Dr. Slaa kutogombea urais 2015 kupitia CHADEMA

Dr. Slaa kutogombea urais 2015 kupitia CHADEMA

Lumumba wakisikia habari hii njema watafurahi sana, maana haya majina mawili yaani DR.Slaa na Mbowe ndiyo kikwazo kikuu kwao - yanawanyima usingizi kabisa.
 
nimeipenda, ongeza juhudi sana kufikia 2025 utakuwa mwandishi na reporter mzuri sana. Usiiache hii kazi ya ushushu.
 
Lumumba wakisikia habari hii njema watafurahi sana, maana haya majina mawili yaani DR.Slaa na Mbowe ndiyo kikwazo kikuu kwao - yanawanyima usingizi kabisa.

Hapana, tunatoa tahadhari kwa watanzania kwa kuwa tunawafahamu kuwa ni malaghai
 
Aseme ameshtuka tu kupoteza ulaji wa bungeni!
 
Imefahamika sasa kuwa katibu mkuu wa Chadema Dr.Wilbroad Slaa hatogombea urais kupitia chama hicho katika uchaguzi mkuu wa 2015 tofauti na inavyodhaniwa na wanachama, wapenzi na wafuasi wa chadema.taarifa za kuaminka toka ndani ya uongozi wa juu wa Chadema makao makuu zinaeleza kuwa chama hicho kimejipanga “kunufaika” na mnyukano uliopo ndani ya ccm kuhusu mgombea urais huku kikijipanga “kumsajili” mmoja wa makada wa ccm atakaeonekana kuwa na nguvu katika kinyang’anyiro cha uteuzi wa mgombea urais kupitia CCM (bila kujali “taswira” yake mbele ya jamii) kama ilivyokuwa kwa Mrema na NCCR- Mageuzi katika uchaguzi wa 1995.

Kuibuka kwa taarifa hizi kumekuja wakati ambapo wanaotajwa kuusaka urais kupitia ccm wakijipanga na kuunda makundi ndani na nje ya ccm ili kujiimarisha kuelekea 2015.uwanja mwingine wa mapambano ya urais umekuwa bunge maalumu la katiba ambalo linadaiwa kuwa turufu pekee ya Samwel Sitta ambaye ametajwa kuwa mmoja wa walengwa wanaosubiriwa chadema iwapo watatemwa na ccm.wengine ni pamoja na edward lowassa na Fredrick Sumaye ambaye imeelezwa kuwa “havutii sana”.Hii ni mara ya pili kwa Lowassa kuhusishwa na mipango ya kujiunga chadema hasa baada ya aliyekuwa kada wa ccm na mfuasi mkuu wa Lowassa huko Arusha Bw.James ole Millya kujiunga chadema.

Nawasilisha

Wala sishangai kwa sababu Slaa hakuwa president material na alikuwa na special mission to deliver. Kwa kuwa ameshakamilisha mission yake na kulipwa stahili zake, unachokisema kna ukweli wa asilimia nyingi.
 
Usipoteze muda wako kuamini anachosema Mbowe,ebu rudi nyuma jikumbushe sakata la shangingi l seriakli (KUB) na sasa liko wapi.

Kwa nini huwa hamsomi post nzima neno kwa neno and in detail kabla ya kujibu?

Did you understood what I wrote?
 
Mwisho utasema na MAALIM SEIF NAYE atagombea kwa ticket ya cdm.
 
Imefahamika sasa kuwa katibu mkuu wa Chadema Dr.Wilbroad Slaa hatogombea urais kupitia chama hicho katika uchaguzi mkuu wa 2015 tofauti na inavyodhaniwa na wanachama, wapenzi na wafuasi wa chadema.taarifa za kuaminka toka ndani ya uongozi wa juu wa Chadema makao makuu zinaeleza kuwa chama hicho kimejipanga “kunufaika” na mnyukano uliopo ndani ya ccm kuhusu mgombea urais huku kikijipanga “kumsajili” mmoja wa makada wa ccm atakaeonekana kuwa na nguvu katika kinyang’anyiro cha uteuzi wa mgombea urais kupitia CCM (bila kujali “taswira” yake mbele ya jamii) kama ilivyokuwa kwa Mrema na NCCR- Mageuzi katika uchaguzi wa 1995.

Kuibuka kwa taarifa hizi kumekuja wakati ambapo wanaotajwa kuusaka urais kupitia ccm wakijipanga na kuunda makundi ndani na nje ya ccm ili kujiimarisha kuelekea 2015.uwanja mwingine wa mapambano ya urais umekuwa bunge maalumu la katiba ambalo linadaiwa kuwa turufu pekee ya Samwel Sitta ambaye ametajwa kuwa mmoja wa walengwa wanaosubiriwa chadema iwapo watatemwa na ccm.wengine ni pamoja na edward lowassa na Fredrick Sumaye ambaye imeelezwa kuwa “havutii sana”.Hii ni mara ya pili kwa Lowassa kuhusishwa na mipango ya kujiunga chadema hasa baada ya aliyekuwa kada wa ccm na mfuasi mkuu wa Lowassa huko Arusha Bw.James ole Millya kujiunga chadema.

Nawasilisha
Hili la Dr. Slaa kugombea au kutogombea, watu tunajua toka 2011!. Nisome hapa [h=3]Urais 2015 tusimlaumu Zitto; Nani anaujua Msimamo wa Dr Slaa?!.[/h]Pasco
 
Back
Top Bottom