Seif al Islam
JF-Expert Member
- Nov 14, 2011
- 2,156
- 640
Imefahamika sasa kuwa katibu mkuu wa Chadema Dr.Wilbroad Slaa hatogombea urais kupitia chama hicho katika uchaguzi mkuu wa 2015 tofauti na inavyodhaniwa na wanachama, wapenzi na wafuasi wa chadema.taarifa za kuaminka toka ndani ya uongozi wa juu wa Chadema makao makuu zinaeleza kuwa chama hicho kimejipanga "kunufaika" na mnyukano uliopo ndani ya ccm kuhusu mgombea urais huku kikijipanga "kumsajili" mmoja wa makada wa ccm atakaeonekana kuwa na nguvu katika kinyang'anyiro cha uteuzi wa mgombea urais kupitia CCM (bila kujali "taswira" yake mbele ya jamii) kama ilivyokuwa kwa Mrema na NCCR- Mageuzi katika uchaguzi wa 1995.
Kuibuka kwa taarifa hizi kumekuja wakati ambapo wanaotajwa kuusaka urais kupitia ccm wakijipanga na kuunda makundi ndani na nje ya ccm ili kujiimarisha kuelekea 2015.uwanja mwingine wa mapambano ya urais umekuwa bunge maalumu la katiba ambalo linadaiwa kuwa turufu pekee ya Samwel Sitta ambaye ametajwa kuwa mmoja wa walengwa wanaosubiriwa chadema iwapo watatemwa na ccm.wengine ni pamoja na edward lowassa na Fredrick Sumaye ambaye imeelezwa kuwa "havutii sana".Hii ni mara ya pili kwa Lowassa kuhusishwa na mipango ya kujiunga chadema hasa baada ya aliyekuwa kada wa ccm na mfuasi mkuu wa Lowassa huko Arusha Bw.James ole Millya kujiunga chadema.
Nawasilisha
Kuibuka kwa taarifa hizi kumekuja wakati ambapo wanaotajwa kuusaka urais kupitia ccm wakijipanga na kuunda makundi ndani na nje ya ccm ili kujiimarisha kuelekea 2015.uwanja mwingine wa mapambano ya urais umekuwa bunge maalumu la katiba ambalo linadaiwa kuwa turufu pekee ya Samwel Sitta ambaye ametajwa kuwa mmoja wa walengwa wanaosubiriwa chadema iwapo watatemwa na ccm.wengine ni pamoja na edward lowassa na Fredrick Sumaye ambaye imeelezwa kuwa "havutii sana".Hii ni mara ya pili kwa Lowassa kuhusishwa na mipango ya kujiunga chadema hasa baada ya aliyekuwa kada wa ccm na mfuasi mkuu wa Lowassa huko Arusha Bw.James ole Millya kujiunga chadema.
Nawasilisha