Wacha1
JF-Expert Member
- Dec 21, 2009
- 16,676
- 8,246
Makamanda,
alipo Dr Slaa hapako siri Wala hapajawahi kuwa Siri. Nilipowaaga Watanzania kupitia Azam TV na baadaye STarTV niliwaambia Watanzania kuwa ninaenda Sabbatical Leave. Nitatumia wakati huo kurudi shule, kujikumbusha mambo mbali mbali mapya katika maeneo yangu ya Masomo. Mwanzoni nilifikiria kuanza na masomo ya Sheria. Hata hivyo nimeanza na masomo ya Psychotherapy na Psychoanalysis. Kwa wale wanaojua Branches mbalimbali ya Falsafa ( Philosophia) watakumbuka kuwa nilisoma Psychology kama sehemu ya Masomo yangu ya Falsafa Seminari Kuu ya Kibosho. Sasa nimeona niingie kwa undani zaidi, kufahamu zaidi Tabia na mfumo wa akili ya Binadamu unavyofanya Kazi. Hadi sasa nimekwisha kuingia kwenye Module insyodeal na Cognitive Therapy, Strategic Family Therapy, Brief Therapy.
Wapenzi wangu nawaomba watulie tu. Kama nilivyowaambia Nimeachana na Active Party Politics, walidhani maana ya kauli hiyo ni kufunga Mdomo. Nilisema pale patakapohitaji kupiga kelele nitapiga kelele kupinga uonevu wa aina yeyote, kupinga ufisadi wa aina yeyote. Nitasimamia misingi yote muhimu katika Taifa langu kwa kutumia haki zangu za Kikatiba ( ikiwa ni pamoja na kusimamia uchumi wa Taifa letu.
Shukrani zangu za dhati kwa kile ambacho ulikuwa unafanya wakati upo CHADEMA (Kutetea haki za wanyonge wa Tanzania ambao ndio walala hoi wa nchi hii na ndio walipa kodi wakubwa wa nchi hii bila wizi wala kukwepa hiyo kodi na kulipa inapotakiwa. Wale wanaokula keki ya taifa bila kunawa mikono hawalipi kodi kwa wakati na hata ile wanayolipa ni ndogo sana pia hawalipi kwa wakati unaokubalika (on time).
Pongezi za dhati kwa kujiendeleza na masomo ambayo huwa tunasema unajifunza kila siku hadi utakapoingia kaburini. Panapo majaliwa ya mwenyezi mungu na rehema zake tele tutaifikisha Tanzania kwa vizazi vijavyo huku tukiwa mashujaa wa kutetea wanyonge wa nchi yetu.