Asubuhi
Kumekucha hapa Tabora.Nimeamka nikiwa na shauku kubwa ya kujua kitakachotokea.Nimekuja hapa Igunga kushuhudia haki ikitendeka. Sikulala vyema jana...mara Kafumu,mara Kashindye ndotoni.Tuache hayo.Mnamo saa 12:30 nikajisogeza viwanja vya Mahakama Kuu hapa Tabora.Nilitumai kuwa nitakuwa wa kwanza kufika.Haikuwa hivyo.Watu walikuwa wamesheheni vya kutosha katika viunga vya Mahakama Kuu.Sijui walilala hapahapa?!
CCM waingia
Wakichagizwa na nyimbo za John Komba,wanachama wa CCM waliwasili hapa Mahakamani.Ingawa hawakuwa wengi kiiivyo,lakini walionekana waliojiandaa.Wakawa wanaimba huku wakizungukazunguka huku na huko viunga vya Mahakama Kuu Tabora. Ni raha ilioje!
CHADEMA nao...
Wanachama na wafuasi wa CHADEMA nao waliwasili kwa mamia.Viwanja vikajaa.Nyimbo za ukombozi za kama Sinema za Sarafina na nyinginezo zilihanikiza anga la Mahakama Kuu.Mwito wa People's power ukatawala. Mwe! Raha kweli...
Wenye kesi...
Mnamo saa mbili hivi,Mwalimu Kashindye aliwasili.Alionekana mchangamfu na mwenye matumaini.Aliongozana na Wakili wake aliyekuwa na Wasaidizi wake wawili.Si mwingine;ni Prof.Abdallah Safari. Wanaongea na kuchekacheka.Sijui nisiendelee?
Dr.Kafumu naye anawasili akiwa na Mawakili wake wawili.Kwakweli siwajui.Labda macho yangu ya kizee yalinizuia kuwaona vyama.Pia,walizongwa mno na washabiki wao.Macho yangu ya kizee yakaninyima uhondo.Ingawa walizongwa kwa shangwe,hawakuwa na furaha.Walinyongea pamoja na kuwa wenye furaha za kulazimisha. Dr.,kwa muda mwingi alikuwa busy kuongea na simu akijitenga mbali na wafuasi wake kufanya hivyo.Huo ndio ukweli.
Dola yaonekana
Magari yaliyosheheni polisi wa kutuliza ghasia yapatayo kama manne yaliwasili.Yakafuatiwa na gari la maji ya kuwasha. Askari wengi hawakushuka magarini.Yamekuwa haya tena? Ila,wananchi wakaendelea na yao.
Mlango wafunguliwa
Mlango wa Mahakama Kuu Tabora,kuruhusu watu waingie chumba cha Hukumu,ulifunguliwa saa 3 kamili.Ilikuwa mshikemshike.Kila mtu alitaka kuingia ndani.Mminyano kwelikweli.Nikapata bahati ya kusukumiwa ndani na kundi la vijana.Nikashukuru pamoja na kupata maumivu ya hapa na pale. Wenye kesi na Mawakili wao;wananchi wa kawaida kila mtu alikaa sehemu yake tayari kwa hukumu.Maongezi ya hapa na pale;huyu na yule yakateka chumba cha Mahakama.
Mara: Coooooooooourrrrrrrrrrrrrrrrt!
Wote tukasimama.Itaendelea kesho kwakuwa nimepata wageni hapa nyumbani kwangu...