Chungurumbira
JF-Expert Member
- Jan 3, 2013
- 2,170
- 571
Sijui taratibu za kanisa lakini sidhani kama anaweza kurudi ghafla ghafla. Watanzania inabidi tujifunze kutokuwasaliti watu wanaopigania mambo tunayoyaamini...
Shocking, taratibu tutawaelewa.Kwasasa lengo ni kumng'oa mkoloni, hata Chenge akija tutampokea, hayo mengine baadae.
CCBRT alifukuzwa pia?
Mkuu, haya ni mambo ambayo wewe unayemkubali Dr. Slaa ulipaswa kusimamia kidete kuhakikisha hadhalilishwi kwa kuendelea kuyapigania. Lugha ile ya Dr. Slaa usikubali ipotee na pia usikubali Dr. Slaa adhalilishwe kwa sababu ya malipo ya posho.
You need to stand up and "fight" for what you believe in. Usikubali kupelekeshwa na waliouza Chama...
Sasa nimegundua logic ya mada yako ,unachotaka kiwatengenezea watu ili waamini ni kuwa.
1-Chama kimeuzwa
2-Alionewa
3-Utaratibu wa kumpata ugombea uraisi haukufuatwa..
Una vitu vingi unavitengeneza kadiri wachangiaji wanavyo changia.
Nnakushauri kajipange tena sababu hizi mbinu ni za kizamani sana na wewe umeganda sehemu moja tu .
Mbona waokota makopo hapa Dar wako wengi tu au nao unasemaje? Na wengine siku ya Ijumaa pale msikiti wa waarabu utawakuta wa mama na wa baba na heshima zao wamekaa mkao wa kusubiria chochote! Dr. Slaa pekee ndiye Jobless!!??
Unaniuliza mie? Kwani mie ndiyo nilimuajiri?
Unanchekesha!
Mkuu, hivi kwanini haujali welfare ya Dr. Slaa?
Wazo zuri.
Naamini Mohammedi Mtoi angeifanya hii kazi kwa ufanisi ila yuko busy na ubunge.
Mkuu Mwita Maranya jaribu kuangalia hili...
Tutawaonea huruma wengi mwaka huu mbona wale 16 wamekosa kura za maoni na wengine kupigana nao si wanakuwa kwenye kundi hilo? Au Dr Slaa tu ndo anakuwa Jobless kwa mtizamo wa ZeMarcopolo? Alishasema atazungumza muda ukifika kama ni kuonewa huruma ni muda huo kwa nini sisi waBongo tunapenda kuendekezaendekeza mambo yasiyo na tija? Kwani akiwa 'jobless' yeye ndo na wewe umekuwa jobless? Habari hii imekaa sijui kinamna gani....haina mashiko!!!!Mkuu, sidhani kama binadamu mwenye moyo anaweza kuacha kuguswa na kinachomsibu Dr. Slaa. Kama tulivyomhurumia Zitto hatuwezi kuacha kumhurumia Slaa. Lakini huruma pekeyake haitoshi, something more than just huruma needs to be done...
Dr. Slaa ameingia rasmi kwenye kundi la watu jobless nchini.
Wakati Mbowe alipowatangazia wajumbe wa baraza kuu la Chadema kuwa Dr. Slaa anaachwa na mawimbi na muda kuna jambo hakulisema kwa ukamilifu.
Katika muda huu ambao Slaa hatashiriki shughuli za chama, hatalipwa mshahara wala posho. Hali hii inamfanya Slaa moja kwa moja kukidhi vigezo vya kuitwa jobless.
Kwa vile Josephine ni mwanamke mpambanaji, anaendelea "kusimamia show" nyumbani katika kipindi hiki ambacho mzee hana kipato.
Ingefaa sana jamii ya watu wanaothamini mchango wa Dr. Slaa wasimame kwa pamoja kumuonyesha kumjali. Kuna njia mbalimbali za kufanya hivyo ikiwa ni pamoja na kuchanga sadaka na kumpelekea.
Mpaka sasa alichopigania Slaa ndani ya CHADEMA kimekuwa defeated na matukio ya hivi karibuni yanadhihirisha kuwa Slaa amekubali matokeo. Hata hivyo, jamii ikimpa nguvu anaweza kupata mawazo na mbinu mpya za kusimamia anachoamini. Kwahiyo ni jambo muhimu kwa jamii inayoamini uwezo wa Dr. Slaa kuchukua hatua za haraka kumuonyesha imani yao kwake.
Wako wapi watanzania wanaosimamia haki na usawa?
Ni wazi kuwa Slaa anadhulumiwa, je mmeungana na waliomtosa Slaa?
Kinachomtokea Slaa sasa hivi kinaweza kuwa fundisho kwa wazee wanaofanya kazi zisizo na pension. Jinsi jamii itakavyolichukua jambo hili pia ni fundisho kwa wengine.
Siasa si ajira!
nakuunga mkono watafutwe watu wenye majina na waaminifu wachangishe fedha hizo na kupitia media watutangazie namna ya kuchangia fedha hizo
i wish you all the best Dr Slaa
Kwa kweli hata mimi ni mfuasi wa Dr. Slaa ni hakuna mfano. Akiitisha mchango wa maisha nitamchangia kama nilivyochangia kukomboa shangingi la Mrema miaka hiyo. God bless you Dr. Dlaa
Dr.Slaa ni Katibu Mkuu wetu
Wambea mna kazi mwaka huu.Tafuteni namna ya kurasimishwa muwe sekta rasmi mlipe kodi sasa
Dr. Slaa ameingia rasmi kwenye kundi la watu jobless nchini.
Wakati Mbowe alipowatangazia wajumbe wa baraza kuu la Chadema kuwa Dr. Slaa anaachwa na mawimbi na muda kuna jambo hakulisema kwa ukamilifu.
Katika muda huu ambao Slaa hatashiriki shughuli za chama, hatalipwa mshahara wala posho. Hali hii inamfanya Slaa moja kwa moja kukidhi vigezo vya kuitwa jobless.
Kwa vile Josephine ni mwanamke mpambanaji, anaendelea "kusimamia show" nyumbani katika kipindi hiki ambacho mzee hana kipato.
Ingefaa sana jamii ya watu wanaothamini mchango wa Dr. Slaa wasimame kwa pamoja kumuonyesha kumjali. Kuna njia mbalimbali za kufanya hivyo ikiwa ni pamoja na kuchanga sadaka na kumpelekea.
Mpaka sasa alichopigania Slaa ndani ya CHADEMA kimekuwa defeated na matukio ya hivi karibuni yanadhihirisha kuwa Slaa amekubali matokeo. Hata hivyo, jamii ikimpa nguvu anaweza kupata mawazo na mbinu mpya za kusimamia anachoamini. Kwahiyo ni jambo muhimu kwa jamii inayoamini uwezo wa Dr. Slaa kuchukua hatua za haraka kumuonyesha imani yao kwake.
Wako wapi watanzania wanaosimamia haki na usawa?
Ni wazi kuwa Slaa anadhulumiwa, je mmeungana na waliomtosa Slaa?
Kinachomtokea Slaa sasa hivi kinaweza kuwa fundisho kwa wazee wanaofanya kazi zisizo na pension. Jinsi jamii itakavyolichukua jambo hili pia ni fundisho kwa wengine.