Dr Harrison Mwakyembe atakuwa Waziri Bora wa Habari kuliko Nape Nnauye

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, amani iwe kwenu.

Nape ameondoka na Mwakyembe ameingia. Kuna watu walikuwa na wasiwasi kuwa huenda Mwakyembe asifanikiwe kuvaa kiatu kilichoachwa na Nape. Hata hivyo kwa muda mfupi aliokalia kiti hicho, amekuwa na ufanisi mkubwa na weledi wa hali ya juu. Amerudisha nyoyo za waliokata tamaa na amepunguza joto lililotanda na mashambulizi dhidi ya Serikali.

Mwakyembe ni shujaa. Alipoteuliwa kuwa Waziri wa Habari, ameanza kazi mara moja na kwa jinsi alivyoshughulikia suala la Nay wa Mitego kwa hakika limethibitisha kuwa jamaa ni mtu muhimu sana kwenye wizara hiyo. Tatizo la Nape ni umri wake. Bado ana utoto mwingi na hivyo kujikuta akiendekeza tamaa zake badala ya kufanya kazi. Aliwagawa wasanii badala ya kuwaunganisha. Amevigawa vyombo vya habari kwa kuvipendelea baadhi na kuviponda vingine.

Kwa ujumla Nape hakuwa kiongozi mtendaji. Aliendekeza majungu na fitina Wizarani. Afadhali ameondoka.

Karibu Dr Mwakyembe. Chapa kazi. Usimpendelee mtu na wala usimuonee mtu. Haijapita hata mwezi tayari Nape amebaki historia
 
Nape aliplay key role katika kuzuia bunge live, hii ni dhambi kubwa kwa umma na itamtafuna kisiasa.

Pili alipeleka muswada wa habari bungeni, ambao kwa upande mmoja una mapungufu makubwa ya kuzuia uhuru wa habari.

Lakini Tangu Nape awe Waziri wa michezo Taifa Stars ya Wakubwa imekuwa kichwa cha Mwendawazimu, Mwakyembe kaingia tu, tumeshinda gemu mbilu in a row!

Nape hajamsaidia Mwenyekiti wa Yanga katika madhila yake, I hope Mwakyembe atasaidia Manji awe huru!

Hata hivyo nampongeza Nape jinsi alivyosimamia suala la kuvamiwa Kituo kimoja cha Habari na Bashite!

Yanga hoyeeee !
 
Kwa majungu, chuki, fitna na kujipendekeza kaka unatisha, we ni chiboko, mola niepushe na huu ugonjwa wa kulamba watu miguu,

Ulitegemea ataandika nini kama sio yale yale anayoyaleta kila siku?

Huyu ndio wale wale, Waziri akisema Jambo atakuja kuliunga mkono na kusema Mawaziri wanafanya kazi.

Rais akija kutengua kilichosemwa na Waziri atasifia na kuunga mkono huku akisema Rais anasikiliza.
 
Siku zote msema kweli ni mpenzi wa Mungu
Ni kweli kaka lakini hata haya unayopost humu Mungu pia hapendi, mbona hukuyasema mapema wakati Nape yupo Waziri, kuyasema muda huu ni kama unajustify alichafanyiwa, ili kionekane kwamba alistahili adhabu ile, hats off Broo sio kwa fitna hizi, wacha nife maskini kuliko kutegemea ridhki zitokanazo na kulamba wakubwa miguu
 
Unafiki, fitna,kujipendekeza huko ndio unaweza!
Bahati mbaya teuzi zimebaki za maprof na madokta tu!
Utaendelea kupiga porojo tu humu ndani
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Nape ameondoka na Mwakyembe ameingia. Kuna watu walikuwa na wasiwasi kuwa huenda Mwakyembe asifanikiwe kuvaa kiatu kilichoachwa na Nape. Hata hivyo kwa muda mfupi aliokalia kiti hicho, amekuwa na ufanisi mkubwa na weledi wa hali ya juu. Amerudisha nyoyo za waliokata tamaa na amepunguza joto lililotanda na mashambulizi dhidi ya Serikali.

Mwakyembe ni shujaa. Alipoteuliwa kuwa Waziri wa Habari, ameanza kazi mara moja na kwa jinsi alivyoshughulikia suala la Nay wa Mitego kwa hakika limethibitisha kuwa jamaa ni mtu muhimu sana kwenye wizara hiyo. Tatizo la Nape ni umri wake. Bado ana utoto mwingi na hivyo kujikuta akiendekeza tamaa zake badala ya kufanya kazi. Aliwagawa wasanii badala ya kuwaunganisha. Amevigawa vyombo vya habari kwa kuvipendelea baadhi na kuviponda vingine.

Kwa ujumla Nape hakuwa kiongozi mtendaji. Aliendekeza majungu na fitina Wizarani. Afadhali ameondoka.

Karibu Dr Mwakyembe. Chapa kazi. Usimpendelee mtu na wala usimuonee mtu. Haijapita hata mwezi tayari Nape amebaki historia
Kwa sababu ile sumu iliozesha ubongo wake hivyo yeye atapelekwa kwa jinsi mtakatifu sana asiyejaribiwa atakavyotaka. Kwa viwango vya kijuha vya mafisiem, ni kweli atakuwa waziri mzuri sana kwenye hiyo wizara ya singeli.
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Nape ameondoka na Mwakyembe ameingia. Kuna watu walikuwa na wasiwasi kuwa huenda Mwakyembe asifanikiwe kuvaa kiatu kilichoachwa na Nape. Hata hivyo kwa muda mfupi aliokalia kiti hicho, amekuwa na ufanisi mkubwa na weledi wa hali ya juu. Amerudisha nyoyo za waliokata tamaa na amepunguza joto lililotanda na mashambulizi dhidi ya Serikali.

Mwakyembe ni shujaa. Alipoteuliwa kuwa Waziri wa Habari, ameanza kazi mara moja na kwa jinsi alivyoshughulikia suala la Nay wa Mitego kwa hakika limethibitisha kuwa jamaa ni mtu muhimu sana kwenye wizara hiyo. Tatizo la Nape ni umri wake. Bado ana utoto mwingi na hivyo kujikuta akiendekeza tamaa zake badala ya kufanya kazi. Aliwagawa wasanii badala ya kuwaunganisha. Amevigawa vyombo vya habari kwa kuvipendelea baadhi na kuviponda vingine.

Kwa ujumla Nape hakuwa kiongozi mtendaji. Aliendekeza majungu na fitina Wizarani. Afadhali ameondoka.

Karibu Dr Mwakyembe. Chapa kazi. Usimpendelee mtu na wala usimuonee mtu. Haijapita hata mwezi tayari Nape amebaki historia
Kweli umehitimu vyema kwenye mafunzo ya kutengeneza fitina na majungu. Pogba atakuzawadia uDc iliyoachwa na yule mjeda aliyelazwa chooni
 
kama unaongelea habari sawa,na amewekwa pale kubana wana habari ila ujue ile ni wizara ya habari,sanaa,utamaduni na michezo.hajui hata wimbo mmoja labda za mbaraka mwinshehe,kwenye michezo ndo kabisa hana abc mweupe kama unga,swala na nay katumwa na bosi wake kulimaliza hivyo kabla hawajaumbuka mahakamani kina bashite na babake
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Nape ameondoka na Mwakyembe ameingia. Kuna watu walikuwa na wasiwasi kuwa huenda Mwakyembe asifanikiwe kuvaa kiatu kilichoachwa na Nape. Hata hivyo kwa muda mfupi aliokalia kiti hicho, amekuwa na ufanisi mkubwa na weledi wa hali ya juu. Amerudisha nyoyo za waliokata tamaa na amepunguza joto lililotanda na mashambulizi dhidi ya Serikali.

Mwakyembe ni shujaa. Alipoteuliwa kuwa Waziri wa Habari, ameanza kazi mara moja na kwa jinsi alivyoshughulikia suala la Nay wa Mitego kwa hakika limethibitisha kuwa jamaa ni mtu muhimu sana kwenye wizara hiyo. Tatizo la Nape ni umri wake. Bado ana utoto mwingi na hivyo kujikuta akiendekeza tamaa zake badala ya kufanya kazi. Aliwagawa wasanii badala ya kuwaunganisha. Amevigawa vyombo vya habari kwa kuvipendelea baadhi na kuviponda vingine.

Kwa ujumla Nape hakuwa kiongozi mtendaji. Aliendekeza majungu na fitina Wizarani. Afadhali ameondoka.

Karibu Dr Mwakyembe. Chapa kazi. Usimpendelee mtu na wala usimuonee mtu. Haijapita hata mwezi tayari Nape amebaki historia
Umekuja lini Tz?

Yaelekea hukuwepo Rais JPM alipotangaza kuachiwa kwa Ney.

Leo Nape amekuwa mtoto, alipokuwa akiwatangazia ,kuwatafutia na kuwapatia
"goli la mkono " alikuwa mzee?

Wakati akizuia matangazo ya Bunge mubashara alikuwaje?

JE HUYO MKOMAVU WAZIRI WAKO BORA ANAWEZA RUDISHA MATANGAZZ MUBASHARA YA BUNGE ????
 
Nape alikuwa ni janga la taifa kwa hivyo yeyote ambaye angekalia hicho kiti ni lazima angen'gaa tu.

Nape ni muasisi wa siasa za chuki na kikabila nchini. Kumbuka ndiye kiongozi wa juu wa kwanza kabisa kutamka kuwa hawezi kuhamia Chadema kwa sababu yeye siyo mchaga.

Nape ndiye waziri aliyetuletea sheria ya ovyo kabisa ya habari ambayo ubovu wake ni wa kiwango cha lami

Nape tena alisifia siasa za goli la mkono. Hata kama ni kweli liatumika, kulikuwa kuna haja gani kulitangaza kwa mbwembwe kiasi kile

Madudu ya Nape ni mengi mno na kilichompata ni stahili yake. Kwanza hata hiyo saga ya Clouds aliichukulia vile kwa sababu tu ya chuki binafsi aliyekuwa nayo kwa RC.
 
Unafiki, fitna,kujipendekeza huko ndio unaweza!
Bahati mbaya teuzi zimebaki za maprof na madokta tu!
Utaendelea kupiga porojo tu humu ndani
Bahati mbaya sipo kwa ajili ya kutaka madaraka
 
Back
Top Bottom