Kwa kawaida hakuna mtu anaweza kwenda na kuanza kupiga mawe kwenye mti usio na matunda ataonekana chizi,bali mti wenye matunda ndio unaopigwa mawe ili kupata matunda yake,ndivyo ilivyo kwa Dr.W.P.Slaa anashambuliwa kila kona ili umdhoofisha kwa sababu mpaka sasa hakuna mbadala wake Tanzania,Anashambuliwa kutoka serikalini,CCM,vyama ingine vya upinzani na hata ndani ya CHADEMA.lakini ukitaka kuamini Dr.Slaa hana mpinzani itisha mkutano popote Tanzania leo waambie wananchi anakuja Dr.Slaa itakushangaza umati utaofurika.
Hili hakuna mtu asiyelijua hata anayekataa ni kwa sababu ya chuki,lakini ukweli utabaki palepale na kila mtanzania anajua hivyo ndivyo ilivyo.Hivyo ningeshauri watanzania badala ya kuendelea kumshambulia kwa lengo la kummaliza kisiasa ni vema tugeuke tumtie moyo na kumuunga mkono tukijua ana kitu cha tofauti ambacho Mungu amekiweka kwake ili kuwa msaada kwa Taifa hili.