Dr. Wilbrod Slaa kesho kuanza rasmi vikao vya chama

Dr. Wilbrod Slaa kesho kuanza rasmi vikao vya chama

Status
Not open for further replies.
attachment.php
 
Hatimaye katibu mkuu wa CHADEMA Dr. Willbrod Slaa kesho ataanza rasmi kuhudhuria vikao vya chama ambapo atahudhuria kikao cha kamati kuu ya Chadema.

Kuonekana kwa Dr. Slaa kesho kutamaliza rasmi mjadala wa muda mrefu na propaganda zilizotawala eti Dr. Slaa kajitoa Chadema.

Katika hatua nyingine, upigwaji wa kura za maoni katika jimbo la Kibamba kwa watia nia wa Chadema utafanyika kesho baada ya mtia nia John Mnyika kupata nafua kutokana na kusumbuliwa na homa kwa muda.

Habari na G Sam

Kwahyo hizi taarifa zilizokuwa zinatolewa na baadhi ya viongozi wa chadema kuhusu Slaa kwamba bado anahudhuria vikao vya kamati mbalimbali zilikuwa ni uongo na kama haikuwa hvyo kwanini waliamua kutumia kauli hizo
 
Yericko,

Siasa ya unafiki sipendi. Nimenyamaza lakini naona mnazidi kunichokoza. Ni afadhali mngelikaa kimya kama nilivyonyamaza mimi. Uwongo wowote na upotoshwaji wowote sitauvumilia. Nitaukanusha hapo hapo. Hata kama una lengo lako ambalo silifahamu naomba sana usitumie jina langu. Nimefundishwa uwongo ni dhambi siko tayari kushiriki dhambi hiyo.

sina kikao chochote cha Secretariat sina mpango wowote ninaopanga kuwasilisha popote. Naomba watanzania wapuuze propaganda zote zinazofanyika kwa jina langu.

Ningehitaji kutuma taarifa yoyote kwa umma ningeliita Press Conference Mwenyewe au ningelitumia utaratibu wowote uliouliozoeleka.

Naomba kutoa onyo kwa mtu yeyote awaye, matumizi ya jina la Dr Slaa yakome.


==========
Moderator:
Baada ya wadau kutaka maoni ya Dr. Slaa yajitegemee na hoja ya Yericko ifungwe, tumeona ni vema kuiweka hoja hii ikijitegemea kama ilivyopendekezwa. Majibu ya msingi yapo hapa

Dr.Slaa alivunjika mkono na hadi sasa ana ulemavu wa kudumu kwa sababu ya kuitetea chadema. yeye mwenyewe alipigwa na kuharibiwa mimba mwaka 2011 kwa sababu ya chadema halafu leo wanapuuzwa kama vile si chochote ndani ya chama.
 
yaani kwa siku hizi hata mtu akisikia Dr. Slaa amekohoa atakuja kuandika huku. Mwacheni basi mwenzenu apumzike
 
Mkuu,mimi huwa sibahatishi!

Lakini bwn.Sam wewe hubahatishi ila hujatuambia ni nini chanzo cha taarifa unayotulisha hadi tuamini hivyo kwa sababu yeye mwenyewe ameshasema ameshauriwa na viongozi wake wa kiroho kupumzika siasa. Leo pia tumemsoma akilalamika kutishiwa maisha. Mimi nasema tuache kumwandika tutakavyo au tusikiavyo hadi yeye mwenyewe atakapojitokeza na kuuweka ukweli wake wazi. Sasa endapo hatutamuona kwenye vikao vya chama vinavyoanza kesho mfululizo tukuweke wapi?
 
Acha uongo na Uzushi nipo hapa kikaoni na nimekaa meza ya tatu

Dr hayupo hapa

Unadanganya kwa maslahi ya nani?

Hapa hayupo Dr slaa...acha uongo usio na tija

Acha uongo...Dr hauyupo hapa

Unadanganya kwa maslahi ya nani?
 
