Najua CUF na Chadema ni vyama tofauti sana na vyenye malengo tofauti. Hata hivyo ukweli ni kwamba Chadema tunawahitaji sana CUF kwa ajili ya kufanikisha mambo mengi. Kwanza ni swala la katiba, CUF wameshika sehemu nyeti maana bila wao katiba haiwezi kupita maana wana zaidi ya 1/3 ya bunge la katiba na referandum pia. Ila kuna mambo chadema na cuf wanakubaliana na hasa serikali tatu na tume huru ya uchaguzi. Pia pamoja na tofauti zilizopo, tunaweza kukubaliana na CUF wao wakatoa mgombea mwenza uchaguzi ujao. Bado ccm wana mbinu za kushinda hivyo umoja ni muhimu sana. Namshauri Dr Slaa baada ya uchaguzi wa uzini akutane na Seif kuangalia uwezekano wa kushirikiana angalao kwenye katiba. Nadhani ndugu zangu mnaona busara kwa hili, nadhani Dr Slaa ataona busara ya ushauri wangu