Papupi
JF-Expert Member
- Feb 3, 2014
- 2,029
- 3,245
SEHEMU YA 85
Moyo wake ulimuuma, ulimchoma kupita kawaida. Akashindwa kujizuia, akakaa chini na kuendelea kulia kama kawaida. Kila mtu aliyemwangalia alimuonea huruma, alionekana kuwa mtu aliyekuwa akipitia matatizo makubwa mno, kwa jinsi mume wake alivyokuwa kipenzi cha watu, kwa jinsi alivyokuwa akipendwa kila siku, hakustahili kuwa katika hali aliyokuwa nayo kipindi hicho.
Rosemary akakumbuka kwamba alikuwa na hati ya nyumba, haraka sana akasimama na kuelekea ndani, alipofika, akafungua kidroo cha kitanda kwa ajili ya kuangalia hati ya nyumba, akaikuta lakini alichokishangaa, haikuwa hati ya nyumba orijino, ilikuwa ni nyingine kabisa ambayo hata sahihi zilizokuwa zimeandikwa, hazikuwa zake na za mumewe.
“Haiwezekanai!”
Akatoka chumbani huku akiwa amechanganyikiwa, akaelekea nje na kumfuata mwanaume yule huku akiwa ameshika ile hati ya nyumba ambayo ilikuwa feki. Alimwambia mwanaume huyo kwamba kulikuwa na mchezo umechezwa, kulikuwa na mtu aliingia chumbani kwake na kuchukua hati orijino na kumuachia feki.
“Mama! Ulishaambiwa kabla kwamba mumeo alichukua mkopo benki, unadhani angepewa bila kuwa na hati ya nyumba ambayo aliiweka kama bondi?’ aliuliza mwanaume huyo huku akimwangalia Rosemary.
“Lakini ilikuwepo mpaka jana nimeangalia, ilikuwepo,” alisema Rosemary.
“Utakuwa umechanganyikiwa mama! Nenda kwanza kapumzike tufanye yetu,” alisema mwanaume huyo, akageuka upande wa pili na kuendelea na kazi yake.
Rosemary akashindwa kuzuiia, siku hiyo nyumba yake ikapigwa mnada. Yalikuwa ni maumivu makali moyoni mwake, hakuamini kama angeweza kupoteza nyumba hiyo, na mbaya zaidi hata kwenye akaunti ya mumewe, fedha zote zilizokuwepo humo, zikachukuliwa kama kukamilisha malipo ya fedha aliyokuwa akidaiwa mumewe.
*** Miongoni mwa matajiri waliojitolea kukisaidia Chama cha Tanzania National Party alikuwa bilionea Adam Matiku. Huyu alikuwa miongoni mwa mabilionea wakubwa nchini Tanzania. Alimiliki kiasi kikubwa cha fedha, alikuwa na kampuni nyingi za usafirishaji, migodi ya dhahabu iliyokuwa Shinyanga na Mererani mkoani Arusha.
Ikifikaga situation kama hii, Wanaume wa Dar es Salaam wana ule msemo wao wanasemaga.. “Mambo ni hivi

”
