Nipo ndugu yangu MOTOCHINI na hongera kwa mtu wako kutangazwa mshindi (sisemi kushinda). Yote sawa tuu na maisha yatasonga kwa slogan hiyo ya Hapakazituu.KAZI TU Chakaza Rafikiangu upoooo
Yaani unawaza namna ambavyo JPM ataunda serikali? Mbona liko wazi kabisa kwamba ataunda kwa kuteua waziri mkuu na mawaziri kutokana na wabunge wa chama chake waliopo? Huo si ndio utaratibu wa siku zote wa kuunda serikali? Hilo nalo ni la kuwaza?Tatizo mnaleta hoja zilizokufa.
Wenzenu wanaangalia ni namna gani JPM ataunda serikali itakayosaidia kutatua kero za wananchi.
Hebu tufanye prediction kidogo ya mambo yatakayoongewa au kugusiwa sana sana na rais wetu mteule siku atakapokua anaapishwa au kufungua bunge au sehemu yoyote kama speech yake ya kwanza kama rais..,,
Mie nasherehekea nikiwa kitandani naumwa, ila nimefurahi sana aisee, sasa ni kazi tu.
Hahahaha Chakaza nduguyangu hapakuwa na jinsi, vyovyote kubwa kununua ikulu ishindikane lowassa hana hata chembe ya kuingia ikulu tuyaache niwakati wa kufanya kazi sasaNipo ndugu yangu MOTOCHINI na hongera kwa mtu wako kutangazwa mshindi (sisemi kushinda). Yote sawa tuu na maisha yatasonga kwa slogan hiyo ya Hapakazituu.ila uchaguzi huu ulikuwa na mambo ambayo huwezi kuamini hasa katika majumuisho ya kura. Kuna mambo mie nilishika mdomo sikuamini kuwa yanaweza kutokea. Mie nilidhani ni huu ushabiki wetu tuu wa ki JF kumbe kuna mambo makubwa mno. Wewe ni pm nikujulishe maana siwezi kuyaandika humu, ni mazito.
Wezi wa kura ndio walioamua, sio walio wengi. Unaniuliza kulalamika kwangu mtandaoni kunanisaidia nini, kwani wewe kunijibu mtandaoni kumekusaidia nini?Sasa kulalamika kwako mitandaoni kunakusaidia nn? Walio wenngi wameamua!
Lazima utakuwa Mirembe Dodoma....Mimi huku niliko ni shangwe tu...
Watu wanaimba 'Lowassa.....Tumemkataa'
Ni kweli kabisa, maana wizi wa kura nao ni mchezo unaohitaji kipaji cha hali ya Juu. Kwa kweli wamecheza kama Pele.hongera Magufuli na Samia, CCM wamecheza kama Pele
Dr. John Pombe Magufuli ametangazwa rasmi kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya 5 baada ya kuongoza kwa kupata kura 58.46%.
Lubuva: Kwa kuwa mheshimiwa Dr. Magufuli, John Pombe Joseph wa CCM amepata kura nyingi zaidi kuliko mgombea mwingine yeyote, kwa niaba ya tume ya taifa ya uchaguzi na kwa mujibu wa vifungu vya 35(e), 35(f) na 81(b) vya sheria ya taifa ya uchaguzi sura 343.
Ninatangaza rasmi matokeo ya uchaguzi ya urais wa mwaka 2015 kwamba
Asanteni kwa kunisikiliza.
- Mheshimiwa Magufuli John Pombe Joseph amechaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania
- Mheshimiwa Samia Hassan Suluhu amechaguliwa kuwa makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Majizi makubwa haya.....Mungu ayalaani !
Hivi unajisikiaje, hasa pale unapogundua kiuhalisia kuwa mkeo au mmeo hakukubali, hakupendi, ila basi afanyeje hawezi kuondoka maana umemuwekea walinzi wa kumzuia asiondoke kwako.
Kwa hali kama hiyo unapotoka na kurudi hapo kwenu; unafurahi kumkuta yupo? Au je yeye anafurahi kukuona umerudi kwake?
