Elections 2010 Dr. Shein na Maalimu Seif wanachuana Z'bar

Status
Not open for further replies.
Asiyekuwepo na lake halipo

Hii inasikitisha sana kwa kweli,Rais anayegombea ZNZ iweje anapigia kura Mikocheni Dar?Hii ina maana kawakosesha kura MOJA MUHIMU wagombea wenzake wa CCM kwenye nafasi ya usheha,Ubunge na Uwakilishi!

Kwa msingi huo Shein HAKUPASWA kugombea ZNZ,alipaswa awe mgombea Ubunge wa jimbo mojawapo la Dar ambako ndiyo makazi yake!
 
Natamani sana CUF ichukuwe zanzibar ili kum'disaprove Mkapa kwenye kauli zake za Jana!
Wazenj hawako tayari kuburuzwa na CCM Tanzania bara.Njia ilio rahisi ni kumchagua Maalim Seif.Wanataka Serikali tatu,wanataka maswala ya raslimali za mafuta yaondolowe kwenye mambo ya muungano,usishangae wakichagua Dr Slaa kwani sera zao zinafanana.
 
Wadi ya vikokotoni

Maalim Seif CUF 204
Dr Shein CCM 96
 
Huu ni ushahidi wa matokeo ya chaguzi zilizopita, anyway, yaliyopita si ndwele, CCM sasa waone matokeo ya uovu wao
 
Hizo ni kura za urais zanzibar za urais muungano chadema ndio wataongoza si mliona watu walivyo jaa kwenye mkutano wa slaa kule zanznibar?
\

Zanzibar wapiga kura 480000

Kagera tu 1,103,000 kwa hiyo zanzibar si chochote. Tunaogopa tu Lindi, Mtwara na Ruvuma basi!!!!!!!!
 
Wakala wagoma kuweka saini Malindi Jimbo la mji mkogwe kura za Rais wa Jamhuri ya Muungano hata hivyo PO
alijaza fomu hio kwa kuonyesha tarakimu zifuatazo
Jumla ya kura 176
Zilizopingwa 155
CUF 104
CCM 28
zilizoharibika 23 yanasubiriwa maamuzi ya juu.
 
kaka usishangilie kabla ya mwenyekiti wa tume kutangaza kihalali, hujuwi sheria za uchaguzi zinasemaje? usishangilie kabla refarii hajapuliza kipyenga cha mwisho, kama wewe ni mwana michezo rejea Mechi ya man united na bayern MUNICh mwaka 1999. MAN ilipigwa bao dakika za mwanzo lakini dakika 2 za mwisho wakashinda mechi.

wewe tulia mpaka filimbi ya mwisho.
 
waooooooooooh! mwaka wao ccm huu

Hata 2000 na 2005 CUF walishinda mkuu!

Hope this time CCM wataachia tu. Hata wanajeshi, polisi na watu wa usalama wa viongozi nao wanachoka ati! Kama unakula msosi wewe peke yako tuuuuuuu utashangaa hata mbwa au paka wao anakupapua!
 
1) Kituo Cha Bwawani-Unguja

Maalaim seif CUF 593
Dr Shein CCM 141

Jimbo la Chake Chake-Pemba
Kituo cha Michakaini
Maalim Seif CUF 956
Dr. Shein CCM 246.
Kituo cha Ngwachani
Maalim CUF 623,
Shein CCM 132.

Wadi ya vikokotoni
Maalim Seif CUF 204
Dr Shein CCM 96

Ziwani -Pemba
*
Maalim Seif CUF 1080
Dr Shein CCM 60

Malindi - Unguja
Maalim Seif CUF 104
Dr Shein CCM 28

Mwiba!,ili kuwarahisishia wafuatiliaji wako wa matokeo, weka sehemu pembeni ya kutoa jumla kwa kila mgombea kwa kila mara unapoonngeza kituo.
Uwe mkweli usije ukaongeza ya kwako.

 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom