Dr Edward Hoseah: Hakuna Mtanzania Aliyehusika na Ufisadi Katika Ununuzi wa Rada!

Ni jibwa lisilo na meno,kazi kubweka na ndege wanaruka angani ambao hatawakamata hata siku moja.nchi yetu shamba la bibi
 
Hakuna ushahidi uliopatikana hakuna kesi wanasheria wanajua hili sasa nyie kama ni mafisi maji tafuteni jaji wenu mahakama yenu mupeleke ushahidi wenu na pia msisahau sheria yenu mtakayoitumia nYAaaaaaaaambaaaaaffFfffffff

Hapo umenena.
 
Lusinde: Ona sera za CCM! Nipigeeeeeeee Nisipigeeeeeeee?

Magamba: Pigaaaaaaaaaaaa


Lusinde: Bendera ya CCM ina rangi ganiiiiiiiiiiiiii????????????? ??

Magamba: Kijaniiiiiiiiiiiiii.

Lusinde: Ukipanda mahindi yanaota rangi ganiiiiiiiiiiiii???????????

Magamba: Kijaniiiiiiiiiiiiii.

Lusinde: Ukipanda mpunga unaota rangi ganiiiiiiiiiiiiii???????????

Magamba: Kijaniiiiiiiiiiiiiiii

Lusinde: Migomba yote ina rangi ganiiiiiiiiiii?????????????

Magamba: Kijaniiiiiiiii.

Lusinde: Piga makofi na vigelegele kwa Chama cha Mapinduzi. CCM Oyeeeeeeeee.

Magamba: Oyeeeeeeeeee.

Ukomo wa akili za mtu mzima, magamba ana aibu zao!!!!!!!!
 
nashangazwa na takukuru kuwa hakuna mtanzania aliye husika na ufisadi ktk ishu ya rada.chanzo itv.wadau nawasilisha
kama hajawajua watz waliohusika mi nawajua, akitaka kuwajua awaite ma-"senior gambas" halafu wasimame mbele ya kioo
(mirror) watawaona tu
 
Hakukosea. BAE Systems wamekiri makosa ya kihasibu na si rushwa ndio maana wamerejesha "chenji". Kwamba kwa hesabu zao mbaya, waliitoza TZ bei kubwa zaidi. Hivyo kosa lote ni lao. Hakuna palipothibitishwa kwamba "vijisenti" kwenye akaunti ya Chenge vinahusiana na rada.

Ndugu zangu hakuna haja ya kuumiza vichwa. Serikali ikiamua kujiibia yenyewe au, even more better, viongozi wa juu pamoja na Rais mwenyewe wakidhamiria kuiibia nchi nyonge kama TZ tena kwa kushirikiana na wageni basi hiyo kesi imeshapotea. Hakuna haja ya kupoteza muda kujadili nyenzo kama Hosea inayotumika kukamilisha "dili" na kupangusa (mop) uchafu wowote unaodondokea pembeni.
 
Tatizo takukuru kazi yao ni kueneza rushwa hapa tz ukitaka kujua kuwa hiyo takukuru ni noma nenda katoe ripot ya rushwa wanampigia mtuhumiwa alafu wewe unadoda na pesa zao za moto.wanakula mishahara ya bure tu hawasaidii kitu ktk vita ya rushwa.
Kwahiyo hiyo walifanya madhambi ya ununuzi wa rada ni watu wa nchi gani? inaboa sana kutufanya watz wote mazumbukuku
 
Sawa imefika mahali wabunge WAZALENDO wapeleke mswada bungeni wa kufuta TAKUKURU kwasababu haifanyi lolote zaidi ya kulinda wahalifu kwa kodi zetu.
 
