DSTV muda sio mrefu tutawaacha mazima

Unapokuwa na smart TV vifurushi vya dst TV au Azam hiyo fedha ungetaman ununue bando la internet ili ustream kilakitu Kwa Uhuru Zaid katika TV yako, na bado nyumbani mtatumia ilo bando Kwa mambo mengine sasa apo huwez kutegemea tena ivi vifurushi vya kawaida vya internet ya voda au tigo NI ghali Sana kutumia kwe smart TV, kwahiyo itakubidi tu uhamie kwenye vitu kama fiber ambayo internet inasambazwa majumbani Kwa waya ambapo unalipa bili kama umeme, ambapo kidogo unakuwa huru na TV yako,sasa huduma kama hi serikali haiwezi imwachie mtu binafsi
 
Utopolo na kiremba chako [emoji41][emoji41][emoji41]
 
Unlimited internet ni around elfu 70 kwa mwezi mpaka laki na 20 kwa mwezi. Inategemea na ISP anaekuuzia net.

Mimi silipii kingamuzi chochote.

Nalipia unlimited internet zuku 70,000 kwa mwezi
mkuu unafanyaje ukitaka kustream mpira kama unatumia Smart Tv, tupe maujanja.
 
Azam hapati EPL...HAPATI.
 
Inawezekana ni mambo ya kibali kama ambavyo azam hana cha Epl.Haya mambo yako kibiashara zaidi.
 
Hata dstv mvua ikinyesha sana mitambo yao inakata.

Kuna kipindi mvua ilinyesha kubwa sana mitambo ikakata na kwangu ikawa mazima haionyeshi. Nimepiga huduma kwa wateja taratibu zote nikafuata bado haikuinuonyesha. Jawabu nililopatiwa ni dishi limeyumba.

Nikawasiliana na mafundi wao wakaja kunirekebishia. Fundi akanipa maelezo mazuri tu. Akiniambua dish likifungwa inabidi likazwe sana ili lisiwe rahisi kucheza au kuyumba wakati wa mvua kubwa au upepo mkali. Lisipokazwa sana husababisha mawasiliano kuzima kabisa ikitokea mabadiliko ya hali ya hewa (mvua/upepo).

Endapo mvua kubwa itanyesha au upepo mkali kitakachotokea ni mawasiliano yatapotea kidogo tu kutokana na hali ya hewa ila yatarudi. Na ndiyo maana dstv kuna maelezo mawasiliano yakikata huwa wanakuambia eidha ni kwa sababu ya hali ya hewa au sababu nyengine.
 
Azam hawezi pata tenda ya kuonesha EPL, maana hapo DStv kajikita kama vile kanjibai alivyojikita kwenye jezi za Simba na ile Mo Extra
 
Hawa Dstv wanazingua.

..........Sasa hivi bora kulipia kifurushi cha 37,000 tu cha 60,000 kwenda juu ni hasara tu.

Wakiendelea kubania hivi tutarudi Azam.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…