Dr. Magufuli, tafadhali badili hotuba

Dr. Magufuli, tafadhali badili hotuba

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Sasa unaelekea 'kuboa'. Unarudiarudia maneno yale yale kila mahali unapohutubu,kwanini? Badili hotuba. Badili maneno. Kuanzia ukumbini Dodoma; uwanjani Dodoma, Dar es Salaam na hata Zanzibar, umekuwa ukisema: 'Sitawaangusha,nitakuwa mtumishi wa wote'. Na jana pia umeyarudia maneno hayo hapa Lumumba. Kurudiarudia kunaonesha kufilisika. Usifike huko.

Nafahamu na nakufahamu kuwa una maneno mengi. Unaweza kubadili maneno na hata kuyaleta matamu kuliko hayo. Kama huo ni msemo wako sawa.

Lakini,badilikabadilika kimaneno ili uvutie. Shauriyo, utapoteza wasikilizaji kwakuwa tu watakuwa wanasikia yale yale. Badilika Tingatinga!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
tatizo hilo si magufuli peke yake mpaka lowassa analo pia tatizo hilo linachangiwa na ccm yani maswala ya chama ni nape, mangula, na yule msomali ktk kuzunguka mikoani kukijenga chama ktk mikutano mbalimbali yenye watu wengi ndo unapata experience ya kuongea leo kama chama cha chadema wote wanajua kuongea coz wanafanya mikutano mingi na kupata experience ya kuongea
 
Tupatupa unataka kumlaumu bure huyo jamaa yenu. Yeye anachokiweza ni kuweka kumbukumbu za kilometa za barabara kichwani. Anaweza kukuambia kutoka Arusha kupitia Chalinze mpaka Gairo kisha Muheza ni kilometa mia nane hamsini na tatu nukta saba mbili pointi thelasini na tatu nukta sita tano.
Na hilo ndio eti lililompa sifa ya kuonekana mtendaji mahiri. Hayo mambo mengine ya kuoganize taasisi mbali mbali za afya,Elimu,maji nk zitafanyaje kazi kuleta maendeleo yeye huko hayupo kabisa. Anajua barabara na madaraja tuu.
Ukweli kiwango cha Urais Magufuli sio kabisa, yeye anastahili kuwa nyapara kusimamia mradi/miradi basi.
 
Magufuli hana sifa ya kuwa rais hats chembe.
Kama MTU anaanza kuonyesha umahiri wa kukariri lugha za makabila mbalimbali si utoto huo????
 
Sasa unaelekea 'kuboa'. Unarudiarudia maneno yale yale kila mahali unapohutubu,kwanini? Badili hotuba. Badili maneno. Kuanzia ukumbini Dodoma; uwanjani Dodoma, Dar es Salaam na hata Zanzibar, umekuwa ukisema: 'Sitawaangusha,nitakuwa mtumishi wa wote'. Na jana pia umeyarudia maneno hayo hapa Lumumba. Kurudiarudia kunaonesha kufilisika. Usifike huko.

Nafahamu na nakufahamu kuwa una maneno mengi. Unaweza kubadili maneno na hata kuyaleta matamu kuliko hayo. Kama huo ni msemo wako sawa. Lakini,badilikabadilika kimaneno ili uvutie. Shauriyo, utapoteza wasikilizaji kwakuwa tu watakuwa wanasikia yale yale. Badilika Tingatinga!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Mkuu,
Na hili la kila anapotaka kuhutubia ni lazima amshukuru sana JK na kuhaidi kutomwangusha unalionaje??? Hata jana kafika mbali sana kwenye hotuba yake pale kwa kusema mara nyingi JK OYEEEE!!!!!! JK Oyeee!!!!!! badala ya CCM Oyeee!!!!. Nikilinganisha jinsi anavyomuongelea JK ni kama vile yeye atamtegemea JK katika mambo mengi sana ya kuongoza nchi. Hili linanipa wasiwasi zaidi, kwani JK ni kati ya viongozi walioturudisha nyuma sana kwa kutokuwa na uongozi wenye vision na hata nia thabiti ya kumuokoa mtanzania. Na ikiwa Magufuli atafanikiwa kuwa Rais na akamtegemea JK kulingana na jinsi anavyomsifia basi watanzania tutegemee maumivu zaidi.

Jambo lingine linalonitia shaka kuhusu Magufuli ni muonekano wake, kwangu mimi simwoni kama mtu mwenye kuwakilisha presidential presence. Magufuli anaonekana kama mtendaji fulani mwenye kupewa majukumu na kuyatekeleza katika uhalisia wake na si Rais kama kiongozi wa nchi. Anyway, sijui wenzangu mnachukuliaje hili la muonekano wake na kila siku JK Oyeeeee!!!!!! badala ya CCM Oyeee!!!! au Tanzania Oyeeee!!!!!!
 
Magufuli hana sifa ya kuwa rais hats chembe.
Kama MTU anaanza kuonyesha umahiri wa kukariri lugha za makabila mbalimbali si utoto huo????

Mnakandya! Angekuwa cDM aaaa kelele zingekuwa nyingi saaaaana!
 
Sasa unaelekea 'kuboa'. Unarudiarudia maneno yale yale kila mahali unapohutubu,kwanini? Badili hotuba. Badili maneno. Kuanzia ukumbini Dodoma; uwanjani Dodoma, Dar es Salaam na hata Zanzibar, umekuwa ukisema: 'Sitawaangusha,nitakuwa mtumishi wa wote'. Na jana pia umeyarudia maneno hayo hapa Lumumba. Kurudiarudia kunaonesha kufilisika. Usifike huko.

Nafahamu na nakufahamu kuwa una maneno mengi. Unaweza kubadili maneno na hata kuyaleta matamu kuliko hayo. Kama huo ni msemo wako sawa.

Lakini,badilikabadilika kimaneno ili uvutie. Shauriyo, utapoteza wasikilizaji kwakuwa tu watakuwa wanasikia yale yale. Badilika Tingatinga!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Kila sehemu anakwambia sitowangusha. Juzi kaulizwa kwa lipi? Akashindwa kujibu...
 
Subiri utumie kura yako, kelele za nini? Huyo wa mchakamchaka ndo anajua kuongea? Zero brain.
 
Mkuu,
Na hili la kila anapotaka kuhutubia ni lazima amshukuru sana JK na kuhaidi kutomwangusha unalionaje??? Hata jana kafika mbali sana kwenye hotuba yake pale kwa kusema mara nyingi JK OYEEEE!!!!!! JK Oyeee!!!!!! badala ya CCM Oyeee!!!!. Nikilinganisha jinsi anavyomuongelea JK ni kama vile yeye atamtegemea JK katika mambo mengi sana ya kuongoza nchi. Hili linanipa wasiwasi zaidi, kwani JK ni kati ya viongozi walioturudisha nyuma sana kwa kutokuwa na uongozi wenye vision na hata nia thabiti ya kumuokoa mtanzania. Na ikiwa Magufuli atafanikiwa kuwa Rais na akamtegemea JK kulingana na jinsi anavyomsifia basi watanzania tutegemee maumivu zaidi.

Jambo lingine linalonitia shaka kuhusu Magufuli ni muonekano wake, kwangu mimi simwoni kama mtu mwenye kuwakilisha presidential presence. Magufuli anaonekana kama mtendaji fulani mwenye kupewa majukumu na kuyatekeleza katika uhalisia wake na si Rais kama kiongozi wa nchi. Anyway, sijui wenzangu mnachukuliaje hili la muonekano wake na kila siku JK Oyeeeee!!!!!! badala ya CCM Oyeee!!!! au Tanzania Oyeeee!!!!!!


Mkuu watu wanachoangalia ni Shati lake lakijani tu basi!
 
JE itakuwaje kwenye mikutano ya kimataifa, itakuwa aliselemaaaa?
 
Back
Top Bottom