Dr Slaa aandaliwa hujuma Iramba

Dr Slaa aandaliwa hujuma Iramba

Status
Not open for further replies.
nimevumilia sana upuuzi wa rage kwenye timu yetu ya simba , lakini hapa nimefikia kikomo , kuanzia leo najivua rasmi uanachama wa simba na ujumbe wa kamati ya ufundi , potelea mbali .

Acha propaganda, wewe sio mwanachama wa SIMBA. ivi unazani mapenzi SIMBA na YANGA unalinganisha na siasa za cdm na ccm, mtu ukiuziwa huku kesho unahamia upande wa pili. Mi namtakafari bubu aliehamia yanga mpaka leo sipati jibu, labda sababu ni bubu.
 
Waandishi wa habari wenye busara wamesusa kuondoka Singida mjini kwenda Kiomboi kwa ajili ya kushiriki propaganda chafu kuhusu Mikutano ya Katiba iliyokuwa inafanywa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Slaa. Leo asubuhi Mwigulu aliwaita waandishi wa habari waende kwenye jengo la CCM ili aondoke nao kwenda Kiomboi, waandishi waligundua kuwa ilikuwa ni njama ya kuwafanya wasishiriki mkutano mkubwa wa katibu mkuu unaofanyika jioni ya leo katika viwanja vya peoples hapa Manispaa ya singida, wakamtolea nje, akaondoka na mwandishi mmoja tu. Kwa mtindo huu ukombozi unaweza kupatikana kama waandishi nao watakuwa wakweli wasishiriki propaganda wakaandika uhalisia bila kupelekeshwa na wanasiasa wa aina ya Mwigulu
 
Waandishi wa habari wenye busara wamesusa kuondoka Singida mjini kwenda Kiomboi kwa ajili ya kushiriki propaganda chafu kuhusu Mikutano ya Katiba iliyokuwa inafanywa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Slaa. Leo asubuhi Mwigulu aliwaita waandishi wa habari waende kwenye jengo la CCM ili aondoke nao kwenda Kiomboi, waandishi waligundua kuwa ilikuwa ni njama ya kuwafanya wasishiriki mkutano mkubwa wa katibu mkuu unaofanyika jioni ya leo katika viwanja vya peoples hapa Manispaa ya singida, wakamtolea nje, akaondoka na mwandishi mmoja tu. Kwa mtindo huu ukombozi unaweza kupatikana kama waandishi nao watakuwa wakweli wasishiriki propaganda wakaandika uhalisia bila kupelekeshwa na wanasiasa wa aina ya Mwigulu

unalifahamu jina la mwandishi aliyeambatana na mwigulu, isje ikawa ni Elisante Mkumbo!!!!!!
 
Waandishi wa habari wenye busara wamesusa kuondoka Singida mjini kwenda Kiomboi kwa ajili ya kushiriki propaganda chafu kuhusu Mikutano ya Katiba iliyokuwa inafanywa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Slaa. Leo asubuhi Mwigulu aliwaita waandishi wa habari waende kwenye jengo la CCM ili aondoke nao kwenda Kiomboi, waandishi waligundua kuwa ilikuwa ni njama ya kuwafanya wasishiriki mkutano mkubwa wa katibu mkuu unaofanyika jioni ya leo katika viwanja vya peoples hapa Manispaa ya singida, wakamtolea nje, akaondoka na mwandishi mmoja tu. Kwa mtindo huu ukombozi unaweza kupatikana kama waandishi nao watakuwa wakweli wasishiriki propaganda wakaandika uhalisia bila kupelekeshwa na wanasiasa wa aina ya Mwigulu


Ni kweli kuwa Muandishi aliyetambulishwa wakati wa mechi hiyo ikiendelea ni mmoja tu.
 
tupeni mrejesho hasa picha za matukio yote mawili, mechi ya simba na mkutano wa dr.slaa
 
Naona ndo ushamaliza kujibu shutuma naibu?

haha...ndio uwezo wao..kule lumumba.Ndio maana wanatafuta sana vyeti vya kusikika ktk maredio manyumbu wengine waogope na kuwaapa kura.

Hata wakienda nje ndivyo wanavyotuwakilisha.watu wakiwashangaaa km kweli walistahili hata kushiriki nao.....wanarudi wakisema ..watu nje wameshindwa amini jinsi alivyowapa majibu ya ufundi.
 
Mwigulu wa ccm, siku hizi natumia mfano wa kijana msomi na -------- kama wewe unavyotumika kama dodoki na dekio.
Shame upon all ccm members and their leaders,
viva cdm
 
tupeni mrejesho hasa picha za matukio yote mawili, mechi ya simba na mkutano wa dr.slaa
Ndugu wana Jamavi, Sina shaka habari za Iramba zimetawala sana jamvi jioni hii. Hata hivyo, sakata hili limechukua sura mpya baada ya vijana 11 wa Chama Cha Mapinduzi wilayani hapa kuja na malalamiko mazito ya kudaiwa kurudisha fedha walizopewa kwa nyakati tofauti ili kuhamasisha ushiriki kwenye mechi ya Simba leo jioni. Vijana hao wamewasilisha maelezo yao kwa mwenyekiti wa CCM wilaya, maelezo ambayo amepatiwa pia kiongozi mmoja wa CHADEMA hapa Kiomboi, na wanajiandaa pia kuyatoa kwenye media. Akizungumza mmojawapo kati ya vijana hao anayejulikana kwa jina la Laurent Kiula amesema; "Tuliitwa siku ya jumanne na aliekuwa mgombea wa Mkutano mkuu wa taifa bwana Daudi Amosi Madelu aliekuwa pamoja na aliewahi kuwa mwenyekiti wa Urughu, Simon Tyosela. Katika kikao hicho, Madelu alitupa kazi ya kuhamasisha mtaa hadi mtaa watu wahudhurie mechi ya Simba jumamosi (leo) badala ya mkutano wa wapinzani wetu CHADEMA na akatuahidi angetupa fedha ya kulifanikisha hilo. Alituomba tuwe 10, lakini baadae alituongezea dada mmoja kutoka Arusha tukawa 11. Siku ya Alhamisi, Madelu alituomba tukutane J.L.C Club iliyo nyuma ya ofic za CCM wilaya na akatuomba feedback. Tulimpa strategies zetu na akatutambulisha kwa dada huyo kutoka Arusha aitwae Scholastika, ambae ndie angekuwa master planner wetu. Alitupa Laki 3 kwa ajili ya mafuta, mabango na T'shirt, ingawa tulimwambia zisingetosha, na Tyosela alituongezea elfu 80. Madelu aliahidi kutupa zingine Ijumaa saa 4 asubuhi pamoja na posho zetu. Jioni ya Ijumaa, Tyosela alituomba tumpelekee T'shirt kadhaa kama ziko tayari, lakini tulimwambia kuwa tumecancel wazo la T'shirt kwa kuwa muda ulikuwa umeisha. Jumamosi asubuhi Madelu alituita Kisiriri Guest haraka. Tukiwa tunaendelea kujadiliana, alipigiwa simu na Mbunge ambae alimpa taarifa kuwa CHADEMA wanaanza mkutano sa kumi, hivyo tujipange vizuri na hapo ndipo tukajua kua mbunge ana taarifa. Cha ajabu, majira ya saa sita mchana, tulisikia matangazo kuwa mkutano wa CHADEMA unaanza saa 7 mchana!! Tulipompigia Mbunge, hakuwa anapatikana na ya Madelu hakuwa anapokea. Ilipofika saa 7, watu wengi walianza kufurika uwanjani kwenye mkutano wa CDM. Kilichonishangaza, mida ya saa 12 jioni tumeitwa na Tyosela na Madelu wakitutuhumu kuwa tulikuwa tunawasiliana na Kitila Mkumbo na viongozi wa BAVICHA Mkoa na wa wilaya ya Singida mjini na kuwavujishia mpango huu huku wakiwa hawana kithibitisho chochote. Cha ajabu zaidi, tumepewa muda hadi kesho turudishe fedha zote kwao la sivyo tutavuliwa uanachama. Yule dada aliekuwa anatusimamia (Skola) ameshaondoka tangu sa'9 alasiri kuelekea Arusha. Huku ni kuoneana, kosa letu ni Lipi"? Anamaliza Laurent ambae anasema alipewa jukumu la kuhamasisha watu wa kata yake ya Bomani. Source: Laurent Kiula Katibu-UVCCM BOMANI-KIOMBOI
 
