Bitabo
JF-Expert Member
- Sep 27, 2011
- 1,900
- 687
Wakuu namuomba Dr Slaa arudi kazini na aokoe hili jahazi. gafla nahisi chama kimepoa mno. Mbowe hasikiki, Slaa nadhani mambo ya ndoa yalikuwa yanamaliza mda na sasa yameisha arudi,. Mambo ya hotuba ya Mnyika ya nishati na madini na mchango wa Selasini umetuachia maswali mengi hasa sisi ambao hatuko ndani ya ''system''. Shutuma juu ya Zitto hasa hili la Tanesco na la uraisi. Swala la Singida na mauaji baada ya mkutano. Dr Slaa nadhani ni wakati muafaka uje mbele ya hadhara na useme lolote ili watanzania tujue CHADEMA inamtizamo gani juu ya haya na mengine ambayo hatujayasikia. Ukimya wenu unafanya wengine tuhisi kuwa kuna msuguano ndani ya chama. Nawasilisha