Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
Gazeti la Tanzania Daima la leo linatutaarifu ya kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru Dr. Hosea ameitikisa Ikulu baada ya kubainika aliongea na Shushushu wa Marekani juu ya JK kuwa ni kikwazo cha vita dhidi ya rushwa kubwakubwa.............na ya kuwa JK amekuwa akizuia mafisadi kushitakiwa kwenye mahakama zetu..........kwa visingizio vya ya kuwa hakuna ushahidi wa kutosha wa kuwafikisha mahakamani kazi ambayo ni ya DCI na DPP.......
Gazeti hili limebaini ya kuwa JK amesononeshwa na madai hayo ya Dr. Hosea pamoja ya kuwa tayari amekwisha kuyapinga hadharani kuwa alinukuliwa vibaya...........
Nionavyo mimi Dr. Hosea ataondolewa hivi karibuni kwa makosa ya kutathmini utendaji wa bosi wake na kwa kufanya hivyo alikosa imani na ni utovu wa nidhamu..................Hii tukiachilia mbali ukweli kuwa JK ni mtu wa visasi sana.....................
Dk. Hosea aitikisa Ikulu
• Serikali yapatwa na kigugumizi kumchukulia hatua
na Edward Kinabo
TAARIFA kwamba Rais Jakaya Kikwete hataki vigogo wa serikali wanaotuhumiwa kwa rushwa wafikishwe mahakamani zimeelezwa kumpa mshtuko mkubwa na kuiweka Ikulu katika wakati mgumu wa kutojua nini cha kufanya kwa sasa.
Mmoja wa watu walio karibu naye kikazi ameliambia Tanzania Daima kwamba tuhuma hizo ni nzito dhidi ya Rais Kikwete.
Kwamba zilionekana kumshtuka, baada ya Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea, kuripotiwa kutoa taarifa hizo kwa mwanadiplomasia mmoja wa Marekani aitwaye, Purnell Delly, walipokutana Julai 14 jijini Dar es Salaam mwaka 2007.
Mtandao wa Wikileaks wa nchini Marekani ndio ulioibua taarifa hizo kuhusu uwezo na nia ya Rais Kikwete katika kushughulikia ufisadi, ukidai kuwa ndiye anayekwamisha kushtakiwa kwa baadhi ya vigogo serikalini wanaotuhumiwa kuhusika katika rushwa kubwa nchini.
Taarifa hizo zilizochapishwa na gazeti la The Guardian la Uingereza na kurejewa na vyombo vya habari vya hapa nchini, zilinukuu taarifa za kibalozi za Marekani zikisema Dk. Hosea alimweleza mwanadiplomasia huyo kwamba ugumu wa kupambana na ufisadi Tanzania unaanzia Ikulu.
"Unajua hizo habari zimemtangaza yeye (Rais Kikwete) na CCM kwamba hawana nia ya kupambana na rushwa, yaani maana yake wananchi wamekuwa wakidanganywa tu.
"Sasa hizo ni tuhuma nzito sana kwa mkuu wa nchi …kama ni kweli au uongo siwezi kuzungumzia hilo lakini ni rahisi watu kuamini kwa sababu aliyetajwa ni Dk.
Hosea…eeh eeh maana huyu aliteuliwa na mwenyewe. "Angesema mwingine labda tusingeamini lakini huyu…kwa kweli ni tuhuma nzito na mwenyewe (Rais Kikwete) zimemnyong'onyeza sana," alisema mtoa taarifa huyo.
Taarifa za kuaminika kutoka ndani ya Ikulu jijini Dar es Salaam zinasema mpaka sasa bado wanatafakari kwa kina hatua za kuchukua ili kupata namna bora ya kusafisha jina la Rais Kikwete na kurejesha imani ya wananchi kwake kuhusu mapambano dhidi ya rushwa.
"Mpaka sasa sijajua hatua yoyote itakayoamuliwa kwa Dk. Hosea lakini najua suala lake bado wenyewe wanalitafakari kwa sababu ni wazi kwamba jina la rais limechafuka sana," alisema mtoa taarifa wetu mwingine.
Alipoulizwa kwa nini Dk. Hosea achukuliwe hatua wakati ameshakanusha kutoa kauli hizo dhidi ya rais, alisema: "Ni kwa sababu maelezo yake ya kukanusha hayana nguvu….yeye amekataa kwamba alisema rais hataki vigogo washtakiwe……badala yake akadai kwamba alichomwambia yule Mmarekani ni kwamba Rais Kikwete hawezi kuruhusu vigogo na watuhumiwa wengine wa ufisadi washtakiwe bila ushahidi kwa sababu serikali inaweza kupata hasara.
"Sasa unaweza kuona waziwazi kuwa hayo maelezo yake ya kukanusha ni ya kutengeneza tu kwa sababu yule Mmarekani sio mbumbumbu wa sheria kiasi hicho hadi ampe maelezo hayo. Ni ukweli ulio wazi kwamba huwezi kumshtaki mtu bila ushahidi – hilo huwezi kuwa na haja ya kumueleza mtu.
"Yaliyofichuliwa na Wikileaks ndio ukweli wenyewe wa aliyoyasema. Na hawa majasusi wa Marekani pengine nyie hamuwajui vizuri, ni watu wanaofanya kazi zao kwa umakini wa hali ya juu. …na hapa nchini wapo wengi tu."
Mkurugenzi wa Mawasialiano Ikulu, Salva Rweyemamu alipoulizwa na chombo kimoja cha habari kuhusiana na tuhuma hizo nzito dhidi ya rais, alijibu kuwa Ikulu haina cha kueleza.
Hiyo ilikuwa ni siku chache tu zilizopita mara baada ya kuripotiwa kwa habari hizo zinazomhusu Dk. Hosea.
Aidha, Tanzania Daima ilipompigia simu Rweyemamu jana ili kujua kama ana lolote la kusema kuhusiana na tuhuma hizo dhidi ya rais, simu yake ilikuwa haipatikani.
Hata alipotumiwa ujumbe uliomtaka kueleza hatua gani Ikulu itachukua baada ya Dk. Hosea kuripotiwa kumtaja rais kwamba hataki vigogo mafisadi washtakiwe, ujumbe huo haukujibiwa hadi tunakwenda mitamboni.
Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amesema taarifa zilizoibuliwa na Wikileaks kuhusu kauli zilizotolewa na Dk.
Hosea kwa mwanadiplomasia huyo wa Marekani, ni ushahidi tosha kwamba Rais Kikwete na CCM hawana nia yoyote ya dhati ya kukomesha rushwa na ufisadi nchini.
Akitoa salamu zake za Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, jana Profesa Lipumba alisema upo ushahidi wa kutosha unaoonyesha jinsi serikali pamoja na watendaji wake husika akiwemo mkurugenzi huyo wa TAKUKURU, wanavyowatetea mafisadi na kuwasafisha.
"Taarifa ya balozi huyu wa Marekani ni kwamba alielezwa na Dk. Hosea kuwa Rais Kikwete hana nia thabiti ya kuwafikisha mahakamani vigogo wa ufisadi walio karibu yake. Ushahidi mwingine ni ule aliowahi kuutoa Rais Kikwete mwenyewe ambapo alikemea watu wanaotaka Mkapa ashtakiwe kwa kuhusishwa na ufisadi wamuache rais huyo mstaafu apumzike Akiendeleza kile alichokiita ushahidi wa Rais Kikwete na CCM kuwalinda mafisadi na wala rushwa wakubwa, Profesa Lipumba alisema: "Pamoja na shirika la upelelezi wa makosa ya jinai la SFO la Uingereza kutoa ushahidi wa rushwa aliyopewa Saileth Vithlan ya dola milioni 12.4 na ushahidi wa kibenki kwamba alitumia dola milioni moja katika akaunti zinazomilikiwa na mwanasheria mkuu wa serikali katika kipindi cha awamu ya tatu, mpaka leo hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.
Gazeti hili limebaini ya kuwa JK amesononeshwa na madai hayo ya Dr. Hosea pamoja ya kuwa tayari amekwisha kuyapinga hadharani kuwa alinukuliwa vibaya...........
Nionavyo mimi Dr. Hosea ataondolewa hivi karibuni kwa makosa ya kutathmini utendaji wa bosi wake na kwa kufanya hivyo alikosa imani na ni utovu wa nidhamu..................Hii tukiachilia mbali ukweli kuwa JK ni mtu wa visasi sana.....................
Dk. Hosea aitikisa Ikulu
• Serikali yapatwa na kigugumizi kumchukulia hatua
na Edward Kinabo
Mmoja wa watu walio karibu naye kikazi ameliambia Tanzania Daima kwamba tuhuma hizo ni nzito dhidi ya Rais Kikwete.
Kwamba zilionekana kumshtuka, baada ya Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea, kuripotiwa kutoa taarifa hizo kwa mwanadiplomasia mmoja wa Marekani aitwaye, Purnell Delly, walipokutana Julai 14 jijini Dar es Salaam mwaka 2007.
Mtandao wa Wikileaks wa nchini Marekani ndio ulioibua taarifa hizo kuhusu uwezo na nia ya Rais Kikwete katika kushughulikia ufisadi, ukidai kuwa ndiye anayekwamisha kushtakiwa kwa baadhi ya vigogo serikalini wanaotuhumiwa kuhusika katika rushwa kubwa nchini.
Taarifa hizo zilizochapishwa na gazeti la The Guardian la Uingereza na kurejewa na vyombo vya habari vya hapa nchini, zilinukuu taarifa za kibalozi za Marekani zikisema Dk. Hosea alimweleza mwanadiplomasia huyo kwamba ugumu wa kupambana na ufisadi Tanzania unaanzia Ikulu.
"Unajua hizo habari zimemtangaza yeye (Rais Kikwete) na CCM kwamba hawana nia ya kupambana na rushwa, yaani maana yake wananchi wamekuwa wakidanganywa tu.
