Duh! Zitto Kabwe naye amekuwa pedeshee!!

Duh! Zitto Kabwe naye amekuwa pedeshee!!

Mdakuzi

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
4,293
Reaction score
6,901
Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe alikuwa na yake kwenye jukwaa la Malaika Band ndani ya ukumbi wa Mango Garden, IJumaa iliyopita (16 January 2015).
Zitto alipanda jukwaani wakati Christian Bella akiimba wimbo wake wa “Nani Kama Mama”, Mheshimiwa akachotwa na hisia za wimbo huo hadi mchozi mwembamba ukamtoka (bila shaka ni kwa kumbukumbu ya msiba wa mama yake mzazi uliotokea mwaka jana), lakini baadae akaimarika na kuthubutu kuuimba wimbo huo.
Mheshimiwa Zitto akaucheza pia wimbo huo, mashabiki wakamiminika jukwaani kupiga naye picha, kwa muda wa takriban dakika 20 alizosimama jukwaani, mbunge huyo akadhihirisha kuwa ni mtu wa watu, Mango Garden ‘ilisimama’ kwa muda.
Kama kuna mapedeshee waliokuwepo Mango Garden, basi jana walizima ngebe zao, Zitto alifunika, alitunza pesa nyingi sana. Christian Bella peke yake alipokea zaidi noti 50 za elfu kumi kumi kutoka kwa Zitto huku zingine zikiwa ni dola za Kimarekani. Watu wanatumia pesa bwana!
zito 1.jpg zitto 2.jpg
Chanzo: Blog ya Saluti5
ZITTO KABWE AFANYA ‘KUFURU’ MALAIKA BAND MANGO GARDEN …awatia wazimu mashabiki, alizwa na wimbo “Nani Kama Mama”, maelfu ya pesa zamtoka jukwaani
 
Kuwa mtu wa kigoma halafu una mtonyo tayari ni P.D.G, sema huu mwaka wa uchaguzi kila mtu achukue nafasi yake kupiga hela za wanasiasa sio kung’ang’ania JF baadae mnakuja kulalamika msio na kazi siasa mwaka huu inaweza wasogeza ndio fursa isiyohitaji mtaji Bella ameanza ila mwishoni mpaka kina bongo flavor watapiga.

Wanasiasa na vyama vya siasa vina spendi mwaka, ukitengeza hata tshirt, banner au scalf inakoa poa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom