Mwachiluwi
JF-Expert Member
- Mar 10, 2022
- 17,796
- 32,148
Chombezo : Dunga Dunga Sehemu Ya Kwanza (1)
Kila siku katika maisha yangu nilikuwa najiona kuwa mimi ndiye kijana ambaye nilikuwa naongoza kwa kutembea na wanawake katika mtaa wetu wa Magomeni Kondoa. Sikujali huyu alikuwa msichana yupi au yupi, kitu ambacho nilikuwa nakitaka ni kuwavua nguo zao tu.
Kulala na wasichana kila wiki ilikuwa ni sehemu mojawapo ya maisha yangu ya kila siku, sikujali kama huyu alikuwa msichana anayejiuza, mtoto wa geti au mke wa mtu. Mtaa mzima walinifahamu kwa tabia yangu ya kupenda wasichana na kufanya nao mapenzi ndani ya chumba changu ambacho kilibarikiwa kuwa na kila kitu.
Nilianza na wanawake wote ambao walikuwa wamepanga nami katika nyumba hiyo ya mzee Hamisi. Sikujali kama wote walikuwa wake za watu au wasichana ambao walikuwa na mabwana zao ambao waliwapangishia vyumba, mimi nilitembea nao.
Sikuishia hapo, bado nilitembea mpaka na ndugu zao ambao mara nyingi walikuwa wakifika ndani ya nyumba hiyo kuja kuwaona dugu zao. Mchezo wa mapenzi ndio ulikuwa mchezo nilioupenda kuliko michezo mingine yote duniani. Sikujali sana kuhusu ugonjwa wa UKIMWI kwani kinga ya mpira wa kondom ndio ilikuwa kitu cha kwanza ambacho nilikuwa nikikipa nafasi. Nilifanya mapenzi na wasichana wa rika zote na maumbo yote, nilifanya na wasichana waliokuwa na ngozi za rangi zote.
Kila mtu mtaani alikuwa akinifahamu kwa jina la Dunga Dunga kwa sababu nilikuwa na uwezo mkubwa wa kudunga sehemu yoyote ambayo nilitaka kudunga. Vijana ambao nilikuwa nakaa nao mtaani wakaanza kuniogopa kwa sababu nilikuwa na uwezo wa kumtongoza msichana yeyote na kufanya nae mapenzi ndani ya wiki moja tu.
Kichwa changu kilikuwa kikifikiria mapenzi kila siku, kama mapenzi ingetokea na kuwa dini, basi naamini mimi ndiye ningekuwa kiongozi wa ibada katika dini hii. Nilitembea na wasichana wa marafiki zangu kwa kuwa tu walikuwa wakinifagilia kwa kutaka kupata kile kitu ambacho kilikuwa kikisifiwa na wasichana wengine ambao nilikuwa nikitembea nao.
Mara nyingi nilikuwa mwanaume shupavu sana kitandani, sikukubali kumuacha msichana baada ya kuzifumania nyavu mara tatu, kila siku ilinipasa kwenda zaidi ya mara tano ndipo nilijisikia kuwa huru. Niliamini katika mapenzi na si mapenzi ya kweli, toka nizaliwe sikuwahi kuwa na mapenzi ya kweli moyoni mwangu, tamaa ya kuwatamani wasichana ndio ilikuwa sehemu kubwa maishani mwangu.
Mtaani nilijifia kwa kujiona kuwa naweza kutembea na msichana yeyote ambaye ningetaka kutembea nae kwa wakati huo. Wapo wengine ambao walisikia majigambo yangu, walinibeza kwa kuniona mshamba wa mapenzi lakini wapo wengine ambao waliniona kuwa mtu hatari ambaye sikutakiwa kupewa nafasi hata mara moja.
Wanawake wakubwa ambao wengi wao walikuwa wakitutafuta sisi vijana walikuwa wakimiminika nyumbani. Magari ya kifahari yalikuwa yakipaki kwa nyakati tofauti katika nyumba ile ambayo nilikuwa nikiishi. Walipenda mambo yangu kitandani kwa kuwa nilifanya kwa kujitolea, yaani kwa moyo mmoja.
Kuwachukua wake wa wakubwa ndio ilikuwa tabia ambayo nilikuwa nimeizoea. Maneno mengi ya vitisho nilikuwa nikipewa kama maonyo na marafiki zangu lakini wala sikutaka kuwasikiliza kabisa. Ningewasikiliza vipi na wakati nilikwishazoea kulala kifuani kwa wanawake mara kwa mara? Masikio niliyaweka pamba kiasi ambacho sikusikia kitu chochote kile.
Bado nilikuwa nikiendelea kujiona mjanja ila kwa watu wengine waliniona kuwa mjinga ambaye nilikuwa sihitaji sana usumbufu kutoka kwa wasichana na hii ilitokana na aina ya wasichana ambao nilikuwa nikitembea nao. Vijana wengi waliniambia kwamba kama nilitaka wanikubali kwamba mimi ni mkali basi ni lazima niwatafute wasichana ambao wangenifanya kunisumbua mpaka kuwapata na si kuwafuata wasichana waliozoea mchezo huu.
“Hatukuamini kama wewe mkali” Hamisi aliniambia.s
Nikabaki nikimwangalia Hamisi, nikatoa tabasamu pana. Kwa nini hawakuwa wakiniamini na wakati nilikuwa na uwezo wa kutembea na wasichana wengi ndani ya wiki moja? Nikabaki nikimwangalia Hamisi kisha nikayapelekea macho yangu kwa vijana wengine ambao walikuwa wamekaa khapo kijiweni.