"Sasa hizo ni tuhuma nzito sana kwa mkuu wa nchi …kama ni kweli au uongo siwezi kuzungumzia hilo lakini ni rahisi watu kuamini kwa sababu aliyetajwa ni Dk.
Hosea…eeh eeh maana huyu aliteuliwa na mwenyewe. "Angesema mwingine labda tusingeamini lakini huyu…kwa kweli ni tuhuma nzito na mwenyewe (Rais Kikwete) zimemnyong'onyeza sana," alisema mtoa taarifa huyo.
Taarifa za kuaminika kutoka ndani ya Ikulu jijini Dar es Salaam zinasema mpaka sasa bado wanatafakari kwa kina hatua za kuchukua ili kupata namna bora ya kusafisha jina la Rais Kikwete na kurejesha imani ya wananchi kwake kuhusu mapambano dhidi ya rushwa.
"Mpaka sasa sijajua hatua yoyote itakayoamuliwa kwa Dk. Hosea lakini najua suala lake bado wenyewe wanalitafakari kwa sababu ni wazi kwamba jina la rais limechafuka sana," alisema mtoa taarifa wetu mwingine.
Alipoulizwa kwa nini Dk. Hosea achukuliwe hatua wakati ameshakanusha kutoa kauli hizo dhidi ya rais, alisema: "Ni kwa sababu maelezo yake ya kukanusha hayana nguvu….yeye amekataa kwamba alisema rais hataki vigogo washtakiwe……badala yake akadai kwamba alichomwambia yule Mmarekani ni kwamba Rais Kikwete hawezi kuruhusu vigogo na watuhumiwa wengine wa ufisadi washtakiwe bila ushahidi kwa sababu serikali inaweza kupata hasara.
"Sasa unaweza kuona waziwazi kuwa hayo maelezo yake ya kukanusha ni ya kutengeneza tu kwa sababu yule Mmarekani sio mbumbumbu wa sheria kiasi hicho hadi ampe maelezo hayo. Ni ukweli ulio wazi kwamba huwezi kumshtaki mtu bila ushahidi – hilo huwezi kuwa na haja ya kumueleza mtu.
"Yaliyofichuliwa na Wikileaks ndio ukweli wenyewe wa aliyoyasema. Na hawa majasusi wa Marekani pengine nyie hamuwajui vizuri, ni watu wanaofanya kazi zao kwa umakini wa hali ya juu. …na hapa nchini wapo wengi tu."
Mkurugenzi wa Mawasialiano Ikulu, Salva Rweyemamu alipoulizwa na chombo kimoja cha habari kuhusiana na tuhuma hizo nzito dhidi ya rais, alijibu kuwa Ikulu haina cha kueleza.
Hiyo ilikuwa ni siku chache tu zilizopita mara baada ya kuripotiwa kwa habari hizo zinazomhusu Dk. Hosea.
Aidha, Tanzania Daima ilipompigia simu Rweyemamu jana ili kujua kama ana lolote la kusema kuhusiana na tuhuma hizo dhidi ya rais, simu yake ilikuwa haipatikani.
Hata alipotumiwa ujumbe uliomtaka kueleza hatua gani Ikulu itachukua baada ya Dk. Hosea kuripotiwa kumtaja rais kwamba hataki vigogo mafisadi washtakiwe, ujumbe huo haukujibiwa hadi tunakwenda mitamboni.
Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amesema taarifa zilizoibuliwa na Wikileaks kuhusu kauli zilizotolewa na Dk.
Hosea kwa mwanadiplomasia huyo wa Marekani, ni ushahidi tosha kwamba Rais Kikwete na CCM hawana nia yoyote ya dhati ya kukomesha rushwa na ufisadi nchini.
Akitoa salamu zake za Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, jana Profesa Lipumba alisema upo ushahidi wa kutosha unaoonyesha jinsi serikali pamoja na watendaji wake husika akiwemo mkurugenzi huyo wa TAKUKURU, wanavyowatetea mafisadi na kuwasafisha.
"Taarifa ya balozi huyu wa Marekani ni kwamba alielezwa na Dk. Hosea kuwa Rais Kikwete hana nia thabiti ya kuwafikisha mahakamani vigogo wa ufisadi walio karibu yake. Ushahidi mwingine ni ule aliowahi kuutoa Rais Kikwete mwenyewe ambapo alikemea watu wanaotaka Mkapa ashtakiwe kwa kuhusishwa na ufisadi wamuache rais huyo mstaafu apumzike Akiendeleza kile alichokiita ushahidi wa Rais Kikwete na CCM kuwalinda mafisadi na wala rushwa wakubwa, Profesa Lipumba alisema: "Pamoja na shirika la upelelezi wa makosa ya jinai la SFO la Uingereza kutoa ushahidi wa rushwa aliyopewa Saileth Vithlan ya dola milioni 12.4 na ushahidi wa kibenki kwamba alitumia dola milioni moja katika akaunti zinazomilikiwa na mwanasheria mkuu wa serikali katika kipindi cha awamu ya tatu, mpaka leo hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.