marekani ili kufichua siri zake.
Hii si mara ya mwanzo kwa Urusi kurudishwa nyuma katika vita namna hii.Mara ya mwanzo ni 1979 kule Afghanistan ambako vifaru vyao vingi na askari walipotea na hata wingu la ndege za kijeshi angani havikusaidia.
Safari nyengine ni kule Chechnya mwaka 2006 ambako hatimae walilazimika kutumia mbinu ya kuwagawa wachechnya badala ya kupigana nao.
Marekani kwa upande mwengine imeshindwa kabisa kupigana wala kuwaondoa madarakani viongozi kadhaa mahasimu dhidi yao mfano Venezuela,Syria,Irani,Korea kaskazini n.k.
Wamelazimika kufanya unyama mkubwa katika nchi za Iraq na Libya ambazo nazo zote wananchi wake hawajaridhika kukaliwa na taifa hilo na ndio maana kila siku wakipata fursa wanalipiza kisasi kinachopelekea Marekani kurudi nyuma.
