Duh... Netanyahu kayakanyaga aisee!

Duh... Netanyahu kayakanyaga aisee!

6 Pack

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2022
Posts
3,670
Reaction score
8,023
Niaje waungwana

Nafikiri mashambulizi ya mwaka jana kati ya Iran na Israel, yalimpofusha sana Netanyahu kwa kuamini kwamba Iran ilikuwa na silaha chache, na dhaifu kwa kuweza kufanya maangamizi katika ardhi ya Israel.

Ikumbukwe kwamba katika mashambulizi yale Iran alitumia makombora ya kawaida na ya masafa mafupi, hivyo hata madhara na uharibifu wake huko Israel haukuwa mkubwa kivile, hali iliyomfanya Netanyahu aamini kwamba Iran haina silaha za maana za kupambana nae, lakini pia aliamini kwamba Iron dome na Thaad zikiongezwa na kurekebishwa vizuri, basi muajemi atachapika vizuri bila kurusha au kuingiza chochote katika ardhi ya Israel.

Masikini, jamaa hakujua kwamba Ayatollah alikuwa anampimia upeo wake wa akili ulipoishia. Akaenda Marekani kuonana na Trump kisha wakapanga namna watakavyoivamia Iran, kutawala anga, na kuzuia kombora kurushwa nchini kwao Israel.

Waswahili wanasema usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Neta akaanza uvamizi kwa mashambulizi ya kushtukiza huku wakiwa wameshajipanga na Marekani, Uingereza, Ujerumani, Ufaransa na washirika wengine kuzuia mashambulizi ya Iran kwenda Israel. Mpaka hapo walikuwa wanajua Iran haina silaha au makombora ya maana ya kupenya ulinzi wao. Kwa bahati mbaya hali ikawa tofauti na walivyotarajia.

Vinu vikaanza kutumwa Israel katika speed na nguvu ya ajabu kiasi ya kwamba Iro dome na Thaad zao zikabaki kama maonesho tu au mavyuma ya kukamatia kumbi kumbi. Iron dome balada ya kuzuia kombora, inazuia nzi na upepo.

Netanyahu akaona maji yamezidi unga, kinachozuiwa hakionekani, akamwambia baba yake Trump aingilie kati. Baba na yeye kuingilia kati kaishia kupiga hewa, huku mzigo ukiwa umeshahamishwa zamani. Baada ya hapo wakafikiri hilo tukio linamfanya muajemi aogope au kusalimu amri, badala yake ikawa kama vile wamempeleka mzaramo mkoleni. Yani ndo amezidisha mashambulizi na kuigeza Tel Aviv kama Mogadishu.

Baada ya plan kushindwa eti wameamua kuomba poo kwa kutaka vita isimame. Muajemi hataki kusikia hilo, bado anaendeleza kipondo tu huko Israel. Japo wao ni mabingwa wa kuficha taarifa, lakini ukiona Trump anakimbilia kutaka mapigano yasitishwe au vita iishe basi ujue ameona madhara makubwa mno yaliofanywa na Iran huko Israel. Maana ni yeye ndio alikuwa anasema eti waachwe waendelee kuchapana. Sasa imekuaje tena kutaka vita isimame. Za kuambiwa changanya na zako.

Vita sio poa. Nina imani Netanyahu anajuta kuanzisha huu mzozo na vita ikisimama naamini hatokuja tena kuigusa Iran kindezi ndezi vile.

Ukiona mtu mzima analia ujue kuna jambo. Fikiria leo hii Trump anapambana ili vita iishe. Ujue kuna jambo kubwa limetokea huko Israel halitakiwi kusemwa 🤣🤣🤣
 
Lengo kuu la Israel kuingia kwenye hii vitani ni kuharibu mpango wa Iran kumiliki silaha za nukes ,sasa kama wamefanikiwa ku obliterate hizo nuclear plants kuna haja gani ya kuendelea kupigana vita? Ingawa waziri wa ulizi wa Israel ametoa amri ya kurespond kwa Israel kwenda Iran with full force soon baada ya Iran kuviolate cease fire agreement .
 
Lengo kuu la Israel kuingia kwenye hii vitani ni kuharibu mpango wa Iran kumiliki silaha za nukes ,sasa kama wamefanikiwa ku obliterate hizo nuclear plants kuna haja gani ya kuendelea kupigana vita? Ingawa waziri wa ulizi wa Israel ametoa amri ya kurespond kwa Israel kwenda Iran with full force soon baada ya Iran kuviolate cease fire agreement .
Muirani ndio anataka muende miaka 3 on battle tuone matokeo huwezi kusinamisha vita mapema hivi daaah
 
Lengo kuu la Israel kuingia kwenye hii vitani ni kuharibu mpango wa Iran kumiliki silaha za nukes ,sasa kama wamefanikiwa ku obliterate hizo nuclear plants kuna haja gani ya kuendelea kupigana vita? Ingawa waziri wa ulizi wa Israel ametoa amri ya kurespond kwa Israel kwenda Iran with full force soon baada ya Iran kuviolate cease fire agreement .
Ushasema kama wamefanikiwa. Je kama hawakufanikiwa na kuona mambo yanakwenda kinyume na matarajio yao je?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom