Mungi
JF Gold Member
- Sep 23, 2010
- 16,975
- 9,580
Leo saa 3:45 usiku Dr Slaa atakuwa Star Tv na Dotto Bulendu.........
Stay tuned!!
========
UPDATES:
Stay tuned!!
========
UPDATES:
Katiba; wananchi wanawaambia waatawala tunataka tuongozwe hivi, si watawala kuwaambia wananchi.
Katiba haitungwi na watawala wala si maelekezo ya serikali kwa wananchi.
Kaburungu na Rugaijamu
Kuna haja gani ya kujibizana na watu ambao mnajua wamekuja hapa makusudi kuwaondoa kwenye mjadala.
Daktari anaendelea kushusha nondo za ukuu wa katiba.
Naona jamaa wa Dar naye yuko sawasawa anassanasema CCM haiko katika misingi ya haki. Anasema kiuhalisia serikali tatu zimekuwepo siku zote.
Huyu Mzee hapa anapiga nondo. Anasema wananchi wameshirikishwa kinadharia. Anamshangaa Rais kwenda kutoa hotuba kupingana na maoni ya wananchi. Tena kwa kuelekeza. Mwananchi Solomon anakubaliana na Daktari Slaa kuwa katiba inapaswa kutokana na wananchi na kwamba hotuba ya Kikwete ilichanganya wananchi.
Maridhiano yatawezekana tu endapo Luna utashi wa kisiasa. CCM inalazimisha mambo yake kuwekwa kwenye katiba.
Kwa suala la katiba yuko tayari hata kuamushwa usiku wa manane kuzungumzia masuala ya watu.
Muda umekuwa mchache mno.Dr Slaa anaweza kuzungumza hata masaa matano na watu wakamsikiliza bila kuchoka.Rais wa Watu.