Dr. Slaa amfuata Lipumba

Dr. Slaa amfuata Lipumba

Amefika Bei??

Hakufika BEI alipokuwa anainadi CDM atafika BEI leo alipoifikisha mpaka FISADI LOWASSA anaiona CDM?Mtakuwa wa choyo wa fadhila.Tusipende kuamini kila kitu kiandikwacho kwenye haya magazeti yanayotafuta profit kwa damu za watanzania.
 
  • Thanks
Reactions: nao
slaa na lipumba wana akili kuliko mamilioni ya wanaukawa wanaotembea kama misukule wakifuata mawazo ya mbowe bila hata tafakuri
 
we mzee hakuna utakachoongea ukubalike,sisi tunataka mabadiliko sio kitu kingine.tunaakika umenunuliwa nendaaa salama.
uso wako na lipumba sijui mtaweka wapi ukawa wakishinda.

Alaaa kumbe
 
Kama ni hivyo basi na aende zake sisi haturudi nyuma. Huku kanda ya ziwa tumeshaamua tayari ni lowasa tu kwani magufuri hawezi ndani ya mfumo wa kijizi na kulindana na pengine tungesema labda kama kuwa na Rais au waziri mkuu ni faida mbona nyerere ametuacha vibaya au hata alikotoka pinda au sumayi kote choka mbaya bora Kwa lowasa monduli kidogo pameendelea. Urais wa magufuri ni wa kwake, Familia yake na wezi wenziye haupati ng'o mambo yote Kwa lowasa.

Si rahis kabisa kwa namna yoyote ile huyu ndugu yenu aende ikulu, mtajifariji wee, mtajipa matumaini weee, mtanunu bodaboda ili kuwaaaminisha watanzania kuwa mnakubalika lakini mwisho wa siku mtashangaa macho yenu, hii nchi si ya wahuni, ni nchi inayoendeshwa kwa misingi ya kidemokrasia na ustarabu. Magufuli ana record yake nzuri tu ambayo ameipata chini ya mfumo huu huu tena amaeshine kweli. ebu waza kidogo na 25.10.2015 mpe mamlaka kamili uone kazi itakavyokuwa mchakamchaka, sio wale wanaoimba mchaka mchaka wakati hawawezi huo mchakamchaka
 
Gazeti la udaku hilo hakuna ukweli hatutaki unafiki wala umbea tunasubiri kauli ya Dr.Slaa mwenyewe.
 
Nakupenda sana Dk,ila nafikiri ulichokipanda moyoni mwetu ni uzalendo na mabadiliko..na ndo haya yamekuja na wewe unatutosa...hatutaenda na wewe ila kweli tutakukumbuka!
 
leo hii mnamtukana dr slaa kweli nyinyi chadema

Unaona raha sana kufarakanisha eh? Mbona sijaona tusi kokote hapa, au macho yangu hayaoni? swala la Dr. Slaa bwana ni la kuacha kama lilivyo na utashi wake uheshimiwe maana hapa tunajaribu tu kufikiri na labda ziko nyingi. All in all anachotakiwa tu kukumbuka Dr. ni kuwa Lowasa nae ni mwanadamu, ampe chance ya kuprove wrong tuhuma zote anazotupiwa na alitotuhumiwa kwa kuwatumikia watanzania kiukweli. Watu hubadilika kwa hiyo si vyema kushikilia makosa ya zamani kihivyooo. Hata yeye alibadilika, alikuwa kasisi awali akaacha, tumhukumu? No tunaheshimu utashi wake
 
Kama ni hivyo basi na aende zake sisi haturudi nyuma. Huku kanda ya ziwa tumeshaamua tayari ni lowasa tu kwani magufuri hawezi ndani ya mfumo wa kijizi na kulindana na pengine tungesema labda kama kuwa na Rais au waziri mkuu ni faida mbona nyerere ametuacha vibaya au hata alikotoka pinda au sumayi kote choka mbaya bora Kwa lowasa monduli kidogo pameendelea. Urais wa magufuri ni wa kwake, Familia yake na wezi wenziye haupati ng'o mambo yote Kwa lowasa.
monduli ingekiwa safi wamasai wasingekuwa wanalala nje na kuuza ugoro
 
Naamini sana misimamo ya slaa hawezi kukaa na mafisadi.
 
Dr Slaa shikamoo unajitambua,maana ingekuwaje uketi meza moja na Lowassa mwenye utitiri wa kashfa na wewe wazijua,Kama ulivyozimwaga Mwembeyanga,Heko Slaa imeipa raha nafsi Yako na kukataa kula matapishi
 
Nyumba haiwezi kuanguka bila kuwa na mpasuko. Lowassa alipaswa kufanya alivyo fanya, upinzani kuwa na nguvu isingewezekana bila ccm kupasuka. bila kukaribishwa Lowassa cdm isingewezekana ccm kupasuka. wenyeviti wa mikoa wanavyo acha uongozi na kumfuata lowassa inatia hamasa na kuona kwamba ccm imepasukia mikononi mwa kikwete.

Ukimya alio ufanya Dr. Slaa anaonesha kuwa na busara za hali ya juu. Huwezi kumfananisha Dr. Slaa na Prof Lipamba -VU
 
Dr slaa pamoja na lipumba hao walikua wanagombania kupewa tiketi ya kugombea urais kupitia ukawa sasa kete Imegeuka wamekasirika na hakuna kinachowasumbua zaidi ya uroho wa madaraka
 
Nenda Dk. Slaa hakika utaishi ndani ya moyo wangu mpaka kufa kwangu, hakika wewe ni mwanasiasa pekee hapa Tanzania kuwahi kutokea ***Mungu akubariki Dk****

Kwani ni bwana wako ili umuweke Moyoni?. Acha ujinga wa kiccm.
 
we mzee hakuna utakachoongea ukubalike,sisi tunataka mabadiliko sio kitu kingine.tunaakika umenunuliwa nendaaa salama.
uso wako na lipumba sijui mtaweka wapi ukawa wakishinda.

Yeye hakumbuki kwamba na yy alitoka CCM, mbowe akamuachia agombee Leo mafuriko yamekuja anakimbia,ss tunasonga na mpaka tuone mwisho
 
Back
Top Bottom