Dr. Justine Katunzi wa UDSM Afariki Dunia

WanaJF ni kweli Dr. Justine Katunzi wa DSM amefariki leo hii akiwa anafundisha darasani. Nathibitisha hilo. Huyu alikuwa Lecturer pale Business School - UDSM na alikuwa akifundisha OB. Aliwahi kuwa Mbunge wa Geita, huko Mwanza. RIP Dr. Katunzi
 
RIP Raha ya milele ampe ee bwana na mwanga wa milele umwangazie apumzike kwa amani AMEN
 
Leo Taifa letu limepoteza mwanazuoni mahiri wa shule ya Biashara ya Chuo kikuu cha Dar es salaam (UDBS).

Taarifa zinasema,kifo hicho kilitokea baada ya kuanguka ghafla na baadaye kupoteza maisha kabla hata ya kufikishwa Hospitali,tukio hilo limetokea wakati alipokuwa akifundisha wanafunzi wa MBA (2nd Year mwaka 2011) jioni ya leo.

Pole sana familia ya marehemu Dr Katunzi, wanajumuiya wa UDSM,wanafunzi wenzangu wa MBA,wanafunzi wote walihitimu Bcom kutoka UDSM kwa miaka aliyokuwepo mhadhiri huyu machachari na mcheshi sana!inauma sana.

Taifa litakumbuka mchango wako mkubwa katika Fani ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu,hakika tutakumbuka na kuyafanyia kazi yale yote uliyotuasa kwa manufaa ya Taifa letu Tanzania.


Bwana alitoa na Bwana ametwaa,jina la Bwana libarikiwe!
Amina
 
J. M. Katunzi, B.A (Dar), MBA (Arizona), PGD (RVB), Ph.D. (London)] - Senior Lecturer [RIP]
 
WanaJF ni kweli Dr. Justine Katunzi wa DSM amefariki leo hii akiwa anafundisha darasani. Nathibitisha hilo. Huyu alikuwa Lecturer pale Business School - UDSM na alikuwa akifundisha OB. Aliwahi kuwa Mbunge wa Geita, huko Mwanza. RIP Dr. Katunzi
RIP Dr. Justine Katunzi
 
Dah! RIP doctor Katunzi, umetufundisha vizuri sana Organization Behavior
 
Alikuwa ni mwalimu wangu HR 200, dah! Alikuwa Anakamata kweli bt he was very good. R.I.P Dr. Katunzi.
 
RIP Dr.kwa wote waliosoma pale UDSM miaka ya nyuma tunamkumbuka sana huyu bwana!alikua anafundisha Principals of Management 1st YEAR na organisation behavior.Pia kwa wale waliosoma MBA EITHER udsm au OUT pia alikua anapiga OB.du RIP phd holder.
 
Back
Top Bottom