Kila siku katika maisha yangu nilikuwa najiona kuwa mimi ndiye kijana ambaye nilikuwa naongoza kwa kutembea na wanawake katika mtaa wetu wa Magomeni Kondoa. Sikujali huyu alikuwa msichana yupi au yupi, kitu ambacho nilikuwa nakitaka ni kuwavua nguo zao tu.
Kulala na wasichana kila wiki ilikuwa ni sehemu mojawapo ya maisha yangu ya kila siku, sikujali kama huyu alikuwa msichana anayejiuza, mtoto wa geti au mke wa mtu. Mtaa mzima walinifahamu kwa tabia yangu ya kupenda wasichana na kufanya nao mapenzi ndani ya chumba changu ambacho kilibarikiwa kuwa na kila kitu.
Nilianza na wanawake wote ambao walikuwa wamepanga nami katika nyumba hiyo ya mzee Hamisi. Sikujali kama wote walikuwa wake za watu au wasichana ambao walikuwa na mabwana zao ambao waliwapangishia vyumba, mimi nilitembea nao.
Sikuishia hapo, bado nilitembea mpaka na ndugu zao ambao mara nyingi walikuwa wakifika ndani ya nyumba hiyo kuja kuwaona dugu zao. Mchezo wa mapenzi ndio ulikuwa mchezo nilioupenda kuliko michezo mingine yote duniani. Sikujali sana kuhusu ugonjwa wa UKIMWI kwani kinga ya mpira wa kondom ndio ilikuwa kitu cha kwanza ambacho nilikuwa nikikipa nafasi. Nilifanya mapenzi na wasichana wa rika zote na maumbo yote, nilifanya na wasichana waliokuwa na ngozi za rangi zote.
Kila mtu mtaani alikuwa akinifahamu kwa jina la Dunga Dunga kwa sababu nilikuwa na uwezo mkubwa wa kudunga sehemu yoyote ambayo nilitaka kudunga. Vijana ambao nilikuwa nakaa nao mtaani wakaanza kuniogopa kwa sababu nilikuwa na uwezo wa kumtongoza msichana yeyote na kufanya nae mapenzi ndani ya wiki moja tu.
Kichwa changu kilikuwa kikifikiria mapenzi kila siku, kama mapenzi ingetokea na kuwa dini, basi naamini mimi ndiye ningekuwa kiongozi wa ibada katika dini hii. Nilitembea na wasichana wa marafiki zangu kwa kuwa tu walikuwa wakinifagilia kwa kutaka kupata kile kitu ambacho kilikuwa kikisifiwa na wasichana wengine ambao nilikuwa nikitembea nao.
Mara nyingi nilikuwa mwanaume shupavu sana kitandani, sikukubali kumuacha msichana baada ya kuzifumania nyavu mara tatu, kila siku ilinipasa kwenda zaidi ya mara tano ndipo nilijisikia kuwa huru. Niliamini katika mapenzi na si mapenzi ya kweli, toka nizaliwe sikuwahi kuwa na mapenzi ya kweli moyoni mwangu, tamaa ya kuwatamani wasichana ndio ilikuwa sehemu kubwa maishani mwangu.
Mtaani nilijifia kwa kujiona kuwa naweza kutembea na msichana yeyote ambaye ningetaka kutembea nae kwa wakati huo. Wapo wengine ambao walisikia majigambo yangu, walinibeza kwa kuniona mshamba wa mapenzi lakini wapo wengine ambao waliniona kuwa mtu hatari ambaye sikutakiwa kupewa nafasi hata mara moja.
Wanawake wakubwa ambao wengi wao walikuwa wakitutafuta sisi vijana walikuwa wakimiminika nyumbani. Magari ya kifahari yalikuwa yakipaki kwa nyakati tofauti katika nyumba ile ambayo nilikuwa nikiishi. Walipenda mambo yangu kitandani kwa kuwa nilifanya kwa kujitolea, yaani kwa moyo mmoja.
Kuwachukua wake wa wakubwa ndio ilikuwa tabia ambayo nilikuwa nimeizoea. Maneno mengi ya vitisho nilikuwa nikipewa kama maonyo na marafiki zangu lakini wala sikutaka kuwasikiliza kabisa. Ningewasikiliza vipi na wakati nilikwishazoea kulala kifuani kwa wanawake mara kwa mara? Masikio niliyaweka pamba kiasi ambacho sikusikia kitu chochote kile.
Bado nilikuwa nikiendelea kujiona mjanja ila kwa watu wengine waliniona kuwa mjinga ambaye nilikuwa sihitaji sana usumbufu kutoka kwa wasichana na hii ilitokana na aina ya wasichana ambao nilikuwa nikitembea nao. Vijana wengi waliniambia kwamba kama nilitaka wanikubali kwamba mimi ni mkali basi ni lazima niwatafute wasichana ambao wangenifanya kunisumbua mpaka kuwapata na si kuwafuata wasichana waliozoea mchezo huu.
“Hatukuamini kama wewe mkali” Hamisi aliniambia.s
Nikabaki nikimwangalia Hamisi, nikatoa tabasamu pana. Kwa nini hawakuwa wakiniamini na wakati nilikuwa na uwezo wa kutembea na wasichana wengi ndani ya wiki moja? Nikabaki nikimwangalia Hamisi kisha nikayapelekea macho yangu kwa vijana wengine ambao walikuwa wamekaa khapo kijiweni.