Jamani hawa viongozi wapimwe Akili maana sasa wanatufanya watoto wadogo.huo ujinga akawaeleze wanawe
 
Wakuu wakati mwingine haya mambo yanafanya kwenye level za kimataifa,ukiitizama sana utagundua kuwa ili utatue tatizo kama ili la Radar yakupasa basi uwe na Rais ambae uamuzi wake akiufanya basi awe ni dictator kwa kuwa kwa mfumo wa Nchi yetu huu wa miaka mitano mitano basi michezo kama hii ikiingia inakuwa ngumu sana kwa walio madarakani kudeal nayo kwa kuwa yahitajika mass support kubwa na assurance kubwa wale watakao kuwa na wajibu wa kudeal na maswala hayo kuwa watakuwa salama hata baada ya uongozi uliotumika kuwatia kitanzini wahusika.I

Ninakiona binafsi hatuna Institutional Government characters system bali tuna instutitional political system yana vyombo muhimu vya kudeal na hayo mambo vimekaa kisiasa na uwezo wake wa kuona ni katika nafasi ya kisiasa.

Tulipasa kuwa na taasisi zisizo na ukomo wa kimadaraka linapokuja swala la ualifu kwenye mali ya umma,yani UWT, PCCB, MAHAKAMA,TUME MAAALUM,POLICE na wengineo wenyekuhusika na dhamana ya kulinda na kutetea mali ya umma walipaswa ku c ordinate pale linapokuja kuwa ni swala la wizi wa kitaifa au mali ya Taifa.

Nina wasiwasi hata kada ya wasomi wa sheria katika vyombo vyetu hivi na taasisi kuu za serikali zenye kutengeneza mikataba na kupitia mikataba kwa niaba ya Serikali je zian wasomi wanokidhi haja ya kusoma mikataba kama hiyo ya kimataifa ya Rada iliyoundwa na wasomi wenye hadhi ya juu duniani.Hivi kwenye vyombo vyetu hivyo tuna wasomi kweli waliopita kwenye vyuo bora duniani kama Harvard,Yale au Oxford.Au ndio hivyo wote hapa hapa nyumbani first degree mchezo umeisha wanakutana na wataalamu wa kubuni vifungu [clause] zilizo enda shule.

Ukitizima mikataba mingi ya wajanja hawa imekaa kuwa implementation and interpretation of the Law itakuwa guided na sheria za Nchi za kimataifa na hata Arbitrator anakuwa ni kulingana na mazingira yao.Kama mkataba utakuwa ni sheria za Uingereza watajenga hoja Arbitrator awe wa kutoka France au Uswis.Saa watanzania sisi bila ya kuwa na wataalamu waliobobea na wako well paid to enjoy life and feel proud to work on behalf of the nation ni swala gumu kweli kutekekezeka?

Ninavyofahamu mimi ukiondoa wataalamu kama wa NASA na Computer engineers watu wengine kitaaluma wanaolipwa vyema ni kada ya wanasheria.Ili nalo limekuwa ni tatizo sana Tanzania.Hakika sijui mishahara ya wanasheria wa Tanzania,Hivi ni mwanasheria gani anaweza kujenga hoja ya kuetetea mikataba ya mabilioni wakati mshahara wake hauzidi hata milioni mbili.

Binafsi ningetamani kuona kuwa serikali inakuwa na cream ya baadhi ya Watanzania,ambao ni well trained and well expose ambao wako field tofauti,Uchumi,biashara,Sheria,Sayansi and technology ambao kazi yao wao ni kushauri na kupitia mambo muhimu yanayohusu serikali ikiwamo mikataba ambayo serikali inategemea kuingia au imeshaingia na hivyo kama kuna uwezekano wa kubolesha kwa niaba ya Taifa ufanye.Style hiyo ya kurecruit Government highest brains ilipaswa kuwa ni endelevu kwenye kila idala,they work and think always on behalf of the Government.Cha msingi wao wawe well paid to the level wasiwe na hofu ya future ya maisha yao na mara mara wawe expose na dunia ili wawe sambamba na nyakati.Sio kuwa haya hayawekena na hakika yanawekena na kikwazo ni kukosa viongozi wenye dhamira ya TAIFA mbele.

Wangekuwa National Brilliant Brains upande wa sheria hakika issue kama hii ya Radar,wangeinyambalua kama wanalia,na kisha kwa heshima Rais anasimama kutundika medal kwenye kifua cha mtu kwa heshima kuwa huyu nae ni mpambanaji aliyeokoa Pesa zetu na kuadabisha wezi wetu.

