Dr. Tulia Ackson, nani amekutuma? Unataka nini? Kwanini?

Dr. Tulia Ackson, nani amekutuma? Unataka nini? Kwanini?

Kwani mkuu unafikiri watumishi wa umma hawana vyama? Akikosa nafasi ya kisiasa anarudi kwenye utendaji ambacho hakiruhusiwi ni kuonesha maslahi ya Chama kwenye utendaji basi.

Pata mantiki ya swali langu, jee huyo angegombea kwa tiketi ya NCCR kutafuta Uspika na akakosa angeruhusiwa kurudi kwenye nafasi yake au hilo linaruhusiwa kwa CCM pekee?
 
Wewe haujuı maana ya kada.Katiba inasema chama kitampendekeza mtu kinayetaka awe spika.Spika sıyo lazima mwanachama hata km ataungwa mkono au kupendekezwa na chama fulani.Huyo Atson hataweza kubabaishwa na bush lawyers wa UKAWA.Nı jembe balaah!
jembe shambani kwako labda.
 
Ag ni mwanasiasa kwa nature ya nafasi yake.Spika sio mwanasiasa,hvyo hakuna kosa wa kasoro.Ameomba nafasi hyo kupitia CCM km ambavyo angeweza kuomba kupitia ACT,NLD n.k.

Huyu pale wizarani anafanya kazi kama katibu mkuu,ndio maana WIZARA hiyo haina katibu mkuu,pia huyu ni Deputy Attorney General ambaye wakati mwingine huwa anaenda mahakamani kuitetea serikali au maslahi ya umma,pale ambapo serikali inawashtaki kijinai chadema,NA yeye akawa mmoja wa prosecutor,inaleta picha gani? Ni wazi picha ni kwamba kada wa Ccm kaanda hati za mashitaka, kada wa Ccm kwa kujificha kwenye cheo cha unaibu mwanasheria mkuu anawashitaki,hatakuwa fair,lazima ukada utamuongoza kuwakomoa wapi zani wake kisiasa,hata kama katika hali ya kawaida angetakiwa asipeleke mashtaka mahakamani
 
Naweza kuamini kuwa sasa umeshaanza kunogewa na vyeo. Ulianza kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba. Ukafuata kuwa kiongozi wa Kamati ya Bunge Maalum la Katiba. Kama hiyo haitoshi, ukateuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Sasa unataka Uspika wa Bunge.

Ukiwa ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, hukupaswa kujitokeza kisiasa na kugombea Uspika wa Bunge. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali si mtu mdogo. Ndiye Kaimu Mwanasheria Mkuu wa Serikali pale ambapo Bunge hufanyika kwakuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali huwa Bungeni Dodoma. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni mtu wa kitaifa zaidi.

Kujianikaanika kama kada wa CCM si jambo jema wala vutizi. Kutakuwa na kitu na watu wanaosababisha. Nani kakutuma? Unataka nini hasa? Kwanini? Dr. Tulia, umejianika kama kada. Watumishi wa Ofisi yako na wananchi kwa ujumla watakuonaje ikiwa utaendelea kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali?

Ili kulinda heshima yako, jiuzulu Unaibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali na urejee Shule Kuu ya Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ukahadhiri pale ambapo Uspika utagoma kupatikana. Ujiuzulu haraka!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
Mkuu VUTA-NKUVUTE ,
  1. Kugombea nafasi yoyote ya uongozi ni moja ya haki za kiraia ambayo kila Mtanzania ana haki hiyo na yuko huru kugombea nafasi yoyote, hivyo Dr. Tulia Akson hajavunja sheria, taratibu wala kanuni yoyote!.
  2. Viongozi wakuu wa vyombo vya dola, wote ni makada wa CCM!, nikimaanisha hata CDF, IGP, Mkurugenzi wa TISS, Jaji Mkuu, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru etc!. Tumemshuhudia Mboma akigombea ubunge!, Mahita akigombea ubunge!, Adadi sasa ni mbunge!, Apson akiongoza kamati ya EL!, etc, hivyo kama kosa ni kujionyesha, then Dr. Tulia ni too genuine kujificha nyuma ya cheo!.
  3. Nimetokea kumfahamu huyu dada, kwanza ni kichwa mbaya!. Nilijoin UDSM wakati yeye amemaliza LL.M na kuwa lecture, hivyo mwaka wangu wa kwanza, somo langu la kwanza ni Law of Contract, mwalimu wangu wa kwanza alikuwa huyu Tulia!. Kwa jinsi alivyo ki miss miss, enzi hizo akiwa mdogo, alionekana kama mtoto wa form Six anafundisha chuo kikuu, na sisi watu watu wa kanda ya Ziwa tunaudhaifu fulani, hivyo kila akifundisha watu wanaconcentrate na masomo, akina sisi mawazo yanatutuma kwenye mengine!, kufunga na kufungua somo lake nika supp, nikarudia nikashindwa ku clear!, hivyo nika carry over, mwalimu ndio huyo huyo!, nikashindwa ku clear nikazungusha!, yaani nikacheza DISCO!.
  4. Nadhani kwao wote ni vichwa!. Last born wao, ambaye pia ni binti, alitoka na 7 points O level, akatoka na 3 points A level na kuongoza kitaifa!.
  5. Kwa perfomance yake niliyoiona wakati wa BMK, kama CCM inataka tupate the best speaker, then watamteua Dr. Tulia, kitakachomponza labda ni ile flipy floppy ya Ana Makinda!.
  6. Tufike mahali moja ya sifa za nafasi ya uspika iwe kusomea sheria kiwango cha LL.M!.
Pasco
 
Makatibu wakuu wa WIZARA hawajawahi kugombea nafasi ya kisiasa wakiwa bado wameshikilia nafasi zao,DK tulia kwa cheo chake ni katibu mkuu,mbona makatibu wakuu wenzake hawawashwi hivyo? Huku nataka kule nataka,ndio maana wengi wenye PHD NA uprofesa ni wachache sana wanaojitambua,wenye digrii ya kwanza NA masters ndio wanafanya wonders,hivi huyu ataacha kumshauri rais asiteue mbunge kuwa mkuu wa mkoa?mbunge kuwa waziri? Kama yeye anataka mihimili yote aimiliki,anatunga sheria na anataka awe mtawala
 
Impartiality of her office as Deputy AG is in serious doubt(conflict of interests).
 
Pasco

Ahasante mkuu,umemaliza kazı.Wengi wanamwongelea huyu mama, hawamjui.
 
Last edited by a moderator:
Pasco

Naona umetoa hoja kama MTU asiyejitambua, sidhani kama umejadili kimantiki,umetumia hisia zaidi,sifa ya kuwa spika ni kwa kuwa alikudisko? Kwa kuwa mdogo wake alifaulu sana?sifa kuu unayoiona ni kujua sheria? Hapo bungeni ni mahakamani? Spika anatunga sheria? Au anaongoza mjadala na mwisho wa siku hana cha kupunguza wala kuongeza! Hovyo kabisa
 
Last edited by a moderator:
Kifungu gani cha sheria au kanuni kinamkataza kuwania hiyo nafasi?

Huoni kuwa dr atakuwa ana....kadi ya chama...na amejingiza kwenye maswala ya kisiasa alitakiwaa ajiuzulu....... sheria za utumishi wa uma zinaruhusu haya ???
 
Halafu Pasco eti ndio aliandaliwa kuwa afisa habari ofisi ya rais kama lowasa angeshinda
 
Last edited by a moderator:
VUTA-NKUVUTE

Kwa haya yanayotokea sasa nimeanza kumuelewa Fatuma Karume, kwenye kipindi cha Madamotto channel 10 aliulizwa kwanini msiende mahakamani kutaka tafsiri ya kufutwa kwa matoeo ya Zanzibar alisema kwenda mahakama ni Imani hivyo hatuna imani sana na wale watakao amua kesi hii kwani wanaonekana kuwa ni makada baadhi yao akatoa mfano wa Jaji Ramadhani amekwenda kugombea uraisi kupitia ccm na kuonyesha kadi yake wakati amefika mpaka hatua ya jaji mkuu hivyo imani itakuwa wapi ktk mahakama.

sasa huyu dada Tulia Ackson hasa shida yake ni nini? mpaka anafanya maamuzi ya kuwania uspika kupitia CCM wakati yeye ni mtumishi wa serikali tena Naibu mwanasheria mkuu wa serikali lini amekuwa kada wa CCM? je tafsiri yoyote ya kisheria anayoitoa inaweza kuwa sawa au itaengamia upande wa chama chake? sasa tunauwakika gani kama bwana Masaju Mwanasheria mkuu wa serikali kama si kada wa CCM?

Maoni yangu akishindwa kupata uspika ni vyema tena ni busara hakajiudhuru nafasi hio kwani tayari ameonekana kuwa ni kada wa CCM ni tafsiri gani atafanya ya kisheria yenye usawa kwa vyama vyote?
 
Last edited by a moderator:
Hata jaji mkuu alichukua fomu ya urais kupitia ccm. Na mwenyekit wa Zec naye
 
Huyu pale wizarani anafanya kazi kama katibu mkuu,ndio maana WIZARA hiyo haina katibu mkuu,pia huyu ni Deputy Attorney General ambaye wakati mwingine huwa anaenda mahakamani kuitetea serikali au maslahi ya umma,pale ambapo serikali inawashtaki kijinai chadema,NA yeye akawa mmoja wa prosecutor,inaleta picha gani? Ni wazi picha ni kwamba kada wa Ccm kaanda hati za mashitaka, kada wa Ccm kwa kujificha kwenye cheo cha unaibu mwanasheria mkuu anawashitaki,hatakuwa fair,lazima ukada utamuongoza kuwakomoa wapi zani wake kisiasa,hata kama katika hali ya kawaida angetakiwa asipeleke mashtaka mahakamani

Mkuu kuna watu hawaelewi kabisa.Ukirefer kesi ya ufafanuzi wa mita 200 iliyofunguliwa na UKAWA huyu naibu AG aliongoza jopo la mawakili wa Serikali kupinga madai ya Ukawa.
 
Huyo atakuwa wa kwanza kuondolewa kwenye hiyo kazi.
 
haya mambo yapo kila mahali mfano chadema kuteua viti maalum ilhali bado ni ccm ajabu kabisa.

Wewe lazima utakuwa uko kama hao wa kwenye Avatar yako yaani kifupi uko bwii
 
VUTA-NKUVUTE

Siyo kujianika, Kanuni za Utumishi wa Umma hazimruhusu kufungamana na chama chochote
 
Last edited by a moderator:
Pasco

Soma kanuni Na miongozo ya Utumishi wa umma, kwa nafasi yake hatakiwi kufungamana na chama, kuwa na wanasheria kama wewe wenye kwenda Na mihemuko badala ya sheria ni hatari sana
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom