Dr. Kikwete??? - samahani lakini...

Dr. Kikwete??? - samahani lakini...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,240
Reaction score
44,485
NImesoma magazeti na kuangalia luninga za nyumbani na mara kwa mara wameanza au wamepania kumtambulisha Kikwete kwa cheo cha Udaktari wa Heshima. Nikajiuiliza kama wanafanya hivyo kwa sababu yeye mwenyewe anataka wawe wanafanya hivyo au wanafanya hivyo kwa sababu wanapaswa kufanya hivyo? Siyo Kikwete tu bali wanafanya hivyo kwa Karume vile vile.

Nafahamu wote wawili wametunukiwa shahada hizo za heshima. Lakini ukizingatia kuwa wanakuwa kwenye habari mara kwa mara kuna umuhimu wa kuwaita hivyo kila wakati? Mbona Mkapa hawamuiti hivyo au Nyerere?

NI kwanini Wamarekani hawamtambulishi Obama kama Dr. Obama au Prof. Obama?

Labda inamsaidia kisiasa na kimtazamo mbele ya wananchi (maana ana shahada moja tu ya kusomea)..

Kama hilo ni kweli, kwanini wasiongezee na vyeo vya Luteni Mstaafu Dr. Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki?

Mimi naamini kuna wakati ambapo angeweza kutumia cheo hicho cha kitaaluma kwa ujiko kama siku moja akiwa na ujasiri wa kwenda kuzungumza na wasomi wa chuo kikuu kimoja nchini basi hapo mnaweza kumtambulisha kama Dr. Kikwete. Maana siwezi kufikiria kwenye mikutano ya kimataifa wakimtambulisha kama Dr. Kikwete anajisikiaje mbele ya ma Dr. wenyewe?

Ila kama inamfanya ajisikie vizuri.. more power to him..
 
Ukichunguza kwa umakini taratiiibu umuhimu wa Masters siku za usoni utakuja pungua na ndipo watu watatafuta PhD kwa bidii kama ilivyo Masters sasa hv! PhD umuhimu wake ukipungua sijui nini kitakachofuatia,maana Undergraduate(Degree) ni kama cheti cha form four au six kwa sasa jinsi watu wanavyochukulia.
 
Tatizo sio yeye, tatizo kuna kasumba inaonekana kujulikana na hizi scholary titles ktk jamii. Sioni sababu ya waziri kupata tabu ya kutunga cheti ambacho akina ulazima ktk utendaji wake ni ushamba tu wanyumbani.

Anachofanya JK ni kuwalizisha umma, kwa kuwa inaonekana hawajui kipimo cha kazi. Wao wanadhani ukiwa Dr ndio tosha hata wakilala njaa kwao sawa.

Kaazi kweli kweli, jamaa wanajua wanadili na akina nani when it comes to crunch time, wakati sisi tupo busy na social networking in most part hapa.
 
Kama hilo ni kweli, kwanini wasiongezee na vyeo vya Luteni Mstaafu Dr. Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki?

Hiyo bold imenikumbusha ya Idi Amin (RIP) wa Uganda : General Field Marshall Conqueror of the British Empire Lord of All the Beasts of the Earth and Fishes of the Sea Idi Amin Dada Oumee - Alipenda sana kujitambulisha kwa staili hiyo. Well it "tends to" give "them" more power and authority.
 
NImesoma magazeti na kuangalia luninga za nyumbani na mara kwa mara wameanza au wamepania kumtambulisha Kikwete kwa cheo cha Udaktari wa Heshima. Nikajiuiliza kama wanafanya hivyo kwa sababu yeye mwenyewe anataka wawe wanafanya hivyo au wanafanya hivyo kwa sababu wanapaswa kufanya hivyo? Siyo Kikwete tu bali wanafanya hivyo kwa Karume vile vile.

Nafahamu wote wawili wametunukiwa shahada hizo za heshima. Lakini ukizingatia kuwa wanakuwa kwenye habari mara kwa mara kuna umuhimu wa kuwaita hivyo kila wakati? Mbona Mkapa hawamuiti hivyo au Nyerere?

NI kwanini Wamarekani hawamtambulishi Obama kama Dr. Obama au Prof. Obama?

Labda inamsaidia kisiasa na kimtazamo mbele ya wananchi (maana ana shahada moja tu ya kusomea)..

Kama hilo ni kweli, kwanini wasiongezee na vyeo vya Luteni Mstaafu Dr. Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki?

Mimi naamini kuna wakati ambapo angeweza kutumia cheo hicho cha kitaaluma kwa ujiko kama siku moja akiwa na ujasiri wa kwenda kuzungumza na wasomi wa chuo kikuu kimoja nchini basi hapo mnaweza kumtambulisha kama Dr. Kikwete. Maana siwezi kufikiria kwenye mikutano ya kimataifa wakimtambulisha kama Dr. Kikwete anajisikiaje mbele ya ma Dr. wenyewe?

Ila kama inamfanya ajisikie vizuri.. more power to him..

Mkuu Mwanakijiji CCJ ina ugomvi na Mengi maaana jana nimecheki taarifa ya Habari ya ITV usiku sikuona Press Release yenu, just curous maana as I know kuna uhusiano mkubwa sana kati ya ya Mengi na Wanamgambo wa CCM
 
Mimi nadhani kuna tatizo kubwa sana katika jamii zetu za kimasikini (wa mawazo na hekima). Watu wanataka waheshimike kwa vyeo na vyeti au majina yao badala ya kujaribu kuheshimika kwa matendo na "legacy" zaidi ... kwa sasa hapa bongo kila mtu yuko busy anasoma masters, wengi wao nilioongea nao wanasoma si kwa sababu walikuwa wanahitaji masters ili kusudi wafanye vizuri katika kazi zao bali kwa sababu wanataka waonekane wasomi....
 
U Dr Tanzania umekosha heshima.
Hata wa heshima !!!How come Karume au Mzindakaya wapewe u dr wa heshima?

Bishop Tutu na Mandela wana u DR wa heshima kutoka top University za duniani .Lakini huwezi kusikia wanajiita .PM wa UK aliyeondoka ,Gordon Brown alikuwa na real Phd,lakini hata siku moja hakujulikana na kujiita Dr Gordon Brown.

Sasa Phd fake za akina Nagu,Kamala,Nchimbi na wengineo ndio zimechafua PHD Tanzania.
 
Ukichunguza kwa umakini taratiiibu umuhimu wa Masters siku za usoni utakuja pungua na ndipo watu watatafuta PhD kwa bidii kama ilivyo Masters sasa hv! PhD umuhimu wake ukipungua sijui nini kitakachofuatia,maana Undergraduate(Degree) ni kama cheti cha form four au six kwa sasa jinsi watu wanavyochukulia.

Umenikumbusha habari nilizosoma hivi karibuni kuhusu ghasia za maandamano zilizotokana na hali ya uchumi nchini Greece. Tatizo moja ni ukosefu wa kazi kwa wale wanaomaliza vyuoni. Kuna wengi wenye shahada za PhD huambulia kazi za u-waiter katika restaurants!
 
Mkuu Mwanakijiji CCJ ina ugomvi na Mengi maaana jana nimecheki taarifa ya Habari ya ITV usiku sikuona Press Release yenu, just curous maana as I know kuna uhusiano mkubwa sana kati ya ya Mengi na Wanamgambo wa CCM

Hawa (kwenye red) ni akina nani -- harakisha jibu tafadhali!
 
udocta wa kupewa kwenye sahani huo ni kuaibishana. ningekuwa ndo mimi nimeitwa hivyo, nisingependa watu waniite docta hivyo kwasababu wanakuwa wananiumbua kuwa sijapata udaktari toka kupiga kitabu, bali ni watu tuwaliamua kufany ahivyo kwa sababu tofautitofauti....ule udocta amepewa kenya walikuwa wanambembeleza na kumhonga juu ya east africa community na uhusiano mwingine kama huo, kwani alistahili kupata tuzo ya aina hiyo kweli?...hamna lolote. udaktari haswa ni ule mtu unapiga kitabu unakomaa hadi uupate, uo wa kuandikiwa muhutasari wa hotuma kila kitu alafu unaambiwa wewe ni dakitari, ni second hand hiyo. mtumbaaa!
 
Mchungaji Doctor Mh. Mbunge Mama noninoo

msiende mbali, ni Dr.Mh.Mbunge mama Rwakatale...bora hata huyu badala ya kujenga mahoteli na biashara za harakaharaka, amejanga shule zenye wanafunzi si chini ya elfu kumi. angeamua angelijenga hotel au business zingine. sasa kikwete amefanya nini?
 
Hawa ni madaktari wa mazingaombwe na PhD za ufisadi no more
 
U Dr Tanzania umekosha heshima.
Hata wa heshima !!!How come Karume au Mzindakaya wapewe u dr wa heshima?

Bishop Tutu na Mandela wana u DR wa heshima kutoka top University za duniani .Lakini huwezi kusikia wanajiita .PM wa UK aliyeondoka ,Gordon Brown alikuwa na real Phd,lakini hata siku moja hakujulikana na kujiita Dr Gordon Brown.

Sasa Phd fake za akina Nagu,Kamala,Nchimbi na wengineo ndio zimechafua PHD Tanzania.


Ni kweli Gordon Brown ana PhD ya History ya chuo kikuu cha Edinburgh . Hata siku moja hajawahi jiita Dr ama kuitwa hivyo. Lakini tumeshuhudia hata wale clinical officers akina Asha Kigoda wanajiita Drs, akina Jakaya Mrisho, na Karume bila hata aibu wanatanguliza mbele Dr. Tunapenda sifa za kijinga....Nchimbi, Kamala, Nagu, Makongoro, Dialo, Mzindakaya list ni ndefu sana

Jamani hata Dr Robert Mugabe si naye ana PhD hizi za heshima?
 
Hiyo bold imenikumbusha ya Idi Amin (RIP) wa Uganda : General Field Marshall Conqueror of the British Empire Lord of All the Beasts of the Earth and Fishes of the Sea Idi Amin Dada Oumee - Alipenda sana kujitambulisha kwa staili hiyo. Well it "tends to" give "them" more power and authority.

haahhaahaaaa!umenichekesha sana nikakumbuka alivyoomba wavae gloves yeye na na hayati mwalimu Nyerere wapapambane uso kwa uso katika ring.Africa hii naamini ule usemi unaosema msomi wa ukweli hawezi kuwa mwanasiasa
 
Sio Gordon Brown tuu, lakini hata hapa kwetu wenye PHD za ukweli kama Magufuli hawatangulizi viujiko vya ajabu ajabu!,
 
Tuache utani kupata PhD bila kuwa na Masters hio PhD ni fake kabisa na haina ile nguvu, nashangaa mno kila raisi lazima apewe PhD,Hivi ni kipi JK kafanya au kufanyia Tanzania hadi atunukiwe hiyo PhD? Mbona Mwinyi hakupewa? TCU toeni muongozo, shule si mchezo bwana watu wanapenda vya bure tu, si sawa kwa wasomi.
 
ni kupenda tu misifa kwa kikwete................kuna watu waliishatunukiwa mashahada ya bure kama hayo lakini wameyatosa na hawataki nkuyatumia kutokana na kutokuwa namantiki yoyote ndio maana wengine walikataa vyeo vingine waliamua kujiita MWALKIMU...
NImesoma magazeti na kuangalia luninga za nyumbani na mara kwa mara wameanza au wamepania kumtambulisha Kikwete kwa cheo cha Udaktari wa Heshima. Nikajiuiliza kama wanafanya hivyo kwa sababu yeye mwenyewe anataka wawe wanafanya hivyo au wanafanya hivyo kwa sababu wanapaswa kufanya hivyo? Siyo Kikwete tu bali wanafanya hivyo kwa Karume vile vile.

Nafahamu wote wawili wametunukiwa shahada hizo za heshima. Lakini ukizingatia kuwa wanakuwa kwenye habari mara kwa mara kuna umuhimu wa kuwaita hivyo kila wakati? Mbona Mkapa hawamuiti hivyo au Nyerere?

NI kwanini Wamarekani hawamtambulishi Obama kama Dr. Obama au Prof. Obama?

Labda inamsaidia kisiasa na kimtazamo mbele ya wananchi (maana ana shahada moja tu ya kusomea)..

Kama hilo ni kweli, kwanini wasiongezee na vyeo vya Luteni Mstaafu Dr. Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki?

Mimi naamini kuna wakati ambapo angeweza kutumia cheo hicho cha kitaaluma kwa ujiko kama siku moja akiwa na ujasiri wa kwenda kuzungumza na wasomi wa chuo kikuu kimoja nchini basi hapo mnaweza kumtambulisha kama Dr. Kikwete. Maana siwezi kufikiria kwenye mikutano ya kimataifa wakimtambulisha kama Dr. Kikwete anajisikiaje mbele ya ma Dr. wenyewe?

Ila kama inamfanya ajisikie vizuri.. more power to him..
 
"Apendaye sifa hupenda kusifiwa, japo hastahili sifa anazopewa" JK na kundi kubwa la viongozi hasa wa serikali hupenda sifa wasizokuwa nazo na sababu kubwa ya kufanya hivi ni kule kupenda kwao kuonekana kuwa " out of a million they stand as one" so watu waanze kuwaabudu na kuwanyenyekea na mwisho huchukua dhima ya kuwaamulia watu wakifikiri wao ndio thinking tank. Kwa hakika huu ni ulimbukeni wa wasiojua, ili waonekane wanajua! Na hii ni tofauti sana na wenye sifa halisi kwani wao huwa hawapendi kusifiwa, maana wanajua thamani ya sifa hizo! . nakumbuka mimi nimefanya kazi ya utafiti na Profesa mmoja toka chuo kikuu cha Minnessota USA, kwa miezi sita bila kujua kuwa ni Prof, nilikuja jua siku mmoja wa wanafunzi wake alipokuja kwa utafiti, hapa namaanisha kuwa wenye sifa stahili huwa hawajitangazi na kujikweza, kama afanyavyo DR JK!
 
Back
Top Bottom