Dr Mary Nagu: Bunge Sasa Lina Amani

Dr Mary Nagu: Bunge Sasa Lina Amani

PakaJimmy

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2009
Posts
16,202
Reaction score
8,788
Dr Mary Nagu amesema Bungeni jioni hii kuwa Bunge sasa lina amani sana baada ya wenzetu wale wanaoleta vurugu kuwa nje!
Pia amesema kuwa vurugu zinazotokea mara kwa mara Bungeni kwa sasa zimehamia mtaani maana waleta fujo wako huko.

Kwa mtu makini yeyote Bunge la tokea Jumatatu limepooza sana, likiwa limejaa makofi na Pongezi.
 
Hawa wanamtesa sana kule jimboni kwake hanang... Asubiri moto 2015
 

Attachments

  • cdm1 6de2b.jpg
    cdm1 6de2b.jpg
    81.1 KB · Views: 1,083
Jioni ya leo ndio nimeamini Hawa viongozi wakiongozwa na Mwigulu Nchemba, Nagu, Hawa Ghasia na wengine nimekubali wana mambo ya hovyo, badala ya kuchangia bajeti wao wanazungumzia beyond doubt kwamba chadema ndio waleta vurugu na Ghasia kaenda mbali zaidi kwa kuwatuhumu ndesa na Mbowe kwamba wakanda wanasababisha vurugu kwa wenzao.

Je mahakama imethibitisha ni CDM?
je tufikirieje kwamba ni wenyewe ndio wauwaji ndio wanajisafisha?
Je tutajuaje kwamba ndio mbinu mpya baada ya kuona wameshindwa?
Kwa hakika nimeona hakuna weledi kabisa kwa watu hawa
 
La amani si kwa sababu halina changamoto-mbona tunajua na huyu Mwandosya anachangia kasahau sumu aliyolishwa na magamba?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mwandosya hakika amechoka sana, anatakiwa apumzike nyumbani na kucheza na wajukuu.
Jioni hii, katika hali isiyo ya kawaida ameipongeza sana Cuf kwa ushindi mnono kwenye uchaguzi wa udiwani, huku akijikwepesha kabisa kuitaja cdm!
Usomi wa Prof. huyu unatatanisha sana.
 
Mwandosya hakika amechoka sana, anatakiwa apumzike nyumbani na kucheza na wajukuu.
Jioni hii, katika hali isiyo ya kawaida ameipongeza sana Cuf kwa ushindi mnono kwenye uchaguzi wa udiwani, huku akijikwepesha kabisa kuitaja cdm!
Usomi wa Prof. huyu unatatanisha sana.

Hivo wewe mbona hujielewi? Mara Mary Nagu mara Mwandosya mara nani sijui. Ebo.
 
La amani si kwa sababu halina changamoto-mbona tunajua na huyu Mwandosya anachangia kasahau sumu aliyolishwa na magamba?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Limwandosya liacheni waje waliue. Si linajifanya halijuhi kuwa CCM kwa sasa mbombo ngafu.
 
wote vilaza tu wenye akili na wenye kujua nini maana ya kuwatumikia wana nchi ni chadema peke yao..inawezekana wanataman sana wasirud bungen mana moto wanaopelekewa na na wabunge wa chadema ni moto wa gass.
 
Walau ametambua kuwa Chadema inawakosesha usingizi Bungeni... lakini wanaenda Bungeni kupigiwa makofi...
 
Jioni ya leo ndio nimeamini Hawa viongozi wakiongozwa na Mwigulu Nchemba, Nagu, Hawa Ghasia na wengine nimekubali wana mambo ya hovyo, badala ya kuchangia bajeti wao wanazungumzia beyond doubt kwamba chadema ndio waleta vurugu na Ghasia kaenda mbali zaidi kwa kuwatuhumu ndesa na Mbowe kwamba wakanda wanasababisha vurugu kwa wenzao.

Je mahakama imethibitisha ni CDM?
je tufikirieje kwamba ni wenyewe ndio wauwaji ndio wanajisafisha?
Je tutajuaje kwamba ndio mbinu mpya baada ya kuona wameshindwa?
Kwa hakika nimeona hakuna weledi kabisa kwa watu hawa

Hata nami nimekubali kwamba Ukiwa na akili kama ya MBUNI halafu kwa njia anazozijua MUNGU ukajikuta na madaraka ni BALAA kwa taifa. Mbuni huzika kichwa mchangani na kuacha mwili ukionekana wazi akidhani amejificha. Kwa tukio la ARUSHA liko wazi mpaka kwa watoto wa chekechea.

Ngoja wajifariji tu lakini kama wana akili sawasawa nadhani wanaanza kuona hasira ya wananchi dhidi ya chama chao.
 
Ukiona waziri anapongeza changamoto kutokuwepo, huyo ni mzembe.
 
Kaka,wewe ndio umejua leo?..hawa shake-well before use kitambo tu!
 
Back
Top Bottom