Nikijielekeza kwenye uchaguzi mkuu uliomalizika sasa; fikara yenye kufanana na mfano huo halo juu ilipita akilini mwangu.
Kuwa ccm hii yenyewe inajua fika kama haikuwalazimisha watanzania kuendelea kuwa nayo! Kama vile watanzania walio wengi wanavyojua ndani ya nafsi zao mapenzi yao kwa chama tawala kwamba ni ya hiyari au ni ya lazima!
Aghalabu ni vyepesi kama nini kuwadanganya watu wengine kuliko kufanya hivyo kwa nafsi yako mwenyewe.
Ndiyo maana baada ya uchaguzi huu unaweza kukuta mtu anashangilia nje lakini kwa ndani nafsi yake inamkanya ikisema muongo wee!
Mungu ni shahidi mwaminifu amina!
Tunataka viwanda, dawa, elimu bure mpaka form 4 though elimu mpaka hapo... maji yawe historia kama alivyoahidi.
Kwani wewe hukujua kwamba kupiga kura bila katiba huru ni kupoteza muda.Usirudie kosa hilo tena.
ni jf wamekosea au ni nec na calculator zaooooo?????
mimi ni mwana ccm ila sipendi unafiki nimekunywa pombe hapa lakini hizi data.........
""Aliongeza kuwa idadi ya wapigakura waliojiandikisha ni 23, 161, 440, waliopiga kura ni 15, 589, 639 sawa na asilimia 67.31 ya wapiga kura wote waliojiandikisha.
Alizitaja idadi ya kura halali kuwa ni kura halali 15, 193, 862 sawa 97.46% kura zilizokataliwa 402, 248 sawa 2.58% hivyo Magufuli amepata kura ambazo ni 8, 882, 935 sawa na 58.46% ya kura zote halali.
Matokeo ya wagombea wengine akiwemo, Anna Mghwira wa (ACT-Wazalendo) 98,763 sawa 0.65%, Chifu Lutalosa Yemba (ADC), 66, 049 sawa na 0.435 huku Edward Lowassa (Chadema) akimfuatia kwa kura Dk. Magufuli kwa kupata kura 6, 772, 848, sawa 39.97% na Hashim Rungwe wa (CHAUMMA) aliyepata kura 49, 256, sawa na 0.32%.
Wagombea akiwemo Janken Kasambala (NRA) 8, 028 sawa 0.03% na Maximilian Lyimo (TLP) 8, 198 sawa na 0.05% Fahmy Dovutwa (UPDP), 7, 785 sawa 0.05%.""
Ukanda Upi wewe takataka? Ina maana Kanda ya Kaskazini Pekee ina wapiga kura asilimia 42?
Ni wachache wanaothubutu kumpongeza JPM.... nahisi ni kati ya marais watakoukuwa na kazi ngumu sana
Kwanza kwa sababu hajachaguliwa na walio wengi,
Pili anaikuta serikali ikiwa katika hali mbaya kuliko alivyoikuta mkapa,
Tatu itamchukua miaka zaidi ya minne watu kumkubali... maana mpaka sasa hana kibali, watu bado wana rais wao mioyoni!!!!
Nne anaikuta CCM ikiwa vipande kukiwa na wasaliti wengi....
Tano anakutana na watanzania waliokata tamaa na maisha hawana hamu na lifisieM lao...
Ongezea mengine
kama mtu anakataa kupata elimu unategema nini hapo???,
1. Watu hao waliokataa elimu ya bure hawana hata uwezo wa kupata milo 3 kwa siku
2. ....................hawana hata nyumba ya tofali
3. ............................................wanakufa kwa kukosa panadol
4............................................hawana hata viatu vya kutembelea jambo ndala za tsh 1000
5.........................................wanakunywa maji machafu anayokunywa punda (mifugo)
6. ......................................................................................
7. ...................................................................
,...............................................................
Umaskini wa mwili na akili ndio mtaji wa ccm, ccm itatawala milele;
Shule zao zipo maporini wanakakia mawe ndio wanaoongoza kwa kutoa mashamba boy na mabeki tatu!
Upo sahihi kabisa ila hawa Ukiwa wameng'ang'ania 6, 772, 848