Dr Lwaitama: CCM wakimsimamisha Dr. Salim A. Salim watashinda Urais

Salim Ahamed Salim, yeye binafsi hana tatizo. Hata Mwalimu Julius Kambarage alimuona kama mtu amayefa kushika nafasi ya urais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania tangu 1985.

Kipindi cha Mzee Ruksa hasa kilikuwa cha Dr. Salim Ahamed Salim, lakini siasa za fitina, uzandiki na mizengwe za CCM ndizo zilizomnyima fursa ya kushika nafasi hii adimu.

CCM wakafanya fitina wakamuweka Mzee Ruksa. Kipindi cha 2005 CCM kiliendeleza siasa zilezile za uzandiki kwa kumzulia kashfa mbalimbali sio yeye peke yake aliyezulia kashfa, bali wagombea wote waliojitokeza kushindana na Kikwete, wote, walizulia jambo ama hili ama lile.

Matokea ya siasa zafitina, makundi na kuchafuana za wana CCM ndiyo zilizotufanya tukapata viongozi DHAIFU.

Tumefika mahali serikali inaua watu, wakristu na waislamu wanaanza kuuana, maandamano kila mahali na uchumi mbaya. Janga hili linawakumba hata walioliasisi na wanamtandao. Wanatamani kurudisha nyuma jua, ndipo wana mkumbuka Salimu.

Inawezekana anayekumbuka shuka kukiwa kumekucha mithili ya mlevi, ni Mwenyekiti wa CCM pekee yake kama ilivyokuwa kwa Nyerere kipindi kile cha 1985.

Kama kuna makundi mengine yenye malengo tofauti na kumpata kiongozi bora, basi hataupata uraisi. Kama wana CCM wamejifunza kwa makosa wakaamua kumchagua na kujutia dhambi zaozanyuma, basi yaweza kuwa nyota njema kwake.

Hata hivyo sasa hivi amezeeka amejaa uoga wa kuzuliwa jambo jingine baya zaidi. Kufaa kwake hata kama atafaa hawezi kufaa kwa kiwango kilekile cha 1985. Anaigopa mizengwe ya CCM hawezi kuthubutu kuleta jambo jipya.

........
Tatizo je CCM wataweza kumasafisha tope walilompaka?Ni mpaka pale wale waliokuwa kwenye mtandao watueleze ukweli na uongo juu ya matope yale waliompaka amasivyo bado hata yeye mwenyewe sidhani kama atakuwa willing kugombea nafasi hiyo.
 
Mpuuzi huyu, ndo maana Marekani walimpiga VETO alipopendekezwa kuwania kiti cha katibu mkuu UN. Waulizeni Wamarekani wanamjua vizuri

.........

You better tell us what happened! Au ndio mambo ya ugaidi?
 
daah huyu jamaa mimi nadhani umri wake umeenda na mikikimikiki ya urais sio mchezo hasa ukizingatia JK anaiacha nchi na chama chake vikiwa hoi hivyo twahitaji mpambnaj, sina shaka na uwezo wake wala usafi wake katika utendaji bali umri wake ndio unanipa waswasi.

.......

Alizaliwa 23 january 1942,mtu wa miaka 71 tunaweza sema mzee sana akina kibaki vipi, naona kama si mzee sana vile.
 
Asungilwemwaifunga unasema"Tatizo je CCM wataweza kumasafisha tope walilompaka?

Ni mpaka pale wale waliokuwa kwenye mtandao watueleze ukweli na uongo juu ya matope yale waliompaka amasivyo bado hata yeye mwenyewe sidhani kama atakuwa willing kugombea nafasi hiyo".

kama kakubali kurudi kamati kuu jee kupewa ulaji kama huo akatae? angalia kina Mangula walivyoondolewa kwa aibu leo hii amerudi tena.
 

Mkuu unapaswa kukubali kuwa kuna siasa na wa nasiasa,hata kama unaichukia ccm ila kuwa loyal kwa huyu mzee.

Tunaitaji kiongozi mwadilifu mwenye nia dhati ya kuwasaidia watanzania regadless chama gani anatokea.
Tafuta cv za wanasiasa wote tunaotarajia waje kuongoza taifa hili uziweke hapa yakwake ikiwemo mwisho utapata jawabu nani ni nani.


.....

Nchi hii hatuhitaji mtu mwenye cv nzuri ya kisiasa tunataka mtu anayeonyesha kwa msemo na matendo yake na aliye kinyume kabisa na tuliyoyazoe! Hatuhitaji mtu wa kuendeleza haya tunayoshuhudia sasa. Hatuhitaji mtu wa kuja kuyaficha machafu yanayoonekana sasa.

Tunataka mtu atakaye yasimamisha haya yanayoendelea sasa na kutugeuza tuelekee kinyume kabisa na haya yanayoendelea sasa. Na mtu wa aina hii kamwe hawezi kutoka miongoni mwao!

Kama tumekuwa tunaelekea mashariki kwa kipindi chote cha miaka 51 basi nadhani tunataka mtu atakaye tugeuza na kuelekea magharibi kabisa maana tunakoelekea tunaenda kutumbukia shimoni!

Tuweni makini sana na mbinu zao chafu maana wanachokitaka sasa ni kutumia mbinu yoyote ili warudi 2015 halafu baada ya hapo kila kitu kitaendelea kama ilivyo sasa na pengine kwa kasi zaidi! Tukumbuke mtu anayewekwa na watu wachache ni kwa ajili ya faida yao na wala si kwa ajili ya wananchi.

Kumbukeni ndugu zangu nia ya mabadiliko tunayoyataka ni kuwanyanganya watawala nguvu na kuirejesha mikononi mwetu umma.

Kamwe hatutaweza kurejeshewa nguvu hiyo na mtawala aliyekaa madarakani miaka mingi ampaka akawa na hati milki ya kutawala milele kama tunavyowasikia baadhi yao wakijiapisha kuwa kamwe hawatamwachia chama kingine kutawala nchi hii!

Ni lazima kwa faida yetu wananchi kumuondoa mtawala huyo na kuweka mwingine ili ajue kuwa nguvu ya kutawala ni ya wananachi na wananchi ndiyo wanaoamua wampe nani na ndiyo wenye kuamua kumnyanganya anapokuwa hafanyi kama walivyo tarajia.

Nia isiwe kukiondoa chama fulani kuweka kingine bali iwe kurejesha nguvu ya kutawala kwa umma wa watanzania ili wawe na sauti ya kuamua ninani anayewafaa kuwaongoza na akishindwa wawe na uwezo wa kusema hatukutaki na akawapisha watu wengine bila kungangania maana nguvu iko kwa umma si kwa serikali na dola kama ilivyo sasa kwa nchi nyingi za afrika.

Wapendwa tunapoelekea kubadilisha utawala tunahitaji kuitumia nafasi hii turejeshe nguvu ya utawala kwa umma wa watanzania ili wanaotaka utawala wajue kuwa umma ndiyo wenye kutoa au kuchukua nguvu hiyo wakiamua.

Lakini ni lazima kujua kuwa aliyekaa madarakani miaka mingi hawezi kukubali kurejesha nguvu hiyo hivihivi atatumia hila na ujanja mwingi iliabaki maana yeye ndiye anajua utamu wa utawala zaidi.

Ni lazima kumkataa kwanza akae pembeni na kumweka mwingine bila kujali atakuwa mzuri kuliko aliyeondoka ila nia ni kumuonyesha yule wa siku nyingi na huyu mpya kuwa nguvu ya kutawala ni ya wananchi na siyo ya chama au serikali fulani.

Huyu mpya atalizingatia hilo maana atajua wazi kuwa kama wameweza kumuondoa mtawala wa miaka mingi sembuse mimi! Hivyo atazingatia matakwa ya wananchi katika utawala wake na atakuwa na na heshima kwa wananchi wake kama mtumishi wao!

Kwa hiyo ni lazima kutambua falsafa inayotakiwa kuwa nyuma ya mabadiliko tunayoyataka. Hatutaki kubadilisha sura za watu tu bali tunataka kurejesha kwanza nguvu ya kumuweka tunayemtaka, wakati wowote bila kutishwa na chochote. Kimsingi tunataka viongozi ambao ni watumishi wetu badala ya watawala!

Kwa mantiki hii ni lazima tukubali kuwa tunahitaji kufanya mabadiliko makubwa yatakayo tupelekea kurejeshwa kwa umma nguvu ya kutawala kama kweli tunataka mabadiliko na kutoka katika kongwa hili.

Afrika tumepata uhuru toka kwa wazungu lakini kumetokea vikundi vingine vidogo katika jamii ambavyo ndo vimechukua nafasi ya wakoloni na kuendelea kuwatawala walio wengi na kuendelea kuwanyonya!

Tuendeleeni kumwomba Mungu ili aseme na mioyo ya watanzania waielewe falsafa hii maana wenzeu wakenya tayari wameshaanza kuelekea huko!
 
Kwa Tanganyika big nooooo kwa sababu makamu atakuwa nani? kwani wakati wa Mwinyi mzee wa ruksa makamu wa rais walimpataje? hakuna anayetaka kukuchuuza kwa wazenji issue ni kuwa kama huyu jamaa akigombea mbinu zipi zitumike kukabiliana naye na ccm yake.
Enzi za Mwinyi kulikuwa hakuna Mgombea Mwenza kama nowdays.
 
Nimekuwa nikiamini ya kwamba kuna uwezekano mkubwa wa chadema kuchukua nchi 2015 hasa ikimsimamisha dr Wilbroad slaa.Lakini tangu tetesi za CCM kumsimamisha dr Salim Ahmed Salim 2015 kushika kasi,nimeingiwa na wasiwasi kama CDM tutaweza kuchukua nchi,hii inatokana na
1 CV ya kuvutia ya dr salim
2 CCM kuanzakumsafishia njia mapema
3 kukubalika kwake kwa watanzaia wengi ata wa vyama vya upinzani
inabidi CDM wajipange vilivyo iwapo CCM watamsimamisha Dr salim.CCM wakijichanga walete mgonbea tofauti, CDM tushangilie ushindi ata kabla ya uchaguzi octoba 2015.
 
Nimekuwa nikiamini ya kwamba kuna uwezekano mkubwa wa chadema kuchukua nchi 2015 hasa ikimsimamisha dr Wilbroad slaa.Lakini tangu tetesi za CCM kumsimamisha dr Salim Ahmed Salim 2015 kushika kasi,nimeingiwa na wasiwasi kama CDM tutaweza kuchukua nchi,hii inatokana na
1 CV ya kuvutia ya dr salim
2 CCM kuanzakumsafishia njia mapema
3 kukubalika kwake kwa watanzaia wengi ata wa vyama vya upinzani
inabidi CDM wajipange vilivyo iwapo CCM watamsimamisha Dr salim.CCM wakijichanga walete mgonbea tofauti, CDM tushangilie ushindi ata kabla ya uchaguzi octoba 2015.

hata mimi namkubali Dr, salim lakini kama atagombea Uraisi kupitia chama cha mafisadi yaani Magamba ,atakuwa tayari amekosa kula za watanzia, labda agombee kupitia Cuf,au NCCR lakini Magamba ajue ameshakosa. Kitu kikubwa ni kwamba watanzania wanataka mabadiliko Dr. Salim hata weza kuwawajibisha magamba waliokula pesa zetu, waliotorosha, twiga wetu na pembe za ndovu, wanaoingia mikataba mibovu kwa faida zao. hataweza kuwawajibisha hao mafisadi sana sana tu atakuwa INACTVE. yupoyupo tu. Labda agombee Visiwani Zanzibar anaweza kuwatetea wanzanzibari . lakini kwa Jamhuri itamshinda hata weza hata siku moja. LABDA AKIGOMBEA KWA CHAMA PINZANI. hapo ataweza kidogo kushindana na DR. wa ukweli. Lakini vinginevyo NO.
 
na ujue wapiga kura wengi nchi hii ni waswahili ambao hawana ajira na elimu ya kutosha!

Hilo ndo tatizo. watanzania wanazichambua vema duru za kisiasa na kumchagua kiongozi kwa utashi wa uwelewa wao kisiasa. Dr Salim alipigwa chini kwa visingizio na kashfa kibao kutoka kwa wanamtandao. kwa ccm sasa chama hakina mvuto wamebaki watu wanaowafanya mtaji wa kisiasa. Tunataka kubadili mfumo mzima wa utawala na njia pekee ni hiki chama chetu (ccm) kukaa pembeni kwanza, tatizo ni mfumo. Salim amshinde vipi slaa
 
uwaziri mkuu wa salim ulikuwa mdororo mno kama mtakumbuka. sikumbuki legacy aliyoacha. alikuwa yupo yupo tu, anakwepa maamzi magumu kama tu jk alivyo.
 
Kikwete nae alianza kusafishiwa njia hivi hivi....na ndio amerufikusha hapa tulipo. Kuirudisha CCM madarakani nikujichimbia kaburi. kuwa naCV Nzuri sio kigezo cha kuwa kiongozi bora. Mfumo wa uongozi na watu watakao mzunguka nu tatizo. Kwamtazamo wangu kuiondoa ccm madarakani kutajenga uwajibikaji sio tu kwa chama kitakacho kuwa madarakani hata kitakacho shindwa.
 
Mbio za vijiti, tangu akiwa na miaka 20 ni kiongozi hadi sasa ni babu mnamtabiria aendelee kutawala? Yaani ccm hamna mtu wa kusimamisha zaidi ya huyo?
 
Hivi kuna mtu anajidanganya kwamba 2015 rais atakuwa mzee wa umri wa kina. Dr. Salim., Slaa.... mnajidanganya.
 
hata kura zikipigwa dar tu, dr slaa bado atamfunika salim. Pamoja na kuwa na vyeo tz dr salim hana legacy zaidi ya kuwapa wanajeshi magari ili wampende. Dr Salim is too old
 
Salim alikuwa PM kwa muda mfupi wa mwaka mmoja tu na aliingia baada ya Sokoine kufariki. Hilo la kupwaya alipwaya lini?
uwaziri mkuu wa salim ulikuwa mdororo mno kama mtakumbuka. sikumbuki legacy aliyoacha. alikuwa yupo yupo tu, anakwepa maamzi magumu kama tu jk alivyo.
 
Back
Top Bottom