CONTROLA
JF-Expert Member
- Sep 15, 2019
- 7,087
- 23,870
Nilikuaga sielewi kwanini kuna sehemu ukipita huruhusiwi kupiga picha, nilikuwa hata sijui kwanini. Nilikuwa sifahamu kwanini familia flani flani hasa za kifalme sio watu wapenda mapicha picha, kujionyesha onyesha.Nilikuwa sitambui kwanini yote hayo ni "marufuku" kwa aina flani ya watu nilidhani tu sababu ya vyeo na nyadhifa zao.
Lakini sasa nimeelewa kwanini yote hayo yalikuwa yanafanyika, na ninakubaliana nao kuwa walikuwa na wapo sawa hata na sasa. Wote ni mashahidi jukwaaa la MMU watu wakitafuta wapenzi, kwenye social networks tofauti watu wakitafuta wapenzi. Picha nyingi zimekuwa zikitumika huko, na nyingi kati ya picha zinazotomika si za wahusika wenye picha wenyewe na wala wao hata hawajui.
Kama kuna jitu lipo huku linatumia picha yake kudanganya watu, matukio ya namna hiyo ni mengi sana. Umeshawahi kukaa chini ukajiuliza hizo picha wanazitoa wapi? Jibu najua unalo ni humu humu mitandaoni kwenye hizi social media. Ndugu zanguni yawezekana hujawahi ona picha yako ikiandikiwa tangazo ndio mana unaona kama hii haikuhusu ila nataka tu kukwambia "ipo siku".
Ipo nini nimesema? (in teacher mpamire's voice)
Nataka kukwambia nini wewe dada wewe kaka hebu leo kata mazoea ya kujipost post huko kwenye mitandao, kama unapenda picha fanya kama walivyokuwa wanafanya wazazi wetu zamani, nenda studio piga picha safisha weka kwa album, kwa kuwa unapenda show off (wageni wakija wape waangalie).
Wakiondoka si wataacha album nyumbani fresh "You are safe" ila usije ukajidanganya kwamba wewe utaendelea kupost picha tu kwasababu haupost picha mbaya.
Unajipa moyo kuwa unavaa kiheshima kwahiyo huoni uoga kujipost (my dear upo hatarini) hivi umesahau tuko ulimwengu wa teknohama eeeh umesahau.
Si eti, unataka jitoa ufahamu hujawahi ona editing wanazofanyiwa watu (acha ni assume hujawahi). Sasa nikwambie kitu, achana na kupost mapicha kwenye masocial media, ipo day moko utanikumbuka nakwambia tena.
Wengine mnawapost watoto zenu aseee mnakosea nasema mnakosea (mnawaonea hao watoto mnajua) subirini wakikua wajiamulie maisha yao.
Usimpost mwanao wewe mama, usimpost mwanao wewe baba kaa na mwanao ndani jaribuni kuelewa hata kwa ufupi somo lile la "privacy and security".
Mimi leo hiii kuna picha zangu nilizipost kwenye akaunt zangu mahali mahali flani, sasa nimesahau password ya kule, bwana wee shida ninayopata kuzitoa zile picha kule zilipo si ndogo.
Sikulazimishi unielewe kama kawaida yangu mimi naandika ila uamuzi ni wako.
Ukiamua kusoma tu ukiamua kusoma na bila kuchukua hatua ni wewe, ila mpaka siku utakapokutana na picha ako imeeditiwa vilivyo ndio tutakumbukana.
Nime Finish.
Lakini sasa nimeelewa kwanini yote hayo yalikuwa yanafanyika, na ninakubaliana nao kuwa walikuwa na wapo sawa hata na sasa. Wote ni mashahidi jukwaaa la MMU watu wakitafuta wapenzi, kwenye social networks tofauti watu wakitafuta wapenzi. Picha nyingi zimekuwa zikitumika huko, na nyingi kati ya picha zinazotomika si za wahusika wenye picha wenyewe na wala wao hata hawajui.
Kama kuna jitu lipo huku linatumia picha yake kudanganya watu, matukio ya namna hiyo ni mengi sana. Umeshawahi kukaa chini ukajiuliza hizo picha wanazitoa wapi? Jibu najua unalo ni humu humu mitandaoni kwenye hizi social media. Ndugu zanguni yawezekana hujawahi ona picha yako ikiandikiwa tangazo ndio mana unaona kama hii haikuhusu ila nataka tu kukwambia "ipo siku".
Ipo nini nimesema? (in teacher mpamire's voice)
Nataka kukwambia nini wewe dada wewe kaka hebu leo kata mazoea ya kujipost post huko kwenye mitandao, kama unapenda picha fanya kama walivyokuwa wanafanya wazazi wetu zamani, nenda studio piga picha safisha weka kwa album, kwa kuwa unapenda show off (wageni wakija wape waangalie).
Wakiondoka si wataacha album nyumbani fresh "You are safe" ila usije ukajidanganya kwamba wewe utaendelea kupost picha tu kwasababu haupost picha mbaya.
Unajipa moyo kuwa unavaa kiheshima kwahiyo huoni uoga kujipost (my dear upo hatarini) hivi umesahau tuko ulimwengu wa teknohama eeeh umesahau.
Si eti, unataka jitoa ufahamu hujawahi ona editing wanazofanyiwa watu (acha ni assume hujawahi). Sasa nikwambie kitu, achana na kupost mapicha kwenye masocial media, ipo day moko utanikumbuka nakwambia tena.
Wengine mnawapost watoto zenu aseee mnakosea nasema mnakosea (mnawaonea hao watoto mnajua) subirini wakikua wajiamulie maisha yao.
Usimpost mwanao wewe mama, usimpost mwanao wewe baba kaa na mwanao ndani jaribuni kuelewa hata kwa ufupi somo lile la "privacy and security".
Mimi leo hiii kuna picha zangu nilizipost kwenye akaunt zangu mahali mahali flani, sasa nimesahau password ya kule, bwana wee shida ninayopata kuzitoa zile picha kule zilipo si ndogo.
Sikulazimishi unielewe kama kawaida yangu mimi naandika ila uamuzi ni wako.
Ukiamua kusoma tu ukiamua kusoma na bila kuchukua hatua ni wewe, ila mpaka siku utakapokutana na picha ako imeeditiwa vilivyo ndio tutakumbukana.
Nime Finish.

