Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Kiongozi wa upinzani nchini ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA Dr Wilbroad Slaa amefanyiwa hujuma kubwa mkoani Morogoro kwa kufukuzwa chumba cha kulala wageni ndani ya chuo cha ufundi VETA, Mikumi Kilosa.

Kiongozi huyo ambaye alikabidhiwa chumba hicho na viongozi wa CHADEMA kikiwa kimelipiwa kila kitu na akaingia lakini ghafla akaja Meneja wa hoteli hiyo Jacob Sumary na kumtaka Kiongozi huyo wa upinzani nchini kuondoka mara moja kwenye hoteli hiyo kwa sababu tayari ilishalipiwa na mtu mwingine.

Kwa ustaarabu mkubwa na kutokutaka mabishano Dr Slaa aliondoka.

Pia katika hatua nyingine umeme ulizimwa mji mzima wa Mikumi jana kuanzia asubuhi hadi usiku katika kile kilichoonekana ni hujuma ya Tanesco ili Dr Slaa ashindwe kuhutubia,hata hivyo mbali na kukosekana umeme mikutano ya Dr Slaa ilifurika umati mkubwa wa watu huku kiongozi huyo akiwaambia maelfu ya watu atawahutubia hata bila vipaza sauti.

Vitendo hivyo vya kihuni alivyofanyiwa Dr Slaa viliwachukiza wananchi wengi wa Mikumi na kusema watalipa kisasi kwa kuindoa CCM madarakani kupitia sanduku la kura.

Source: Nipashe/Mwananchi


attachment.php

 

Attachments

  • mwananchi.JPG
    mwananchi.JPG
    92.6 KB · Views: 3,833
Najua Hii ni njia ya Kukandamiza demokrasia kwa njia ya kuwatumia Makada wa Chama Tawala!! Ila Najua hii yote itashindwa na Aibu itawarudia akina Joel!! Usipende Kuzuia maji ya mafuriko kwa Udongo!!
 
Uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii, sasa chiki ndio hujenga au hubomoa zaidi?
 
Duu jamani.....! Tunaelekea wapi tena Huku. Hivi CCM hawajui mbinu wanazozitumia kuwakomoa CDM matokeo yake zinawarudia wenyewe?

Mie naamini huyo Meneja wa Hotel amepewa amri toka kwa Mabosi wake afanye hicho kitendo so asingeweza kukataa ili alinde maslahi yake.
 
Inaonesha jamaa haendeshi biashara zake kihalari km yule mzee wa zamani alivyokuwa anawatishia wafanyabiashara kwa kusema ukitaka biashara zako ziende vizuri support ccm..........huyu atapata anachotafuta kwa kumdhalilisha rais wetu mtarajiwa
 
Me naona huyo meneja na hao Tanesco wamefanya vizuri,
kwa sababu wameongeza hasira za mabadiliko kwa wananchi,
Dr. Slaa usichoke najua wanakukubali kimoyo moyo ila kwa sababu ya wakubwa wanashindwa kuweka wazi.
 
Viva cdm hata wazime mwaka mzima poa tu hata uhuru kulikuwa na vikwazo kibao lakini tuliupata
 
Aiseeee baba yangu hayo ni majaribu tu hata Yesu alijaribiwa cha msingi Dr Slaa songa mbele tu sisitupo nyuma yako
 
Duh, that's too bad for the hotel manager! Atakuwa mnazi wa CCM.
Na hii VETA ni taasisi ya umma. Sasa siku tukiwaondoa CCM sijui mameneja wa aina hii watajificha wapi. Na watu wa aina hii wako wengi sana. Tunao kina Mwema polisi, kina Zoka idara ya usalama...
 
Inaonesha jamaa haendeshi biashara zake kihalari km yule mzee wa zamani alivyokuwa anawatishia wafanyabiashara kwa kusema ukitaka biashara zako ziende vizuri support ccm..........huyu atapata anachotafuta kwa kumdhalilisha rais wetu mtarajiwa
jamaa hana skills za biashara...
 
acheni raia wasikilize wapime na waamue wenyewe, hii mambo ya kuwa treat kama watoto wa chekechekea inaleta picha mbaya kwa chama chetu ambacho kimsingi ndicho chenye sera nzuri kuliko za cdm.
 
Tulijua na haya yatajitokeza kama njia ya kukandamiza vuguvugu la maendeleo, lakini yapo mengi zaidi yanakuja tusishangae hili kuna mkakati hata wa kuchoma matairi njia atakayopita Dr.slaa.Mkoa wa morogoro unaongozwa na mhuni watanzania wengi waliowahi kucheza mpira timu ya taifa watanzania za kihuni karibu wote.Bendera mmoja wapo mtashuhudia mengi kuelekea 18/8/2012 hapo moro mjini.Hizi ni dalili za kukaribia ukombozi, muda wa mavuno umekaribia tuvumilie
 
Uo ni ubabe wa kishangingi, inafurahisha kuona kila mtendaji anafikiri anafanya kitu ili kuidhalilisha cdm kumbe ndo wanakiaribia chama tawala.
 
Back
Top Bottom