Uwa namuona mtu kama TINDU LISSU na baadhi ya gineus wengine wa sheria,natamani nimngoe kwenye siasa afungiwe kwenye vyumba vya sheria full vivyozi maisha yake yeyeni kucheza na mikataba mikubwa ya Serikali na kuunda mikataba mikubwa ya Serikali uku akizunguka duniani kote kuona ni aina gani ya mikataba inatufaha kuteletea maendeleo miaka hamsini na mia ijayo kwenye rasilimali tulionayo Watanzania ya Madini na maliasili zingine.

Lakini tulivyo wanamuona kama kiwingu baada ya kumuon kama Asset,hivi ni lini tutapa kionngozi atake identify watu [Asset] na sio mashindano kuona fulani akipewa kazi fulani atasifiwa na kuonekana kafanya jambo la maana kwa Taifa.Mungu katuumba kila myu na talent zake,hakika mpaka sasa kuna watu wako well talented kwenye fani nyingi sana wengine wamekimbia Nchi wako zao ughaibuni hawana mchango wowote kwa Taifa,wanafaidisha Mataifa mengine.

Nalia sana na mfumo badal ya kutengeneza mfumo wenye kujenga watu walio makini kwa Taifa,na wawe well paid ili kuwaondoa kwenye mashaka ya kurubunika wawe responsible kuleta mambo ambayo ni mema na positive kwa Taifa,hata kama Marais watapita lakini wanazikuta cream zinawasaidia kujenga Taifa na zinazidi kujijenga na kuongezeka huku Marais nao wanapiata kwa mujibu wa katiba na sheria za Nchi.Haya mambo ya Radar angeondoka Kikwete matokeo na majibu yake kama tungekuwa na mfumo yangeendelea kwa kuwa tungekuwa na mfumo unaojiendeleza kupitia mambo mbalimbali na tofauti tofauti Nchin na Nje ya Nchi.
 
Aliyenifurahisha zaidi ni Kikwete pale aliposema kuwa Tanzania inahitaji msaada wa vifaa/nyenzo na ujuzi ili waweze kupambana na rushwa! Nimebaki najiuliza, Kikwete na serikali yake wahitaji kifaa gani kuchunguza EPA? wanahitaji nyenzo gani kuchunguza Meremeta, Deep Green? Hapo Arumeru kwenyewe rushwa inatolewa nje nje, Kikwete anahitaji wafadhili toka Ulaya wamnunulie magunia ya kuwaweka wale wanaotoa rushwa?

Na kama kweli Tanzania inahitaji msaada, mbona Hosea ameweza kufanya uchunguzi wa kina na kugunduwa kuwa hakuna mtanzania(!!!) aliyehusika kwenye rushwa ya RADA! Alitumia kifaa/nyenzo gani huyu bwana Takukuru?

By the way, Hosea anakumbuka wikileaks yake kuhusu rushwa na armi za wakubwa?


KAULI YA HOSEA ANGEITOA KATIKA NCHI INAYOJENGA UCHUMI KAMA iSRAEL, kENYA, nIGERIA, MAREKANI, Ghana na Botswana angefukuzwa kazi. Lakini katolea kauli yake katika n"chi isiyojuua kujenga uchumi, basi kila mtu anaiona kama ni wimbo wa sadaka!
Hii ndio sera mpya iitwayo "Tamba uone!
 
Hivi kweli hii nchi usimamizi na uzalendo havipo tena..

Raia wa Uingereza wameona uozo wa ununuzi wa rada wakalalamika hadi kwenye bunge lao, sisi huyu mjinga anasema hakuna rushwa kwa nini???

Je Nani alifanya procurement ya hii rada?
Je nani aliidhinisha mkataba wa manunuzi?
Je nani alilipa hela ya manunuzi??

je hawa wote hawapashwi kuadhibiwa????
 
Sio kauli ya kushangaza kwani hosea huyo huyo aliwahi kusemakuwa hata katika kutoa zabuni kwa kampuni tata ya richmond hakukuwa na dalili ya rushwa (achilia mbali rushwa yenyewe)


Haya mambo ni magumu! Hapo kwenye Richmond aliyeshiriki ni Mohamed Galle si ndiye aliyefikishwa mahakamani!
 
Back
Top Bottom