Usipokuwa stable hawa jamaa hawafai..Dondoshwa na Cult hafai
Usipokuwa stable hawa jamaa hawafai..Dondoshwa na Cult hafai
I know what you mean mkuu.
Lakini ni muhimu kukumbushana mambo kama haya ambayo yanatukumbusha tumetoka wapi, tulitakiwa kuwa wapi na wapi tulipo sasa; wapi tunataka kuelekea na tufanye nini ili kufika huko tunapopataka.
Bila hivyo tutakua tuna-manufacture vyibuda na hatimaye kupiga hatua moja mbele, mbili nyuma.Naunga mkono mkuu ni muhimu kutafakari katika safari yetu kama sote ni mamba au kuna kenge kati yetu mfano Shibuda tushamuona, historia ni matukio ya juzi na jana ili yatupe muelekeo ya ku-anticipate ya kesho
Homie, huyu jamaa alivuruga sana harakati za demokrasi kwa kuwasaliti vijana wa Mwanga, Bangwe, Buzebazeba, Gungu, Majengo, Kibirizi na Ujiji. Sasa anavuna matunda ya usaliti wake, magamba walimtumia sasa wamemtelekeza.
Vijana wa KG walikesha kule ukumbi wa kuhesabu kura Bangwe kuhakikisha hakuna kura haziingizwi ukumbini wakati wa kuhesabu. Walipigwa na FFU kwa ajili yake, matokeo yake usaliti.
Historia ya Dk Kaburu hunifanya nisimuamini sana Zitto.
Nikienda mbinguni na kumkuta, nitamuomba mungu niende kwa shetani! Serious
Anakula urojo kwa kuthamini mbinu za kuangamiza upinzani. Nasikia kahamia Kigamboni, akila pensheni kwa dhuluma hii.
Ningependa kujuzwa alipo huyu bwana mkubwa aliyekuwa mwiba wa CCM akiwa CHADEMA na hatimaye kuhamia CCM.
Kama ni mcheza Darts, basi hapo umepiga kwenye BULL. Huyu bwana kwa sasa anaishi KIGAMBONI naona huo mgao alioupata aliamua kwenda kujenga kibanda chake huko ili ajifiche vizuri.Sikilizeni! Dr Aman Walid Kabourou aliihama CDM kwa pesa ya EPA. Mwenye jukumu la kuhakikisha anahamia CCM alikuwa Maranda ambaye magamba wammefunga jela. Maranda na Dr Kabourou wana uhusiano wa kidugu, na ndiyo sababu kila siku kesi ya Maranda ilipokuwa inatajwa ama kusikilizwa pale Kisutu Dr Kabourou alikuwepo. Baada ya kukwapua pesa ya EPA, Mangulla akampa Maranda kazi ya kuhakikisha analirejesha jimbo la Kigoma Mjini CCM. Kumbuka waratibu wakuu wa EPA ndani ya CCM walikuwa Mangulla, Rostam, Mama Meghji na Salome Mbatia. Dr Kabourou akapewa sh 147 millioni kutoka zile za EPA, aliandikiwa hundi na Maranda. Ushahidi upo kwenye ripoti ya uchunguzi ya Hosea, Mwanyika na Mwema. Dr Kabourou akaahidiwa ubunge wa Afrika Mashariki, akapata. Siku hizi sijui alipo! Atakuwa anatafutiwa nafasi, subirini.
Kama ni mcheza Darts, basi hapo umepiga kwenye BULL. Huyu bwana kwa sasa anaishi KIGAMBONI naona huo mgao alioupata aliamua kwenda kujenga kibanda chake huko ili ajifiche vizuri.
dah! Umenikumbusha tambwe hiza, mwanzoni wakati anajiunga ccm alipewa kakitengo pale kwa kina nape, walipoona sasa amekwisha nasikia wamechukua cheo wamemuacha anashangaa tu!Hata mimi nilikua najiuliza kuhusu huyu jamaa. Ila alikosea sana kurudi gambani huyu ni sawa na akina Masumbuko Lamwai wamepotea kabisa hata ndugu yangu Tambwe Hiza wote hawa kushinei baada kurudia gamba
Acha kua unangea maneno yasio na msingi ilimradi tu uchangie mada bwana,ngoja nikufundishe kitu kaka,yani ni kwamba kuhama chama sio dhuluma kwa yeyote na sisi Wenye ujuzi huwa hatuangalii vyama kaka sisi huwa tunaangalia maendeleo kwa hiyo mtu sio lazima awe chadema au CUF ndo afanye maendeleo,kwahiyo kuhama chama kwa huyu bwana isiwe nongwa.