Ndugu wana Jamavi, Sina shaka habari za Iramba zimetawala sana jamvi jioni hii. Hata hivyo, sakata hili limechukua sura mpya baada ya vijana 11 wa Chama Cha Mapinduzi wilayani hapa kuja na malalamiko mazito ya kudaiwa kurudisha fedha walizopewa kwa nyakati tofauti ili kuhamasisha ushiriki kwenye mechi ya Simba leo jioni. Vijana hao wamewasilisha maelezo yao kwa mwenyekiti wa CCM wilaya, maelezo ambayo amepatiwa pia kiongozi mmoja wa CHADEMA hapa Kiomboi, na wanajiandaa pia kuyatoa kwenye media. Akizungumza mmojawapo kati ya vijana hao anayejulikana kwa jina la Laurent Kiula amesema; "Tuliitwa siku ya jumanne na aliekuwa mgombea wa Mkutano mkuu wa taifa bwana Daudi Amosi Madelu aliekuwa pamoja na aliewahi kuwa mwenyekiti wa Urughu, Simon Tyosela. Katika kikao hicho, Madelu alitupa kazi ya kuhamasisha mtaa hadi mtaa watu wahudhurie mechi ya Simba jumamosi (leo) badala ya mkutano wa wapinzani wetu CHADEMA na akatuahidi angetupa fedha ya kulifanikisha hilo. Alituomba tuwe 10, lakini baadae alituongezea dada mmoja kutoka Arusha tukawa 11. Siku ya Alhamisi, Madelu alituomba tukutane J.L.C Club iliyo nyuma ya ofic za CCM wilaya na akatuomba feedback. Tulimpa strategies zetu na akatutambulisha kwa dada huyo kutoka Arusha aitwae Scholastika, ambae ndie angekuwa master planner wetu. Alitupa Laki 3 kwa ajili ya mafuta, mabango na T'shirt, ingawa tulimwambia zisingetosha, na Tyosela alituongezea elfu 80. Madelu aliahidi kutupa zingine Ijumaa saa 4 asubuhi pamoja na posho zetu. Jioni ya Ijumaa, Tyosela alituomba tumpelekee T'shirt kadhaa kama ziko tayari, lakini tulimwambia kuwa tumecancel wazo la T'shirt kwa kuwa muda ulikuwa umeisha. Jumamosi asubuhi Madelu alituita Kisiriri Guest haraka. Tukiwa tunaendelea kujadiliana, alipigiwa simu na Mbunge ambae alimpa taarifa kuwa CHADEMA wanaanza mkutano sa kumi, hivyo tujipange vizuri na hapo ndipo tukajua kua mbunge ana taarifa. Cha ajabu, majira ya saa sita mchana, tulisikia matangazo kuwa mkutano wa CHADEMA unaanza saa 7 mchana!! Tulipompigia Mbunge, hakuwa anapatikana na ya Madelu hakuwa anapokea. Ilipofika saa 7, watu wengi walianza kufurika uwanjani kwenye mkutano wa CDM. Kilichonishangaza, mida ya saa 12 jioni tumeitwa na Tyosela na Madelu wakitutuhumu kuwa tulikuwa tunawasiliana na Kitila Mkumbo na viongozi wa BAVICHA Mkoa na wa wilaya ya Singida mjini na kuwavujishia mpango huu huku wakiwa hawana kithibitisho chochote. Cha ajabu zaidi, tumepewa muda hadi kesho turudishe fedha zote kwao la sivyo tutavuliwa uanachama. Yule dada aliekuwa anatusimamia (Skola) ameshaondoka tangu sa'9 alasiri kuelekea Arusha. Huku ni kuoneana, kosa letu ni Lipi"? Anamaliza Laurent ambae anasema alipewa jukumu la kuhamasisha watu wa kata yake ya Bomani. Source: Laurent Kiula Katibu-UVCCM BOMANI-KIOMBOI


Mimi nilishasema hata awalete Barca, mkutano wa CHADEMA utafana kama ilivyokuwa leo.

Imekula kwao.
 
Huyu Molemo nae ni wa kupuuzwa, sasa hapo hujuma ipo wapi?

Watu waache kuburudika kwa sababu ya Dr Slaa?

Kama ikitokea wananchi wamependezwa na ujio wa Dr Slaa, basi waende wakamsikilize.

Mwisho wa haki yako, mwanzo wa haki ya mwingine. Simple.

Duuh! ama kweli we HAMY-D
 
Hahahahahaa hii Club yetu ya simba nayo inajidhalilisha, wanaenda kutumika kisiasa na wao wakijua, nawapa pole sana wana Iramba, hapo ndo kitakuwa kipimo chanu cha akili..


Na imejidhalilisha kwa kiasi kikubwa tu. Hebu fikiria Timu kubwa kama Simba F.C kutoka na matokeo ya 3-1 dhidi ya Timu ya Iramba Combine ambayo imeandaliwa kwa wiki mbili tu.

Isitoshe, Iramba F.C ni Timu ya vijana wanaotoka maeneo tofauti ya Jimbo la Iramba Magharibi na wamefanikiwa kuwaaibisha kwa kiasi kile.

Cha aibu zaidi ni kuwa kipindi cha kwanza mlitoka 2-1 na Iramba Combine. Mwishowe mkaamia kubadilisha Timu yote na kuwaingiza wachezaji wenye majina kama Kiemba, Ledondo na Choro wa Znz ili kuziba aibu na wakaambulia goli moja tu.

Je, msimu huu wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara mkikuta na Timu kubwa kama Young Africans si mtapigwa 10-0 nyie.

Na kwa kuthitisha kuwa mpango huu uliandaliwa na akili finyu za Mwigulu Nchemba na Ismail Aden Rage, timu ua Simba F. C itaelekea Tabora kucheza na timu za Jimbo la Ismail Aden Rage.

Kwa Ushauri wa bure, FUKUZA Ismail Aden Rage pale Msimbazi kwani ni MAJANGA.
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom