Drywall na ujenzi wa kisasa

Nyumba ya drywall tupu inajengwa hivi:
42ea44d7896cf30fa82b52cb90a53cc7.jpg


Halafu wanamalizia kwa kuweka siding. Hii nyumba tofali zipo kwenye msingi tu.

42beca2fbc56d26b2903d2c098a16b13.jpg
Hizi nyumba za USA tunazijua unafikiri unaweza kujenga Maramba mawili hio. Watakata hizo mbao mkuu. Huku wanakata grill au wanatoboa hadi ukuta wa tofali hizo mbao si watakufanya mtaji?
 
Hizi nyumba za USA tunazijua unafikiri unaweza kujenga Maramba mawili hio. Watakata hizo mbao mkuu. Huku wanakata grill au wanatoboa hadi ukuta wa tofali hizo mbao si watakufanya mtaji?

Pima faida na hasara yake. Halafu jiulize USA na Tanzania ni wapi wana vifaa vizuri vya kutobolea ukuta. Bila ya kusahau nyumba za Tanzania zina majirani na wapangaji. Hata jogoo wakiona songombingo wanaweza kupiga kelele
 
Pima faida na hasara yake. Halafu jiulize USA na Tanzania ni wapi wana vifaa vizuri vya kutobolea ukuta.
Wewe unafikiria nini? Wanaotoboa no vibaka. Unafikiri USA kuna vibaka wa kuja kuiba flatscreen au home theatre? Unafikiri kwanini bongo tuna grills madirishani na milangono wakati USA kuna milango tupu tena mingi ya plastiko na vioo?
 
Drywall ndio habari ya dunia kwa sasa hasa katika kuta za ndani. Drywall sio mbao ni madini ya gypsumrrr yaliyofungwa ndani ya karatasi nzito.

Drywall ina faida zifuatazo:

- Ina unafuu wa bei.

- Inadhibiti hali ya hewa ndani ya nyumba.

- Ujenzi wake ni rahisi na wa haraka.

- Ni ngumu kuwaka moto. Karatasi la nje litaungua lakini madini ya gypsum yanaungua kwa moto wa joto kali sana.

-Muonekano wake ni mzuri na wa kupendeza.

-Inarahisisa kupitisha mabomba na waya za umeme

- Kuna zisizopitisha maji (waterproof)

-Haina uzito mkubwa sana hivyo haihitaji msingi na zege la nyumba nzito.

-Ni rahisi kuirepea, au hata kuitoa na kuweka nyingine.

Inaweza kufanywa iwe na uwezo wa kutopitisha sauti(soundproof)


1a52da744f12d868663bbed51f344201.jpg


8d6716de3f40a91ce40368428bfba754.jpg


e24225a04634b24be8e54787dc77af26.jpg
Ni nzuri lakini hakuna siri hapo nyumbani. Sauti chumbani inasikika hadi barazani....sio sound proof......jipangeni mnao taka kutumia hizi
 
Wewe unafikiria nini? Wanaotoboa no vibaka. Unafikiri USA kuna vibaka wa kuja kuiba flatscreen au home theatre? Unafikiri kwanini bongo tuna grills madirishani na milangono wakati USA kuna milango tupu tena mingi ya plastiko na vioo?

Inategemea na eneo unaloishi. Hii ni Marekani.
2282aef4b2b79ddf37620127b995ef60.jpg
 
Mabadiliko na maendeleo ya kweli hufanywa na wananchi sio serikali.

Tusijitishe wenyewe kwa kuogopa maendeleo. Kuna watanzania wengi hawajaona ujenzi huu. Wakijifunza hapa na kuelewa faida zake na wakaona ni ujenzi unaowafaa, huo ni mwanzo wa mabadiliko.
Na ndipo watakapofikiria jinsi ya kupambana na hao vibaka watakaovunja ukuta.
Kusema ukweli nyumba hizi ni salama. Kwanza ieleweke hakuna drywall inayowekwa kama ukuta wa nje. Hii ina maana mpaka kibaka akifika kwenye drywall ameshaingia ndani ya nyumba.

Na pia muda atakaotumia kukata mbao na drywall afadhali ang’oe mlango au dirisha.

Kuta za nje zinajengwa kwa tofali, vioo au siding. Kwa Marekani kwenye nyumba za makazi ya watu siku hizi wanatumia siding kwa nje ndani wanaweka drywall. Tofali za nje zinatumika kwa mapambo tu.
 
Matengenezo yake ni rahisi unaweza kuziba au kuweka kipande kingine cha drywall mwenyewe bila ya kutumia fundi.
Unajuanhizi ndoa za kibongo ugomvi ni kawaida sana, mke na mume wakisukumana kidogo tu litachanika lote hilo, vipi paa likivuja na kulilainisha kama boksi..
 
Unajuanhizi ndoa za kibongo ugomvi ni kawaida sana, mke na mume wakisukumana kidogo tu litachanika lote hilo, vipi paa likivuja na kulilainisha kama boksi..

Fujo za nyumbani ni kawaida popote pale duniani. Hizi kuta zinatumiwa na watu ambao kuvuta bangi ni ruksa kwa mujibu wa sheria.

Paa likivuja linaacha madoa tu kama ya kwenye silingi bodi. Likiloa kabisa unatoa na kuweka kipande kingine.
 
Hayo makitu ndiyo yanawekwa ndani ya drywall.
8929bf1a0f795837ac5e072bf1d88d1c.jpg
Hizo ni insulating materials ili kuhifadhi joto nyakati za summer or winter kunapowashwa aircon au heaters...

Sasa kwa 'bongo' ukijenga nyumba halafu yakawekwa hayo madude na nyumba isiwe na AC, wakati wa joto unaweza ukatamani kuvua ngozi...
 
Hizo ni insulating materials ili kuhifadhi joto nyakati za summer or winter kunapowashwa aircon au heaters...

Sasa kwa 'bongo' ukijenga nyumba halafu yakawekwa hayo madude na nyumba isiwe na AC, wakati wa joto unaweza ukatamani kuvua ngozi...

Nyumba za Bongo hata AC hazihitaji. Zinahitaji madirisha ya kupitisha hewa. Wabongo hatujui jinsi tulivyojaliwa hali ya hewa nzuri.
 
Drywall ndio habari ya dunia kwa sasa hasa katika kuta za ndani. Drywall sio mbao ni madini ya gypsumrrr yaliyofungwa ndani ya karatasi nzito.

Drywall ina faida zifuatazo:

- Ina unafuu wa bei.

- Inadhibiti hali ya hewa ndani ya nyumba.

- Ujenzi wake ni rahisi na wa haraka.

- Ni ngumu kuwaka moto. Karatasi la nje litaungua lakini madini ya gypsum yanaungua kwa moto wa joto kali sana.

-Muonekano wake ni mzuri na wa kupendeza.

-Inarahisisa kupitisha mabomba na waya za umeme

- Kuna zisizopitisha maji (waterproof)

-Haina uzito mkubwa sana hivyo haihitaji msingi na zege la nyumba nzito.

-Ni rahisi kuirepea, au hata kuitoa na kuweka nyingine.

Inaweza kufanywa iwe na uwezo wa kutopitisha sauti(soundproof)


1a52da744f12d868663bbed51f344201.jpg


8d6716de3f40a91ce40368428bfba754.jpg


e24225a04634b24be8e54787dc77af26.jpg
WEKA HABARI KAMILI MKUU
 
Back
Top Bottom