Chama ni watu viogozi tumewajiri ili waongoze jahazi,mtei mwenyewe ameasisi chadema lkn yeye sio chadema chademe ni wanachama
 
Acha uongo na Uzushi nipo hapa kikaoni na nimekaa meza ya tatu

Dr hayupo hapa

Unadanganya kwa maslahi ya nani?

Hapa hayupo Dr slaa...acha uongo usio na tija

we nae acha kudanganya..tangu lini umekuwa chadema
 
dr kafika mtalaam au ndio ..kutufanya watoto..
ndio siasa kuna watu wana misingi yao..
 
Acha uongo na Uzushi nipo hapa kikaoni na nimekaa meza ya tatu

Dr hayupo hapa

Unadanganya kwa maslahi ya nani?

Hapa hayupo Dr slaa...acha uongo usio na tija
Meza ya tatu ipi?
Sasa Dr.Yuko Wapi?
 
KaKamanda yupo na hato mtu hapa na akatwi mtu hapa hiki ni chama makini sana msitegemee mpasuko nyinyi ugueni vidonda mungu atawaponya
 



sasa mkuu tukuweke kwenye kundi la Yericko nyerere na wewe ....

hivi mkiandika ukweli mnapungukiwa nini..?
Majibu ya Mbowe.

Mbowe-Tumekubaliana na Katibu Mkuu apumzike kwa muda, kwamba sis tuendelee na atakapokuwa tayari ataungana nasi mbele ya safari.

Mbowe-Chama hiki hatukiendeshi kwa siri, tunakiendesha kwa mikakati.

Mbowe-Tulilazimika kutumia kila mbinu halali ambayo inakiwezesha chama chetu kusaka matumaini na matarajio ya wananchi.

Mbowe-Tuliridhika pasipo shaka kwamba ugeni wa Edward Lowassa katika chama chetu ni mpango wa Mungu.

Mbowe-Umoja wetu ndio ushindi, fursa iliyojitokeza ni nadra.

Mbowe-Mtikisiko huu umekuja kwa CCM kipindi ambacho Watanzania wanamatamanio ya mabadiliko

Mbowe-Hatuwezi kuwa chama cha kuendelea kuhubiri mabaya ya jana tukashindwa kuhubiri maendeleo ya kesho

Mbowe- Kipigo wanachopata CCM, hawajawahi kukipata tangu tuanze siasa za vyama vingi

Mbowe-Kila tunayeweza kumpokea kutoka vyama vilivyo nje ya UKAWA tutamchukua

Mbowe-Mungu ameamua kutumia chama chetu kujeruhi na kuangusha CCM.

Mbowe-CHADEMA ni chama cha siasa, ni chama makini, chama makinI ni chama cha watu, chama kisichokuwa makini ni chama cha viongozi.
 
Acha uongo na Uzushi nipo hapa kikaoni na nimekaa meza ya tatu

Dr hayupo hapa

Unadanganya kwa maslahi ya nani?

Hapa hayupo Dr slaa...acha uongo usio na tija

Na anyamaze kimya tumechoshwa na propaganda za Lumumba. Kwanza yeye wala sio mwanachama wa chadema hicho kikao angehudhuria Jforum?
 
Hivi mtu kusema uongo unapata faida gani? au huyu nae alikuwa anamuongelea Dr Manyaunyau kuwa watakuwa pamoja kwenye kikao chao cha makaburini Sinza?
 
Hatimaye katibu mkuu wa CHADEMA Dr. Willbrod Slaa kesho ataanza rasmi kuhudhuria vikao vya chama ambapo atahudhuria kikao cha kamati kuu ya Chadema.

Kuonekana kwa Dr. Slaa kesho kutamaliza rasmi mjadala wa muda mrefu na propaganda zilizotawala eti Dr. Slaa kajitoa Chadema.

Katika hatua nyingine, upigwaji wa kura za maoni katika jimbo la Kibamba kwa watia nia wa Chadema utafanyika kesho baada ya mtia nia John Mnyika kupata nafua kutokana na kusumbuliwa na homa kwa muda.

Habari na G Sam

kesho tena?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom