Dr.Slaa: TBC ni adui wa Mabadiliko

Dr.Slaa: TBC ni adui wa Mabadiliko

Kipenzi Changu

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
58,055
Reaction score
134,368
Katibu mkuu wa Chadema,Dr.Slaa amesema TBC ni adui wa mabadiliko kutokana na tabia ya kukata matangazo mara kwa mara wapinzani wanapochangia bungeni, Kitendo alichofanyiwa Tundu Lissu si cha mara ya kwanza!

Ikumbukwe pia Dr. Slaa alikuwa bingwa wa kukatiwa matangazo. Hata Lissu mwenyewe amekuwa akifanyiwa hivyo mara kadhaa.

Source: Tanzania Daima
 
kwel wanaboa maana sisi wengine hatukamati star tv
 
Leo ndo msubili Gred ya taifa ya umeme inakatwa umeme nchi nzima kwa matengenezo kidogo yalioathiliwa na mvua zinazoendelea kunyesha kwenye baadhi ya mikoa mbalimbali.
 
Mkuu huyu katibu wa UKAWA naona sasa kakosa hoja kabisa kumbe likitokea tatizo la kitalamu imekuwa adui wa maendeleo mwambie kuwa yeye ndiye adui wa maendeleo anayenyanyasa vijana kwenye chama na kuwanyima fulsa za uongozi kwahofu ya kuzidiwa maalifa.
 
Huyu mzee naye kabakiza jina tu hakuna hata anachofanya kwa sasa kwenye ujenzi wa siasa na nchi hii kwa ujumla ni kutoa matamko tu basi.
 
Chadema si walisusia kuangalia TBC Sasa imekuwaje? Au wanaangalia kisiri sana??!.
 
Chadema si walisusia kuangalia TBC Sasa imekuwaje? Au wanaangalia kisiri sana??!.

Umeambiwa TBC wameingia mkataba na bunge kuonyesha shughuli za bunge la katiba. Kwa hiyo watu wanaangalia muda huo wa mkataba pekee.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Chadema si walisusia kuangalia TBC Sasa imekuwaje? Au wanaangalia kisiri sana??!.

Hiyo ni hoja dhaifu sana wanaoangalia mjadala huu wa bunge la Katiba siyo CDM peke yao, wapo watu wengi wanaotaka kujua juuu ya mijadala inayoendelea. Tunapaswa kupata hoja za watu wote hata kama tunatofautiana nao, TBC wanachofanya ni upuuzi ambao tukipata Katiba mbovu itawaathiri wao na hata watoto wao. TBC iachie wajumbe washindane kwa hoja siyo kwa mbinu chafu.
 
Mkuu huyu katibu wa UKAWA naona sasa kakosa hoja kabisa kumbe likitokea tatizo la kitalamu imekuwa adui wa maendeleo mwambie kuwa yeye ndiye adui wa maendeleo anayenyanyasa vijana kwenye chama na kuwanyima fulsa za uongozi kwahofu ya kuzidiwa maalifa.

Naona unaweka maneno kufurahisha nafsi, si kuboresha mjadala. Kuna cheo kinaitwa 'Katibu wa UKAWA'? Labda kama umekianzisha kwenye comment yako hii.

Soma kwa makini, conclusion ya Katibu Mkuu Dkt. Slaa haiko event-driven kwa kuangalia tukio la juzi pekee, bali trend ya chombo hicho. Ndiyo maana umekumbushwa kilichokuwa kikitokea wakati Dkt. Slaa alipokuwa Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni na mbunge mahiri bungeni, namna ambavyo TBC hawa hawa walikuwa wakifanya waliyofanya juzi.

Lakini pia conclusion hiyo haijafanyika kw akuangalia matangazo ya Bunge Maalum la Katiba pekee, bali trend ya TBC katika masuala mengi mengi ambayo si tu yanakwenda kinyume na matakwa na maslahi ya wananchi (mabadiliko) bali pia yanakinzana na taaluma, weledi na maadili ya uandishi wa habari. That's very serious kuliko unavyoweza kufikiri wewe.

Tunajua mathalani ambavyo siku hizi Waziri amekuwa akichagua nani na nani wahojiwe pale nje ya bunge au kwenye Kipindi cha Jambo asubuhi. Tunajua....tunajua...

Kama ni suala la fursa kwa vijaa, CHADEMA chini ya uongozi wa Mwenyekiti Mbowe na Katibu Mkuu Dkt. Slaa, imekuwa mfano wa kuigwa kwa vyama na taasisi zingine nchini namna ambavyo kimetoa fursa na kujenga mazingira ya kuwakuza, kuwajenga na kuwatumia vijana kutimiza majukumu makubwa kwa ajili ya umma. Matunda yake yanaonekana.
 
Chadema si walisusia kuangalia TBC Sasa imekuwaje? Au wanaangalia kisiri sana??!.

Kuna pesa za walipa kodi hapo...zilizotumika na bunge kuingia mkataba na TBC kufanya matangazo ya moja kwa moja ya bunge. Lazima wawe responsible and accountable.
 
Huyu mzee naye kabakiza jina tu hakuna hata anachofanya kwa sasa kwenye ujenzi wa siasa na nchi hii kwa ujumla ni kutoa matamko tu basi.

Kauli kama hii labda inaweza kumfaa yule mkuu wa nchi ambaye aliwahi kutamka hadharani, wananchi wake wakimsikia na dunia ikimsikiliza kwamba hajui kwa nini wananchi wake na nchi yake ni maskini. Mtu wa namna hii ndiyo hawajui wanachokifanya na bila shaka wataacha 'majina' tu...
 
Mkuu huyu katibu wa UKAWA naona sasa kakosa hoja kabisa kumbe likitokea tatizo la kitalamu imekuwa adui wa maendeleo mwambie kuwa yeye ndiye adui wa maendeleo anayenyanyasa vijana kwenye chama na kuwanyima fulsa za uongozi kwahofu ya kuzidiwa maalifa.

Hilo tatizo la kitaalam mbona halijatokea wakati kigwangalla anawasilisha utumbo?
 
katika suala la kitaifa hasa hili la katiba c lakufanyia mzaha kama TBC wanavyolichukulia aisee...TBC wanafanya uhuni uliokidhiriii..wanafanya uhahini kabisa wanawanyima wananchi taarifa muhimu za kitaifa.chombo cha serikali kinachoendeshwa na wananchi kwa kulipa kodi mbalimbali za nchii.TBC kuna takiwa kufanywe reshaflle ya nguvu kuanzia mkurugenzi hadi staffs wake sababu tumechoshwa na utendaji wao wa kazi hasa huu wa kukata matangazo kisa ati wao ndio dominance wa kuonyesha bunge la katiba hiyo HATUTAKI tunataka pia uwepo wa vyombo vingine vya habari vyenye uwezo wakurusha matangazo ya katiba live fro mjengoni DODOMA.
 
Kama TBCCM wameshindwa kutekeleza masharti ya mkataba, basi wajitoe ili kazi hiyo ifanywe na ITV Daima. Magamba naomba mtulie dawa iingie---Dr Tundu Antipas atakuwepo Mjengoni Hospitali leo kuanzia saa 3 asubuhi kuwapa dozi kamili dhidi ya ugonjwa wa kichaa unowasumbua magamba. Hata mkitaka chanjo mtapata leo---tulieni mtibiwe mpate kupona.
 
Mkuu huyu katibu wa UKAWA naona sasa kakosa hoja kabisa kumbe likitokea tatizo la kitalamu imekuwa adui wa maendeleo mwambie kuwa yeye ndiye adui wa maendeleo anayenyanyasa vijana kwenye chama na kuwanyima fulsa za uongozi kwahofu ya kuzidiwa maalifa.

Nikweli kabisa....
View attachment 151253
 
Naona unaweka maneno kufurahisha nafsi, si kuboresha mjadala. Kuna cheo kinaitwa 'Katibu wa UKAWA'? Labda kama umekianzisha kwenye comment yako hii.

Soma kwa makini, conclusion ya Katibu Mkuu Dkt. Slaa haiko event-driven kwa kuangalia tukio la juzi pekee, bali trend ya chombo hicho. Ndiyo maana umekumbushwa kilichokuwa kikitokea wakati Dkt. Slaa alipokuwa Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni na mbunge mahiri bungeni, namna ambavyo TBC hawa hawa walikuwa wakifanya waliyofanya juzi.

Lakini pia conclusion hiyo haijafanyika kw akuangalia matangazo ya Bunge Maalum la Katiba pekee, bali trend ya TBC katika masuala mengi mengi ambayo si tu yanakwenda kinyume na matakwa na maslahi ya wananchi (mabadiliko) bali pia yanakinzana na taaluma, weledi na maadili ya uandishi wa habari. That's very serious kuliko unavyoweza kufikiri wewe.

Tunajua mathalani ambavyo siku hizi Waziri amekuwa akichagua nani na nani wahojiwe pale nje ya bunge au kwenye Kipindi cha Jambo asubuhi. Tunajua....tunajua...

Kama ni suala la fursa kwa vijaa, CHADEMA chini ya uongozi wa Mwenyekiti Mbowe na Katibu Mkuu Dkt. Slaa, imekuwa mfano wa kuigwa kwa vyama na taasisi zingine nchini namna ambavyo kimetoa fursa na kujenga mazingira ya kuwakuza, kuwajenga na kuwatumia vijana kutimiza majukumu makubwa kwa ajili ya umma. Matunda yake yanaonekana.
Vipi unakubaliana na hili?
View attachment 151256
 
Huyu mzee naye kabakiza jina tu hakuna hata anachofanya kwa sasa kwenye ujenzi wa siasa na nchi hii kwa ujumla ni kutoa matamko tu basi.

kwa vyovyote umewahi kumchungulia mama yako chooni.
 
Back
Top Bottom