Hakikwanza
JF-Expert Member
- Dec 11, 2010
- 4,034
- 1,003
Mpaka sasa hatma yako juu ya CHADEMA ni kizungumkuti, toka Mh Lowasa alipo jiunga na CHADEMA na kupewa form ya kugombea urais. Nikuombe Dr. Slaa tunaomba utoe msimamo wako ili kuiondoa sintofahamu hii. Pia msimo wako ujue kuwa Tanzania inahitaji ukombozi kwa njia yeyote toka mikono ya mfumo dhalimu na fedhuri wa CCM. Watanzania walio wengi wanasubiri msimamo wako wafanye maamuzi sahihi.
Tahadhari hakuna adui wa kudumu hasa anapoungana nawe na kukusaidia kupambana na adui zako anao wajua fika either kwa kuwa pamoja nao. Tunakuomba usamehe yote kiongozi wetu mpendwa ili tuikomboe nchi. Urais ni taasisi, nina imani tutashinda tukiwa pamoja na tutashindwa tukigawanyika. Watanzania wanaimani sana na UKAWA hivyo ni muda wa kushikamana, kukubaliana na kupendana kuliko kipindi chochote kile. Mungu ibariki Tanzania na UKAWA.
Tahadhari hakuna adui wa kudumu hasa anapoungana nawe na kukusaidia kupambana na adui zako anao wajua fika either kwa kuwa pamoja nao. Tunakuomba usamehe yote kiongozi wetu mpendwa ili tuikomboe nchi. Urais ni taasisi, nina imani tutashinda tukiwa pamoja na tutashindwa tukigawanyika. Watanzania wanaimani sana na UKAWA hivyo ni muda wa kushikamana, kukubaliana na kupendana kuliko kipindi chochote kile. Mungu ibariki Tanzania na UKAWA.