Teknolojia, I respect you Comrade..!!
Linapokuja suala la siasa jaribu kidogo suala la Dini likae pembeni, Nafurahi kusikia kwamba kwa Kawaida wewe si mdini, Lakini funga Novena kwaajili ya pepo huyu mchafu anayekunyemelea! Binafsi nani ni Mkatoliki, lakini linapokuja suala la kuchagua kiongozi, Dhehebu langu na Dini yangu huweka pembeni. Uwezo, Uchapakazi, Maono ya kazi ndivyo huchukua nafasi. Kamwe Dini, Dhehebu halijawahi kuwa kigezo ktk kumchagua kiongozi yeyote maishani mwangu, Natamani sana iwe hivyo hata kwako.
Kwa yanayotokea kwa Dr Slaa.
Mkuu Tek, Dr Slaa mpaka tunapoandika haya hakuwa amechukua fomu kugombea nafasi ya Urais ndani ya Cdm. Kinachotokea kudelay kwa Dr Slaa ni kusimmia misingi tu hakuna kingine chochote. Na kinachotokea kwa Mbowe na Lowassa ni hamu ya kuongoza na Matamanio ya kuiondoa ccm Madarakani. Hakuna suala lolote linalohusiana na Misingi ya Dini ili kufikia Maamuzi hayo. Ondoa mawazo hayo Kamanda wangu.
BACK TANGANYIKA