Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

Haya ndio matatizo la kuchanganya siasa na uchumi. Kwa kumtendea visivyo Dr. Slaa, je huyo meneja ameonyesha ukomavu wa kutaaluma? Je, amevutia wateja au amewafukuza?

Kwa kuzima umeme siku nzima ili kumkomoa Dr. Slaa, umesimamisha shughuli zenye thamani kiasi gani ambazo utekelezaji wake huhitaji nishati ya umeme? Kwa utendaji huu, tusitegemee maendeleo yoyote.
 
Jamani huyu Meneja anaitwa Jacob Sumary ni ndugu yake na Sioi Sumary aliyegombea ubunge na Joshua Nassary huku Arumeru Mashariki, Nasary alivyompiga chini Sioi kwa ushirikiano mkubwa kabisa na viongozi wote wa CDM akiwemo Dr. Slaa sasa huyo Meneja ndo kalipa kisasi kwa njia hiyo. Nadhani kajidanganya coz Dr atalala popote mpaka kitakapoeleweka
 
Huyo Manager wa Hotel kitendo alichofanya ni cha kijinga sana na mimi naamini hicho chumba Dr. Slaa alikuwa amelipia.

Ninamkubali sana huyu mzee maana anaenda kulala kwenye guest ya bei rahisi kuliko JK analala Hoteli mpaka ya dola 1500 per night.
 
OOOOh! Mungu Mkubwa nilidhani wamemteka na kumtesa kama Dr. Ulimboka.Kama ni hilo tu hakuna shida ingeshindikana hata kwenye nyumba ya mpiga Kura angelala.

Mbona huyo Dr. hana shida na hotel kubwa hizo zina wafaa magamba ndiyo maana aliondoka bila ubishi.
 
Jamani huyu Meneja anaitwa Jacob Sumary ni ndugu yake na Sioi Sumary aliyegombea ubunge na Joshua Nassary huku Arumeru Mashariki, Nasary alivyompiga chini Sioi kwa ushirikiano mkubwa kabisa na viongozi wote wa CDM akiwemo Dr. Slaa sasa huyo Meneja ndo kalipa kisasi kwa njia hiyo. Nadhani kajidanganya coz Dr atalala popote mpaka kitakapoeleweka

mkuu una uhakika kama huyo Manager ana undugu na familia ya marehemu mzee Solomono Sumari?
 
jamaa hana skills za biashara...
...Unajua katika ajira za SU kama VETA ambapo huenda huyo meneja alichomekwa tu hapo basi anakwenda kwa amri za wabwana wakubwa tu. Anakosa hata ujasiri wa kuhoji kwa nini mteja aliyelipiwa chumba ghafla aondolewe kwa kisingizio kuwa mteja mwingine amelipia.....Ni udhaifu unaowatafuna magamba....:eek2:
 
Wakina Ndugai wapo wengi sana nchi hii........
Ole wao!
 
Mzee Madikizela Mandela utawala wa kidhalimu wa Makaburu walimuweka ndani miaka 27.

Japokua walimpa masharti kadhaa ili wamtoe alikataa na bado akaja kua Raisi huru wa watu wa Afrika ya Kusini.sembuse huyo meneja wa hoteli pamoja na serikali ya CCM? 2015 TIME WILL TELL.
 
Bora hata walimzuia yawezekana hata wangemzuru, hili limekuwa fungisho kwa chadema next time nunueni gari la lenye sehemu ya rest room kwa ajiri ya viongozi wetu
 
Unapozima umeme maana yake uzalishaji unaotegemea nishati ya umeme nao unasimama. Effect ya kusimama huko ni kwamba TANESCO wanatakosa mapato (kwa muda wote ambao mzalishaji hatumii umeme), lakini pia serikali kwa ujumla wake inakosa mapato.

Kwa kifupi kuzima umeme ni economic sabbotage, sasa nani anahujumu uchumi, wapinzani?
 
Kuwabadilisha enyi wajinga na Wachumia-tumbo wote

Mjinga ni wewe kila siku unakuja na ID mpya ungekuwa unajitambua wala usingekuwa na Multiple ID's kwa ajili ya kutolea matusi humu JF...nashangaa mods wanaachia upuuzi huu unaendelea JF.
 


Pia katika hatua nyingine umeme ulizimwa mji mzima wa Mikumi jana kuanzia asubuhi hadi usiku katika kile kilichoonekana ni hujuma ya Tanesco ili Dr Slaa ashindwe kuhutubia,hata hivyo mbali na kukosekana umeme mikutano ya Dr Slaa ilifurika umati mkubwa wa watu huku kiongozi huyo akiwaambia maelfu ya watu atawahutubia hata bila vipaza sauti.



msitufanye wajinga kiasi hiki! hivi tanesco hawajui kama kuna ma generator sikuhizi hadi wajisumbue kukata umeme ..?
:wacko:
 
Haya ndio matatizo la kuchanganya siasa na uchumi. Kwa kumtendea visivyo Dr. Slaa, je huyo meneja ameonyesha ukomavu wa kutaaluma? Je, amevutia wateja au amewafukuza?

Kwa kuzima umeme siku nzima ili kumkomoa Dr. Slaa, umesimamisha shughuli zenye thamani kiasi gani ambazo utekelezaji wake huhitaji nishati ya umeme? Kwa utendaji huu, tusitegemee maendeleo yoyote.
Spot on........
 
Nafikiri ni wakati sahihi sana kufikiria swala la camping facilities na generator kwenye mikutano kama hii.

Tatizo kama kuna kitu chochote unakitegemea kutoka kwenye current system kufanikisha kazi ya kisiasa, watakitumia kama strategy ya kukukomoa.

Mara nyingi tunashuhudia mikutano ya cdm inaporushwa live kwenye tv, umeme unakatwa etc,

Camping vogn ambayo inaungwa kwenye gari kwa nyuma ni bei rahisi sana na inakuwa na facilities zote za nyumba. Its just an advice maana as we approach 2015 there will be alot of gorrilla tactics
 
Back
Top Bottom