Dr. Mwakyembe, muda wako umefika

Dr. Mwakyembe, muda wako umefika

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Muda wako umewadia. Muda wako wa kusema ukweli zaidi. Lowassa amekuchokoza leo mjini Dodoma. Amedai kuwa yeye hakuhusika na Richmond. Sakata la Richmond, I mean. Amedai kuwa sakata hilo lilitungwa na kulenga Uwaziri Mkuu wake tu.Hakukuwa na zaidi. Kwa maana nyingine, Dr. Mwakyembe na Kamati yako teule ya Bunge mlitunga kashfa ya Richmond. Yaani,Dr.Harrison Mwakyembe na Kamati yake ni wazushi na waongo!

Dr. Mwakyembe, umepata nafasi adhimu na adimu isiyo na msimu. Nafasi ya kusema hata yale ambayo hukusema Bungeni Dodoma ulipokuwa ukiwasilisha Ripoti ya Kamati yako. Ukweli juu ya sakata la Richmond. Kama Lowassa ameruhusiwa na chama na Serikali kusemea kashfa hiyo, wewe na iliyokuwa Kamati yako hamzuiwi. Mkinyamaza,mtasadifu ukweli wa jina la waongo na wazushi mlilopewa leo hii Dodoma.

Ukiwa nguli wa tasnia ya Sheria, Dr. Mwakyembe panga hoja zako nawe uzungumze na watanzania. Kama huna pesa ya kukodi ukumbi,waite waandishi hata nyumbani kwako. Watakuja na kukusikiliza. Muda wa kulinda heshima yako huu.Kama Lowassa kamwaga mboga, wewe Dr. Mwakyembe mwaga ugali.

Liwalo na liwe!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)
 
Hapa hata kama Mwakyembe alikosea kitendo cha Lowassa kukaa kimya Zaidi ya miaka 8 anaonyesha jinsi gani alivyo mnafiki na hafai. Taifa letu likionewa atakaa kimya? Kwangu hii imemshusha Zaidi kuliko kumjenga.
Ina maana alijitoa Muanga mafisadi waendelee kula nchi. Huyu hana ubavu wa kukemea wizi ambao ndo adui namba moja sasa hivi
Badala ya kuongelea Elimu Kwanza sera inayotakiwa ni UFISADI SASA BASI.
 
CCM ya wale waliojiita ati wapiganaji - imeshachoka!! walizidiwa kete baada tu ya kukubali zile teuzi, mbaya zaidi kiongozi wao naye kashaharibu record yake baada ya kuvurunda kwenye katiba mpya!!

Siasa ni timing!! - mjini hapa.
 
Ama kweli kuwa na mvi nyingi sio wingi wa busara, yani anakana, kumbe hata shetani akitubu na kuomba msamaha anaweza kusamehewa.Khaa!! Sasa ulijiuuzuru kulinda heshima hipi ambayo inanyanyasa roho yako kwa miaka nane???
 
Nakuhakikishia kama utamwamsha lowasa usiku umwambie ni mwanasiasa gani unaemwogopa tz ,atakwambia ni dr mwakyembe na swali hlo hlo hata ukimfuata rostam na kumwuliza bdo atakwambia ni dk mwakyembe.lowasa amefanya kosa kubwa sana kujaribu kumwngiza dr mwakyembe kwenye hili na yeye anajua dk mwakyembe sio mtu wa kukurupuka na nilisha wahi kumuonya mzee kuhusu hili.
 
.....

....mwingine anakwenda kuharisha Arusha kweli kipindupindumagambaniesins kimepiga hodi !!!
 
Hapa hata kama Mwakyembe alikosea kitendo cha Lowassa kukaa kimya Zaidi ya miaka 8 anaonyesha jinsi gani alivyo mnafiki na hafai. Taifa letu likionewa atakaa kimya? Kwangu hii imemshusha Zaidi kuliko kumjenga.
Ina maana alijitoa Muanga mafisadi waendelee kula nchi. Huyu hana ubavu wa kukemea wizi ambao ndo adui namba moja sasa hivi
Badala ya kuongelea Elimu Kwanza sera inayotakiwa ni UFISADI SASA BASI.
Alikaa kimya kukinusuru chama!!
 
VUTA-NKUVUTE

Mwakyembe aliyeikana tafiti yake ya Phd kwenye maoni ya Katiba mpya,ndo nguli wa sheria unayemtaja? Yule Mwakyembe kwanini uamini report yake ya Kamati teuli ilihali aliisaliti research yake ya taaluma? Mwakyembe naye ni opportunist tu. Mwakyembe na Sitta wote #Wasaka tonge tu hao!
Nashauri Lowasa amwage Mboga na Ugali vyote,
 
Last edited by a moderator:
Hivi mwakyembe dr??????????? Naomba kujuzwa au ndio kama Dr Mrema....na KJ
 
VUTA-NKUVUTE

Huwa nakuaminia sana kwamba unajuwa mengi kumbe wewe upo gizani? Mwakyembe ni tayari mateka hana tena ujanja ana kashfa ya mabilioni ya mabehewa ya TRC na taarifa za uhakika nimezipata kutoka magogoni.

Lowasa mnqmchukulia poa lakini ukweli ni kwamba ameshamaliza kazi alikuwa anaawawchw mropoke tu.

Ole Sendeka baada ya kuona kimbunga ni kizito kajisalimisha mwenyewe na kupamba Lowasa bungeni.

Mwakyembe tulimpenda sana ila ufisadi ukampenda zaidi bora angekufa kwa sumu tu kuliko hasara aliyotuingiza shenzi kabisa huyu.

VOTE FOR UKAWA.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom